Wafahamu waarabu/usiyoyajua kuhusu waarabu

Wafahamu waarabu/usiyoyajua kuhusu waarabu

Ushahidi upi uliokuwa nao kuwa mababu zenu wamefanywa watumwa na waarabu? Sijui mnakuwa mnajitoa akili au ndio chuki zenu mkikosa la kusema! 😀 😀 😀 Nyerere aliwaambia wanawake wanafagilishwa barabara unguja kwa maziwa au nani kawafundisha mambo haya? Sio nyinyi mliokuwa mkiwauza ndugu zenu vijijini kwa wazungu kisa unapewa kioo ujitizame?

Nianze kukupangia kila nchi na Colonial Master wake akisha tutajua nani kashamiri kwa biashara ya utumwa?

Mwarabu katoka Oman kaja Zanzibar Enzi hizo, kufika tu, kaifanya Zanzibar Mji mkuu wa Oman. Ivi unaweza kunambia taifa gani limefanya ivo kwa Afrika zaidi ya kuwadharau tu? Nyie na CCM ya Zanzibar mkieneza chuki dhidi ya Waarabu, lakini walivokuja na meli yao kina Balozi wakafunga bandari hamna kazi kuwapisha waarabu waingie, mnajifanya watumwa kabla ya kutumwa 😀
Huenda ni kweli Japo nami niliaminishwa hivyo shule, lakin hata ukiangalia vitabu vya history picha nyingi za warabu ni zakuchora tu. Ila wazumgu ni picha kabisa zilizopigwa na camera. So, huenda ni kweli na bado natamani kujua zaidi black and white kuhusu wahusika wa utumwa baina ya warabu na Wazungu.
 
mkuu Kilawo na tupo wengi tu kaka. Jirani zangu hapo mama yao alikuwa mtumwa kutoka kilwa. Aliolewa na Muarabu na watoto wakabahatika kwenda shule mmoja wao ni Meneja wa Bank moja kubwa tu huku tulipo ni juzi tu nimetoka kula futari kwenye villa yake. Mwegine ni mchezaji mpira analipwa fedha ndefu na ako na maisha mazuri sana tu. Mkuu Kilawo hizi huwa ni dhana tu za watu wanazipata kupitia vitabu tu lakini ukweli ndio huo. Wapo walioowa na kuolewa ingawa inawezekana ni kwa idadi ndogo lakini wapo.
 
Huenda ni kweli Japo nami niliaminishwa hivyo shule, lakin hata ukiangalia vitabu vya history picha nyingi za warabu ni zakuchora tu. Ila wazumgu ni picha kabisa zilizopigwa na camera. So, huenda ni kweli na bado natamani kujua zaidi black and white kuhusu wahusika wa utumwa baina ya warabu na Wazungu.
Mashuleni wanafundisha Historia kupitia story ambayo Serikali inataka iwe. Lakini ukweli utabaki kuwa ukweli tu, aliekuwa akiuza na kununua watumwa ndio hao hao wazungu wanaoabudiwa leo na kuonekana wa maana. Wamekuja Afrika wakafisidi rasilimali zetu, wakawachukuwa waafrika na kwenda kuwatuma marekani mashambani. Mwarabu kaja hata hakufika mbali, kaishia Lamu hapo basi tena utakuta story zinavozungumzwa kumfanya muarabu aonekane kinara wa utumwa, watu hata hawafikirii, kinara wa utumwa ata Uganda hajafika? Je wale waliotawala Afrika Nzima wao watakuwa nani? Tusirudi nyuma sana, SA tu apo si juzi jamaa katiwa kwenye shimo la mavi na wazungu?

Mwarabu kaja Zanzibar, kapapenda, akaleta Maendeleo, TV channel ya Kwanza Zanzibar, Taa barabarani kabla New york ni Zanzibar, Gorofa EA nzima ni Zanzibar, Mifereji majumbani kwanza Zanzibar, Zanzibar hio hio ilikuwa ikitoa misaada kwa uingereze wakati wa Vita, Leo eti wanasema Mwarabu kinara wa utumwa, Utumwa huo kamtuma nani? Hebu na waje waniambie, mwarabu kaondoka Zanzibar au Afrika na rasilimali gani? Karafuu zenyewe pemba kazileta Mwarabu kutoka bara la Asia uko.

