Wachezaji wa Tanzania wajenge utamaduni wa kustaafu kwa hiari kuchezea Timu ya Taifa

Wachezaji wa Tanzania wajenge utamaduni wa kustaafu kwa hiari kuchezea Timu ya Taifa

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Kuna utamaduni wenzetu wanao, mchezaji akifikisha umri au stage fulani anatangaza mwenyewe kwamba mwaka huu ni mwaka wangu wa mwisho kutumikia timu ya taifa.

Hii ina faida kubwa sana kwa mchezaji. Kama umecheza kwa muda mrefu, watu watataka waweke kumbukumbu zako za mwisho ukichezea timu ya taifa. Waliokuwa wanakukubali watakuja viwanjani kukupongeza katika kila mechi zako za mwisho, watanunua jezi zako na kuomba uzisaini, watapiga picha na wewe, nk. Unaweza kuingia mkataba na kampuni fulani wakakutengenezea bidhaa kama t-shirts utakazozisaini na kuziuza. Ni kumbukumbu nzuri kwa mchezaji na wale waliokuwa wanakusapoti.

Ukiwasiliana na mamlaka za soka, wanaweza hata kukuandalia mechi rasmi ya kirafiki au kuchagua mechi iliyo katika ratiba ambayo inakuwa ndiyo ya mwisho kwako ya kukuaga rasmi. Mapato ya mechi hiyo kama ni ya kirafiki unaweza kupewa wewe kama zawadi na unaweza kutoa asilimia fulani kwa ajili ya jamii yenye uhitaji. Familia yako inaweza kuwepo pale, unaweza kucheza kwa dakika fulani tu na ukiingia au ukiwa unatoka watu wanasimama kukupigia makofi. Ni kumbukumbu unayoweza kuiweka kwa ajili ya familia yako kwa muda mrefu sana.

Sasa wachezaji wetu, sijui ni tamaa au labda kivuli cha kucheza timu ya taifa kinawabeba huko wanakocheza wanapata fursa au heshima fulani kwa hiyo wanaogopa kuipoteza. Wanang'ang'ana weee mwisho wa siku wanaachwa kiholela tu.
 
Kuna utamaduni wenzetu wanao, mchezaji akifikisha umri au stage fulani anatangaza mwenyewe kwamba mwaka huu ni mwaka wangu wa mwisho kutumikia timu ya taifa.

Hii ina faida kubwa sana kwa mchezaji. Kama umecheza kwa muda mrefu, watu watataka waweke kumbukumbu zako za mwisho ukichezea timu ya taifa. Watakuja viwanjani kukupongeza katika kila mechi zako za mwisho, watanunua jezi zako na kuomba uzisaini, watapiga picha na wewe, nk. Ni kumbukumbu nzuri kwa mchezaji na wale waliokuwa wanakusapoti.

Ukiwasiliana na mamlaka za soka, wanaweza hata kukuandalia mechi rasmi ya kirafiki au kuchagua mechi iliyo katika ratiba ambayo inakuwa ndiyo ya mwisho kwako ya kukuaga rasmi. Familia yako inaweza kuwepo pale, unaweza kucheza kwa dakika fulani tu na ukiingia au ukiwa unatoka watu wanasimama kukupigia makofi. Ni kumbukumbu unayoweza kuiweka kwa ajili ya familia yako kwa muda mrefu sana.

Sasa wachezaji wetu, sijui ni tamaa au labda kivuli cha kucheza timu ya taifa kinawabeba huko wanakocheza wanapata fursa au heshima fulani kwa hiyo wanaogopa kuipoteza. Wanang'ang'ana weee mwisho wa siku wanaachwa kiholela tu.
Africa we are the same ata wewe ukipata pa kupata ni hadi ufe ndio unaridhika..
 
Africa we are the same ata wewe ukipata pa kupata ni hadi ufe ndio unaridhika..
Hapana. Mimi nikikaa sehemu moja au nikifanya kitu kile kile muda mrefu naboreka. Napenda na siogopi kujipa changamoto.
 
