Wachungaji na Mashehe wanafiki! - Mmevuna mlichopanda!

Wachungaji na Mashehe wanafiki! - Mmevuna mlichopanda!

Na hili suala lisiishie kwa taasisi za kidini pekee........hata wabunge nao walipe Kodi......hivi mtu unajiitaje kiongozi wakati kipato chako hutoi mfano wa kulipa kodi.............ndio maana hao viongozi hawaoni uchungu kusamehe kodi akina Jitu, Somaiya, and the like...........Damn!
 
Ni kweli inawezekana kuwa baadhi ya viongozi wa madhehebu walikuwa wakitumia msamaha wa kodi vibaya, lakini hata hivyo serikali ilipaswa kufanya uchunguzi wa kina na kubaini ni wapi kulikuwa na mapungufu kabla ya kutoa uamuzi wa kufuta msamaha wa kodi. Jambo hili si dogo na nadhani linahitaji mjadala wa ushirikishwaji kwa wadau mbali mbali ili kupata njia mbadala ya kuondoa malalamiko na athari zinazoweza kujitokeza kutokana na uamuzi huu wa serikali.
 
Kodi tulipe hasa wale wenye kipato cha kawaida na cha chini, ila wachimba madini migodi, mahoteli makubwa wanasamehewa kwa jina la kuvutia wawekezaji, halafu na tulizolipa watu kawaida zinaishia kwa akina RA et al wakiiba hata zikiwa huko benki kuu, bora tuache kulipa kabisa. wizi mtupu! nimechoka kabisa na serikali hii
 
Kwa nini isiwe viongozi wa dini -- unatumia mashehe na wachungaji ( hujataja mapadri )
 
Kwa nini isiwe viongozi wa dini -- unatumia mashehe na wachungaji ( hujataja mapadri )

kwani mapadre siyo wachungaji? grrrrrrr!! mwisho utasema mbona hujata masista na makatekista na pia walimu wa madrasa!
 
Mazee it seems like hapa tulikuwa tajadiliana vitu visivyokuwepo. Waziri Mkulo kwenye taarifa ya habari ya saa mbili amenukuliwa akisema kodi iliyoondolewa ni kwa bidhaa/vifaa viingizwavyo nchini na mashirika ya kidini kwa minajili ya kibiashara.
 
Mazee it seems like hapa tulikuwa tajadiliana vitu visivyokuwepo. Waziri Mkulo kwenye taarifa ya habari ya saa mbili amenukuliwa akisema kodi iliyoondolewa ni kwa bidhaa/vifaa viingizwavyo nchini na mashirika ya kidini kwa minajili ya kibiashara.

Hiki ndicho alichosema Mkullo:

(xii) Kuondoa msamaha maalum wa Kodi ya Ongezeko la Thamani
(VAT Special Relief) kwa asasi zisizo za kiserikali (NGOs) na
mashirika ya dini. Hatua hii itahusisha madhehebu yote ya dini
ambayo ni pamoja na Waislamu, Wakristo, Wahindu, Mabohora
nk. Hata hivyo, vifaa vya kiroho na ibada vitaendelea kupata
msamaha wa kodi;

hilo la kwa "minajili ya biashara" limetokea upande wangu..
 
Kwa muda mrefu tumetaka kuwasha moto wa mapambano ya kweli.

Kuni zimekusanywa lundo kutoka misitu ya huko Lindi,Mtwara, Mlimba na Mufindi.
Kuna Petroli,Dizeli na Kerosine zilizochumbuliwa Zanzibar, Makaa ya Mawe kutoka Mgodi wa Kiwirana wa Benjamin Mkapa na Anna, Gas ya Songosongo tele.
Zaidi kuna midomo ya Watanzania zaidi ya Milioni 40 ikiwa kwenye mode ya kupuliza moto endapo kutakuwa na jitihada zozote za moto huo kutaka kuzima pindi ukiwashwa.

