Masulupwete
JF-Expert Member
- Feb 15, 2012
- 2,366
- 2,424
Wadau,
Haya ni mawazo yangu na sitaki kulazimisha mtu kukubaliana au kupingana nayo. Asilimia kubwa ya wadada wa mitandaoni ni waongowaongo na wajanjawajanja sana.
Anaweza kukwambia yupo ubungo kumbe yupo kinyerezi, anaweka picha yake ikijionesha ni mdada wa kiuno cha nyigu kumbe mwenyewe halisi ni bonge wa tele kwa tele juu chini, anaweza kukwambia umtumie hela ya mafuta ili aje na gari yake kumbe hata toothpick hana.
Anaweza kukwambia anamiliki mashamba ya machungwa na matikiti kwao kumbe hata Msamvu stend hajui panafananaje.
Anaweza kukwambia hana mtoto kumbe anao tena si mmoja ni watano.
Anaweza kukwambia yupo wilaya ya jirani umtumie nauli aje, unatuma nauli ndani ya dk sifuri mwenzio huyo anachomoza toka hapo mtaa wa pili.
Anaweza kukwambia umtumie vocha akupigie, ukituma imekula kwako anapigia watu wengine ikiisha anabip.
Nyie wadada wa mitandao msifanye hivyo mumwogope Mungu kwani anawaona.
Sent using Jamii Forums mobile app
Haya ni mawazo yangu na sitaki kulazimisha mtu kukubaliana au kupingana nayo. Asilimia kubwa ya wadada wa mitandaoni ni waongowaongo na wajanjawajanja sana.
Anaweza kukwambia yupo ubungo kumbe yupo kinyerezi, anaweka picha yake ikijionesha ni mdada wa kiuno cha nyigu kumbe mwenyewe halisi ni bonge wa tele kwa tele juu chini, anaweza kukwambia umtumie hela ya mafuta ili aje na gari yake kumbe hata toothpick hana.
Anaweza kukwambia anamiliki mashamba ya machungwa na matikiti kwao kumbe hata Msamvu stend hajui panafananaje.
Anaweza kukwambia hana mtoto kumbe anao tena si mmoja ni watano.
Anaweza kukwambia yupo wilaya ya jirani umtumie nauli aje, unatuma nauli ndani ya dk sifuri mwenzio huyo anachomoza toka hapo mtaa wa pili.
Anaweza kukwambia umtumie vocha akupigie, ukituma imekula kwako anapigia watu wengine ikiisha anabip.
Nyie wadada wa mitandao msifanye hivyo mumwogope Mungu kwani anawaona.
Sent using Jamii Forums mobile app