Wachungaji na Mashehe wanafiki! - Mmevuna mlichopanda!


I think it is sheer short sighteedness kwa mtu kuiona miradi mingi ya kidini na kijamii kwa mtindo huu wa jumla ya magari yaliyoingizwa na kodi iliyokosekana.Long term scope ya miradi hii ya kijamii ambayo inatekelezwa na mashirika haya ya kidini ina far reaching impact kuliko kodi inayoweza kupatikana.
Kwa hii leo, kwa level of governance tuliyonayo (na si miaka hii tu ya karibuni) miradi mingi ya kiserikali siyo endelevu ukilinganisha na ile ya kidini, hii ni pamoja na ukweli kuwa wote wanafaidika na misamaha ya kodi.
 
Last edited:


Sina utaalamu sana wa mambo ya budget za nchi na sina utaalamu sana wa misamaha ya kodi kwa nchi mbali mbali , Lakini kwa nchi ninayo ishi kwa sasa, ninatambua kabisa kabisa kwamba misamaha katika kodi mbali mbali ipo hasa kwa mashirika ya kidini na hizo Non Goverment Organization ( NGo´s)

Nadhani wenzetu waliliona hili lina nafasi kubwa katika jumuiya zao..Ndugu zangu wa Tanzania, Ukitaka kusikia vyanzo vya machafuko ndani ya nchi kimoja wapo ni hiki ambacho Tanzania inataka kukipitisha. Kuzifutia misamaha taasisi zisizo za Kiserikali na mashirika ya kidini maana yake ni kuwapokonya ama kuwanyima huduma za muhimu wananchi walio wengi..!

Ni asilimia kubwa sana ya watanzania wanategemea mashirika na taasisi zisizo za kiserikali katika kujiendeleza na kupata huduma zilizo muhimu kwa maisha yetu ya kila siku. Mashule, Hospital,vyuo,sehemu za kutunzia watoto yatima ,vituo vya kupambana na maambukizi ya virus vya ukimwi na mengine mengi. Hivi ni baadhi ya vitu ambavyo Serikali yetu ya Kitanzania haiwezi kuvifanyia mdhaha hata kidogo.

Ndio serikali inaweza kuwa na vituo kama hivyo lakini, huwezi kulinganisha huduma zitolewazo na Serikali na huduma zitolewazo ktk mashirika ya kidini au taasisi zisizo za kiserikali. Nimesomea kwenye shule za serikali na za Kidini, nimeshafanya kazi serikalini na kwenye taasisi/ mashirika yasiyo ya Kiserikali. Tofauti ni kubwa sana.

Sitopenda kuingilia Budget ya nchi, Bali kwa ushauri wangu kwa faida ya Taifa langu haya Mashirika ya Kidini na Taasisi zisizo za kiserikali zipeni misamaha ya kodi. Msipo fanya hivyo maana yake mnalirudisha taifa kwenye Kipindi cha miaka ya 70`s

Serikali ya CCM inaweza kuja kujutia faida hiyo inayotegemea kuja kuipata kwa kukusanya Kodi katika hayo mashirika/ asasi.

Sitegemei aliyetoa ushauri wa kuyafutia msamaha wa kodi mashirika ya kidini pamoja na NGO´s alitokea NIGHT CLUB au Bar kwa wakati huo,siwezi jua kwani ni kawaida yetu watanzania kutoa maamuzi mazito hasa pale tunapo kuwa walevi. na Ulevi pia waweza kuwa wa madaraka, au pia nafasi ile ya kutoa maamuzi uliipata kwa njia zisizo sahihi.....Kupeana, INATIA SHAKA...!

Amkeni viongozi wetu, Tupo kwenye Karne nyingine kabisa, Ujanja ujanja mnao taka kuufanya katika kukusanya mapato ya nchi zauwezi kuwa na nafasi kabisa kwa wakati tulionao..PATO LA NCHI LINAKUSANYWA PALE KWENYE FAIDA.

I weje mjifutie kodi kwa miaka miwili pale mnapo kwenda kuchimba madini yenye faida kubwa ktk ardhi yetu kwa kisingizio cha kujiweka sawa?? Una uhakika gani madini yaliyopo ardhini yanaweza kuchimbwa zaidi ya miaka miwili unayo tegemea kulipwa kodi ??