Tatizo, wapi kiberiti?

Kwa mtaji huu wa kuramba ushuru wapiga sala, hatuhitaji kibiriti tena moto huu utaanza wenyewe kwa Cheche za Kifikra zitakazo zaliwa kutokana na msuguano wa ndani kwa ndani kati ya Imani na undava wa serikali.
Hatumhitaji nabii Isaya kuja kutoa utambuzi wa nani atalala ngoma.

Ni rahisi ni vema na ni bora kwa serikali kuamua kupapasa kende za simba 7000 wenye njaa kali ya kwenda bila mlo kwa wiki 2 kuliko kugusa na kuchezea hisia za wanadini. Huu si mchezo wa hatari tu kwa serikali ni mchezo wa kutekeleza kifo chake.

Serikali zote katika kipindi fulani cha uhai wake zimewahi kulazimika kusalimu amri mbele ya vyombo vya kidini na kuangamia au kumezwa kiaina.

Je serikali ya CCM itapona kwenye hili??
 
Kwa nini isiwe viongozi wa dini -- unatumia mashehe na wachungaji ( hujataja mapadri )

Mimi nilidhani wewe ni mtaalamu wa lugha kumbe hamna kitu namna hii?

Kwa kimombo yaani ile lugha ya is and was Mchungaji anaitwaje na Padri anaitwaje?

Padry Padree? Sheep Grazer?Priesti Pasta Reverandi Faza??? Meeeni Idonti No!
 
Madela,

Kenya na uganda wameondoa misamaha..mbona poa tu??

What is so unique na dini Tz?

Kwa nini tz as a nation ni waoga hivi ktk kufanya maamuzi?? Why???
 
Nadhani unahitaji ku-revise chanzo cha umaskini nchini. FYI, Chanzo cha umasikini wa mtu mweusi ulianza hata kabla ya kuja kwa wakoloni na dini za kigeni.

dini zinaweza kuchangia umasikini.
tatizo la hizi dini linakuja hasa ni pale wanapowaambia waumini kuwa kuna miujiza. kwamba wakiombewa watapewa kwa miujiza vitu kama mf. wanaotaka viwanja mbezi, wanaotaka kufaulu mitihani, kupata wachumba, kazi nzuri, heshima nk.
na makanisa mengi hasa ya kilokole wana imani hii ndiyo maana waumini wengi hushinda makanisani wakiomba miujiza.
jamani hii dunia ya leo (sayanzi na technologia) kuna miujiza???????????
 
Tunashukuru na mjadala mzuri.
Tungewaunga mkono mashekhe na ma askofo na wachungaji kama wange kubali kuondolewa misamaha ya kodi kwa sasa mashule ya seminari na mahospitali garama zake ziko juu kuliko hata za binafsi vikiwemo na vyuo vyao, kulinganisha na zamani wakati wa nyerere kama walivyotaja, vilikuwa bure. Kwa kuwa serikali imerudisha kodi wangeonyesha uzalendo na upendo juu ya wananchi na waumini wao, kwa kuanza kudai serikali itoze kodi kwa wawekezaji uchwara kama tunavyoona railways inawanyonya wananchi kila siku na mashirika mengine ya umma na ya watu binafsi. Kisha wakaomba pia serikali ikusanye kodi na mapato mengine ya madini na maliasili, ili serikali ianze kuleta maendeleo kwa wananchi, hapo tungewaunga mkono kwa kuandamana nao na kuipinga serikali kwa kila hali. Kwa sababu siku zote mtetezi wa mwananchi mbele ya serikali ni taasisi za kidini. Lakini tumesikitika sana wao wanaweka maslahi yao mbele na kukumbatia mafisadi ambao wanawachangia. Kwa hivyo sasa maskini hatuna nafasi katika taasisi za kidini. Hiki ni kiboko cha mwenyezi mungu na sisi hatuta waunga mkono. Wacha waandamane wenyewe !
 
