Wafanyabiashara ni wengi kuliko waajiriwa lakini watanzania wanaoishi angalau maisha standard waajiriwa ni wengi, Tuendelee kuponda ajira?

Wafanyabiashara ni wengi kuliko waajiriwa lakini watanzania wanaoishi angalau maisha standard waajiriwa ni wengi, Tuendelee kuponda ajira?

Ndo maana hapo juu kuna mtu kasema waajiriwa hawajui 'how money works' probably na wewe upo hilo kundi

Cheki unashangaa mtu kuzungusha billion 3 na hata hana gari. Ningekua nakufaham ningekupeleka kkoo siku moja ukakutane na watu aina hio.

Ukishakua mfanyabiashara akili yako ipo kwenye kufanya hela yako izalishe zaidi, na wala sio kuitumia zaidi. Gari ni liability in disguise chief, wala sio asset. Ndo maana hata bank hawakupi mkopo kwa gari, labda microfinance za uchochoroni huko.

Pia Wafanyabiashara hawanunui magari, magari yanajinunua kwa ajili yao.

Tukirudi kwenye mada yako, 90% ya wafanyabiashara wameajiri watu directly au indirectly, wameajiri hadi serikali, banks, etc. Sasa sijui unaongelea wafanyabiashara wapi hao wanaoishi maisha magumu. Au unasemea machinga na mawinga.

Na kingine pita mtaani kwako angalia watu wote wanaoheshimika. Kama ni mwajiriwa basi ni mwajiriwa na ana biashara yake, lkn pure mwajiriwa hata kwenye jumuiya hapewi nafasi ya kuongea unless wafanyabiashara wameisha.
Gari sio liability ni basic need kwa mtu anaeweza kuligharamia bila kutikisika kiuchumi, gari litamsaidia kufika anakotaka kwa urahisi, kuokoa muda, kukaa comfortably, n.k.

Kwa akili yako wewe hata kujenga choo ni liability utakuwa unashusha kimba porini maana choo cha nyumbani hakikuingizii pesa
 
Ni kama umeandika point ila kuna kitu umesahau. Sio kila aliyejiajiri ni mfanyabiashara. Tofauti ya aliyejiajiri na aliyeajiriwa ni moja tu. Ni kwamba mmoja anajipangia mambo yake na mwingine anapangiwa na mwajiri wake. Ila wote kwa pamoja wanakula msoto. Tena yule aliyejiajiri kuna wakati anakula msoto mkali zaidi kwasababu asipoenda ofisini ndo kakosa riziki. Hakuna cha mshahara mwisho wa mwezi. Hili kundi la waliojiajiri ni kubwa mno nchini kuliko walioajiriwa.

Mfanyabiashara yeye anakuwa kashavuka hiyo hatua ya kujiajiri. Huyu anakuwa kafika stage ya kuajiri watu wengine kumfanyia kazi zake. Hata asipoenda ofisini kazi zinaendelea. Yaani kajiajiri na kuajiri. Kuna baadhi ya wafanyabiashara ili kutoingilia sana hesabu za kampuni huwa wanajipangia kabisa mshahara na kulipwa kama wafanyakazi wake. Hili kundi nalo lina wafanyabiashara wadogo hadi wakubwa. Na ni waajiriwa wachache sana wa vipato vya juu wanawazidi hili kundi kwa pesa.
 
Nilichomuelewa mtoa mada yeye kawachukua watu wote ambao hawajaajiliwa kawaweka kundi la wafanyabiashara [emoji1787][emoji1787][emoji1787],mwambieni arudi mtaani akafanye utafiti wa wajasiriamali,wafanyabiashara,wakulima,mawinga,madalali na machinga
 
Gari sio liability ni basic need kwa mtu anaeweza kuligharamia bila kutikisika kiuchumi, gari litamsaidia kufika anakotaka kwa urahisi, kuokoa muda, kukaa comfortably, n.k.

Kwa akili yako wewe hata kujenga choo ni liability utaona hakikuingizii faida utakuwa unashusha kimba porini
Huna akili af huna heshima

Umeprove huwezi kujenga hoja, siwezi endelea argue na wewe.

