Wachezaji kama Makame wa Fountain Gate wanapaswa kujitambua

Kweli wewe mbumbumbu
Kwaiyo unakataa kwamba Bakhresa haimiliki Azam media, Azam fc- na Azam beverages
Suala la kumuimba GSM mashabiki wa Yanga haihisiani kuwa anamiliki Yanga

GSM ni mfanyabiashara yupo Yanga kunufaika na Yanga inufaike

Kudhamini Yanga sio kifungo kwamba asijitangaze kwenye timu zingine

Matangazo ya GSM yapo kwenye magazeti, redio, Tv na mabango sio kwenye timu, yeye anatangaza biashara zake

Na nyie Simba kama mpo tayari kaongee nae awadhamini, msibaki mnalia tu
 
GSM ana ushawishi mkubwa katika timu ndiyo maana hadi mfanyakazi wake ndiyo anasimamia kila kitu pale Yanga.

Hayo makaratasi ya katiba ni makaratasi tu ndiyo maana timu inajivalia tu majezi kinyume cha matakwa ya hiyo hiyo katiba. Na ndiyo maana anaimbwa yeye na siyo SportPesa ambaye kwenye vitabu ndiyo anatoa pesa nyingi mara dufu ya anayotoa GSM.

Na ni kwa sababu ya ushawishi huo ndiyo maana watu wana wasiwasi kuwa atatumia ushawishi huo alionao ndani ya Yanga kuhakikisha kuwa udhamini wake ndani ya timu zingine unainufaisha Yanga. Uzuri alijisnichi mwenyewe kwa kauli zake za "Yanga Bingwa".

Ungekuwa na uelewa hata kidogo wa mambo ya sheria usingekaza kaubongo kako hako ka jongoo.
 
Ila huu ni mtindo umezoeleka wa Yanga kurubuni mchezaji kwa kumuahidi watamsajili kwa nia alegeze katika mechi dhidi ya timu yake ila baada ya mechi wanamtosa. Walifanya hivyo sana tu katika kombe la shirikisho. Walimfanyia pia yule mshambuliaji wa Medeama mwenye rasta. Ni timu ya janja janja.
 
Ni sahihi kabisa, haikuishia kwa Medeama tu bali Yanga ilienda mbali sana kwa kuwarubuni wachezaji wa TP Mazembe, USMA, Belouizdad walegeze ili Yanga ishinde. Na ikawafuata wachezaji wa Al Ahly wacheze chini ya kiwango ili Yanga isifungwe uwanja wa Mkapa na kule Misri wafungwe magoli machache. Yanga hii ina pesa sio mchezo ina uwezo wa kuhonga mchezaji yeyote yule hata kutoka kwenye vilabu vikubwa Africa.
 
Hersi alitoka jukwaani akaenda kuongea na mchezaji wa Mazembe wakati timu zinatakiwa kurudiana baada ya wiki moja.

Msimu uliopita katika mechi 8 kuanzia makundi hadi robo fainali, Yanga ilishinda mechi 2 tu.

Na hapa hatuongelei hongo ya pesa. Naongelea hongo ya ahadi na kumrubuni mchezaji kwa kumuhadaa. Utamuhadaa mchezaji wa Al Ahly au USMA wakati unanuka jasho zaidi yake aliyetoka kucheza mechi?
 
Hersi alitoka jukwaani akaenda kuongea na mchezaji wa Mazembe wakati timu zinatakiwa kurudiana baada ya wiki moja.

Msimu uliopita katika mechi 8 kuanzia makundi hadi robo fainali, Yanga ilishinda mechi 2 tu.
Ni kweli kabisa mkuu, katika maongezi yake akamwambia kuwa awaambie wachezaji wenzie kuwa wacheze chini ya kiwango maana akicheza yeye peke yake chini ya kiwango haitosaidia Yanga kushinda kwasababu watabaki wachezaji 10 ambao wanaweza kusahihisha makosa ya mtu mmoja.

Enhe mkuu endelea kutupa za ndani kabisa kuhusu ushindi wa Yanga kule Algeria dhidi ya USMA, Hersi alienda kuongea na nani? Na kile kipigo cha Belouizdad cha goli 4 ni nani aliyefatwa na Hersi.
 
Kama haujui wachezaji wanavyohongwa muulize Hersi atakuhadithia. Unaongea kama uko Busokelo ndani ndani hauna clue ya kinachoendelea katika dunia ya mpira.
 
Kama haujui wachezaji wanavyohongwa muulize Hersi atakuhadithia. Unaongea kama uko Busokelo ndani ndani hauna clue ya kinachoendelea katika dunia ya mpira.
Kwani hapa ana hadithia Hersi au wewe? Wewe unayejifanya unajua ndio utuambie Belouizdad na USMA walivyoongwa
 
Kwani hapa ana hadithia Hersi au wewe? Wewe unayejifanya unajua ndio utuambie Belouizdad na USMA walivyoongwa
Kwa jinsi unavyoongea inabidi kwanza nikufundishe jinsi ya kuvuka barabara. Nikianza na hayo mengine nitakuwa nakutesa tu mwaya.
 
Kwa jinsi unavyoongea inabidi kwanza nikufundishe jinsi ya kuvuka barabara. Nikianza na hayo mengine nitakuwa nakutesa tu mwaya.
Kesho urudi kijiweni kwenu ukawaombe wakulishe tango pori la namna Belouizdad na USMA walivyofungwa kwa kuhongwa.
 
Mmeona GSM hatoshi mnaanza kuhamia kwa wachezaji hapo bado mtani sijui ndo kupenda simba na Yanga kuliko mpira hata sielewi mie😂😂😂.

Nb: Hasajiliwi Yanga anabaki huko huko aliko
 
Bado hamjasema .... Tukifungwa ni sawa ..tukishinda tunanunua mechi watu wa hovyo kabisa nyie ... Mlipoanza kishindashinda kimipango mkasahau timu lenu bovu Yanga gari imewaka Tena mnaanza kelele kama mbwa wa sokoni...badooo ..... Milembe waongeze tu hospital ya Kanda ya kila Kanda maana mtachanganyikiwa sanaaaa. ....
 
Huyu naye katokea wapi?

Yaani achanganyikiwe mtu anayeongoza ligi na katika mechi 3 za CAFCC anahitaji ushindi mmoja na sare moja tu aende robo fainali?

Kama huyo anachanganyikiwa inakuwaje yule ambaye mwanzoni mwa msimu alikuwa anaimba anafungwaje halafu ghafla akaanza kukimbilia nyumba za ibada kuombea washambuliaji wake? Ghafla wapemba wakamlambisha koni, wanyamwezi wakamlambisha asali, baada ya kuzoea hiyo tabia akapakwa mafuta na waarabu. Hapohapo anahitaji kushinda mechi zake zote zilizobaki za CAFCL ili kwenda robo fainali?

Kichaa anadhani wengine wote ni vichaa yeye pekee ndiyo mzima.
 
Si walikataa wenyewe kile kipindi cha CEO Barbra. Halafu leo wanalalamika.
Makolo ni JOKA la mdimu, linalozuia watu wasiende kuchuma ndimu wakati lenyewe wala halina shida nazo.
 
Wauluze akina chama na baleke

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Unaongea na watu wenye akili ndogo sana hiyo hoja yako wala hawaielewi

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Kwa hiyo unataka walegeze kwa simba pia. Rage ajengewe mara maana viongozi wenu wanawaona mipang'ang'a
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…