Wanalamika pale interests zao zinapoguswa. Kama kweli wao ni Watu wa Mungu, mbona hawakutoa tamko lolote wakati wanachama wa CHADEMA walipopigwa na Green Guards wa CCM kule Busanda, kama ilivyotokea, na hatimaye hao waliopigwa kufunguliwa mashtaka ya kufanya fujo na Polisi? Haki ilikuwepo kweli?

Hawa si Watu wa Mungu hawa?

Mara kadhaa kwenye hotuba za Salat Jumaa, Masheikh wanatuhubiria Waislam kuyakemea maovu tunapoyaona. Sisi Waumini tunakemea, wao walimu wetu wanapaswa kuwa mstari wa mbele. Mbona hawakemei?

Leo, misamaha ya kodi imeondolewa, ndio wanakaa kimya? Mbona Waziri Nagu (kabla ya muswada huu kwenda Bungeni) alitangaza kusudio la Serikali kufuta misamaha ya kodi kwenye taasisi za kidini na NGO? Ina maana hawakuliona? Au walidhania serikali inafanya dhihaka?

Well, hii si dhihaka, hii ni sabotage kwa Watanzania. Sasa nadhani mnaelewa wapi CCM inaelekea. Mkiichagua tena 2010, litakalotokea shauri yenu. Mimi simo!

./Mwana wa Haki

Mbowe: Nataka kugombea Moshi Vijijini, tumwondoe Kimaro.
 
Wanalamika pale interests zao zinapoguswa. Kama kweli wao ni Watu wa Mungu, mbona hawakutoa tamko lolote wakati wanachama wa CHADEMA walipopigwa na Green Guards wa CCM kule Busanda, kama ilivyotokea, na hatimaye hao waliopigwa kufunguliwa mashtaka ya kufanya fujo na Polisi? Haki ilikuwepo kweli?

Hawa si Watu wa Mungu hawa?

Mara kadhaa kwenye hotuba za Salat Jumaa, Masheikh wanatuhubiria Waislam kuyakemea maovu tunapoyaona. Sisi Waumini tunakemea, wao walimu wetu wanapaswa kuwa mstari wa mbele. Mbona hawakemei?

Leo, misamaha ya kodi imeondolewa, ndio wanakaa kimya? Mbona Waziri Nagu (kabla ya muswada huu kwenda Bungeni) alitangaza kusudio la Serikali kufuta misamaha ya kodi kwenye taasisi za kidini na NGO? Ina maana hawakuliona? Au walidhania serikali inafanya dhihaka?

Well, hii si dhihaka, hii ni sabotage kwa Watanzania. Sasa nadhani mnaelewa wapi CCM inaelekea. Mkiichagua tena 2010, litakalotokea shauri yenu. Mimi simo!

./Mwana wa Haki

Mbowe: Nataka kugombea Moshi Vijijini, tumwondoe Kimaro.
Mwanaharakati kwanza naomba ufute usemi wako kwamba mashehe na mapadri ni wanafiki.

Hiyo siyo lugha nzuri kwa viongozi wetu wa kidini lakini naomba pia nikupe pole kwa kukipenda chama chenye mwelekeo wa kikabila. Pole sana maana chadema hawana sera zaidi ya kutangaza ukabila lakini kama wewe ni mchaga nakutakia kila la kheri
 
I have been always in support of KULIPA KODI...... however......
Tujiulize in the first place kwanini hizi taasisi za kidini zilipewa misamaha ya kodi...what was the rationale............
na sasa serikali kuondoa kodi what is the rationale..............

Hizi taasisi za kidini inatakiwa ziwe audited/assessed na iangaliwe ni shughuli zipi wazifanyazo zilipiwe kodi na zipi zisamehewe.....mfano zile shughuli ambazo ni huduma kwa jamii hospitali and the like.....serikali should think again....zile za kibiashara mfano radio stations and the like....zilipe kodi

Serikali itoe muongozo kwenye hilo ili kusitokee kutokuelewa............