Waniambie rasilimali waliowapokonya waafrika hawa waarabu ni ipi kiasi kwamba waitwe vinara wa utumwa?

Mpaka Kesho Afrika inaibiwa rasilimali na Wazungu, nenda Congo tu apo uone ukoloni wa mamboleo!

Walisema kuwa Beit Al Aab (house of Wonder) Nguzo zake zilijengwa kwa vichwa vya watumwa. Mungu Kawadhalilisha lile jengo miaka michache nyuma liliporomoka Nguzo, hakuna ata kipande cha mfupa wa kuku. Zile zama za kudanganywa zimekwisha, siku izi mambo yapo wazi!

Walisema Bi Khole alikuwa analala na mtumwa kila siku akisha anamkata uume wake..... Ukiwauliza ushahidi hawana! Wapo kuchafua historia ya watu tu, wanataka tuamini kuwa utawala wa kisultani ulikuwa wa kidhulma, huu wa saivi tuuite vipi basi? Zanzibar ipo nyuma kwenye kila kitu.
 
Habari zenu watu wa JF..

Leo tupate kujua kidogo kuhusiana na hawa watu tunaowaita "Waarabu"...Nimepitia pitia kidogo nchi zao na pia kusoma vitabu vyao vinavyoelezea maisha yao...haya yafuatayo ndio niliopata kuyafahamu kutoka kwa "waarabu":-

1.Neno "uarabu"-"arab" ni neno linalowakilisha asili/tamaduni/culture na sio rangi kama wengi tujuavyo.

2.Duniani kuna nchi 22 za kiarabu,yani waishipo waarabu nazo ni-Lebanon,Syria,Morocco,misri,Tunisia,Iran,iraq,Jordan,kuwait,Qatar,Saudi arabia,Somalia,Djibouti,Comoro,Sudan,Palestina,Mauritania,Algeria,Oman,UAE,Bahrain na Yemen.

3.Waarabu wote sio Waislamu,Na Waislamu wote sio waarabu..ingawa kundi kubwa la waarabu ni waislamu,wachache sana ndio wakristo na Wayahudi.

4.Waarabu ni watu ambao wanawaheshimu sana Wazee na Watawala wao...Ni mwiko sana kukosoa,kudhihaki na hata kumfokea mtu aliyekuzidi umri au aliye mtawala wako.Wana Heshima yenye hofu kubwa yaweza ikawa kuliko taifa zingine zote.

5.Sio Mataifa yote ya kiarabu vazi lao la utamaduni ni kanzu,la hasha,bali yapo mataifa ya kiarabu ni nadra sana kumuona mtu kavaa kanzu nayo ni mojawapo Syria,Misri na Lebanon.

6.Kwenye Lugha ya kiarabu,lugha/ishara ya mwili(body language) ni kitu muhimu sana kuliko hata maongezi yenyewe..Pata muda tizama clips zao.

7.Lugha ya kiarabu ni miongoni mwa lugha inayozungumzwa kwa mfanano karibia mataifa yote ya kiarabu...mfano kwenye kiingereza kuna kiingereza cha wales,australia,marekani n.k

8.Sifa kubwa ya waarabu katika ulaji chakula ni "kutumia mkono" yaani no kijiko no uma..hata awe tajiri kiasi gani dhana yake ya kwanza kwenye kula ni "mkono wake"..Hii imepelekea kupenda kuwa na hotel/migahawa yao mahsusi.

9.Ukiwa kwenye mkutano/meeting ni mwiko kutizama saa iwe ukutani au mkononi,ukifanya hivyo ni ishara ya kuwadharau walioko kwenye mkutano.

10.Mahusiano ya kifamilia/undugu yana nguvu sana kwa waarabu..kwa mfano unaeza kuta nyumba moja wanaishi karibia ukoo/yani bibi wa bibi mpaka babu wa babu na wajukuu wake.

