Wafahamu macelebrity wa JF na sifa zao

Wafahamu macelebrity wa JF na sifa zao

Niko JF tangu kitambo na wengi sana humu mmenikuta nishaijua hii mitaa sema sikua active sana kwenye huu mtandao pendwa ila katika kuishi humu nimegundua kuna watu wenye ushawishi sana humu JF sijui tuwaite Jelebrity au sio?!

Unakuta kuna raia umu hata wakicomment nukta watu wanamiminika kureply likes kibao. Kuna haja JF iwatambue hawa watu wapate verification ya account zao. Kuna watu ambao nyuzi zao ndo zinaongoza kwa kupata engagement achana na umaarufu wa uzi wa kula kimasihara.

Naomba niwatambue wafuatao kama watu wa nguvu sana humu jukwaani kutokana na mchango wao kupitia post zao, na ikiwezekana wajipost siku moja moja tuwajue, siku tukikutana nao mtaani tuwabless mbili tatu moyo uelee.

1. MSHANA JR: Namuonaga kama mtu fulani mwenye hekima sana kupitia thread zake, usizipite thread za huyu mwamba kama unataka kupata madini mbalimbali.

2. Mzabzab: Huyu mwamba matusi sana, yuko sana mitaa ya jukwaa la mahusiano kule. Uzi wa jukwaa la MMU bila comment ya huyu mwamba bado sana huo haujaenda mjini.

3. Gentamicine: Kama shabiki wa Chelsea na Simba huwa lazma nipitie jukwaaa la Sports na huyu jamaa anakiwasha sana uko na kutoa za ndani, though anaonekana raia hawamuelewi, mpikaji sana wa data.

4. Robert Heriel: Mzee wakuitwa Taikon wa Fasihi, mwamba anatoa zile ngumu kumeza. Yaani kupitia misimamo yake so huwa siwezi kupita uzi aliyouanzisha huyu jamaa.

5. Rikiboy: Mzee wa uzi wa kula kimasihara, yaan jamaa katoa hit song moja ya kudumu mpaka mwisho wa hii app. Moja ya uzi ambao uko active mda wote, washatokea watumishi na wahubiri wakashindwa kuuzuia.

6: Sky Eclat: Yuko JF since 2012, namuona kama Lady Jay Dee wa humu JF. Huyu madam nawish nimuone yukoje

Toa appreciation zako kwa wana JF wengine unaowakubali, ambao wanafanya vizuri.[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji115][emoji115]
Chai
 
Back
Top Bottom