Wachina washikwa wakiiba mchanga wa dhahabu wakiupeleka mbele

Wachina washikwa wakiiba mchanga wa dhahabu wakiupeleka mbele

[MENTION][JFMP3][/JFMP3][/MENTION]
wapo wamesogezwa Saza mwana wa mfalme ndio mmliki mwangalizi wake ni mulugo naibu waziri elimu

Aisee hapa bongo kazi ipo, ndio maana amepewa kazi ya kusimamia elimu ya watoto wetu yani tutaendelea kupiga factor matokeo mpaka siku ya mwisho wa dunia.
 
ktk vyombo vya hbr leo,yamekamatwa malor saba ya wachina yakisafirisha mchanga wenye madini bila kibali.swali la kujiuliza ni kwamba kama hawa watu ndo tumewapa karibu migodi yote,je wameshaiba kiasi gani sasa,kwa serkali makini huo wiz ungekuwa ndio kipimo sasa wa kuwa na mashaka juu ya uwepo nchini na kuwa na mashaka juu ya mikataba yao,kwa masikitiko hakuna kesi yeyote hapo,nawasilisha.
 
ktk vyombo vya hbr leo,yamekamatwa malor saba ya wachina yakisafirisha mchanga wenye madini bila kibali.swali la kujiuliza ni kwamba kama hawa watu ndo tumewapa karibu migodi yote,je wameshaiba kiasi gani sasa,kwa serkali makini huo wiz ungekuwa ndio kipimo sasa wa kuwa na mashaka juu ya uwepo nchini na kuwa na mashaka juu ya mikataba yao,kwa masikitiko hakuna kesi yeyote hapo,nawasilisha.

sio bure mikataba hyo ,kuna wanaonufaika na hilo,
 
Najaribu kujiuliza iv kule kwao mtanzania anaweza fanya ivyo?
 
Shhhhhhhhhhhhhhh!!! Waskuskie kina philip marmo,utaokotewa porini wewe!alisema wachina ni watu muhimu kabisa kwetu.

kama ni muhmu ndo watuibie?watz tuwe makini na ulinzi wa mali zetu,itafika sasa tulianzishe kama ya mtwara,
 
Walimsamehe mwana mfalme wetu kunyongwa acha wajilipie fadhila
 
Mwanga nilioupata tokana na tukio hili ni kuwa kumbe kuna fursa ya makampuni ya madini kuuza mabaki ya mchanga kwa vibali, kwa wadau wengine za wa utafuta madini.

Na naamini vibali hivi lazima vinatoka na kuratibiwa na ofisi/idara za madini.

Kama hivi ndivyo, kwa nini vibali hivi visingekuwa vinatolewa kwa wachimbaji wadogo wa maeneo husika ili kupunguza migogoro ya wawekezaji na wachimbaji hao?

Kufanya biashara ya kuuziana mabaki ya mchanga na makampuni makubwa ambayo yameingia kwa mlango wa uwekezaji ni sawa na watu hawa sasa kugeuka kufanya biashara ya umachinga huo ni ubabaishaji!!!!
 
Kama mlisikiliza vizuri taarifa ya habari haojamaa kitu kilicho watia hatiani ni kibari cha kusafirishia na si kingine huo mchanga kwa jina la wachimba madini unaitwa marudio hatawewe kama unapesazako unanunua na unapeleka utakako
 
kama ni muhmu ndo watuibie?watz tuwe makini na ulinzi wa mali zetu,itafika sasa tulianzishe kama ya mtwara,



Intelijesia yetu inafanya kazi kwenye mikutano ya Chadema tu. Lakini kwenye uwizi wa rasilimali zetu bado hatuna Intelijesia ndio tumetuma wataalam kwenda kusoma.
 
Kiukweli wachina ni janga lingine kwa africa
.jaribu kucheki vipindi vya africa investigate vya aljazeera utaona walivyo na fujo.
 
Mwanga nilioupata tokana na tukio hili ni kuwa kumbe kuna fursa ya makampuni ya madini kuuza mabaki ya mchanga kwa vibali, kwa wadau wengine za wa utafuta madini.

Na naamini vibali hivi lazima vinatoka na kuratibiwa na ofisi/idara za madini.

Kama hivi ndivyo, kwa nini vibali hivi visingekuwa vinatolewa kwa wachimbaji wadogo wa maeneo husika ili kupunguza migogoro ya wawekezaji na wachimbaji hao?

Kufanya biashara ya kuuziana mabaki ya mchanga na makampuni makubwa ambayo yameingia kwa mlango wa uwekezaji ni sawa na watu hawa sasa kugeuka kufanya biashara ya umachinga huo ni ubabaishaji!!!!
 
yani hii nchi ni ya ajabu sana hv wachina wanachukua mchanga wa dhahabu sasa wanapeleka wapi? Kwani mbeya wana mitambo? Na kama hyo mitambo ipo ni ya nani? Na kama wataisafisha hiyo michanga na dhahabu hyo ikipatikana itakuwa ya nani? Au ni mitambo ya kinana na riz? Jamani hii serikali aiogopwi na hata wageni


usishangae hao wachina kuwa na mitambo ya kuchenjulia dhahabu maana Dar tu wana mitambo mingi ya kusindika maji tena kwa kutumia brand za makampuni mengine kama Uhai, Kilimanjaro, nk. Wana magereji bubu na mengine chini ya ardhi!!!!
 
Naomba nifafanue kwa hao wachina na biashara zao.

