Wadau wa JF, ni Mkono/Mguu wa Kulia au wa Kuume?

Wadau wa JF, ni Mkono/Mguu wa Kulia au wa Kuume?

Kichankuli

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2008
Posts
887
Reaction score
190
Watanzania tunaaminika kuwa ndiyo wenye asili ya Lugha ya Kiswahili. Lakini kuna maneno mengi ambayo tumekuwa tukiyatumia isivyostahili. Mathalan, ni lipi jina sahihi la mkono ambao wengi wetu huwa tunautumia sana kama kiongozi wa shughuli zinazofanywa na miili yetu, je ni mkono wa kuume au wa kulia?.

Ningependa nipate maoni yenu wadau wa JF kabla na mimi sijatoa yakwangu ninayoyafikiria. Uwanja ni wenu
 
Watanzania tunaaminika kuwa ndiyo wenye asili ya Lugha ya Kiswahili. Lakini kuna maneno mengi ambayo tumekuwa tukiyatumia isivyostahili. Mathalan, ni lipi jina sahihi la mkono ambao wengi wetu huwa tunautumia sana kama kiongozi wa shughuli zinazofanywa na miili yetu, je ni mkono wa kuume au wa kulia?.

Ningependa nipate maoni yenu wadau wa JF kabla na mimi sijatoa yakwangu ninayoyafikiria. Uwanja ni wenu

Kichankuli... Ni che mosi?

Majibu yote ni sahihi... Kwani Kandili na taa si kitu kilekile?
 
Watanzania tunaaminika kuwa ndiyo wenye asili ya Lugha ya Kiswahili. Lakini kuna maneno mengi ambayo tumekuwa tukiyatumia isivyostahili. Mathalan, ni lipi jina sahihi la mkono ambao wengi wetu huwa tunautumia sana kama kiongozi wa shughuli zinazofanywa na miili yetu, je ni mkono wa kuume au wa kulia?.

Ningependa nipate maoni yenu wadau wa JF kabla na mimi sijatoa yakwangu ninayoyafikiria. Uwanja ni wenu

Yanaashiria maana moja lakini matumizi yake hutegemea sana muktaza (context). Kwa mfano nadhani si sahihi kusema 'mkono wa kuume'; sahihi ni 'mkono wa kulia'. Vivyo hivyo si sahihi kusema 'upande wa kulia'; bali 'upande wa kuume'.
 
Fikra zangu zinanituma kwamba usahihi ni mkono/mguu kuitwa wa kuume. Aidha fikra zangu zinanieleza kwamba matumizi yaliyozoeleka sana ya kuuita mkono wa kulia yanatokana na desturi za Kiafrika kwamba mkono wa kuume ndiyo haswa makhsusi kwaajili ya kuchukua, kusafirisha na kukitia mdomoni chakula. hebu angalia sentensi hizi:
1: Chumba cha kulia chakula
2: Meza ya kulia chakula
3: Kijiko cha kulia Ubwabwa
4: Mboga za kulia chakula cha jioni
5: Sahani ya kulia makande

Sasa mkono wa kulia chakula ni upi? kwa waafrika ndo mkono wa kiume; kwa wazungu ambao wanatumia mikono yote, wakati mwingine, huku uma na huku kisu sijui jibu litakuwa lipo
 
Yanaashiria maana moja lakini matumizi yake hutegemea sana muktaza (context). Kwa mfano nadhani si sahihi kusema 'mkono wa kuume'; sahihi ni 'mkono wa kulia'. Vivyo hivyo si sahihi kusema 'upande wa kulia'; bali 'upande wa kuume'.

Kama alivyosema mkuu SMU hapo juu yote ni sawa lakini matumizi yake hutegemea zaidi muktadha,ie jinsi(lengo) unavyotaka kulitumia neno husika(angalia mfano wa SMU hapo juu)
 
Yanaashiria maana moja lakini matumizi yake hutegemea sana muktaza (context). Kwa mfano nadhani si sahihi kusema 'mkono wa kuume'; sahihi ni 'mkono wa kulia'. Vivyo hivyo si sahihi kusema 'upande wa kulia'; bali 'upande wa kuume'.

upande wa kuume nimesikia leo hii (MALI MPYA) mkono wa kuume ndio kawaida.
 
Back
Top Bottom