Rais mstaafu B. Mkapa alitumia nyia na mbinu mbali mbali katika kukusanya na kuongeza pato la nchi, na alifanikiwa japo alikuwa na udhaifu wake, Na hakukuwa na malalamiko makubwa japo wananchi waliguswa kwa njia moja au nyingine.

Nina uhakika kama kiongozi hatoweza kupata nafasi ya kudadisi na kuchunguza kwa umakini shughuli na wajibu wake ndani ya nchi hata maamuzi yake hayatokuwa ya busara na faida kwa wale wanaomzunguka.

Utakapo mwachia fisi kazi ya kupanga budget ya kondoo atakwambia ni kumkamata kondoo na kumkamua chakula alichokwisha kula kisha ukigawe tena. Na hili ndilo linaloendelea kwa sasa ndani ya nchi yetu.

Mtawakamuwa wananchi mpaka lini ?

Mungu anamakusudi kabisa ndani ya Taifa letu, Na kilio cha watanzania kimemfikia,"Bwana yu karibu na waliopondeka roho huwaokoa" (Zaburi 34:1 Na pia imeandikwa: Simama ukaitende maana shughuli hii ya kuhusu wewe, uwe na moyo mkuu nami ni pamoja nawe..!

Basi watanzania wenzangu Tusimameni tukaitende shughulii hii ya kulikomboa Taifa letu la Kitanzania lililopo nimodomi mwa mbwa mwitu maana shughulii hii inatuhusu sisi na Mungu yu pamoja nasi..!! Mungu Ibariki Tanzania ..!!!
 

Mkuu hapa Serikali imeangukia Pabaya...!! Wasipo badirisha hii Budget kiama chao kitakuwa kimefika..!! No one will stand !!!!
 
Hivi kama Kenya na Ug. wameweza kutoa misamaha ya kodi kwa % kubwa kwa nini Tz tunaogopa??

Huu woga unatoka wapi?
 


Taxi exemption zipo dunia nzima sio Tanzania tu..!! loop holes zinakuwepo endapo hakuna utawala bora..!!
 
Taxi exemption zipo dunia nzima sio Tanzania tu..!! loop holes zinakuwepo endapo hakuna utawala bora..!!

Tufanye tu kwa sababu ipo dunia nzima???!!!

Kwani lazima tudese kila kitu kinachofanyika duniani? Kuiga tembo kunya mwishowe ni kupasuka msamba.

Kama umeguswa na hili pole sana lakini habari ndio hiyoooo, mmekwepa vya kutosha...
 
kodi na zilipwe sio na taasisi za dini tu ......na waanze wabunge, wafuatiwe na kuongezwa kwa kodi kwa mawaziri.
 
kodi na zilipwe sio na taasisi za dini tu ......na waanze wabunge, wafuatiwe na kuongezwa kwa kodi kwa mawaziri.

Naogopa kuchangia thread hii!! inatisha! labda kama watu hawajui ukweli! inatisha, kwangu naona faraja!

Kwanza sioni tatizo la hili swala;

(1) Kwanza itawapa discipline wachungaji watumie mapato ya kanisa kikamilifu
(2) Tutawapata wachungaji wa kweli!
(3) Makanisa yatabuni mirai na njia mbadala ya kupata fedha,
(4) Itapunguza ombaomba na hivyo kulitimiza lile neno afadhali kutoa kuliko kupokea, wengi wataanza kutoa then watabarikiwa (Acts 20:35)
(5) In long term; itasaidia watu wajue umuhimu wa kuwa serious kuchagua viongozi wa serikali, ambao watatumia vyema kodi wanazotoa
 
Over 30% ya total budget ilikuwa misamaha ya kodi??????????????

Uwii??????????????

Sasa ni kitu gani hapo hakieleweki??

Nchi zingine, masheik na wachungaji hulipwa salari kama wafanyakazi wengine..na kuna ministries of Church Affairs!

Kama kuna ukata waombe serikali iwasidie pesa kidogo ya mishahara!!

Ila kodi lazima ilipwe!

Think once again..30% exemption???????? This is too much!
 
