Wachaga, huu utaratibu wa kujenga kaburi kabla ya kufa umeanza lini?

Wachaga, huu utaratibu wa kujenga kaburi kabla ya kufa umeanza lini?

TODAYS

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2014
Posts
14,747
Reaction score
24,250
Nimeshtushwa kidogo kutoka kwa huyu ndugu Kimaro.

Mkoa wa Kilimanjaro, katika kijiji cha Mbosho, wilayani Machame, kutana na Patrick Kimaro, mwenye umri wa miaka 59, ambaye amejingea kaburi lake.




Kimaro amesema ni sehemu tu ya kujiandaa na maisha ya baadae na kuongeza kusema amefanya hivyo akiwa na akili timamu bila kushinikizwa, lakini bado, kwa baadhi jambo hilo kwao linatia ukakasi.

Anasema, 'nilionja machungu baada ya kuandaa mazishi ya wazazi wangu'

Baadhi wanalichukulia kama uchuro kwa misingi kwamba linaweza kuleta kisirani katika familia.

Hatua hii ya Bwana Kimaro imewashangaza wengi, ndani ya kijiji chake na nje ya mipaka ya kijiji hicho. Kwa sababu sio jambo lililozoeleka katika jamii ya kiafrika hasa jamii ya kichagga anayotoka Kimaro.





Source: BBC
 
Sioni ubaya wowote. Inawezekana wanafanya hivyo kwa sababu pia Wakristu wengi ni Wakristu. Kumbuka Yesu Kristu alizikwa kwenye kaburi lililokuwa limeandaliwa kitambo kwa ajili ya kumzika Yosef wa Armathayo. Ilikuwa kawaida kabisa kwa Wayahudi wenye uwezo kuandaa makaburi yao siku nyingi kabla hawajafa.

Mimi binafsi naona ni jambo zuri maana linaondoa usumbufu kwa ndugu kuja kuandaa kaburi ukishakufa.
Makaburi yanayochimbwa ukishakufa mara nyingi yanachimbwa na watu huku wanakunywa konyagi au wanavuta bangi. Ni heri kujiandalia mkazi yako ya milele mapema ikiwezekana

Hongera sana Patrick Kimaro nawasihi na wengine waige huu mfano
 
aliyejemga kaburi maarufu anaitwa Sabasita ni askari wa muda mrefu nchini kikosi maalum unajua kazi aliyoifanya mpaka sasa nadhani amefanya vyema maana anajua aliyoyafanya
 
Mara nyingi waliotangulia wanaacha msala kwa waliyobaki ie kuzikwa kijijini. Ni vizuri kujiandaa.
 
Naona hataki kuja kuzikwa sehemu ambayo hana uhakika nayo kwa ubora...si unaona amejiwekea hata paa juu, ili awe na kivuli na mvua pia isimnyeshee akishazikwa...
... kuna video alikuwa anahojiwa akasema makaburi ya familia including wazazi wake yako hapo hapo shambani kwake ila hataki kuzikwa shambani; kaamua kuzikwa jirani kabisa na nyumba; in fact anadai wazo lake la awali alitaka ajenge kaburi lake chumbani kwake ila akahisi wajuku na vitukuu watakuja kukimbia nyumba so akaamua kulijenga nje.
 
Sioni ubaya wowote. Inawezekana wanafanya hivyo kwa sababu pia Wakristu wengi ni Wakristu. Kumbuka Yesu Kristu alizikwa kwenye kaburi lililokuwa limeandaliwa kitambo kwa ajili ya kumzika Yosef wa Armathayo. Ilikuwa kawaida kabisa kwa Wayahudi wenye uwezo kuandaa makaburi yao siku nyingi kabla hawajafa.

Mimi binafsi naona ni jambo zuri maana linaondoa usumbufu kwa ndugu kuja kuandaa kaburi ukishakufa.
Makaburi yanayochimbwa ukishakufa mara nyingi yanachimbwa na watu huku wanakunywa konyagi au wanavuta bangi. Ni heri kujiandalia mkazi yako ya milele mapema ikiwezekana

Hongera sana Patrick Kimaro nawasihi na wengine waige huu mfano
We utaiga?

Sent from my TECNO KE5 using JamiiForums mobile app
 
Nimeshtushwa kidogo kutoka kwa huyu ndugu Kimaro.

Mkoa wa Kilimanjaro, katika kijiji cha Mbosho, wilayani Machame, kutana na Patrick Kimaro, mwenye umri wa miaka 59, ambaye amejingea kaburi lake.




Kimaro amesema ni sehemu tu ya kujiandaa na maisha ya baadae na kuongeza kusema amefanya hivyo akiwa na akili timamu bila kushinikizwa, lakini bado, kwa baadhi jambo hilo kwao linatia ukakasi.

Anasema, 'nilionja machungu baada ya kuandaa mazishi ya wazazi wangu'

Baadhi wanalichukulia kama uchuro kwa misingi kwamba linaweza kuleta kisirani katika familia.

Hatua hii ya Bwana Kimaro imewashangaza wengi, ndani ya kijiji chake na nje ya mipaka ya kijiji hicho. Kwa sababu sio jambo lililozoeleka katika jamii ya kiafrika hasa jamii ya kichagga anayotoka Kimaro.





Source: BBC
Kwa hiyo umeona wachaga tuu....
Yule wa iringa je hujamwona?mbona kawaida sana hilo.
Mbona wako hadi wanaochonga jeneza kabisa
 
Ni vyema maana watu hawachelewi kutupiana msala nani achimbe kaburi na marehemu azikwe wapi.

Ikifaa akanunua na jeneza lake safii awekee kwa stoo. Miaka 59 kuelekea 60 inatosha sana kwa kuishi
 
Huyu Mwamba ana Stress za matukio aliyokuwa anafanya "enzi zake" zile..
 
Nimeshtushwa kidogo kutoka kwa huyu ndugu Kimaro.

Mkoa wa Kilimanjaro, katika kijiji cha Mbosho, wilayani Machame, kutana na Patrick Kimaro, mwenye umri wa miaka 59, ambaye amejingea kaburi lake.




Kimaro amesema ni sehemu tu ya kujiandaa na maisha ya baadae na kuongeza kusema amefanya hivyo akiwa na akili timamu bila kushinikizwa, lakini bado, kwa baadhi jambo hilo kwao linatia ukakasi.

Anasema, 'nilionja machungu baada ya kuandaa mazishi ya wazazi wangu'

Baadhi wanalichukulia kama uchuro kwa misingi kwamba linaweza kuleta kisirani katika familia.

Hatua hii ya Bwana Kimaro imewashangaza wengi, ndani ya kijiji chake na nje ya mipaka ya kijiji hicho. Kwa sababu sio jambo lililozoeleka katika jamii ya kiafrika hasa jamii ya kichagga anayotoka Kimaro.





Source: BBC
Huo ni utamaduni wa wayahudi. Na inasemekana asili ya wachaga ni huko uyahudi....!!!
 
aliyejemga kaburi maarufu anaitwa Sabasita ni askari wa muda mrefu nchini kikosi maalum unajua kazi aliyoifanya mpaka sasa nadhani amefanya vyema maana anajua aliyoyafanya
Hili ndio jibu sasa, hiyo kazi yake ya upolisi amefanya uovu mwingi.Alikuwa morogoro huyu
 
Back
Top Bottom