Wadau hebu njooni tushauriane

Wadau hebu njooni tushauriane

Katika hali kama hii, jambo la msingi ni kusimama katika haki yako kwa utulivu na busara, huku ukihakikisha unatumia njia sahihi za kudai haki bila hasira au haraka isiyo na mpango. Hebu tuangalie hatua unazoweza kuchukua:

1. Tumia Lugha ya Staha Lakini Madhubuti
Unapowasiliana na wahusika, weka msimamo wako wazi kwa kutumia lugha yenye heshima lakini isiyoacha mwanya wa kuchezewa. Unaweza kuwaambia moja kwa moja kwamba umekuwa mvumilivu kwa muda mrefu na sasa unahitaji majibu ya wazi ndani ya muda fulani.

2. Kumbukusha Wajibu Wao Kisheria
Kwa kuwa una warrant ya miezi sita, ni haki yako kupata suluhisho kwa simu yako. Duka linawajibika kuhakikisha ama wanaitengeneza bila gharama yoyote au wanakupa simu nyingine endapo tatizo halirekebishiki. Unaweza kuwatajia Sheria ya Haki za Mlaji (Consumer Protection Act), ambayo inaeleza wazi wajibu wa muuzaji katika masuala kama haya.

3. Wasilisha Malalamiko Rasmi Ukiambatanisha na Onyo la Hatua za Kisheria
Ikiwa wanakuzungusha bila suluhisho la wazi, andika barua rasmi kwa duka ukiweka maelezo ya ununuzi, tarehe ya tatizo, na hatua ulizochukua. Katika barua hiyo, eleza kuwa ikiwa hawatatoa majibu ndani ya muda fulani (mfano, siku 7 za kazi), utachukua hatua za kisheria. Unaweza kutaja hatua kama:

Kuwasilisha malalamiko rasmi kwa Fair Competition Commission (FCC) kwa mujibu wa Sheria ya Ushindani wa Haki (Fair Competition Act, 2003).

Kuwasilisha kesi kwa Tanzania Consumer Advocacy Society (TCAS), taasisi inayotetea haki za walaji.

Kufuata hatua za kisheria kupitia mwanasheria ili kufungua kesi ya madai ya uzembe wa biashara (Breach of Contract).


Wasilisha barua hiyo kwa njia ya barua pepe au hata kwa mkono ikiwa inawezekana, na hakikisha unapokea uthibitisho wa kupokewa kwake. Kama bado hawatoi majibu yanayoridhisha, unaweza kufikisha malalamiko yako kwa mamlaka husika mara moja.

4. Tumia Mitandao ya Kijamii Kama Njia ya Shinikizo
Wafanyabiashara wengi huhofia sifa mbaya kwenye mitandao ya kijamii. Ikiwa hawatoi ushirikiano, waandikie ujumbe mfupi wa heshima kwenye kurasa zao rasmi ukiwauliza lini utapata suluhisho. Hii inaweza kuharakisha majibu.

5. Epuka Hasira na Maamuzi ya Kukurupuka
Kama ulivyosema, hutaki uonekane umekurupuka au huna hekima. Jenga hoja zako kwa utulivu, hakikisha una kumbukumbu zote za mazungumzo yenu, na usikubali kuachwa kwenye hali ya kutegemea ahadi zisizotimizwa bila kuchukua hatua stahiki.

Mwisho, kumbuka kuwa kila jambo linahitaji mbinu sahihi. Ukiwa na msimamo wa kiungwana lakini thabiti, ni vigumu kupuuzwa.
 
Zemanda ananichekesha sana, toka wajuba wampore manzi wake anatumind wanawake wote humu..!! 😹

Nikajua kale ka ushamba kameisha kumbe bado wamemuingiza kwenye 18 watoto wa kkoo 🤣
Badala ya kunifariji unanicheka hivi ni kweli?
 
MREJESHO:

Nimepata mawasiliano na m'miliki wa duka na baada ya kuongea nae akaniambia atalishughulikia hili swala bila shida akinielezea kuwa kiutaratibu wanatakiwa kucheki simu kama inashida gani kwanza na kupata ripoti ya fundi then ndipo waamue cha kufanya kwa mujibu wa ripoti ya fundi.

