Tetesi: WADUDU ni hatari: Chukua tahadhari unapokuja mapumziko maeneo ya Moshi na Arusha

Tetesi: WADUDU ni hatari: Chukua tahadhari unapokuja mapumziko maeneo ya Moshi na Arusha

Mgeni wa Jiji

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2017
Posts
9,758
Reaction score
18,431
Habari Wakuu wa JF,

Niende moja kwa moja kwenye mada. Hii itaweza kuwa msaada kwa ndugu zetu wanaopanga kuja likizo ya sikukuu za mwisho wa mwaka maeneo ya Arusha na Moshi.

Kuna mambo kadhaa ni muhimu kuweza kuyajua hasa kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri (magari) na wale wanaopendelea kwenda maeneo ya starehe nyakati za usiku.

Umewahi kusikia kuhusu kundi la vijana wanaojiita WADUDU?, basi ndugu yangu hili ni kundi hatari zaidi la vijana wanaojihusisha na mambo mengi kwa ukanda wa kaskazini. Achana na wale unaowaona kwenye mitandao ya kijamii.wakiwa na viongozi wa kiserikali.

Wale naweza kukwambia kuwa wale sio WADUDU wenyewe.

Sasa ndugu yangu ukija ukanda huu wa kaskazini inakupasa kuishi kwa tahadhari sana hasa nyakati za jioni, usiku, asubuhi na nyakati zote uwapo barabarani.

Ngoja nikupe picha ya namna rahisi ya kuwatambua.hawa ni WADUDU.

Kwanza ukikutana na piki piki mara nyingi huwa kwenye makundi, mbili na zaidi zinakimbia sana inawasha taa ya spot mchana na wamepakizana vijana wawili au watatu. Jua hapa nimekutana na WADUDU kama unaweza wapishe wapite usitake kuweka nao mashindano, kuna hatari kubwa ya kuharibiwa gari lako na hutawakamata.

Kwa haraka mtu anaweza kusema labda mmewalea hao WADUDU. Ni kweli kuna.uzembe mkubwa umefanyika kuanzia jamii hadi vyombo vinavyolinda raia na mali zao.

Sasa kwanini nilisema uwapishe sababu kuna hatari ukaharibiwa gari lako na usalama wako kuwa mdogo sana.

Hawa viumbe kwanza wanakuwa wamelewa na sio ajabu ukawakuta wanatafuna mirungi na kuvuta bangi wazi wazi, wapo na sime au mapanga, rungu zile za kimasai, minyororo yenye kufuli au mipini ya jembe.

Sasa wanavyokuwa spidi njiani na wamewasha hizo taa wakihisi umewaziba ni ama wapige gari lako na hivyo walivyovibeba au wakuzibe njia na kukufanyia uhalifu wa ajabu hasa kwa usiku.

Bara bara za kuwa makini sana ni barabara ya Moshi Arusha naweza kusema hiyo bara bara hazipiti dakika 10 hawajapita WADUDU.

Tukiacha haya ya bara barani sasa tuangalie ya usiku.

Kwanza usiende sehemu ya starehe usiyoijua na ikitokea ukaenda basi hakikisha upo na mwenyeji au kama upo mwenyewe wahi kuondoka na ukiondoka ondoka kwa tahadhari sana.

Kamwe usipishane kauli na mtu maeneo ya starehe, kama utani unaweza ukapoteza uhai wako hivi hivi ukiona.

Kama itatokea umetoka sehemu ya starehe usiku ukahisi kuna piki piki zinakufuata basi jua upo mtegoni, ikitokea piki piki ikaja mbele yako kamwe usijaribu kusimama wala usisimame.

Ukiwa unajua unapoelekea hakuna watu basi usiende huko bali badili safari elekea ama kituo cha polisi au sehemu yenye watu maana hapo wanakutegea ufike unapoenda wafanye uhalifu wao.

Visa ni vingi sana hivyo ni muhimu ndugu zangu muwe na hiyo tahadhari.