Wanabodi,
Kwanza wakuu ni muhimu tufahamu kwa nini hizi NGO zimekuwepo dunaini na zimeweza vipi kuchangia ktk ustawishaji wa jamii. Tukianza ku question matatizo yanayosababiushwa na watu binafsi kuweza kuvihukumu vyombo hivi basi nasi tunakuwa hatuna hoja..
Kusema kweli sikubaliani kabisa na maelezo ya Mwanakijiji wala mapendekezo yake kwa sababu hayakuzingatia kazi ya vyombo hizi ktk jamii..Na ndiuo maana vimekuwa katikati ya misukumo miwili ya Kiutawala ktk social and economic issues.

Huwezi kuwaweka ktk Biashara kwa sababu wanachukua nafasi ya sehemu ambazo biashara imeshindwa kutoa huduma hizo kwa maskini na huwezi kuipa serikali majukumu ya hizi NGO kwa sababu NGO hujikita ktk sehemu (huduma) ambazo serikali imeshindwa kuzitekeleza..
Maisha bora kwa wananchi wote ni mbiu ya kitaifa na haiwezi kutekelezwa kwa kutegemea aina mbili tu za usambazaji huduma kwa jamii yaani Biashara au serikali..Tunahitaji sana NGO pale serikali na wafanyabiashara wanaposhindwa kutoa huduma hizo kikamilifu hasa kwa nchi maskini kama yetu. Matatizo ya wahalifu yashughulikiwe kisheria kama raia wengine wanapovunja sheria..
Kibaya zaidi kinachojitokeza hapa ni kwamba hukumu inayotolewa na serikali imetazama upande mmoja tu wakati wawekezaji (wafanyabiashara) wanaepuka kodi mara 20 zaidi ya hizi NGO kupitia hii misamaha ya kodi..Na Viongozi wetu nchini wanaepuka kodi mara 10 zaidi ya hizi NGO lakini utaona bajeti imetazama upande mmoja kuweka sheria ngumu kitaifa..

Kisha mkuu Mwanakijiji kawaita Masheikh na Machungaji WANAFIKI... kwa kile walichosimamia kupinga serikali, lakini wanapolia na kuandamana inakuwa Unafiki..kumbuka wanaoandamana sii wale walioiba wala wanaopenda Ufisadi isipokuwa wapo wanaochukua majukumu zaidi ya dini kuliko kujiingiza ktk siasa za Bongo. Wanajua athari za kujitosa kichwa kichwa ktk maswala ya Ufisadi na pengine makanisa au misikiti yao imewahi pokea michango toka kwa mafisadi haohao wanaoshutumiwa leo...It's a Catch 22.

Mapungufu ya taratibu za utekelezaji ktk taasisi za serikali husika ndio chanzo kikubwa cha ukiukaji wa sheria hizi zilizofukiwa makabatini.. Ukitazam kodi zetu inakuwaje kweli mfanyabiashara afanyiwe estmate ya kodi yake kutokana na biashara inayokusudiwa hata kabla hajaanza uzalishaji?.. Utakuta mtu analipa kodi ya mwaka iliyokisiwa wakati serikali haifahamu pato la mhusika kwa mwaka mzima. Hizi tax exemptions zipo kwa kila diplomatic, mashirika ya nje ambayo toka yaingie nchini ni zaidi ya miaka 10 hawajalipa hata ndululu na wanatajirika kichizi.. lakini utakuta serikali ipo kuwatetea hawa watu, leo vyombo vinavyowasaidia wananchi moja kwa moja vinahukumiwa kwa makosa ya waajiriwa wake..kisha basi hata wasifikishwe mahakamani kujibu tuhuma hizo tayari bunge linakaa kupitisha mswada ambao hauna ushahidi zaidi ya utafirti ambao wanashindwa kuufikisha mahakamani..

Sheria zipo na kama kuna mtu kakiuka sheria hiyo kwa kutumia vyombo hivi afikishwe mahakamani, kesho utaona utendaji mzuri wa kazi na sii kutunga sheria ambayo inaathiri huduma zinazowafikia wananchi moja kwa moja na kila siku ya maisha yao...