11.Umri hauna nafasi katika kujitegemea yani kuwa huru na makatazo au amri au huduma za wazazi..yani mtu anaweza akafika hata miaka 40 lakini akawa anahudumiwa na wazazi wake.

12.kwa kawaida uchukua zaidi ya mwaka na miezi saba kujua lugha ya kiarabu kwa ufasaha.

13.kinywaji kikubwa katika nchi za waarabu ni kahawa...

AHSANTENI NI HAYO TU YA KWANGU....MENGINE KUHUSU WAARABU NAHISI TUTAYAPATA KUTOKA KWA WACHANGIAJI...[emoji120]
Nimekuja mbiyo nikijua utazungumzia adhabu za kukata kichwa, kukata mikono na kuua kwa kuponda na mawe
 
Huenda ni kweli Japo nami niliaminishwa hivyo shule, lakin hata ukiangalia vitabu vya history picha nyingi za warabu ni zakuchora tu. Ila wazumgu ni picha kabisa zilizopigwa na camera. So, huenda ni kweli na bado natamani kujua zaidi black and white kuhusu wahusika wa utumwa baina ya warabu na Wazungu.
Mkuu nitakupa dokezo kwa swali lako.
1. Biashara ya Utumwa iliyofanyika Afrika Magharibi inaitwa WEST AFRICAN SLAVE TRADE
2. Biashara ya Utumwa iliyofanyika Africa Mashariki inaitwa EAST AFRICA ARAB SLAVE TRADE

Unapata hisia yoyote kwanini ile # 1 hamna neno European?? Ila kwenye hii # 2 neno Arab ni MUHIMU?? Ukiwaza vyema utajua.
 
Ushahidi upi uliokuwa nao kuwa mababu zenu wamefanywa watumwa na waarabu? Sijui mnakuwa mnajitoa akili au ndio chuki zenu mkikosa la kusema! 😀 😀 😀 Nyerere aliwaambia wanawake wanafagilishwa barabara unguja kwa maziwa au nani kawafundisha mambo haya? Sio nyinyi mliokuwa mkiwauza ndugu zenu vijijini kwa wazungu kisa unapewa kioo ujitizame?

Nianze kukupangia kila nchi na Colonial Master wake akisha tutajua nani kashamiri kwa biashara ya utumwa?

Mwarabu katoka Oman kaja Zanzibar Enzi hizo, kufika tu, kaifanya Zanzibar Mji mkuu wa Oman. Ivi unaweza kunambia taifa gani limefanya ivo kwa Afrika zaidi ya kuwadharau tu? Nyie na CCM ya Zanzibar mkieneza chuki dhidi ya Waarabu, lakini walivokuja na meli yao kina Balozi wakafunga bandari hamna kazi kuwapisha waarabu waingie, mnajifanya watumwa kabla ya kutumwa 😀
Acha ubishi usio naamaana wewe "" ..kutetea tetra ujinga tu ....""" Yule billali bin wabaa ...swahaba wa mtume ambaye alikuwa na asili ya Ethiopia alifikaje Makkah...wakati alikuwa mtumwa kule
 
Ushahidi upi uliokuwa nao kuwa mababu zenu wamefanywa watumwa na waarabu? Sijui mnakuwa mnajitoa akili au ndio chuki zenu mkikosa la kusema! 😀 😀 😀 Nyerere aliwaambia wanawake wanafagilishwa barabara unguja kwa maziwa au nani kawafundisha mambo haya? Sio nyinyi mliokuwa mkiwauza ndugu zenu vijijini kwa wazungu kisa unapewa kioo ujitizame?

Nianze kukupangia kila nchi na Colonial Master wake akisha tutajua nani kashamiri kwa biashara ya utumwa?