Maana ya kustaafu timu ya Taifa ni kuaga kutotumikia timu ya Taifa wakati bado mchezaji ana uwezo wa kuendelea timu ya Taifa.

Kwani wale malegendari kama Lunyamila, kizota au Mwameja waliwahi rasmi kumtangazia nani, wapi na lini wamestaafu Taifa stars.

Kuustaafu timu ya Taifa ni culture ngeni kwny nchii.
Kwetu kustaafu ni kuachana na soka mazima..

Hata hiyo DRC ina mazee, akina Cedric Bakambu, Gael Kakuta, Britt Ambassongla, Yannick Bolasie hawajastaafu..
Hawa wanamzidi samatta umri na profile..

Unastaafuje fursa wewe.

Unaweza kuamini Lucas Podorsk yule mjerumani bado anacheza soka hadi Leo akiwa na 41...yupo Poland.. anachezea Gornik Zabre.
 
Maana ya kustaafu timu ya Taifa ni kuaga kutotumikia timu ya Taifa wakati bado mchezaji ana uwezo wa kuendelea timu ya Taifa.
Point yangu ilikuwa hiyo. Ungeishia hapo ningekuona muelewe, mwisho wa siku umekwenda kingine kabisa.

Kwani wale malegendari kama Lunyamila, kizota au Mwameja waliwahi rasmi kumtangazia nani, wapi na lini wamestaafu Taifa stars.

Kuustaafu timu ya Taifa ni culture ngeni kwny nchii.
Kwetu kustaafu ni kuachana na soka mazima..
Ndiyo maana hata kichwa tu cha habari kinasema "Wachezaji wa Tanzania wajenge utamaduni wa kustaafu kwa hiari kuchezea Timu ya Taifa". Kwa maana hiyo natambua kuwa ni utamaduni mgeni ila wenye manufaa kwa mchezaji kama nilivyoelezea.

Using'anga'nie sehemu hadi siku unapoondolewa unaona umevunjiwa heshima. Wengi wanakuja kugundua hilo wakina wameshachelewa.
 
Si useme tu umemlenga Samatta

Captain wa maisha🤣🤣
Tusitajane majina. Ukweli ni kuwa hili limekuwa linawasumbua wachezaji wengi sana kwa muda mrefu. Majuto ni mjukuu, watu hawajui ni wakati gani wa kuondoka, ukichelewa kidogo tu inakula kwako. Nyerere alilijua hilo.

Mchezaji inafika wakati anaanza kujiuliza:
"Daah, mbona siitwi tena?"
"Daah, mbona bado nina uwezo?"
"Daah, ningejua ningejitangazia zangu kuwa nastaafu kuliko kuachwa hivi!"
 
Tusitajane majina. Ukweli ni kuwa hili limekuwa linawasumbua wachezaji wengi sana kwa muda mrefu. Majuto ni mjukuu, watu hawajui ni wakati gani wa kuondoka, ukichelewa kidogo tu inakula kwako. Nyerere alilijua hilo.

Mchezaji inafika wakati anaanza kujiuliza:
"Daah, mbona siitwi tena?"
"Daah, mbona bado nina uwezo?"
"Daah, ningejua ningejitangazia zangu kuwa nastaafu kuliko kuachwa hivi!"
WAtajwe tu mficga ugonjwa kifo humuumbua
 
Mnataka hao wachezaji wastaafu na wakati huo huo kama Shirikisho la mpira wa miguu mkiw hamna mkakati wowote ule wa kuingiza wachezaji wengine wapya na wenye uwezo maradufu kwenye hiyo timu ya Taifa!!

Jifunzeni kwanza kwa wenzenu waliofanikiwa kwenye hiki kipengele nilichokitaja hapa. Kinyume na hapo mtaendelea tu kutafuta wachawi, kumbe nyinyi wenyewe ndiyo wachawi.
 
Back
Top Bottom