Wachambuzi wetu wanachumbua dereva wa bodaboda apigwe na dereva wa fuso

Wachambuzi wetu wanachumbua dereva wa bodaboda apigwe na dereva wa fuso

Huo mfano wako hausadifu hiki ninachokisema hapa. Simba, Yanga, Al-Ahly na mamelodi ni timu ambazo ziko robo finali ya CAF champions, hii inatosha kumfanya mchambuzi mwenye akili kuwa hizi timu uwanjani ziko na ulinganifu hata kama kwenye uwekezaji (pesa na majengo, miundombinu) zimezidiana sana. Kama ni swala la kuwekeza tu ziko timu ambazo zimewekeza sana kuliko simba na yanga lakini hazifika hatua hii ya robo finali, hivyo Kwa mchambuzi mwenye utimamu wa mwili na akili ingetosha kuondoa factor ya uwekezaji na kubakiza factors za upambanaji kiwanjani, teamwork, mbinu za mabenchi ya ufundi na mchango wa mashabiki uwanjani.

Huo mfano wako wa Man city na RB Leipzia ni mwendelezo wa ukosefu wa weredi kwenye uchambuzi kwakuwa Man city na RB haziko zote kwenye robo final ya EUFA champions kama zilivyo simba na al-ahly.

Ukiona mchezaji anacheza Afrika kiwango chake bado ni cha Afrika tu, wachezaji bora duniani wamenyakuliwa na timu za Ulaya, timu zetu za Afrika zina wachezaji wanaolinganalingana na kuzidiana tu viwango vya kujituma, motivation wanazopewa (pesa, mazingira na mabenchi ya ufundi).
Good good analysis........
 
Wewe una matatizo kichwani. Kwa hiyo Man city akikutana nusu fainal na Dortmund unafikiri kuna mchambuzi ataitabiria Dortmund kushinda mbele ya man city? Kwa hiyo yanga wakicheza na underdog kama akina Prison huwa wanajiachia tu kisa wanacheza na underdog? Hakuna kufarijiwa uwezo ni mdogo na wachezaji wenu wa kutoa mataulo golini.
Lazima mfahamu kuwa hii dunia Ina wachezaji wazuri na wenye vipaji ambao timu kubwa haziwezi kuwasajili wote. Ndio maana unawaona akina Mayelle, pacome, nzengeli, Ibrahim Bacca ambao walikuwa hawafahamiki wamekwenda kuibukia Yanga. Sio kwamba Al-ahly na mamelods wamewachukua wachezaji wooote wazuri Africa na timu nyingine Zina makapi TU. Kinachokosekana ni Wachezaji wa timu ndogo kujituma na kujielewa tu. Ndio maana Ihefu wallifunga Yanga na prison waliifunga Simba na arsenal aliukosa ubingwa wa ligi kwa kufungwa na "timu ndogo" EPL. Ni Wachezaji kujituma TU ndio kunakoleta tofauti n sio ukubwa wa uwekezaji.
 
Nimeshuhudia dereva wa lori akichomolewa na kupigwa na dereva wa bodaboda baada ya dereva wa lori kumsukumia mtaroni dereva wa bodaboda.

Sio kwamba timu ikiwekeza sana lazima mara zote iifunge timu yenye uwekezaji mdogo. Wachambuzi wetu wanazilazimisha Al-Ahly na Mamelodi izifunge Simba na Yanga kwenye mashindano ya CAF champions eti kwakuwa zina uwekezaji mdogo kuliko al-ahly na mamelodi. Uchambuzi wa aina hii hauonyeshi weledi. Wachambuzi wanasahau factors za muunganiko wa timu, ari za wachezaji (self motivation) na uzuri wa mabenchi ya ufundi ya kila timu.

Ni kweli uwekezaji wa lori ni mkubwa kuliko uwekezaji wa bodaboda na ni kweli lori linapoigonga bodaboda mara zote lori litaiharibu zaidi pikipiki, lakini sio kweli kwamba mara zote dereva wa lori ana nguvu zaidi kuliko dereva wa bodaboda.

Timu zote zina wachezaji waliozifikisha timu zao robo finali, Pale uwanjani wanacheza wachezaji (madereva) sio pesa (malori na bodaboda).
Na wewejkwa fikra zako ukichambua kati ya young vs mamelod au simba vs al ahly unadhani nani watapewa nafasi kubwa ya ushindi..
 
Lazima mfahamu kuwa hii dunia Ina wachezaji wazuri na wenye vipaji ambao timu kubwa haziwezi kuwasajili wote. Ndio maana unawaona akina Mayelle, pacome, nzengeli, Ibrahim Bacca ambao walikuwa hawafahamiki wamekwenda kuibukia Yanga. Sio kwamba Al-ahly na mamelods wamewachukua wachezaji wooote wazuri Africa na timu nyingine Zina makapi TU. Kinachokosekana ni Wachezaji wa timu ndogo kujituma na kujielewa tu. Ndio maana Ihefu wallifunga Yanga na prison waliifunga Simba na arsenal aliukosa ubingwa wa ligi kwa kufungwa na "timu ndogo" EPL. Ni Wachezaji kujituma TU ndio kunakoleta tofauti n sio ukubwa wa uwekezaji.
Unafikiri ni kujituma na kujielewa tu ndio kunaipa mafanikio akina Man city au Real Madrid ? Kwamba fulham au westham hawjitumi na kujielewa kuliko liverpool ndio maana hawana mafanikio kama liverpool? Suala la kuwepo wachezaji wazuri kadhaa ndani ya timu ya kawaida hilo ni suala la kawaida lakini haiondoi ukweli kuwa timu zinazidiana ubora.
 