Tunayaona haya ktk Ufisadi, wanaofikishwa mahakamani ni wale samaki wadogo.. mbali na Rostam kukubali Upapa na kumwita Mengi kuwa ni Nyangumi ina maana kwamba Rostam hakatai kuwa yeye ni Papa Fisadi!, lakini kilichofanyika ni kukataa kununua mitambo ya Dowans lakini asifikishwe mahakamani kwa makosa yaliyotangulia hadi tukavunja mkataba na Dowans..

Hatukuvunja mkataba na Dowans kwa sababu walishindwa kufua umeme! wala hatukuvunja mkataba na Dowans kwa sababu nyinginezo zaidi ya kuwa shirika hilo liligundulika kuwa feki na mkataba ulioingiwa haukuwa halali pia (Mapendekezo ya kamati ya Mwakyembe)..Rostam hakuulizwa, kuitwa wala kuvunja mikataba ovyo..
Na kibaya zaidi ni kwamba gharama ya umeme wa Richmond/Dowans ilikuwa kubwa kuliko mashirika mengine yote yaliyotuuzia umeme kwa kiwango sawa na mashirika hayo..WATU wametajirika kutokana na mikataba mingi mibovu na bunge limeshindwa kuweka sheria wala kutazama upande huo kwa sababu tu wahusika ni wao wenyewe..
 
Kweli unafiki wa viongozi wa dini nao budi ubadilike. Kwa mfano, wamekuwa mstari wa mbele kusifia watu wenye kushukiwa kuwa ni mafisadi. Sasa wanapoanza kubadili msimamo, kama ule wa kanisa katoliki kuanza kuelimisha wapiga kura badala ya kuwaasa kuchagua chama kilichopo madarakani, then hii ndo dawa yao. Nafikiri kuandamana hakuta leta maana yoyote ile mana makusudio yao ni ustawi wa roho na mwili wa watu. Wajipange kushare hizo gharama na hao maskini.Halafu nao wabadilike, maana sio wote wanaosamehewa kodi wanaenda kusaidia walengwa.
 
ukipanda mahindi utavuna mahindi tu wala si maharage..Viongozi wa dini mligeuza migongo na kuona wananchi wanaongea pumbapumba sasa kilio cha nini? Welcome aboard tulie na kuomboleza pamoja.
 
Ndahani,
Mkuu wangu unapotosha hoja yako hapa.. Hakuna Mchungaji wala Sheikh anaye run hizi NGO ila hupokea misaada kutoka ktk hizi NGO.. Sasa kama una ugonvi na Sheikh au mchungaji ktk maswala ya siasa mfuate yeye lakini huyo Sheikh au mchungaji ana jukumu jingine zaidi ya mapenzi yake ktk isasa za Tanzania.. Nalo ni kupokea na kutoa huduma za kikanisa au Msikiti kwa waumini wake..
Ubadhirifu wa kodi za serikali unafanywa na waajiriwa wa hizi NGO na siii Wachungaji wala Masheikh!..Muulize huyo waziri yale mabati 3800 yaliyouzwa mtaani na Mchungaji gani!..Na ikiwa mwizi ni toka NGO moja iweje uyahukumu mashrika yote ya misaada hata kama hayajakiuka sheria!..
 

Mkuu sawa kabisa hapa tupo ukurasa mmoja.

Anavosema Mkullo, kama mtu aliuza mabati au simenti au tuseme chakula cha msaada, alifanya uhalifu na alipaswa ashtakiwe kwa kuvunja mkataba, na siyo kuja na hoja dhaifu ya kuwafutia misamaha ya kodi!

Mi najiuliza, ni lini wataacha kupandisha bei za bia na sigara na soda,, na kuendelea kusamehe kodi mafuta yanayotumika kwenye kuchimba madini, mahoteli, nk? hatuna tatizo kubwa kuliko tunavofikiri kweli?
 