Serikali pia lazima ikumbuke kuwa si kila biashara ifanyazo hizo taasisi ni kwa ajili ya manufaa kibiashara............inawezekana kabisa kuwa charge wanazotoza ni ili kugharamia shughuli za uendeshaji wa hizo shughuli.........na ndio maana hapo mwanzi nimesema hizo taasisi ziwe audited kujua what is what
Hizo hospitali na shule ndiyo wanatakiwa walipe haswa. shule nyingi zinazomilikiwa na taasisi za kidini karo zao ni za juu sana,Mahospitali vile vile ada zao za juu,vyuo vile vile kwa ujumla wanajiendesha kibiashara na bado hata ukitaka nafasi kwenye hizo shule pamoja na ada na vigezo vingine kutimiza bado lazima umjue fulani.Kwa mfano kwenye mahospitali madaktari na watumishi wengine wanapelekwa huko kufanya kazi na serikali na kulipwa na serikali lkn bado mashirika yanawatoza wagonjwa bei mbaya kwa kutoa huduma.Jamani hizo huduma zamani ndiyo ilikuwa nafuu na si sasa.Haya mashirika huduma zao zote kwa jamii kwasasa ni ghali.Ninachoitaka hii serikali isiishie kwa mashirika ya dini vipi kwa wanaochukua mrahaba bila ya kulipa kodi au kulipa kiduchu?Na huko nako kwanini wasiende!Mkulo na nenda kwa hao wakezaji mufilisi pia.
 
Mwanaharakati kwanza naomba ufute usemi wako kwamba mashehe na mapadri ni wanafiki.

Hiyo siyo lugha nzuri kwa viongozi wetu wa kidini lakini naomba pia nikupe pole kwa kukipenda chama chenye mwelekeo wa kikabila. Pole sana maana chadema hawana sera zaidi ya kutangaza ukabila lakini kama wewe ni mchaga nakutakia kila la kheri

Ipole, naitwa Mwanahaki, au Mwana wa Haki ukipenda.

CUF ilitangaziwa sana propaganda na CCM kwamba ni chama cha Waislam. Sasa, Mbunge wao mahiri, Wilfred Lwakatare, ni MUISLAM?

Tuzungumzie hoja iliyopo, kwamba tunaupiga vita Ufisadi hata kama fisadi tunayemwona ni Kasisi, Katekista, Sheikh, Imam au Padri!

Kubali kuliita jembe kwa jina lake, jembe. Si kitu kingine.

Sijawahi kuona chama chochote kile kinachotangaza Sera ya Ukabila. Wilbroad Slaa, Mbunge wa Karatu, ni Mchagga? Maana umetaja Wachagga. Zitto Kabwe, Halima Mdee, Mhonga Said? Hao nao pia ni Wachagga?

Hizo ni propaganda, Wananchi wanaujua ukweli. Hawazitilii maanani tena!

Mimi si mwanachama wa Chama chochote kile, ila nitaitumia CHADEMA kuleta mabadiliko, kisha chama kipya cha kuwazindua Wananchi kitaanzishwa. 2015 CCM itaondoka madarakani rasmi! Hamna kiongozi anayefaa kuwa Rais baada ya Kikwete! HATA MMOJA!
 
MwanaHaki, Zitaumbwa MBINGU MPYA na nchi zitageuka 2015 ama ni vipi mkuu. Kwa hiyo baada ya Kikwete hata wewe MwanaHaki hufai siyo?
 
Siku hizi dini imekua biashara na kuna baadhi ya watu wamekua waki tumia huu msamaha wa kodi kuji nufaisha. Kuna "viongozi" wengi tu wa dini wana tumia makanisa yao kama biashara sasa kama wana jiendesha kibiashara kwa nini wasi tozwe kodi? After all makanisa/misikiti mingi ina tegemea sadaka za wananchi kwa hiyo hawawezi kulalamika wakati jasho za pesa zao tunazi tolea sisi tunao wachangia.
 