Baada ya kuzungumza nae Tarehe 2 mwezi February na kunipa ahadi hiyo,nikawa naendelea kumtafuta ili kunipa mrejesho kama amefikia wapi. Na katika hatua hiyo alipokea simu mara tatu akisema yupo busy na kazi na ameshindwa kufika dukani atakwenda siku inayofuatia.

Hili jambo likanipa mashaka sana kwasababu haiwezekani zipite siku tatu mtu hajakwenda dukani kwake. Mara ya mwisho kuzungumza nae tarehe 7 February,aliniambia ndio anaelekea dukani tuwasiliane jioni au kesho anipe mrejesho. Nilipiga simu jioni kuanzia saa moja jioni hadi saa nne usiku simu haipokelewi.

Niliendelea kupiga simu siku iliyofuatia pia hakupokea siku nzima. Leo sasa ikabidi niende tu pale dukani. Nikawakuta vijana wake na kuongea nao ambapo walionesha ushirikiano mdogo na walionekana kama kunikwepa hivi. Ilibidi niwaamuru kumpigia boss wao sababu simu yangu hapokei wakampigia na kumuuliza kuhusu swala langu akawajibu tu kuwa yeye alishazungumza na mimi na ameshanipa mrejesho jambo ambalo si ukweli sababu amekuwa hapokei simu zangu.

Akawaambia kuwa tatizo la simu yangu ni kuwa imekufa display na hiyo ndio ripoti ya fundi. Nikamwambia amuulize sasa nini kinatakiwa kufanyika sasa, akamwambia kuwa inatakiwa kununuliwa display yaani kioo kipya kwa gharama za mteja sababu warrant yao haibebi gharama ya manunuzi ya kioo kipya.

Sasa nikauliza kwa huyu muhudumu, mimi nahusika vipi na kununua kioo kipya cha simu wakati sijafahamu hata chanzo cha hiyo damage simu imezima tu bila sababu as if ilikuwa imekwisha chaji?

Sijawahi kuidondosha wala kuigonga wala kuipa damage yoyote,iwaje simu izime ghafla tu na kioo ndio kiwe tatizo?

Nikawaambia basi nitafutieni simu nyingine ambayo itareplace hii kwasababu mimi sijui hapa naanzia wapi ina maana nikiishia hapa na haya malekezo yenu tafsiri yake ni kuwa nilitoka nyumbani nikaja kununua simu kopo nikatupa pesa yangu then kirahisi tu niachane na hili swala liishie juu juu tu hivi?🤔

Wale vijana hawakuwa na majibu ya kunipa zaidi ya kusema "boss sisi hatuna maamuzi nje ya hapo maana mwenyewe ndio katupa hayo majibu".

Nimeondoka pale dukani nikiwa nimekasirika sana na kuchefukwa. Nimechukua ile simu ikiwa katika hali yake ya ubovu na kurudi home hadi hapa muda huu nawapa mrejesho hasira hazijaanisha.

Kioo kipya cha simu nimetazama hapa mitandaoni bei yake ni laki tano.

Kuna kitu kinaniambia huyu mwenye duka anajua anachokifanya. Hivi simu haijaanguka,haijagongwa popote,inakufaje kioo aisee?🤔

Sasa nataka nifanye maamuzi ya kupeleka hii kesi mahakamani ili tufanye kufuata taratibu za kisheria pengine yeye ataweza kuiambia mahakama kuwa ni kwa utaratibu upi simu inaweza kuzima tu halafu kioo kiwe ni tatizo then mteja ndie awajibishwe kwa tatizo ambalo sio physically inflicted kwenye hiyo simu?

Ni bora ningekuwa nimeidondosha au hata imeweka crack mtu anaweza sema ni sababu,yaani kioo hakiwaki kabisa na simu ukibonyeza power button inafanya kuvibrate bila reaction yoyote kwenye kioo sio mwanga waka kuonyesha chochote.

Hii kitu imenifundisha sana na kunipa umakini kimsingi kuanzia sasa sitathubutu kununua simu yoyote used au refurbished sababu naona kuna elements za utapeli na kukwepa kuwajibika kwa baadhi ya wauzaji ambao si waaminifu.
 
MREJESHO:

Nimepata mawasiliano na m'miliki wa duka na baada ya kuongea nae akaniambia atalishughulikia hili swala bila shida akinielezea kuwa kiutaratibu wanatakiwa kucheki simu kama inashida gani kwanza na kupata ripoti ya fundi then ndipo waamue cha kufanya kwa mujibu wa ripoti ya fundi.