Mwarabu katoka Oman kaja Zanzibar Enzi hizo, kufika tu, kaifanya Zanzibar Mji mkuu wa Oman. Ivi unaweza kunambia taifa gani limefanya ivo kwa Afrika zaidi ya kuwadharau tu? Nyie na CCM ya Zanzibar mkieneza chuki dhidi ya Waarabu, lakini walivokuja na meli yao kina Balozi wakafunga bandari hamna kazi kuwapisha waarabu waingie, mnajifanya watumwa kabla ya kutumwa 😀
Too bad hujasoma Historia....kamsome Tippu tippu kwanza.
 
Acha ubishi usio naamaana wewe "" ..kutetea tetra ujinga tu ....""" Yule billali bin wabaa ...swahaba wa mtume ambaye alikuwa na asili ya Ethiopia alifikaje Makkah...wakati alikuwa mtumwa kule
Sijasema kuwa waarabu hawakufanya utumwa totally, waarabu hawakufanya utumwa kama mnavojidai. By the way, Who freed Bilal?
 
Too bad hujasoma Historia....kamsome Tippu tippu kwanza.
Historia mnayofundishwa mashuleni? Nimeisoma hio, lakini ndio yale yale nloyasema, ni historia ambayo Serikali inataka iwe hivo.

Tulifundishwa mashuleni kuwa House of Wonder Nguzo zake zimejengwa kwa vichwa vya watumwa ndio maana zile nguzo zipo very strong, miaka michache nyuma jumba liliporomoka upande mmoja, mfupa wa jogoo hamna ndani yake, saa bufur la hao watumwa liko wapi kwenye izo nguzo kama wanavofundisha watoto?
 
Historia mnayofundishwa mashuleni? Nimeisoma hio, lakini ndio yale yale nloyasema, ni historia ambayo Serikali inataka iwe hivo.

Tulifundishwa mashuleni kuwa House of Wonder Nguzo zake zimejengwa kwa vichwa vya watumwa ndio maana zile nguzo zipo very strong, miaka michache nyuma jumba liliporomoka upande mmoja, mfupa wa jogoo hamna ndani yake, saa bufur la hao watumwa liko wapi kwenye izo nguzo kama wanavofundisha watoto?
Pale kanisa la Anglican Mkunazini kuna caves zinaenda mpaka darajani na ndio ilikuwa njia ya kupitishia watumwa kuwaingiza kwenye majahazi ni nani alikuwa anafanya hiyo biashara?
 
Mkuu nitakupa dokezo kwa swali lako.
1. Biashara ya Utumwa iliyofanyika Afrika Magharibi inaitwa WEST AFRICAN SLAVE TRADE
2. Biashara ya Utumwa iliyofanyika Africa Mashariki inaitwa EAST AFRICA ARAB SLAVE TRADE

Unapata hisia yoyote kwanini ile # 1 hamna neno European?? Ila kwenye hii # 2 neno Arab ni MUHIMU?? Ukiwaza vyema utajua.
Nakuelewa! Ila mkuu naomba niambie, hao wazungu walipokua wakifanya hiyo biashara hapa EA, warabu walikua wameshaondoka? Ina maana hawakuhusika hata kidogo? Au walihusika lkn si kwanamna wanvyozungumzwa?
Kuna taarifa kuwa wao walikua madalali.
 
Nakuelewa! Ila mkuu naomba niambie, hao wazungu walipokua wakifanya hiyo biashara hapa EA, warabu walikua wameshaondoka? Ina maana hawakuhusika hata kidogo? Au walihusika lkn si kwanamna wanvyozungumzwa? Kuna taarifa kuwa wao walikua madalali.

Kwanza ieleweke hamna jamii ambayo inawza kujitoa kwenye lawama za biashara ya utumwa. Lakini inabidi kuelewa kuwa majina ya East Africa ARAB slave Trade dhidi ya West African Slave Trade ni mkakati wa wazungu hususan Wamissionary wa enzi zile kuwachora Waarabu kama kuwa ndio pekee waliokuwa wakifanya jambo hili. Wazungu WOTE waliokuja kutafuta vyanzo vya Nile au kuiona Milima na Maziwa kama Tanganyika walielekezwa na Waarabu hapo Unguja. Lakini HAMNA walipodiriki kulipa fadhila kwa kuwataja HAO waliowaelekeza.

