Wachezaji 10 wa kigeni uwanjani sio sawa

Unadhani watanzania wangapi watapata namba Nigeria, Ghana, Senegal, cameroon, Rwanda, Uganda, NK? Unachoongea hukijui. Rwanda imeruhusu wageni 3 Tu kwenye klabu
ndio wakaze sasa ili wawepo ktk hao watatu....sio kulia lia nyumbani wanaokaa majumbani ni wanawake na hta hao wanawake siku hizi ni nadra sana kukaa nyumbani .....wanaume kazikazi ukae nyumbani uolewe
 
mimi ningekuwa TFF ningeruhusu hata timu ikitaka kusajili timu nzima wa nje wasajili tu hakuna mambo ya kuleana leana hapa watu wanabebwa hawabebeki mtu unamkuta mchezaji mkubwa yupo mitaani kunywa konyagi na kuvuta mibange pamabv
 
kwani burnley,huddersfield,brighton,norwich wana uwezo sawa wa kusajili wachezaji na timu kama man u,arsenal,city,chelsea n.k au hiyo sheria ya kusajili wachezaji wengi wa kigeni iliwekwa kwa ajili ya timu za big 6 kule uingereza?au leicester city walivyochukua ubingwa walikuwa na kina ronaldo na messi?
'MPIRA WA MIGUU NI SAYANSI' in kashasha's voice

JIKUNE UNAPOWEZA ...PAMBANA NA HALI YAKO..........
 
huwezi kufananisha Morogoro na Dar es Salaam. Tanzania hakuna wachezaji bali kuna vijana wasiojulikana wanaopenda kucheza mpira. Haijulikani walianza vipi na lini kucheza mpira lakini tunataka watuletee mafanikio, hii haiwezekani na haitawezekana kama tutaendelea kuokoteza vijana mitaani. Hatutaweza kuwashindanisha vijana wetu na wachezaji wa nje ambao wamekuzwa kwenye vitaru vya kuchezea mpira tangu utotoni. TFF imechemsha hapo, badala ya kusimamia uanzishwaji wa vitalu vya kukuzia vipaji vya mpira wao wanataka ku import vipaji kutoka kwenye nchi zilizowekeza kwenye mpira. Huku ni sawa na kuzipatia ajira nchi ncho kwa vijana wao.

Tff inakwepa jukumu la kukuza mpira nchini
 
Akili yako ilivyo ndogo unadhani timu makini huko nje zitachukua mchezaji wetu tu hovyohovyo. Tff inachotakiwa hapa ni kuhamasisha uanzishwaji mkubwa wa vituo vya kulelea vipaji hapa nchini. Ikiwezekana kila timu iliyoko ligi kuu na wadau wengine wawe za vitalu hivyo badala ya kuwa na wachezaji wanaotumia ujanjaujanja, bangi katika mpira. Hapo ndio utaweza kupata vijana wengi wanaoweza kuuzika nchi za nje sio eti kwa kuleta wachezaji 10 wa kigeni kwenye timu. Bora hata yule anaesema tuwape uraia wa tanzania wachezaji wa kigeni wenye vipaji na hadhi ya kuchezea timu ya taifa kuliko utumbo wako unaoupigia debe kwa niaba ya Simba.
 
Hapa ume tumia akili ndogo sana ku reason. Argentina walikuwa na messi WC 2018 wametolewa mapema, URENO walikuwa na Ronaldo WC 2010 Russia. Wametolewa mapema. Sasa utasema hao wachezaji wasilipwe pesa nyingi kwa kigezo hicho? Kwa nini hampend kutumia akil? Manchester ilikuwa na wachezaj wa gharama sana but ubingwa kachukua Man United. Huwez sikia Manchester wanaponda

 
mbona povu jingi mkuu,hizo akili zako za matopeni na huo ubongo wa chura ......nani aliyeipigia simba debe hapa?unafikiri kwa kutumia nini bro?maana wanipa mashaka kidogo.....SAFI SANA TFF ONGEZENI HATA WAFIKIE 20 HAO WACHEZAJI WA KIGENI
 

unapoteza muda wako kujibizana na huyu mtu aisee .....ndio hawa wakiona madukani kuna vitu vya thamani wanalaani kwanini waweke vitu hivyo hahahah eti kisa yeye hana pesa hajui kuwa kuna watu `wanavihitaji na pesa za kununua wanazo....ndio yaleyaleeeeeee ya mkulu na madreamliner hahahahahaha watazipanda wengine na wewe utafaidika indirect
 