Wiki hii nimerejea toka Chunya, eneo la Makongolosi, Mwaoga, Pantamela, Saza na Mkwajuni.
Maeneo hayo ni maarufu kwa uchimbaji mdogomdogo wa dhahabu ambapo wananchi huchimba na kisha kujipatia mawe, mawe ambayo huyapeleka kwenye crusher na kusagwa kuupata unga wa dhahabu ambao huchujwa kwa teknolojia ya kienyeji na kuambulia ama Points au hata Grams kadhaa za dhahabu.
Katika process zao za kuuosha huo mchanga na kuambulia dhahabu, huwa kuna udongo ambao hubakia. Udongo huo hujazana na kufikia mafurushi makubwa ambayo kwa wajasiriamali huyapima na kubaini ni asilimia ngapi ya dhahabu imesalia katika hayo 'marudio' na kisha huyafanyia uzalishaji mpya wa teknolojia ya kisasa kunasa dhahabu ikiwemo kwa kutumia 'cyanide processing'. Uzalishaji huo ambao ni RAHISI sana, hupelekea wajasiriamali hao kujipatia dhahabu kuanzia kilo moja mpaka kilo 5 kutegemea na aina ya tanks ulizojenga.

Aina hizo za uzalishaji wa dhahabu (sio uchimbaji), ni wa kienyeji na unaopaswa kufanywa na wazawa kwani hauhitaji mtaji mkubwa sana na uzoefu wangu si zaidi ya mil 400 unaweza kufungua na kuanza kuzalisha walau hata kilo 2 za dhahabu. Uzoefu huo ninao na nimeshuhudia.

Furushi moja la marudio ya udongo wa dhahabu huuzwa kati ya mil 10-60 kwa furushi, ambapo hawa wawekezaji wa nje ndio wameipandisha bei ya marudio na kuwafanya wazawa kushindwa kumudu ushindani kulingana na mitaji yao.

Pale wilaya ya Chunya pekee yapo makampuni zaidi ya 6 yakifanya shughuli hizo kienyeji. Wapo KASCO amewekeza bil 4 katika biashara hiyo, wapo Caspian eneo la kijiji cha Mwaoga, wapo hao wachina ambao wamekamatwa, wapo wahindi, wapo wazungu, wapo waarabu katika kijiji cha Pantamela.

Wapo wazawa kama vile Nyamaswa, wapo KICOL ambao wapo Mwaoga.

Biashara hiyo ilianzia eneo la Geita, Nyarugusu, Ishokera na kutawanyika maeneo mengine. Teknolojia hiyo ya uzalishaji dhahabu kienyeji imetokea Zimbabwe.

Ukifika Chunya utakutana na Wazimbabwe, Zambians na raia wa mataifa mengineyo wakijichumia dhahabu huku tumelala.

Kwa nini wachina wamekamatwa kirahisi?
Pale wilaya nzima ya Chunya kumeingia ushindani mkubwa wa kupata udongo wa marudio ya dhahabu, tena gharama zake zimekuwa ni kubwa sana. Kutokana na hilo basi, imepelekea Wachina kufata na kununua marudio Nzega na kuyasafirisha kwa malori hadi Makongolosi na kuweka hifadhi ya kutosha kuendesha uzalishaji huo. Serikali pale Chunya yajua fika kabisa.

Kwa sasa, udongo huo unagombaniwa sana katika kijiji cha Kitunda wilayani Sikonge mkoani Tabora, vikumbo vimeshamiri sana pale.

Mimi ni shuhuda wa yote yanayoendelea pale Chunya, wachina wamechomewa pia na wafanyakazi wao kwa kuwalipa malipo duni sana.

Chanzo: Mimi mwenyewe!
 
Nawashauri wadau, tembeleeni remote areas mtajionea fursa lukuki za ukwasi. Yapo mengi sana yakiendelea, nimepata kushuhudia sumu ya kusafishia dhahabu iitwayo 'Cyanide' na 'Carbon' zikisafirishwa kienyeji mno na hata watumiayo hawana tahadhari zozote zikitumiwa.

Nchi hii ndivyo ilivyo, yapasa nasi raia kuchangamkia fursa hizo. Ila wapo vigogo kadhaa kwenye biashara hiyo pale Chunya, na zawaletea faida kubwa sana. Hata jimboni LUPA mpango ni uleule mpaka kuleee 'kambi katoto'.

Na migodi hiyo pale Chunya, hakuna kodi ilipwayo na hao waitwao wawekezaji.

Maeneo ya kuendeshea migodi wanapewa BURE na wanakijiji, zaidi wao wanaombwa tu kuchangia shughuli za maendeleo. Yaani serikali kule imewekwa mfukoni.
 
Rock City:

Ndiyo maana nimeeleza hapo awali, Makampuni haya makubwa ya uchimbaji dhahabu yamekosa ubunifu. Kuondoa misuguano na wachimbaji wadogo maeneo yao Teknologia hii wangewawezesha wao na kuwauzia kwa bei watakayomudu ili badala ya kugombania maeneo ya kuchimba wangekuwa na chanzo mbadala cha kupata kipato.

Kwa maelezo yako biashara hii ni halali kosa la Wachina waliokamatwa ni kukosa kibali cha kusafirisha huo mchanga.

Hata maelezo ya polisi yanasema toka trh 2 mpaka trh 15 wamekuwa wakiyaruhusu yapite ila ya trh 31 wameyakamata sababu hayakuwa na kibali!!
 
Ingelikuwa ni huko China halafu raia wa nje kafanya hivyo...angenyongwa au kupigwa risasi kimyakimya...
 
Back
Top Bottom