DOKEZO Wafanyabiashara Kibaha tunaishi kama digidigi, tunawakimbia Halmashauri ambao wanafunga maduka yetu

DOKEZO Wafanyabiashara Kibaha tunaishi kama digidigi, tunawakimbia Halmashauri ambao wanafunga maduka yetu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kufunga Biashara sio Solution.
kwa kawaida leseni ni funguo ya kuanza kufanya biashara, kama hauna solution ya kwanza ni kupatiwa elimu na kusajiliwa mara moja ila kama hautoi ushirikiano kinachofuata ni kufungiwa hiyo biashara yako lengo la elimu ni kukupa muongozo wa utendaji wa hiyo biashara na hata ukipata hiyo leseni ukikiuka masharti afisa anahaki ya kukunyang'anya hiyo leseni
 
kwa kawaida leseni ni funguo ya kuanza kufanya biashara, kama hauna solution ya kwanza ni kupatiwa elimu na kusajiliwa mara moja ila kama hautoi ushirikiano kinachofuata ni kufungiwa hiyo biashara yako lengo la elimu ni kukupa muongozo wa utendaji wa hiyo biashara na hata ukipata hiyo leseni ukikiuka masharti afisa anahaki ya kukunyang'anya hiyo leseni
Ukifungia Biashara hata hicho kidogo hupati hebu fikiria vizuri.
 
Halmashauri ya Kibaha Mjini imeanzisha oparesheni kamata kamata na kufunga biashara tangu wiki iliyopita.

Wanafika kwenye sehemu za biashara wakikuta unadaiwa kiasi chochote kile wanakutoa kwenye biashara yako, wanafunga na makufuli makubwa na kukutka kwenda kuchukua Control Number ili ulipie, kiwango kikianzia Tsh. 70,000

Oparesheni hiyo inafanyika kwenye maduka kuanzia maeneo ya Kibaha Mili Moja kupanda hadi Shule ya Maili Moja Msingi, Kwa Mang'umbi, Tankini hadi Mitaa ya Muheza.

Kinachoniuma ni kuona wanafungia hadi biashara ndogondogo, mtu ana kifremu chake anatakiwa kwenda kulipia, hawataki kusikia maelezo ya aina yoyote ile.

Kinachoendelea sasa ni Watu kufunga biashara zao, wakiwakwepa maafisa wa Halmashauri, hivi Rais Samia si alipiga marufuku hii staili ya kufunga biashara kisa tu mtu au watu wanadaiw kodi fulani ya Serikali au watasema yale ni maneno ya Kisiasa?

Hivi kwani si Rais Samia alisema hakuna kufunga biashara kwa sababu za mambo kama hayo, kwa nini hawawapi nafasi Wafanyabiashara wakajieleza na kama ni kulipa walipe kwa ustaarabu.

Mtu ana kifrem chake kidogo kaweka cherehani, jamaa wanapiga kufuri na kumtaka alipe Shilingi 70,000 wakati yeye mwenyewe ukute hiyo hela anaipata baada ya mwezi kwa tenda zake za kushona kwa bukubuku au 500
Ni uelewa mdogo
 
Leseni ni fees sio kodi mnaweza hata kufanya shilingi 5000.
hata hiyo elfu tano unayosema watu hawatoacha kulalamika, kwa kawaida halmashauri nyingi zinatoza ushuru wa sokoni(vizimba) au ktk stendi za daladala 500/= lakini tazama wafanya biashara na hao makondakta wanavyolalamika
 
hata hiyo elfu tano unayosema watu hawatoacha kulalamika,
Watu wanacholalamika ni fedha wanazotoa kuibiwa kwenye Manispaa na Halmashauri.

Fees lazima ziwe Affordable ili kuwashawishi Watu wengi kufungua Biashara ili wakue wawe walipakodi wakubwa lakini kuwapiga mikwara na kuwafungia ni ninyi mnakosa na wao wanakosa huo sio ujinga kweli?!🤔
 
Watu wanacholalamika ni fedha wanazotoa kuibiwa kwenye Manispaa na Halmashauri.

Fees lazima ziwe Affordable ili kuwashawishi Watu wengi kufungua Biashara ili wakue wawe walipakodi wakubwa lakini kuwapiga mikwara na kuwafungia ni ninyi mnakosa na wao wanakosa huo sio ujinga kweli?!🤔
ubadhirifu wa fedha upo kigezo kikubwa tunaona hati chafu zinazotolewa na mkaguzi mkuu, lakini sio kigezo cha kutolipa kodi cha msingi ni kuwachagua viongozi imara watakao simamia vyema rasilimali zetu zikiwemo hizo kodi zetu zinazokatwa na hawa mabwana wa halmashauri na manispaa/majiji
 
Halmashauri ya Kibaha Mjini imeanzisha oparesheni kamata kamata na kufunga biashara tangu wiki iliyopita.

