MURUSI
JF-Expert Member
- Jun 25, 2013
- 4,537
- 8,824
Utapia mloa ni changamoto kubwa sana Tanzania, na utapia mloa ni ukosefu wa virutubiaho muhimu mwilini hasa sana Protein. Utapia Mlo ni ugonjwa wa Aibu kubwa sana hivyo ni lazima tuchukue hatua sasa.
MWaka 2023 Wakati Raisi Samia akizima Mwenge kule Babati Manyara alikili kwamba Pamoja na na jitihada kubwa za Serikali kupambana na utapia mlo Tanzania bado tatizo ni kubwa sana.
Mikoa yenye kiwango cha juu cha cha utapiamlo ni;
Iringa, Njombe, Rukwa, Geita, Ruvuma, Kagera, Simiyu, Tabora, Katavi, Manyara, Songwe na Mbeya.
KWa mujibu wa Twaweza Tanzania hupoteza Watoto 43,000 kila mwaka kutokana na utapia mlo.
Nini kinasababisha utapia mlo?
Sababu kubwa hapa ni moja tu Umasikini ambao hupelekea jamii kuto mudu kuwapatia watoto chakula Bora au Chakula chenye virutubisho hasa Protein na kujikuta watoto wanapewa chakula cha wanga wakati wote hivyo kudumaa na hata kupoteza maisha pia.
Wadudu Protein(Edble Insects) ni wapi?
Hawa ni wadudu ambao wanaweza kutupatia Protein na virutubisho vingine na ambao wanapatikana kwenye mazingira yetu.
Wadudu hao ni kama vile,Panzi,Senene,Crickets na Kumbikumbi.
Kumbikumbi; Picha kwa mujibu wa mtandao.
Senene; Chanzo cha picha ni Wikipedia.
Nini kifanyike?
Wadau mbalimbali ikiwemo Serikali ihamasishe sana uvunaji wa hawa wadudu; Wavunwe kwa wingi ili wasaidie katika swala zima la lishe. Hawa wadudu wapo mitaani wamejaa na sana wengi wanakuwepo wakati wa mvua nyingi.
Ni sehemu chache sana ambako hawa wadudu wanavunwa hasa Kanda ya Ziwa, Mikoa ya magharibi kama Kigoma.
Elimu ya matumizi ya hawa wadudu.
Bado pamoja na kwamba wanavunwa kwa kiwango kidogo sana, ila matumizi yake bado hayajajullikana sana, wengi huokota na kwenda kuuza au kula kama wanavyo kula Karanga,kumbe wanaweza vunwa wakakaushwa na kuchanganywa kwenye unga wa Ugari au Uji kwa ajili ya watoto
Unga wa Senene,Panzi,Kumbikumbi, na Criket unaweza changanywa pamoja na unga wa ngano kwa ajili kupikia Mandazi,Chapati,au unga wa mchele kwa ajili ya kupikia Vitumbua pia.
Unga wa Panzi: Picha kwa mujibu wa Mtandao.
Wadudu hawa wamekuwepo sana, kabla hata ya ujio vyakula vya kigeni amnavyo asilimia kubwa havima virutubisho na ni hatari sana.
Tuanze sasa kuangalia namna tunaweza punguza utapia mlo kwa kuwekeza sana kwenye wadudu hawa ambao kwanza ukiachana na Protein ila pia watatusaidia kuhifadhi mazingira.Hatutahitaji kufyeka mapori ili kulima Protein.
Wadudu hawa ni zawadi kutoka kwa Mungu tunaweza wapata Bure kabisa endapo tutahamasisha uvunaji wake.
Wadudu hawa ni salama, ni Chakula salama walicho kula Babu zetu kabla ya ujio wa Wakoloni.
Picha kwa mujibu wa mtandao.
Tukiamua tunaweza maliza utapia mloa kwa watoto kwa njia rahisi sana na rafiki kwa mazingira.
MWaka 2023 Wakati Raisi Samia akizima Mwenge kule Babati Manyara alikili kwamba Pamoja na na jitihada kubwa za Serikali kupambana na utapia mlo Tanzania bado tatizo ni kubwa sana.
Mikoa yenye kiwango cha juu cha cha utapiamlo ni;
Iringa, Njombe, Rukwa, Geita, Ruvuma, Kagera, Simiyu, Tabora, Katavi, Manyara, Songwe na Mbeya.
KWa mujibu wa Twaweza Tanzania hupoteza Watoto 43,000 kila mwaka kutokana na utapia mlo.
Nini kinasababisha utapia mlo?
Sababu kubwa hapa ni moja tu Umasikini ambao hupelekea jamii kuto mudu kuwapatia watoto chakula Bora au Chakula chenye virutubisho hasa Protein na kujikuta watoto wanapewa chakula cha wanga wakati wote hivyo kudumaa na hata kupoteza maisha pia.
Wadudu Protein(Edble Insects) ni wapi?
Hawa ni wadudu ambao wanaweza kutupatia Protein na virutubisho vingine na ambao wanapatikana kwenye mazingira yetu.
Wadudu hao ni kama vile,Panzi,Senene,Crickets na Kumbikumbi.
Kumbikumbi; Picha kwa mujibu wa mtandao.
Senene; Chanzo cha picha ni Wikipedia.
Nini kifanyike?
Wadau mbalimbali ikiwemo Serikali ihamasishe sana uvunaji wa hawa wadudu; Wavunwe kwa wingi ili wasaidie katika swala zima la lishe. Hawa wadudu wapo mitaani wamejaa na sana wengi wanakuwepo wakati wa mvua nyingi.
Ni sehemu chache sana ambako hawa wadudu wanavunwa hasa Kanda ya Ziwa, Mikoa ya magharibi kama Kigoma.
Elimu ya matumizi ya hawa wadudu.
Bado pamoja na kwamba wanavunwa kwa kiwango kidogo sana, ila matumizi yake bado hayajajullikana sana, wengi huokota na kwenda kuuza au kula kama wanavyo kula Karanga,kumbe wanaweza vunwa wakakaushwa na kuchanganywa kwenye unga wa Ugari au Uji kwa ajili ya watoto
Unga wa Senene,Panzi,Kumbikumbi, na Criket unaweza changanywa pamoja na unga wa ngano kwa ajili kupikia Mandazi,Chapati,au unga wa mchele kwa ajili ya kupikia Vitumbua pia.
Unga wa Panzi: Picha kwa mujibu wa Mtandao.
Wadudu hawa wamekuwepo sana, kabla hata ya ujio vyakula vya kigeni amnavyo asilimia kubwa havima virutubisho na ni hatari sana.
Tuanze sasa kuangalia namna tunaweza punguza utapia mlo kwa kuwekeza sana kwenye wadudu hawa ambao kwanza ukiachana na Protein ila pia watatusaidia kuhifadhi mazingira.Hatutahitaji kufyeka mapori ili kulima Protein.
Wadudu hawa ni zawadi kutoka kwa Mungu tunaweza wapata Bure kabisa endapo tutahamasisha uvunaji wake.
Wadudu hawa ni salama, ni Chakula salama walicho kula Babu zetu kabla ya ujio wa Wakoloni.
Picha kwa mujibu wa mtandao.
Tukiamua tunaweza maliza utapia mloa kwa watoto kwa njia rahisi sana na rafiki kwa mazingira.
Attachments
Upvote
6