Wachezaji wa Simba SC leo mkitoka sare au mkifungwa na Namungo FC kwa Mkapa tafuteni vichochoro vya kukimbilia tumeshachoka kuwavumilia

Wachezaji wa Simba SC leo mkitoka sare au mkifungwa na Namungo FC kwa Mkapa tafuteni vichochoro vya kukimbilia tumeshachoka kuwavumilia

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Wengine kwa Mpira wenu Mbovu na Matokeo mabaya sasa tumeshakonda na tukiona Soka zuri, la Kitabuni, linalovutia la Yanga SC na Ushindi wao mfululizo ndiyo Hasira zinatupanda na Machungu kutuzidia Mioyoni na Rohoni.

Wachezaji wa Simba SC ukomo Wetu wa Kuwavumilia umeshafika Kikomo na leo Ole wenu mtoke Sare au mfungwe na Namungo FC Uwanja wa Mkapa ndiyo mtatujua Mashabiki wa Simba SC tukichoka na Upuuzi huwa tunakuwaje na mtajua kwanini Wimbo wa Taifa hauna Kolabo au kwanini Nyoka hana Ugoko.

Tayari nimeshaagiza TOYO tatu kutoka Mkuranga na Kibiti zinakuja na Lundo la Bakora / Fimbo zilizotengenezwa Kiustadi ili Kumuingia Mtu vizuri Mwilini aweze Kushika Adabu na Kumkumbusha juu ya Wajibu wake kwa Majukumu ambayo yanamfanya alipwe Mamilioni ya Pesa kama Mshahara wake kwa Mwezi.

Najua Mshauri wa Simba SC Crescentius Magori huwa upo sana hapa Jamiiforums na unapenda mno Kusoma Mada zetu Wadau wa Simba SC na najua hata Uzi huu utausoma hivyo ukishausoma tafadhali wafikishie Wachezaji hii Taarifa na hizi Bakora hazitoishia tu Kwao leo bali zitahamia pia Kwenu Viongozi na hasa hasa Mwenyekiti Mangungu, CEO Barbara na Mwenyekiti wa Bodi Salim Abdallah na Bakora zitakazobakia zitamalizika katika hicho Kitambi chako Kikubwa Magori.

Tena huyu Mangungu anatukera sana!
 
Mi SAA hizi sitaki tena kuangalia mpira wwte ule wa NBC premier League, unaorushwa wala kipindi chochote cha michezo iwe ni kwenye redio, tv au iwe ni uchambuzi wa magazeti ya michezo, sina moyo wa kusikiliza au kuangalia hivyo vitu tena, Kwa sasa Niko likizo kwenye Mambo ya michezo, ntakuwa napita hu huku kuangalia umbea tu wa hapa na pale.
 
Mi SAA hizi sitaki tena kuangalia mpira wwte ule unaorushwa wa NBC premier League, wala kipindi chochote cha michezo iwe ni kwenye redio, tv au iwe mi uchambuzi wa magazeti ya michezo, sina moyo wa kusikiliza au kuangalia hivyo vitu tena, Kwa sasa Niko likizo kwenye Mambo ya michezo, ntakuwa napita hu huku kuangalia umbea tu wa hapa na pale.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Babra mwenyewe siku izi kaingia mitini kama vile amesusa amewaachia timu kina magori nafikiri na yeye yuko mbioni kubadilishia gia angani Kama bosi wenu alivyofanya maana sio kwa ukimya huu na kanavyopendaga kuonekana kwenye camera kila tukio, sio bure katakuwa kanatafuta namna ya kuchomoka maji yamezidi unga hali ya hewa imekuwa nzito kwake.
 
Mi SAA hizi sitaki tena kuangalia mpira wwte ule unaorushwa wa NBC premier League, wala kipindi chochote cha michezo iwe ni kwenye redio, tv au iwe mi uchambuzi wa magazeti ya michezo, sina moyo wa kusikiliza au kuangalia hivyo vitu tena, Kwa sasa Niko likizo kwenye Mambo ya michezo, ntakuwa napita hu huku kuangalia umbea tu wa hapa na pale.
Nina hasira sana tu na huyu Mangungu.
 
Babra mwenyewe siku izi kaingia mitini Kama vile amesusa amewaachia timu kina magori nafikiri na yeye yuko mbioni kubadilishia gia angani Kama bosi wenu alivyofanya maana sio kwa ukimya huu na kanavyopendaga kuonekana kwenye camera kila tukio, sio bure katakuwa kanatafuta namna ya kuchomoka maji yamezidi unga hali ya hewa imekuwa nzito kwake
Hauko mbali na Ukweli Ndugu kwani huyu CEO Barbara na Mwenyekiti Mangungu wanawadharau mno Wazee wa Simba SC hasa kwa Maelekezo ya Kiutamaduni ambayo huwa wanawapa na Wao sasa wameamua Kunyamaza na Jahazi likianza Kuzama Nungwi taratibu tu.
 
Mkuu shabiki wa michezo anayejitambua hawezi kupiga wala kutukana timu au wachezaji hata siku moja!

Kwanza tunapaswa kujua kuwa huu mpira wa bongo unachezwa ndani na nje ya uwanja! Hii ndio sababu GSM waliwahi kusema Yanga wasipochukua ubingwa wasilaumiwe wachezaji!

