Wachambuzi bora watano wa soka nchini

Wachambuzi bora watano wa soka nchini

dr rick 2006 alipoulizwa nan atawin world cup bila hofu akasema italy huku ikiwa ya mwisho kundini imefungwa mechi moja na kusuruu moja na mech iliyosalia dhid ya german ambayo imempiga saudia goli nane italy wakashinda game ya mwisho na mwisho wwkafika finnal hapo ndio nilipomfaham rick abdala mzee wa mikeka mfolow insta na fb muone mikeka yake coz ananipa sana hela ya kula
Kuweka rekodi sawa: Ujeremani waliwafunga Saudi Arabia goli nane mwaka 2002 na sio 2006.
 
Asante sana!
Wewe una mawazo kama yangu kila mahali. Pia nilikuwa natafuta jina la huyo Kashasha, nilisahau jina lake, nilimuona Tbc nikapiga saluti. Kwa Tz, kwangu huyu ndo namba moja. Umeongea ya Dr. Leakey, uko sawa kabisa na pia nafikiri watu wanamkubali sababu ni mmoja wa wachambuzi wa kwanza kuanza onekana ktk tv enzi za dtv na premier ligi enzi zile, ila hayupo technically au tactically kabisa. Yeye likifungwa goli atakumbushia kwa kulilinganisha na goli lililofungwa kipindi fulani. Kiufupi ni mzee wa historia ktk matukio ya soka. Edo na Leah wanajitahidi sana, bado vijana ila Dauda ni majungu na kuponda, bado sana!


duh kumbe bado mnadekea TBC?
 
Dr Leakey anajua historia sio tactics za soka hii ni sababu ya kusoma sana magazeti toka zamani zamani. Ana story sana za kupaka nakshi na chumvi nyiingi, sasa iliposhamili Internet akapotea.
 
Hivi nani anayejua kuchambua sasa kama wote wanapondwa,, kama huna sema napita utaeleweka tu eti!
 
1. Mimi mwenyewe (tycoon Makaveli jr. El classico Diego simeone )
2.Edo kumwembe
3.Kashasha
4. Ricky abdallah
5. haji manara

Hao wengine mtafte pakuwaweka, ila shaffih ni kiazi tena mviringo, na dr ricky ni bingwa wa history
 
Moja mie, hao wengine tafteni pakuwaweka, ila shaffih dauda sijawah kumkubali huyu jamaa, ni km kinyonga vile
 
Leaky, Kumwembe, Shafii, Haji, Kashasha. Nawakubali kibwana na Jeff leya kama upcoming
 
Tatizo tunachanganya wachambuzi na wasimulizi. Pia kuna wale wambea wa mpira. Wapo uptodate na masuala ya mpira. Mchambuzi lazima ajue mifumo na aina ya wachezaji au uchezaji. Kujua historia na umbea wa mpira inakuwa bonus kwake. Huyu ndio Kumwembe.
Dr Leaky anajua historia ya mpira. Umetoka wapi na uko wapi.Si sana mifumo.
Wengine hakuna sehemu waliyobobea zaidi ya kupekua mitandao na kujua umbea wote wa mpira.
 
Uchambuzi ni pamoja na kujua Historia basi Dr.Leakey yuko vizuri zaidi kwa hapo, kwa uchambuzi wa kitaalamu katika game basi nampa Alex Kashasha...

Kwa Ngonjera uchambuzi wa upande mmoja au ligi moja tu na kufata matukio basi hapa wanaingia wote waliobaki kina Haji Manara, Shafih Dauda, Edo Kumwembe, Ibra Masoud, Alex Luambano.. Etc.

Na wapo wachambuzi watangazaji jina Maulid kitenge, Katanga, Dr. Muwa. Etc.

Japo hao niliowataja mwisho wanaweza pia kuelezea masuala ya mpira kitaalamu so ki uzoefu bali kujifunza au kuiga kupitia uchambuzi wa vyombo vya habari vya ng'ambo..
 
Gang Chomba na AC Milan,jamaa anajua kuichambua AC Milan kwa lugha zote english,swahili,kimakonde,kiitaliano,kiarabu,kihausa na hata kisomali dah jamaa ananiacha hoi sana akiisifia AC Milan yaani sidhani kama kuna shabiki kama yeye wa AC Milan mwenye roho ngumu kama yeye,maana AC Milan hii kama inashiriki La Liga inashika mkia inashuka daraja haifikishi hata pointi 10 mwisho wa msimu na ushindi wao draw san siro giusseppe meazza.
 
Dr. Leaky uchabuzi wake haupo technically sana kama ulishamfuatilia vizuri. Yeye anaweza kutoa historia pia na reaction za mashabiki kwa timu fulani. Pia kinachoonekana anajua kuchambua ni kwasababu anapenda sana mpira na ni mmoja ya watanzania ambaye mara nyingi anaweza kusafiri kwenda Ulaya kuangalia gemu fulani mfano hizi za Champions League au Euro na WC. Kwahiyo uzoefu wake ndio unasabaisha hivyo.

Lakini kwenye ufundi zaidi Mwl. Kashasha ni zaidi ya wote kwa mtazamo wangu. Yule mzee nimemfuatilia sana. Akiangalia mpira dakika 15 tu anaweza kutabiri timu inafungwa kama haitabadili mfumo fulani. Aisee jaribu kumfuatilia huyu mzee huwa ananipa raha sana jinsi alivyo technically.

Eddo Kumwembe pia ni mzuri

Jeff Leya nae ni mzuri

Manara namkubali

Shafii Dauda bado sana huyu

Huyo Dr.??Ricky ni mjanja wa mjini ambae hukariri habari za soka toka mitandao mbalimbali ya michezo toka ulaya na kuja kuwakoga watu mbele ya TV ambao humuona ni mjuzi wa mambo ya soka wakati ni wa kawaida tu.
Hata Shaffi nae yupo kama
Rick(sio Leakey) japo huyu huwa anajiongeza kuipa maana ya kile anachokichambua.
Hawa ndio the best;
1.Eddo
2.Kashasha.
 
Huyo Dr.??Ricky ni mjanja wa mjini ambae hukariri habari za soka toka mitandao mbalimbali ya michezo toka ulaya na kuja kuwakoga watu mbele ya TV ambao humuona ni mjuzi wa mambo ya soka wakati ni wa kawaida tu.
Hata Shaffi nae yupo kama
Rick(sio Leakey) japo huyu huwa anajiongeza kuipa maana ya kile anachokichambua.
Hawa ndio the best;
1.Eddo
2.Kashasha.

Hatupo tofauti katika mitazamo yetu.
 
appoh dr leakey nipe spelling za jina lake fb.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom