Wabunge wanatuona ‘SISI’ wananchi ni wajinga sana

Wabunge wanatuona ‘SISI’ wananchi ni wajinga sana

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Tunategemea Wabunge wawe watetezi wa wananchi kwenye masuala mbalimbali kurahisisha maisha yetu badala yake wao ndio wamekuwa wawakilishi wa serikali kutugandamiza.

Wabunge wameridhia serikali kupunguza kodi kwenye bia na kuongeza kodi kwenye mafuta ya petrol, hawaoni kuwa ni mzigo kwa mwananchi, wameongeza tozo ya kodi kwenye miamala ya simu, mbaya zaidi wazo hili lilitolewa na mbunge kwa mgongo wa kodi ya uzalendo.

Wabunge ni wabinafsi sana eti mshahara wao hautoshi wanaomba waongezewe, wanajiona wao ni special kuliko madaktari, wanapokea sh 13.8M kwa mwezi mbali na posho ya sh 120,000 ya kikao kwa siku, hii kama sio dharau kwa wananchi nini.

Hawana faida kwetu na kwa nchi wamebaki kututungia sheria mbovu na kandamizi, binafsi sioni faida ya mbunge wangu zaidi ya kujinufaisha yeye na familia yake kupitia kura yangu.

Wanatudharau sana sisi wananchi, hawako ‘accountable’ wala ‘resiponsible’ kwa wapiga kura wao kwa vile wanajua once wakishachaguliwa hakuna wa kuwawajibisha hadi miaka 5 iishe.

Nashauri tuirejee katiba ya Warioba iliyopendekeza wabunge kama hawa tuwaondoe hata kabla ya kipindi chao kwisha, bila kufanya hivyo wataendelea kutuona sisi wapiga kura wajinga siku zote.
 
Tunategemea Wabunge wawe watetezi wa wananchi kwenye masuala mbalimbali kurahisisha maisha yetu badala yake wao ndio wamekuwa wawakilishi wa serikali kutugandamiza.

Wabunge wameridhia serikali kupunguza kodi kwenye bia na kuongeza kodi kwenye mafuta ya petrol, hawaoni kuwa ni mzigo kwa mwananchi, wameongeza tozo ya kodi kwenye simu, mbaya zaidi wazo hili lilitolewa na mbunge kwa mgongo wa kodi ya uzalendo.

Wabunge ni wabinafsi sana eti wanasema mshahara wao hautoshi wanaomba waongezewe kweli hawa wanatuwakilisha? Kama sio dharau ni nini.

Hawana faida kwetu na kwa nchi wamebaki kututungia sheria mbovu na kandamizi, binafsi sioni faida ya mbunge wangu zaidi ya kujinufaisha yeye na familia yake kupitia kura yangu.

Wanatudharau sana sisi wananchi, hawako ‘accountable’ wala ‘resiponsible’ kwa wapiga kura wao kwa vile wanajua once wakishachaguliwa hakuna wa kuwawajibisha hadi miaka 5 iishe.

Nashauri tuirejee katiba ya Warioba iliyopendekeza wabunge kama hawa tuwaondoe hata kabla ya kipindi chao kwisha, bila kufanya hivyo wataendelea kutuona sisi wapiga kura wajinga siku zote.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
JamiiForums-981320052.jpg
 
Upandacho ndicho uvunacho!

Ukipanda mazao kwa kufuata kanuni bora za kilimo, utavuna mazao bora.

Ukipanda mazao kisha yakaharibiwa kabla ya mavuno, utavuna kidogo ama hautovuna kabisa.

Usipopanda chochote hautovuna chochote!
 
Mpaka sasa naona cheo cha ubunge ni mzigo kwa taifa. Nashauri wafutwe wote tuwe na mabaraza ya madiwani tu. Sheria za nchi zitungwe na Baraza kuu la madiwani litakalohusisha uwakilishi wa madiwani wachache kutoka kila mkoa.

Haya masuala ya tume huru wanayoyapigania wapinzani ni lengo la kwenda bungeni kula fedha za wananchi tu. Hakuna mwenye uchungu na wananchi sio wabunge wa CCM wala CHADEMA. Wote ni mizigo.
 
wananchi wenyewe ndo wajinga.

2025 watagawiwa tisheti na kangamoko wabunge hawahawa mang'ombe warudi mjengoni.

yaani huyo mfumuko wa bei ufumuke tu mkate tununue 10,000
Acha waisome namba.
 
Bila shaka watawakilisha waliowachagua. Wakuwakilishe wewe mwananchi wakati ni serikali iliwachagua?
Ni wawakilishi wa serikali kwa wananchi. That is convoluted but that is what you get from an even more convoluted constitution.
 
Pale ni zaidi ya kusanyiko,lile ni genge la wahuni.
Pale kuna kikundi cha wahuni waliochaguliwa kihuni kwa ajili ya maslahi ya wahuni. Hakuna mbunge hata mmoja mwenye moral authority ya kujitapa kuwa yuko bungeni legally. Bytheway kuuita lile kusanyiko kuwa ni BUNGE ni kukosea na kulikosea heshima neno bunge.
 
wananchi wenyewe ndo wajinga.

2025 watagawiwa tisheti na kangamoko wabunge hawahawa mang'ombe warudi mjengoni.

yaani huyo mfumuko wa bei ufumuke tu mkate tununue 10,000
Mkuu, labda we' mwenzetu, ulipata bahati kuwa na m' bunge aliyepatikana kutokana na kura 'halali na haki'!
 
Mpaka sasa naona cheo cha ubunge ni mzigo kwa taifa. Nashauri wafutwe wote tuwe na mabaraza ya madiwani tu. Sheria za nchi zitungwe na Baraza kuu la madiwani litakalohusisha uwakilishi wa madiwani wachache kutoka kila mkoa.

Haya masuala ya tume huru wanayoyapigania wapinzani ni lengo la kwenda bungeni kula fedha za wananchi tu. Hakuna mwenye uchungu na wananchi sio wabunge wa CCM wala CHADEMA. Wote ni mizigo.
Dawa idadi ya majimbo ipunguzwe.
 
Back
Top Bottom