Hivyo tunapaswa kujua ni wapi club inakwama au kukwamishwa, ndipo na sisi tukamatie hapo! Tujikaguwe kama kweli club ipo mazingira masalama? Lazima pia tukumbuke kwamba kuna baadhi ya watu waliokuwa kwenye front line ya mikakati na siri zote za ushindi wa timu katika misimu iliyopita kama Haji Manara ambao sasa hivi wako kwa mahasimu wetu, hawa wanaweza kuhusika kutoa siri za mikakati ya ushindi wa club, Hivyo kuna haja ya kubuni na kubadili mbinu tulizozowea kuzitumia.

niwasihi wanasimba wenzangu tuwe watulivu, bado ni mapema kuanza kuchachamaa, vinginevyo tutajitoa mchezoni na kuwapa faida wapinzani wetu!
 
Wacheni kulalamika angalia wapi mnakosea, mnao wachezaji wa kutosha na wa kuweza kubadili upepo mambo kupiga watu wazima bakora hayawezi badilisha upepo huu Bali mtazidi kupoteana.

Hebu mjifunze ustaarabu na ustahimilivu kwetu sisi Wapenzi na mafans wa Young African, waga hatubabaiki na mambo hayo maana tunaupenda mchezo wenyewe ambao tulianza kuupenda kabla ya kupenda timu yetu pendwa.

Na kwa mambo haya ya fimbo Leo namungo anawaoa mtihani mwingine mugumu, maana kwake mechi ya Leo Ni muhimu ukizingatia mechi ijayo atakuwa na mtihani mugumu kutoka kwa wananchi, hivyo Leo hawezi kujulegezea. Go go go Chirwa, Kikoti, Blaize, Moringa, Kichuya etc, piga hao Makolo wachapeni bakora vizuri.
 
Mashabiki wa simba acheni kuwapandisha Presha wachezaji wenu, viongozi wenu na benchi zima la ufundi. Tambueni mpira ni dk 90, unadunda na pia una matokeo matatu!

Hivyo kuweni wavumilivu na pia muwe wepesi wa kukubali matokeo. Hakuna timu isiyo penda kushinda mechi zake. Hivyo timu inayocheza vizuri, basi istahili kishinda. Na ile inayo ruka ruka tu uwanjani, basi na iadhibiwe.
 
Ga
Wengine kwa Mpira wenu Mbovu na Matokeo mabaya sasa tumeshakonda na tukiona Soka zuri, la Kitabuni, linalovutia la Yanga SC na Ushindi wao mfululizo ndiyo Hasira zinatupanda na Machungu kutuzidia Mioyoni na Rohoni.

Wachezaji wa Simba SC ukomo Wetu wa Kuwavumilia umeshafika Kikomo na leo Ole wenu mtoke Sare au mfungwe na Namungo FC Uwanja wa Mkapa ndiyo mtatujua Mashabiki wa Simba SC tukichoka na Upuuzi huwa tunakuwaje na mtajua kwanini Wimbo wa Taifa hauna Kolabo au kwanini Nyoka hana Ugoko.

Tayari nimeshaagiza TOYO tatu kutoka Mkuranga na Kibiti zinakuja na Lundo la Bakora / Fimbo zilizotengenezwa Kiustadi ili Kumuingia Mtu vizuri Mwilini aweze Kushika Adabu na Kumkumbusha juu ya Wajibu wake kwa Majukumu ambayo yanamfanya alipwe Mamilioni ya Pesa kama Mshahara wake kwa Mwezi.

Najua Mshauri wa Simba SC Crescentius Magori huwa upo sana hapa Jamiiforums na unapenda mno Kusoma Mada zetu Wadau wa Simba SC na najua hata Uzi huu utausoma hivyo ukishausoma tafadhali wafikishie Wachezaji hii Taarifa na hizi Bakora hazitoishia tu Kwao leo bali zitahamia pia Kwenu Viongozi na hasa hasa Mwenyekiti Mangungu, CEO Barbara na Mwenyekiti wa Bodi Salim Abdallah na Bakora zitakazobakia zitamalizika katika hicho Kitambi chako Kikubwa Magori.

Tena huyu Mangungu anatukera sana!
Game linaanza saa ngap mkuu ???
 
Mkuu shabiki wa michezo anayejitambua hawezi kupiga wala kutukana timu au wachezaji hata siku moja!
Kwanza tunapaswa kujua kuwa huu mpira wa bongo unachezwa ndani na nje ya uwanja! Hii ndio sababu GSM waliwahi kusema Yanga wasipochukua ubingwa wasilaumiwe wachezaji!
Hivyo tunapaswa kujua ni wapi club inakwama au kukwamishwa, ndipo na sisi tukamatie hapo! Tujikaguwe kama kweli club ipo mazingira masalama? Lazima pia tukumbuke kwamba kuna baadhi ya watu waliokuwa kwenye front line ya mikakati na siri zote za ushindi wa timu katika misimu iliyopita kama Haji Manara ambao sasa hivi wako kwa mahasimu wetu, hawa wanaweza kuhusika kutoa siri za mikakati ya ushindi wa club, Hivyo kuna haja ya kubuni na kubadili mbinu tulizozowea kuzitumia.
niwasihi wanasimba wenzangu tuwe watulivu, bado ni mapema kuanza kuchachamaa, vinginevyo tutajitoa mchezoni na kuwapa faida wapinzani wetu!
Ulipoharibu nikumtaja huyo Haji Manara!!
 
Back
Top Bottom