Kwangu mimi Molinga ni bonge la strika ila tu kuna kipindi alikosa "match fitness". Na makocha wa Yanga wameshindwa kabisa kumtengenezea pacha wake. Ana nguvu, ana uwezo wa kuficha mpira hata akiwa amezungukwa na mabeki wawili na ana uwezo mzuri sana wa kutoa pasi za mwisho. Kiufundi Molinga anatakiwa acheze pamoja na straika mwenzake mwenye jicho kali la goli. Kazi ya Molinga iwe tu kumtengenezea mwenzake afunge kwa sababu yeye Molinga sio "finisher" mzuri sana japo mara moja moja huwa anafunga. Lakini iwapo Yanga wameshindwa kumtumia kwa kumtengenezea pacha wake uwanjani basi ni vizuri wamuache akatafute maisha sehemu nyingine.