Nimeshuhudia dereva wa lori akichomolewa na kupigwa na dereva wa bodaboda baada ya dereva wa lori kumsukumia mtaroni dereva wa bodaboda.

Sio kwamba timu ikiwekeza sana lazima mara zote iifunge timu yenye uwekezaji mdogo. Wachambuzi wetu wanazilazimisha Al-Ahly na Mamelodi izifunge Simba na Yanga kwenye mashindano ya CAF champions eti kwakuwa zina uwekezaji mdogo kuliko al-ahly na mamelodi. Uchambuzi wa aina hii hauonyeshi weledi. Wachambuzi wanasahau factors za muunganiko wa timu, ari za wachezaji (self motivation) na uzuri wa mabenchi ya ufundi ya kila timu.

Ni kweli uwekezaji wa lori ni mkubwa kuliko uwekezaji wa bodaboda na ni kweli lori linapoigonga bodaboda mara zote lori litaiharibu zaidi pikipiki, lakini sio kweli kwamba mara zote dereva wa lori ana nguvu zaidi kuliko dereva wa bodaboda.

Timu zote zina wachezaji waliozifikisha timu zao robo finali, Pale uwanjani wanacheza wachezaji (madereva) sio pesa (malori na bodaboda).
Hivi mkuu Tanzania tuna wachambuzi? Hawa hawa akina Kazumari? Hawa hawa akina Baba Levo, Mwalimu wa UPE Oscar Oscar? Akina Shaffi Dauda? We are not serious!
 
Unafikiri ni kujituma na kujielewa tu ndio kunaipa mafanikio akina Man city au Real Madrid ? Kwamba fulham au westham hawjitumi na kujielewa kuliko liverpool ndio maana hawana mafanikio kama liverpool? Suala la kuwepo wachezaji wazuri kadhaa ndani ya timu ya kawaida hilo ni suala la kawaida lakini haiondoi ukweli kuwa timu zinazidiana ubora.
Mkuu ni pamoja na gari ya wachezaji. Hivi unataka kuniambia Bochum kumfunga Bayern ana wachezaji Bora kuzidi Bayern FC? Wachambuzi wasidanganye watu kwenye soka kila kitu kinawezekana! Al Ahly na Mamelodi wanaweza kukalishwa tena vizuri tu! Tuwape hamasa wachezaji wetu lila kitu kinawezekana! Mamelodi na ubora wake lakini alitolewa kamasi na TP Mazembe!
 
Tunatiana moyo tu naiona yanga ikifanya mikimbio mikimbio tu uwanjani shughuli ni nzito mamelodi ni level nyingine.
 
Na wewejkwa fikra zako ukichambua kati ya young vs mamelod au simba vs al ahly unadhani nani watapewa nafasi kubwa ya ushindi..
Timu itakayojituma, kutumia nafasi na yenye bahati. Kumbuka kuwa ziko siku ambazo magori yanagonga mwamba na kutoka nje na ziko siku timu inacheza na wachezaji pungufu kwa bahati mbaya na ziko siku kipa na beki wanajichanganya wenyewe kwa bahati mbaya. Ndiyo maana uliona Simba ilitoka sare na Al-ahly.
 
Unafikiri ni kujituma na kujielewa tu ndio kunaipa mafanikio akina Man city au Real Madrid ? Kwamba fulham au westham hawjitumi na kujielewa kuliko liverpool ndio maana hawana mafanikio kama liverpool? Suala la kuwepo wachezaji wazuri kadhaa ndani ya timu ya kawaida hilo ni suala la kawaida lakini haiondoi ukweli kuwa timu zinazidiana ubora.
Unaongelea timu zenye wachezaji ambao wamezifikisha timu zao kwenye robo finali achana na Fulham na man city. Zungumzia Man City na PSG au Byern
 
Na wewejkwa fikra zako ukichambua kati ya young vs mamelod au simba vs al ahly unadhani nani watapewa nafasi kubwa ya ushindi..
Usiangalie historia ya timu, angalia current form (cross sectional study). Angalia Leo timu Iko na akina nani.
 
Hivi mkuu Tanzania tuna wachambuzi? Hawa hawa akina Kazumari? Hawa hawa akina Baba Levo, Mwalimu wa UPE Oscar Oscar? Akina Shaffi Dauda? We are not serious!
Tafuta clips zao Kabla ya mechi ya marudio ya Yanga vs CR Belouzdad ndio utajua hatuna wachambuzi.
 
Madereva wa malori makubwa akili zao wanazijua wenyewe
Wachambuzi wetu wanadhani dereva wa treni ana nguvu nyingi kuliko derva wa Bajaj, mara zote na siku zote madereva wa Bajaj lazima wabondwe na wale wa magari moshi. Nonsense¡!
 
ukisikiliza maswali wanayouliza kwenye mikutano ya pre-matches utajua tu tuna vihiyo wengi kwenye tasnia.
 
Wachambuzi wetu wameumbuka kwa mara nyingine kwa Yanga vs mamelodi. Warudi wakaangalie video clips zao Kabla ya mechi.
 
Tunatiana moyo tu naiona yanga ikifanya mikimbio mikimbio tu uwanjani shughuli ni nzito mamelodi ni level nyingine.
Umeona ulichoandika hakina uhalisia? Hujui mpira, unataka Simba
 
Back
Top Bottom