Nakubaliana na wewe kuwa si wote wanatumia vibaya misamaha ya kodi ingawa wapo. Kwasababu misamaha inatolewa kwa NGO au mashirika ya dini bila ubaguzi, inawezekana pia kukawa na influence ya baadhi wa viongozi wa juu wa dini wasio waaminifu maana hao pia wapo. Ninachotaka kusema pia ni kuwa kuandamana haitabadili sana mwelekeo na inaweza kuleta picha kuwa wanajaribu kulazimisha mabadiliko. Badala yake imapct ya decision hii ndio inaweza kufanya serikali ibadili nia au la. Pamoja na yote, mwelekeo wa wakuu wa dini kusema waziwazi sasa kuchukia mambo mabaya yanayoendelea inaweza pia ikawa ni msukumo. Na nimechukulia tu kwa jumla kwamba kanisa katoliki inawezekana ndilo lina mashirika mengi yenye kupata misamaha hii ya kodi, ingawa sina data za back up kwa hilo. Ujasiri wao wa kusema tubadilike katika chaguzi za viongozi sio kitu kidogo kisiasa. Kina imapact pia ambayo inaweza kuwa na negative consequences kwa utawala. Tusisahau pia Dini haitakiwi kuwa na double starndard. Kwnye ubaya ni lazima isimame na kusema hapana. Kwa muda mrefu hawa jamaa wamekuwa kama hawaoni au watazamaji tu na wahusika wa mambo yasioeleweka wakawa ni mashujaa wao in some occasions.Hapo nahisi ndipo penye unafiki wenyewe unaozungumziwa
 
Ndahani,
Unajua mkuu wangu kitu kimoja ambacho mimi siku zote sikubaliani nacho ni kutafuta sababu ili kukiuka ukweli na sheria.. na mara zote Tanzania imekuwa ikitumia mifano hi ktk kujenga hoja. Tukizungumzia Ufisadi wa Rostam basi watu wataanza mbona wewe Mkandara unafanya hili au lile ambalo halihusiani kabisa na ufisadi unaozungumziwa..
Kama unakumbuka Mtikila aliwahi kumwita Roistam fisadi.. ikaja kuwa aliwahi kupokea msaada kutoka kwa Rostam, basi issue ya Ufisadi wa Rostam ikafa wakati tunafahamu fika kwamba Mtikila alipokea fedha zile kama msaada wa kanisa lake..Hivyo naye akawa fisadi mpokeaji..Na nyote humu mlimshutumu kwa kupokea fedha za Rostam.
Hivyo kuwashutumu Masheikh ambao kula yao hutokana na misaada kisha ukawaingiza ktk siasa za Bongo ambazo majority wa viongozi, makanisa, misikiti wamewahi pokea misaada hii ni kuwazulia unafiki.. Ex Presidaa Mkapa aliiba ngapi?..Mabillioni, yeye na Mkewe.. haya nambie ni dhehebu gani hawakupata msaada wa Mkapa kwa njia yoyote ile.. leo umtake kiongozi wa msikiti au kanisa atangaze kupinga Ufisadi wa Mkapa wakati anajua wazi kuwa Mkapa ndiye aliyeweka msingi wa jengo la ibada..kweli huyu mnakuja muunga mkono kwa jinsi tunavyoendelea kufikiri!