Niwatakie maandalizi mema ya sikukuu za mwisho wa mwaka.
 
hawana lolote, was*nge tu hao! juzi tu hapa nimekuja hom nikalaza kausafiri kangu mgombani, kwasababu hom hakuna geti, eti asubuhi nakutana na machalii wadudu km wa5 hivi, wananiambia braza D vp, tumeona pira lako ila tukala bati hatukutaka kulidhuru kwa7bu ww tunakufaham ni bro wetu wa kitaa long https://jamii.app/JFUserGuide... Sema nn kamilot! fanya ata kaki ase tukashtue kwa mma babuu, nikawambia mm mwenyewe mdudu mstaafu, acheni hizo machalii zangu tafuteni mishe za maana, nikawahurumia tu kutokana na hali zao nikawapa teni. ni watoto wadogo sana kiumri, ila tuwaelimishe tu wataelewa.
 
hawana lolote, was*nge tu hao! juzi tu hapa nimekuja hom nikalaza kausafiri kangu mgombani, kwasababu hom hakuna geti, eti asubuhi nakutana na machalii wadudu km wa5 hivi, wananiambia braza D vp, tumeona pira lako ila tukala bati hatukutaka kulidhuru kwa7bu ww tunakufaham ni bro wetu wa kitaa long JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala... Sema nn kamilot! fanya ata kaki ase tukashtue kwa mma babuu, nikawambia mm mwenyewe mdudu mstaafu, acheni hizo machalii zangu tafuteni mishe za maana, nikawahurumia tu kutokana na hali zao nikawapa teni. ni watoto wadogo sana kiumri, ila tuwaelimishe tu wataelewa.
Niamini mimi hao sio WADUDU bali watoto vibaka tu wa mtaani. MDUDU hawezi kukuomba elfu 5 hata siku moja. Na MDUDU huwezi mkuta na mishe mishe za mtaani kwao.

MDUDU utamkuta barabarani spidi ama anafuata mzigo au anawaisha mzigo. Na hapo ndipo tatizo lilipo hawezi kukubali uwe kizingiti kwake kirahisi rahisi.

Ufahamu utasaidia sana namna yakuepuka na kujilinda.

Fikiri tu hao vibaka wa mtaani kwenu wameacha sababu wanakujua wewe ni home boy, waza wasingekuwa wanakujua, sahizi ungeshakula hasara tayari.

Ila bado, tahadhari izingatiwe.
 
Mkuu kwa hii reply ni wazi hujui unachokiongea kiongozi.
Arusha naendaga nakunywa bia natoka bar saa 8, na sikutani na hao wadudu
Arusha Kuna amani kabisa

Tuishi kiume piga mazoezi kaza mwili
Tembea na Beto muda wote
Tusikubali unyonge eti wadudu sijui Nini,
Yaani kidume unazuzuliwa na vibaka wa Arusha
 
Arusha naendaga nakunywa bia natoka bar saa 8, na sikutani na hao wadudu
Arusha Kuna amani kabisa

Tuishi kiume piga mazoezi kaza mwili
Tembea na Beto muda wote
Tusikubali unyonge eti wadudu sijui Nini,
Yaani kidume unazuzuliwa na vibaka wa Arusha
Uongo na ubishi havisaidii kitu Mkuu. Muhimu ni wanaokuja likizo wawe na tahadhari, wajue hali ilivyo.

Tuishie hapo kiongozi.
 
Uongo na ubishi havisaidii kitu Mkuu. Muhimu ni wanaokuja likizo wawe na tahadhari, wajue hali ilivyo.

Tuishie hapo kiongozi.
We muoga tu
Yaani Mtanzania aogope vibaka kwenye nchi yake
Arusha wanaenda wageni wengi na amani ipo, we Mtanzania unaogopaje vibaka
 
Habari Wakuu wa JF,

Niende moja kwa moja kwenye mada. Hii itaweza kuwa msaada kwa ndugu zetu wanaopanga kuja likizo ya sikukuu za mwisho wa mwaka maeneo ya Arusha na Moshi.

Kuna mambo kadhaa ni muhimu kuweza kuyajua hasa kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri (magari) na wale wanaopendelea kwenda maeneo ya starehe nyakati za usiku.

Umewahi kusikia kuhusu kundi la vijana wanaojiita WADUDU?, basi ndugu yangu hili ni kundi hatari zaidi la vijana wanaojihusisha na mambo mengi kwa ukanda wa kaskazini. Achana na wale unaowaona kwenye mitandao ya kijamii.wakiwa na viongozi wa kiserikali.

Wale naweza kukwambia kuwa wale sio WADUDU wenyewe.

Sasa ndugu yangu ukija ukanda huu wa kaskazini inakupasa kuishi kwa tahadhari sana hasa nyakati za jioni, usiku, asubuhi na nyakati zote uwapo barabarani.