Wanafika kwenye sehemu za biashara wakikuta unadaiwa kiasi chochote kile wanakutoa kwenye biashara yako, wanafunga na makufuli makubwa na kukutka kwenda kuchukua Control Number ili ulipie, kiwango kikianzia Tsh. 70,000

Oparesheni hiyo inafanyika kwenye maduka kuanzia maeneo ya Kibaha Mili Moja kupanda hadi Shule ya Maili Moja Msingi, Kwa Mang'umbi, Tankini hadi Mitaa ya Muheza.

Kinachoniuma ni kuona wanafungia hadi biashara ndogondogo, mtu ana kifremu chake anatakiwa kwenda kulipia, hawataki kusikia maelezo ya aina yoyote ile.

Kinachoendelea sasa ni Watu kufunga biashara zao, wakiwakwepa maafisa wa Halmashauri, hivi Rais Samia si alipiga marufuku hii staili ya kufunga biashara kisa tu mtu au watu wanadaiw kodi fulani ya Serikali au watasema yale ni maneno ya Kisiasa?

Hivi kwani si Rais Samia alisema hakuna kufunga biashara kwa sababu za mambo kama hayo, kwa nini hawawapi nafasi Wafanyabiashara wakajieleza na kama ni kulipa walipe kwa ustaarabu.

Mtu ana kifrem chake kidogo kaweka cherehani, jamaa wanapiga kufuri na kumtaka alipe Shilingi 70,000 wakati yeye mwenyewe ukute hiyo hela anaipata baada ya mwezi kwa tenda zake za kushona kwa bukubuku au 500
Na huku mbeya mkuu na mbuga zetu, fukwe, visiwa vinauzwa na maduka wanafunga wanakusanya hela tu. Wakinyimana wanatumbuana
 
Vi
ubadhirifu wa fedha upo kigezo kikubwa tunaona hati chafu zinazotolewa na mkaguzi mkuu, lakini sio kigezo cha kutolipa kodi cha msingi ni kuwachagua viongozi imara watakao simamia vyema rasilimali zetu zikiwemo hizo kodi zetu zinazokatwa na hawa mabwana wa halmashauri na manispaa/majiji
Hakuna kiongozi imara atatoka nje ya CCM mkuu viongozi imara watatoka ndani ya chama humo humo. Na hivyo hatuitaji kiongozi imara zaid ni taasis imara zitakazo simamia rasilimali zote za nchi. Na kiongozi mmoja
 
Lipa kodi tu , unataka sewage system nzuri , usafi , taka zizolewe n.k na laki tu ya kodi unazua. Tulipe kodi tujitegemee
 
Hii nchi ina Marais wangapi? Mama Samia si alipiga marufuku huu tabia ya kufunga biashara za watu?

Sasa unafunga biashara ya mtu hizo pesa za kuwalipa akazitowe wapi?

Kwanini wasitowe demand note ya mwezi mmoja?
Raisi hafiki kila kata ili tatizo la wateule kuanzia Rc,Dc na wakurugenzi
 
Leseni inatakiwa iwe bure ili kuondoa mzigo kwa wafanyabiashara.
Huyu ni mwanaCCM . Ni kipofu haoni ubaya wa CCM wala uzuri wa nchi.


Ukimuuliza makodi yote ya pango la nyumba nchi nzima na Zile za NHC miji yote Tanzania zinatumikaje hawezi akakupa jibu zaidi ya mama anaupiga mwingi bila kujua kuwa kuna pesa nyingi zinaliwa wa urefu wa kamba ya kila idara na wizara badala ya pesa zote kuingia hazina na kuondosha mianya ya upigaji kwa kufuta taratibu za kila idara kukusanya mapato na tozo halafu wafanye marumizi yao na zinazobaki ndio ziende hazina.
 
Nchi haina utaratibu wa kulea na kustawisha wafanyabiashara wa ndani.
Ilitakiwa mtu asajili biashara bure, tin bure na leseni bure.
Afanye biashara baada ya mwaka ndio apangiwe kulipia kodi, na leseni.
Kwa mazingira ya sasa ni ngumu kwa mfanyabiashara kustawi kwa kutumia mtaji wake,
ni awe na kona kona nyingi ili aweze kuishi.

Na ndio maana biashara ya kuuza nje hakuna, fedha za kigeni hakuna.
Hii ya kukusanya nyingi, na kutumia kwa wingi.
haitakaa uchumi wa nchi ukawa sawa, labda ccm itoke
 
Back
Top Bottom