Last edited:
"Kuna watu wamekuwa mamilionea kwa kutolipa kodi kupitia mgongo wa dini…kwa kweli hawa wanaopata hii misamaha wanaitumia vibaya, kwani wanasingizia dini wakati wanaenda kufanya biashara," alisema Mkulo.

Waziri huyo alitoa mfano wa moja ya madhehebu lililoagiza mabati 4,000 kwa ajili ya ujenzi wa kanisa likatumia mabati 200 tu na mengine mmoja wa viongozi wa kanisa hilo akaenda kuyauza kwa bei ya soko. Pia alitoa mfano wa madhehebu ya dini ambayo yaliagiza tani 5,000 za sukari kutoka Malawi kwa ajili ya kituo cha watoto yatima, lakini tani tano tu zilienda Singida kwenye kituo hicho na tani zingine zilizobaki zilikwenda Makambako na kufungwa kwenye mifuko na kuwauzia wananchi.

Katika kuelezea namna baadhi ya watu wanavyonufaika na misaada hiyo, alitoa mfano wa kiongozi mmoja wa kidini aliyeagiza magari kwa ajili ya kanisa lakini akayatumia magari hayo kwa kuanzisha kampuni ya kitalii (tour operator) kwa ajili ya kukodisha kibiashara. Alitoa mfano wa taasisi zisizokuwa za kiserikali (NGOs) kuwa kuna zinazotumiwa na wafanyabiashara kuagiza vifaa mbalimbali sio kwa ajili ya matumizi ya kijamii bali kibiashara.

"Hawa wanatumiwa na wafanyabiashara licha ya kuwa zipo chache zinafanya kazi vizuri." Hata hivyo, Mkulo alisema jopo hilo la kitaalamu ambalo limefanya uamuzi huo limeona kuwa msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani uendelee kutolewa kwa kwa vifaa vya elimu, huduma za afya na vifaa vya hospitali ambavyo vitaagizwa na taasisi za kidini.

Ila alisisitiza kuwa vifaa vitakavyoingizwa na taasisi za kidini kwa lengo la biashara ni lazima zilipewe ushuru na akatoa mfano taasisi ya St Gasper inayoendesha hoteli na zingine zinazofanya biashara hiyo iwapo zitaagiza vifaa vya hoteli ni lazima zilipie kodi. Alisema serikali haiwezi kukubali kuendelea kupoteza kiasi kikubwa cha fedha kwa kutoa msamaha kwa vifaa ambavyo sio vya kiroho au ibada ila wanataka kuhakikisha vifaa vya biashara vinatozwa kodi vyote."

Source: Habari leo!
 
Siku hizi dini imekua biashara na kuna baadhi ya watu wamekua waki tumia huu msamaha wa kodi kuji nufaisha. Kuna "viongozi" wengi tu wa dini wana tumia makanisa yao kama biashara sasa kama wana jiendesha kibiashara kwa nini wasi tozwe kodi? After all makanisa/misikiti mingi ina tegemea sadaka za wananchi kwa hiyo hawawezi kulalamika wakati jasho za pesa zao tunazi tolea sisi tunao wachangia.

Ni kweli MF1, tena cha kusikitisha hata watu wa nje wanakuja kutajirikia kupitia taasisi za kidini, wanakuja kwa gear ya kutoa misaada na kuendesha biashara zao wakifanikiwa wanaondoka na kuuza taasisi kwa watu wengine wakidai kuwa wamefanya mabadiliko, taasisi nyingi zinaendeshwa kibiashara, ni magari mangapi yanayoagizwa na taasisi zetu za kidini na ya nasamehewa kodi kumbe ni kwa ajili ya matumizi ya watu binafsi,

hata wafanyabishara wanatumia taasisi za dini kuingiza vitu bila ushuru,
 
Back
Top Bottom