Ngoja nikupe picha ya namna rahisi ya kuwatambua.hawa ni WADUDU.

Kwanza ukikutana na piki piki mara nyingi huwa kwenye makundi, mbili na zaidi zinakimbia sana inawasha taa ya spot mchana na wamepakizana vijana wawili au watatu. Jua hapa nimekutana na WADUDU kama unaweza wapishe wapite usitake kuweka nao mashindano, kuna hatari kubwa ya kuharibiwa gari lako na hutawakamata.

Kwa haraka mtu anaweza kusema labda mmewalea hao WADUDU. Ni kweli kuna.uzembe mkubwa umefanyika kuanzia jamii hadi vyombo vinavyolinda raia na mali zao.

Sasa kwanini nilisema uwapishe sababu kuna hatari ukaharibiwa gari lako na usalama wako kuwa mdogo sana.

Hawa viumbe kwanza wanakuwa wamelewa na sio ajabu ukawakuta wanatafuna mirungi na kuvuta bangi wazi wazi, wapo na sime au mapanga, rungu zile za kimasai, minyororo yenye kufuli au mipini ya jembe.

Sasa wanavyokuwa spidi njiani na wamewasha hizo taa wakihisi umewaziba ni ama wapige gari lako na hivyo walivyovibeba au wakuzibe njia na kukufanyia uhalifu wa ajabu hasa kwa usiku.

Bara bara za kuwa makini sana ni barabara ya Moshi Arusha naweza kusema hiyo bara bara hazipiti dakika 10 hawajapita WADUDU.

Tukiacha haya ya bara barani sasa tuangalie ya usiku.

Kwanza usiende sehemu ya starehe usiyoijua na ikitokea ukaenda basi hakikisha upo na mwenyeji au kama upo mwenyewe wahi kuondoka na ukiondoka ondoka kwa tahadhari sana.

Kamwe usipishane kauli na mtu maeneo ya starehe, kama utani unaweza ukapoteza uhai wako hivi hivi ukiona.

Kama itatokea umetoka sehemu ya starehe usiku ukahisi kuna piki piki zinakufuata basi jua upo mtegoni, ikitokea piki piki ikaja mbele yako kamwe usijaribu kusimama wala usisimame.

Ukiwa unajua unapoelekea hakuna watu basi usiende huko bali badili safari elekea ama kituo cha polisi au sehemu yenye watu maana hapo wanakutegea ufike unapoenda wafanye uhalifu wao.

Visa ni vingi sana hivyo ni muhimu ndugu zangu muwe na hiyo tahadhari.

Niwatakie maandalizi mema ya sikukuu za mwisho wa mwaka.
Bado unaishi ile miaka ya 1960, ile miaka ambayo watu walikuwa wanahamasishana kuogopa wahalifu? Mtu au kikundi cha watu kikiwa ni cha wahalifu, watu wanahamasishana kuwaogopa na kijihadhari nao utadhani ni wale nyumbu wa Manyara wanaelezana juu ya simba. Huu ni ujinga wa hali ya juu. Wahalifu wanatakiwa waogope raia wema na siyo raia wema waogope wahalifu.
 
Bado unaishi ile miaka ya 1960, ile miaka ambayo watu walikuwa wanahamasishana kuogopa wahalifu? Mtu au kikundi cha watu kikiwa ni cha wahalifu, watu wanahamasishana kuwaogopa na kijihadhari nao utadhani ni wale nyumbu wa Manyara wanaelezana juu ya simba. Huu ni ujinga wa hali ya juu. Wahalifu wanatakiwa waogope raia wema na siyo raia wema waogope wahalifu.
Kwanini ukilala unafunga milango?, kwanini simu yako unaiweka mfukoni?, kwanini gari lako ukishuka unafunga milango?.

Unafanya hayo ili kujikinga na uhalifu na unajikinga na uhalifu sababu unauogopa uhalifu na waalifu.

Fikiria kabla yakujibu Mkuu.
 
Serikali imewalea sana hao mbwa wanaojiita wadudu badala ya kuwasaidia vijana wasizidi kupotelea kwenye huo upumbavu ndio kwanzaaa makonda anafurahi nao na hawajali kwa sababu madhara yanayo letwa na hao mbwa hayazigusi familia zao na mslahi yao
 
Back
Top Bottom