Baada ya kuzungumza nae Tarehe 2 mwezi February na kunipa ahadi hiyo,nikawa naendelea kumtafuta ili kunipa mrejesho kama amefikia wapi. Na katika hatua hiyo alipokea simu mara tatu akisema yupo busy na kazi na ameshindwa kufika dukani atakwenda siku inayofuatia.

Hili jambo likanipa mashaka sana kwasababu haiwezekani zipite siku tatu mtu hajakwenda dukani kwake. Mara ya mwisho kuzungumza nae tarehe 7 February,aliniambia ndio anaelekea dukani tuwasiliane jioni au kesho anipe mrejesho. Nilipiga simu jioni kuanzia saa moja jioni hadi saa nne usiku simu haipokelewi.

Niliendelea kupiga simu siku iliyofuatia pia hakupokea siku nzima. Leo sasa ikabidi niende tu pale dukani. Nikawakuta vijana wake na kuongea nao ambapo walionesha ushirikiano mdogo na walionekana kama kunikwepa hivi. Ilibidi niwaamuru kumpigia boss wao sababu simu yangu hapokei wakampigia na kumuuliza kuhusu swala langu akawajibu tu kuwa yeye alishazungumza na mimi na ameshanipa mrejesho jambo ambalo si ukweli sababu amekuwa hapokei simu zangu.

Akawaambia kuwa tatizo la simu yangu ni kuwa imekufa display na hiyo ndio ripoti ya fundi. Nikamwambia amuulize sasa nini kinatakiwa kufanyika sasa, akamwambia kuwa inatakiwa kununuliwa display yaani kioo kipya kwa gharama za mteja sababu warrant yao haibebi gharama ya manunuzi ya kioo kipya.

Sasa nikauliza kwa huyu muhudumu, mimi nahusika vipi na kununua kioo kipya cha simu wakati sijafahamu hata chanzo cha hiyo damage simu imezima tu bila sababu as if ilikuwa imekwisha chaji?

Sijawahi kuidondosha wala kuigonga wala kuipa damage yoyote,iwaje simu izime ghafla tu na kioo ndio kiwe tatizo?

Nikawaambia basi nitafutieni simu nyingine ambayo itareplace hii kwasababu mimi sijui hapa naanzia wapi ina maana nikiishia hapa na haya malekezo yenu tafsiri yake ni kuwa nilitoka nyumbani nikaja kununua simu kopo nikatupa pesa yangu then kirahisi tu niachane na hili swala liishie juu juu tu hivi?🤔

Wale vijana hawakuwa na majibu ya kunipa zaidi ya kusema "boss sisi hatuna maamuzi nje ya hapo maana mwenyewe ndio katupa hayo majibu".

Nimeondoka pale dukani nikiwa nimekasirika sana na kuchefukwa. Nimechukua ile simu ikiwa katika hali yake ya ubovu na kurudi home hadi hapa muda huu nawapa mrejesho hasira hazijaanisha.

Kioo kipya cha simu nimetazama hapa mitandaoni bei yake ni laki tano.

Kuna kitu kinaniambia huyu mwenye duka anajua anachokifanya. Hivi simu haijaanguka,haijagongwa popote,inakufaje kioo aisee?🤔

Sasa nataka nifanye maamuzi ya kupeleka hii kesi mahakamani ili tufanye kufuata taratibu za kisheria pengine yeye ataweza kuiambia mahakama kuwa ni kwa utaratibu upi simu inaweza kuzima tu halafu kioo kiwe ni tatizo then mteja ndie awajibishwe kwa tatizo ambalo sio physically inflicted kwenye hiyo simu?

Ni bora ningekuwa nimeidondosha au hata imeweka crack mtu anaweza sema ni sababu,yaani kioo hakiwaki kabisa na simu ukibonyeza power button inafanya kuvibrate bila reaction yoyote kwenye kioo sio mwanga waka kuonyesha chochote.

Hii kitu imenifundisha sana na kunipa umakini kimsingi kuanzia sasa sitathubutu kununua simu yoyote used au refurbished sababu naona kuna elements za utapeli na kukwepa kuwajibika kwa baadhi ya wauzaji ambao si waaminifu.
Halafu ukaamua kuwaacha wakutapeli kienyeji hivyo? Au kuna hatua utazifuata kupata haki yako?
 
Back
Top Bottom