Wachaga, huu utaratibu wa kujenga kaburi kabla ya kufa umeanza lini?

aliyejemga kaburi maarufu anaitwa Sabasita ni askari wa muda mrefu nchini kikosi maalum unajua kazi aliyoifanya mpaka sasa nadhani amefanya vyema maana anajua aliyoyafanya
sabasita ni wa morogoro huyu
 
Kwani inatofauti gani na kulipia eneo kwa ajili ya kaburi pale utakapokufa kama alivyofanya gavana mstaafu wa BOT? Au kama ilivyo USA.. ni maandalizi kuepusha kero kwa wanaobaki!
 
Kwani inatofauti gani na kulipia eneo kwa ajili ya kaburi pale utakapokufa kama alivyofanya gavana mstaafu wa BOT? Au kama ilivyo USA.. ni maandalizi kuepusha kero kwa wanaobaki!
binafsi nimeipenda!
 
Kuchimba shimo la kuzikwa na kulije gea haikuanza leo kuna bwana 1 kule mkoani kagera wilaya muleba kata tarafa kamachumu kijiji bushagala huyu bwana jina lake alikuwa akiitwa birunduli ukiwa unaenda ndorage ukipita kamirabala mbele kidogo kuna kijumba cha ghorofa 1 huyu bwana alichimba shimo(kabiri)akiwa bado yuko hai miaka ya 1970

Kafa muwaka 1989 kazikwa hapo kwa wanao mfahamu huyu mtu alikuwa anafukuzwa na nyerere kipindi cha vita ya uganda ikisemekana alikuwa rafikie na idd amini dada baada ya vita nyerere alimsamehe alikuwa akiishi uhamishoni mambasa kenya miaka hiyo huyu birunduli alikuwa maarufu mkoani kagera watu wazima wanafahamu makeke yake

Hata njombe mbona wabena na wakinga kujichimbia shimo na kulijengea hili wazikwe humo baada ya kufa imekuwa fasheni yao
 
Naomba useme Kimaro sio wachaga[emoji2959]
Yaani UTUKOME
 
I meant Tunda mzazi mwenzie na Whozu ni mtoto wa mzee sabasita
Ndio ni baba halal wa tunda,miaka flani alitutaabisha sana arusha,baadae akaamishiwa Morogoro...

Kujiandalia Jeneza na sehem ya kuzikwa ni jambo sahihi sana kwa upande wangu...
Cha kwanza ni vyema nijue sehem ninayoenda kulala usingizi wa milele nikiwa hai, jeneza langu najiandalia mwenyewe ninalolitaka,na kama nina pesa ya kutosha pia naanda fungu kwa ajili ya mazishi yangu..
Ukatae ukubali kifo ni jambo la lazima..
Uwe mwema ama mwovu lazima tufe.

Kujiandalia kila ukiliona jeneza lako lazima ukumbuke siku za mwanadam kuishi ni chache...

Tukumbuke kumcha Mungu.
 
H
 
Ni ulimbukeni tu, labda kuyumba kwa dishi, hiyo pesa iliyotumika angewaachia wengine waendelee na maisha. Tulizaliwa watupu na tutarudi udongoni watupu.

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
 
Binadamu huwa wananishangaza sana wanapojipa matumaini kuwa hawatokufa, sote tutakufa huo ndio mwisho wetu ukiamua kujiandaa sio jambo baya
 
Hiv kwa mfano amepata safari ya kwenda India kwa matibabu ndege ikaanguka baharin asionekane hilo kabur wanalifanyaje.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…