Cha kukusaidia ni kwamba JIULIZE mbona pamoja na Waarabu kuwatangulia wazungu huku kwetu kwa miaka karibia 800, mbona HAMNA historia ya waarabu WAKIZIPIGA na wabantu?? Kwanini?? Kama kweli walihamisha wabantu wote kama watumwa (sisemi hawakufanya!!) mbona hamna mahali walizipiga?? Kuna mtu anapandikiza FITNA
 
Acha ubishi usio naamaana wewe "" ..kutetea tetra ujinga tu ....""" Yule billali bin wabaa ...swahaba wa mtume ambaye alikuwa na asili ya Ethiopia alifikaje Makkah...wakati alikuwa mtumwa kule
Du kumbe unamfahamu huyu Jamaa. Kweli alikuwa mtumwa. Ila Mtume Muhammad Akamkomboa kutoka utumwani ila wengi hutaka kuhusisha kuwa waislam ndio walikuwa wanawafanya watumwa.
 
Umeleza ilivyo vizur mno kama vile ccm kwa nje hujasema kwa ndani ila tuyaache hayo
 
Mashuleni wanafundisha Historia kupitia story ambayo Serikali inataka iwe. Lakini ukweli utabaki kuwa ukweli tu, aliekuwa akiuza na kununua watumwa ndio hao hao wazungu wanaoabudiwa leo na kuonekana wa maana. Wamekuja Afrika wakafisidi rasilimali zetu, wakawachukuwa waafrika na kwenda kuwatuma marekani mashambani. Mwarabu kaja hata hakufika mbali, kaishia Lamu hapo basi tena utakuta story zinavozungumzwa kumfanya muarabu aonekane kinara wa utumwa, watu hata hawafikirii, kinara wa utumwa ata Uganda hajafika? Je wale waliotawala Afrika Nzima wao watakuwa nani? Tusirudi nyuma sana, SA tu apo si juzi jamaa katiwa kwenye shimo la mavi na wazungu?

Mwarabu kaja Zanzibar, kapapenda, akaleta Maendeleo, TV channel ya Kwanza Zanzibar, Taa barabarani kabla New york ni Zanzibar, Gorofa EA nzima ni Zanzibar, Mifereji majumbani kwanza Zanzibar, Zanzibar hio hio ilikuwa ikitoa misaada kwa uingereze wakati wa Vita, Leo eti wanasema Mwarabu kinara wa utumwa, Utumwa huo kamtuma nani? Hebu na waje waniambie, mwarabu kaondoka Zanzibar au Afrika na rasilimali gani? Karafuu zenyewe pemba kazileta Mwarabu kutoka bara la Asia uko.

Waniambie rasilimali waliowapokonya waafrika hawa waarabu ni ipi kiasi kwamba waitwe vinara wa utumwa?

Mpaka Kesho Afrika inaibiwa rasilimali na Wazungu, nenda Congo tu apo uone ukoloni wa mamboleo!

Walisema kuwa Beit Al Aab (house of Wonder) Nguzo zake zilijengwa kwa vichwa vya watumwa. Mungu Kawadhalilisha lile jengo miaka michache nyuma liliporomoka Nguzo, hakuna ata kipande cha mfupa wa kuku. Zile zama za kudanganywa zimekwisha, siku izi mambo yapo wazi!

Walisema Bi Khole alikuwa analala na mtumwa kila siku akisha anamkata uume wake..... Ukiwauliza ushahidi hawana! Wapo kuchafua historia ya watu tu, wanataka tuamini kuwa utawala wa kisultani ulikuwa wa kidhulma, huu wa saivi tuuite vipi basi? Zanzibar ipo nyuma kwenye kila kitu.
Umekazania zanziba zanzibar zanzibar zanzibar...



Nakukumbusha pia Mwarabu pia Alipita Ujiji,kilwa,Kondoa,kilosa,Bagamoyo,tabora,nzega,Mtwara n.k


Sasa naomba hoja zako zijikite na hayo maeneo mengine.



Hiyo Zanzibar yenyewe Njaa tupu.
 
Back
Top Bottom