Umenigusa mkuu. Kwakweli chadema wakati mwingine wananiudhi hasa pale ambapo kila tatizo la nchi, wao wanachukulia point ya kupata cheap popularity, hawaoni hata jema moja la serikali! Pamoja na kuwa ni mshabiki wa baadhi ya wanasiasa wa chadema hasa Tundu Lissu lakini Wakati mwengine Chadema nawafananisha na wimbo wa Ndio mzee wa prof Jay. Kimsingi mapenzi yangu kwa chadema yamepungua kwa zaidi ya 60%, kama watampitisha slaa, zito au mbowe kugombea urais, siwapi kuru yangu labda wampitishe tundu lissu maana ndio mtu pekee mwenye hekima ndani ya chadema, mnyika bado mdogo sitamzungumzia kwasasa. Kwaujumla wakiendelea na siasa zao za kueneza chuki dhidi ya serikali iliyo madarakani, Nawatabilia chadema kifo kama cha cuf au nccr mageuzi