MO hangover! Ikiisha akili zitawaridia.
Maadam sisi hatuko vizuri sana kwenye kuandaa vipaji hatutakuwa na Wachezaji wanaoweza kushindanishwa na wachezaji wazuri kutoka nje. Unless tunaleta mitumba kama akina Okwi, Mavugo, Sserukuma...
 
mbona povu jingi mkuu,hizo akili zako za matopeni na huo ubongo wa chura ......nani aliyeipigia simba debe hapa?unafikiri kwa kutumia nini bro?maana wanipa mashaka kidogo.....SAFI SANA TFF ONGEZENI HATA WAFIKIE 20 HAO WACHEZAJI WA KIGENI
Hata Ulaya wanayo sheria ya kulinganisha uwiano wa gharama za kusagili kwa timu zilizoko kwenye ligi moja. hUWEZI KUWA NA TIMU 2 TU KATI YA 20 AMBAZO ZINASHIRIKI LIGI HUSIKA ZINAZOWEZA KUTUMIA KIWANGO FULANI CHA USAJILI WA WACHEZAJI KUZIDI TIMU NYINGINE KWENYE LIGI. kAMA IKO TIMU MOJA INAYOWEZA KUSAJILI WACHEZAJI 10 WA KIGENI KWA WAKATI MMOJA HAIWEZI KURUHUSIWA KUCHEZA LIGI MOJA NA TIMU AMBAZO HAZIWEZI KUSAJILI HATA MCHEZAJI MMOJA, aU TIMU MOJA TU INATUMIA SH. 2 BIL KUSAJILI HAIWEZI KUCHEZA LIGI MOJA NA TIMU ZINAZOTUMIA SH. 500,000 TU KWENYE LIGI
 
walipandaje ligi kuu?kinachoangaliwa ni uwezo na sio aina au thamani ya wachezaji usitudanganye ndugu yangu,hivi unataka kuniambia thamani ya kikosi cha MAN CITY ina uwiano au inalingana na thamani ya kikosi cha HUDDERSFIELD au WOLVES? hivi thamani ya kikosi cha BARCELONA au R.MADRID inalingana na HELAS PALMA au GIJON?

HEBU TUONDOLEE HUO UZWAZWA WAKO .........

SAFI SANA TFF KWA HILI
 
Wewe huna unachofahamu kwenye mpira bora ukae kimya ujifunze kwa wengine. Kwani PSG walipotaka kumsajili Neymar waliambiwa wafanye nini kwanza kabla ya kuruhusiwa kumsajili?
 
Naona wachezaji 10 wa kigeni itakuwa safii, maana italeta upinzani wa kugombea namba kwa wazawa ili wasibweteke.
 
Klabu zipi Kwa majina zilipendekeza Wachezaji 10?
 
England timu zao zimejaa wazawa lakini ni waingereza wangapi wanacheza nje ya England, timu Yao ya taifa ina ubora gani duniani?
Wewe hujui kuwa ENGLAND tayari ni nje?
 
Wewe hujui kuwa ENGLAND tayari ni nje?
Ukisikiliza hoja za Karia za kutetea wachezaji wa 10 wa kigeni unaisikia harufu ya mdhani wa Simba tu basi. Kweli kila mtu ana price tag yake!!! Hiyo pesa ya kulipa wachezi 10 x 20 = 200 wa kigeni kwanini isitumike kuendeleza soka la watoto na vijana?. Hata huko Senegal, Ghana, Nigeria, Cameroon, Misri, Algeria, Mali, nk ambako mpira unachezwa hawajafikia 'upuuzi' huu wa kwetu tunaoupendekeza.
 
Wewe huna unachofahamu kwenye mpira bora ukae kimya ujifunze kwa wengine. Kwani PSG walipotaka kumsajili Neymar waliambiwa wafanye nini kwanza kabla ya kuruhusiwa kumsajili?
wewe kweli zwazwa sasa hapo umeandika nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…