Wafanyabiashara Halali wa Mbagala wanawezaje kulipa kodi ikiwa Wamezibwa 100% na Wamachinga?

Wafanyabiashara Halali wa Mbagala wanawezaje kulipa kodi ikiwa Wamezibwa 100% na Wamachinga?

Bongo tunaishi kama mashetani. Maendeleo huwa yanakuja na vilio ni vyema Serikali ikapangilia miundombinu wakati huu kuliko kusubiri ongezeko liwe kubwa zaidi.

Kuna raha yake jiji likipangiliwa vizuri.
 
Kuna kariakoo pia Yani ni kero kabisaaa,Watu na majiko wanapika ugali,Wanakaanga chips,sambusa,mihogo,wanapika Tena chini ya transforma!!!
Bado wauza kahawa,mishikaki wanatembea na majiko yao ndani ndani kwenye maduka ktk maghorofa. Na zaid mavyakula yanauzwa hovyo watu wanaumwa tumbo na kuharisha(Nimeshuhudia na wengi nawajua inawatokea baada ya kula)

Yani kkoo kushakua Sasa ni pahovyo mnoo.
Ajabu mkuu wa mkoa na team yake wanashindwa kuona haya machache!Basi hebu wazibiti matumizi holela ya moto kkoo na hao machinga wawapange basi daah
 
Kkoo mtu chini ya transforma Tena mbele ya duka la mtu kaweka Banda la chipsi,anachoma mihogo,vitumbua.Usalama uko wapi namna hii?
Kweli ghafla moto ukamate,si wenye maduka washapoteza mali zao.
Mamlaka husika watolee macho,Bora wasisitize ujengaji wa migahawa na hotel ambazo wataeza kuzicontrol.
Naunga mkono wamachinga kujitafutia vipato vyao ila wapangwe vizuri na wamachinga wa upishi barabarani hapana kabisa
 
Uzuri wa Mbagala vitu ni bei chee, Kuna nyanya za 200, mboga mboga fungu 300, maisha ya kule ni rahisi mno
 
Nimepita Mbagala wiki hii nikielekea kwenye Shamba langu Mkuranga, Hakika Mbagala ni Nchi nyingine kabisa, Utaratibu wao wa kuishi ni tofauti kabisa na Utaratibu wa Tanzania.

Wamachinga wamepanga bidhaa kuanzia kwenye milango ya maduka ya watu hadi katikati ya Barabara bila wasiwasi wowote, Wala hawaogopi hata milango ya Benki! yaani ni kama Mbagala haina serikali yoyote ile na ni kama hakuna mgambo wala polisi, Kumbukeni hawa Wamachinga hawalipi kodi yoyote ile, Ugali wa Mama Lishe unasongewa barabarani na magari yanasubiri msongaji amalize ndio yapite, Hili kwangu ni jambo la Ajabu mno!

Marafiki zangu wa kihindi wanaofanya biashara eneo hilo nilipowahoji kuhusu hali hiyo wamenieleza kwamba wanatishwa kulogwa ikiwa watafanya kampeni yoyote ya kuwazuia walioziba Milango yao!

Taarifa za chini chini zinaeleza kwamba Meya wa Eneo hilo, ambaye anatajwa kutisha kwa Ushirikina ndiye mlinzi wa Kwanza wa mambo hayo, anaunga mkono kila uchafu wa Wamachinga bla kujali athari zake, Kimsingi Wafanyabiashara wa Mbagala wanachosubiri ni kudura za Mungu, Hali yao ni mbaya kuliko nilichoandika.
Chadema baada ya wamachinga kuwapiga chini Sasa mshawageuza maadui
 
Nimepita Mbagala wiki hii nikielekea kwenye Shamba langu Mkuranga, Hakika Mbagala ni Nchi nyingine kabisa, Utaratibu wao wa kuishi ni tofauti kabisa na Utaratibu wa Tanzania.

Wamachinga wamepanga bidhaa kuanzia kwenye milango ya maduka ya watu hadi katikati ya Barabara bila wasiwasi wowote, Wala hawaogopi hata milango ya Benki! yaani ni kama Mbagala haina serikali yoyote ile na ni kama hakuna mgambo wala polisi, Kumbukeni hawa Wamachinga hawalipi kodi yoyote ile, Ugali wa Mama Lishe unasongewa barabarani na magari yanasubiri msongaji amalize ndio yapite, Hili kwangu ni jambo la Ajabu mno!

Marafiki zangu wa kihindi wanaofanya biashara eneo hilo nilipowahoji kuhusu hali hiyo wamenieleza kwamba wanatishwa kulogwa ikiwa watafanya kampeni yoyote ya kuwazuia walioziba Milango yao!

Taarifa za chini chini zinaeleza kwamba Meya wa Eneo hilo, ambaye anatajwa kutisha kwa Ushirikina ndiye mlinzi wa Kwanza wa mambo hayo, anaunga mkono kila uchafu wa Wamachinga bla kujali athari zake, Kimsingi Wafanyabiashara wa Mbagala wanachosubiri ni kudura za Mungu, Hali yao ni mbaya kuliko nilichoandika.
Baada ya wewe kuandika haya utawasaidia kwa lipi!
 
Mkuu hebu jaribu siku moja kupita Mbagala, hakuna serikali kabisa!
Mbagala ni kero.
Usisahau na uhalifu upo hadharani, wale wa minada fake njia ya Chamanzi. Wanaonwa hawakamatwi.
Siwezi kulea mtoto wangu au kuishi huko Mbagala.
 
Kiukweli watanzania wengi tunalalamika viongozi hawafuati sheria ila sisi pia ni wavunjifu wakubwa. Hao machinga wakiondolewa kwa nguvu watalalamika kwa kutumia kisingizio cha unyonge na umaskini. Pia watapata watetezi wengi wakiwemo baadhi ya wapinzani. Serikali ifanye maamuzi magumu.
Serikali ime-collapse siku nyingi. Kipande kidogo cha serikali kilichobaki wima ni kile kinachohusika na uuaji, utesaji, ukandamizaji na propanda ili watawala wachache waendelee kufaidi. Iko siku kila mtu ataelewa maana ya maneno haya.
 
Back
Top Bottom