Ni sisi wananchi tunatakiwa kutenganisha vitu hivi.. Kiongozi wa NGO (sii mchungaji) kaagiza mabati 4,000 kati yake mabati 3,800 kauza na kuwapa kanisa mabati 200 na mchungaji kapokea mabati 200 kaezeka kanisa lake.. iweje leo tunashutumu viongozi wa kanisa waliopokea mabati 200 wakati swala ni yale mabati 3,800 yaliyouzwa mtaani?..
Haya serikali inaondoa msamaha wa kodi kwa mashirika haya wakati wanajua wazi kwamba mabati 3,800 yaliuzwa mtaani na yanahitaji kulipiwa kodi..kwa nini wasifanye hivyo?
Kuweka sheria haiwezi kurudisha kodi ya mabati 3,800 wala kuongeza kodi kwa sababu NGO zote zinapokea misaada pia, hawana cash wala hawa run huduma hizi kwa kutegemea kubnunua vifaa isipokuwa misaada inayotolewa na wafadhili toka nje..
Sasa unapowaondolea msamaha wa kodi ni lazima ufikirie kwamba haitawezekana kwa NGo hizi ku function hata kidogo..Hakuna NGO dunaini inalipa kodi ni mfumo ambao haukutungwa na Masheikh wala Wachungaji. Na mara zote unataka ufuatiliaji wa nyaraka zake kwa ukaribu zaidi kuepuka ukiukaji wa kulipa kodi.. Na ukweli ni kwamba NGOs huwa zinafuatiliwa zaidi ktk utendaji wake wa kazi kuliko hata mashirika ya kawaida kwa sababu kuna loopholes ambazo zinahitaji umakini sana...
Sasa basi ikiwa serikali yetu inashindwa kufuatilia matumizi ya hizi NGOs na huduma wanazozitoa badala yake tunatafuta urahisi wa kutoa maamuzi kuepuka lawama za baadhi za wananchi..
Mkuu utanisamehe kwani nionavyo mimi wanafiki ni sisi... Siku zote tumesimama hapa kusimamia upande wa haki ya wananchi lakini imefika ktk swala hili tunaondoa malengo yetu na kuwaadhibu kwa kosa ambalo halihusiani nao kabisa. Je, ile haki tunayosimamia siku zote imekwenda wapi? kuna tofauti gani kati yako wewe na huyo Sheikh au Mchangaji ikiwa hata wewe ktk swala hili unaona vizuri wananchi au waumini wote waadhibiwe kwa makosa ya Sheikh au Mchangaji!..Kwa nini tusisimamie haki kila siku bila kujali nani mwakilishi wa hoja hiyo..
 
JF members wengine hii imewagusa pabaya!!

Je kuna makontainer mmekuwa mnatuma Tz kwa mgongo wa dini bila kulipia kodi??

Poleni! Anzeni kulipia kodi tangu sasa !
 
Mzalendohalisi,
I know where U come from.... sifanyi hivyo hata siku moja..
Mimi natazama haki ya huduma za makanisa na misikiti pia kuponyesha serikali yetu kuingia ktk matatizo makubwa na jamii yake.
Trust me, hili swala litazua utata ambao CCM haijawahi kuupata! pengine wewe huelewi siasa za NGOs dunaini..
 
Kutoa misaada siyo excuse ya kufutiwa kodi bila vipimo.hapa kuna options mbili tu, ya kwanza ni kodi kurudishwa kama ilivyofanya serikali na ya pili ni kusamehe a fixed amount ya kodi kwa mwaka.hii misamaha ya kodi isiyo na vipimo maalum ndio inaacha mianya ya ufujaji.
 
ZeMarcopolo,
Mkuu huwezi kuweka fixed amount kwa sababu kila kijiji au sehemu inahitaji vitu tofauti.. Swala kubwa ni ufuatiliaji wa hii misaada. kama mtu kaingiza mabati 4,000 project nzima inayohitaji mabati 4,000 inatakiwa kupitishwa na vyombo vya serikali toka huko kunakohitajika. Hatua kwa hatua.
Kama kanisa linajenga shule ya sekondary au Zahanati ni lazima kiongozi wa serikali iwe wilaya au mkoa ana habari kwamba kanisa au Zahanati inahitaji mabati 4,000. Mara zote hizi NGOs huomba misaada kutokana na shida iliyopo na kama wamepewa mabati 4,000 ina maana initial plan waliyowakilisha kwa wadhamini ni ujenzi unaohitaji mabati hayo... Hiyo plan iko wapi na nani kaipitia hadi kupitisha mabati 4,000 ambayo hayahitajiki..
Hivyo kinachotakiwa ni mkono wa kiongozi wa serikali..mara zote misaada inayoingia nchini huwa tayari matatizo yapo na hesabu kamili ya kile kinachohitajika ipo..Huwezi kujenga kanisa linalotaka mabati 200 yakaingizwa 4,000 bila chombo cha serikali kufahamu yalihitajika mabati 200 tu..
Hii inaonyesha uzembe uliopo sii wa NGOs bali serikali yenyewe.. Hivyo kilichotakiwa kufanywa ni kuhakikisha kuna misingi bora ya kupokea misaada kama hii na jinsi ya kuepuka wizi kama huu..Kutolipa kodi ni criminal case na sheria zipo iweje tutafute sababu nje ya kosa la wazi kama hili!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…