Ignore list + 1
 
Mfanya biashara kama hatapata janga, yupo juu zaidi ya mwajiriwa. Fanya uchunguzi utagundua mfanya biashara anaishi maisha mazuri kuliko mwajiriwa. Mfanya kazi ukinywa beer 2 tu kila siku mshahara unaisha ila mfanya biashara anapeta.
Hilo halipingiki lakini idadi ya hao ni wachache, tena ni mabilionea
 
Huna akili af huna heshima

Umeprove huwezi kujenga hoja, siwezi endelea argue na wewe.

Ignore list + 1
Wewe ni mweupe umedhani ukitaja liability wengine hatujui, nikujulishe ya kwamba hayo mambo mimi nimeyasomea darasani kwa miaka, wewe umegoogle kwa juu juu tu ukahisi unajua kila kitu kuhusu liability na asset, its more than that !! hata hio id unayojiita kali linux nina uhakika wewe ni mweupe kwenye hacking
 
Mfanya biashara kama hatapata janga, yupo juu zaidi ya mwajiriwa. Fanya uchunguzi utagundua mfanya biashara anaishi maisha mazuri kuliko mwajiriwa. Mfanya kazi ukinywa beer 2 tu kila siku mshahara unaisha ila mfanya biashara anapeta.
Siku moja mwaka 2006 niko na rafiki yangu bar moja inaitwa Jogoo House Arusha mida ya jioni kama saa 11 hivi. Kukawa na watu wengi sana hiyo siku. Kwenye meza tulikaa na mama mmoja hivi. Yule mama akavunja ukimya kwa kusema "leo bar imejaa kwa sababu ya hawa waalimu na vijimishara yao ambayo inakaa tu kwenye mfuko wa shati"... akaendelea kusema yaani hapa wamepita bar baada ya kutoka soko kuu kununua mazagazaga ya nyumbani. Na kweli chini ya meza tuliona mifuko ya plastic imejaa vitu.
 
Wafanya kazi wengi wanaishi maisha magum ukitaka kuona ilo magufuli alivowanyima kutopandisha daraja kipindi chake walikuwa wanaishi maisha magum sn hata ss ivi wengi wanaishi maisha magum wachache wanaofanya kazi mashirika ya umma ndo wapo poa ila sio wale wa tamisemi mtu anakopa mpk take home inakuwa laki 2 ss uyo si bora boda boda anakuwa ana maisha mazuri
 
Msome jamaa vizuri halafu weka hoja zako. Bro unaamini kabisa mtu anunue gari hata kama la mkopo halafu ashindwe kununua mafuta?? Sio kweli,
Mkuu,
Unaishi mkoa gani? Huku dasalama tuna magar Ila sometimes hatunaga pesa ya MAFUTA
 
Wafanya kazi wengi wanaishi maisha magum ukitaka kuona ilo magufuli alivowanyima kutopandisha daraja kipindi chake walikuwa wanaishi maisha magum sn hata ss ivi wengi wanaishi maisha magum wachache wanaofanya kazi mashirika ya umma ndo wapo poa ila sio wale wa tamisemi mtu anakopa mpk take home inakuwa laki 2 ss uyo si bora boda boda anakuwa ana maisha mazuri
Wana maisha magumu kuzidi wafanyabiashara machinga, wauza karanga, figili, n.k. ?????
 
Huyu anashindwa kutofautisha kati ya Mfanyabiashara, Machinga, Dalali na Winga. Anawaweka kundi moja ndo maana wanakuwa wengi machoni pake.

Sio kila mjasiriamali ni mfanyabiashara.
Hao wote ni kundi moja tafauti ni bidhaa na huduma tu
 
Mfanya biashara kama hatapata janga, yupo juu zaidi ya mwajiriwa. Fanya uchunguzi utagundua mfanya biashara anaishi maisha mazuri kuliko mwajiriwa. Mfanya kazi ukinywa beer 2 tu kila siku mshahara unaisha ila mfanya biashara anapeta.
Mbona mimi nakunywa kreti na nahonga na hela haiishi?
 
NIAMBIE MZEE WA VIWANGO

Je siye boda boda na hao watumishi wa umma nani anaishi standard life?
 
Wafanya kazi wengi wanaishi maisha magum ukitaka kuona ilo magufuli alivowanyima kutopandisha daraja kipindi chake walikuwa wanaishi maisha magum sn hata ss ivi wengi wanaishi maisha magum wachache wanaofanya kazi mashirika ya umma ndo wapo poa ila sio wale wa tamisemi mtu anakopa mpk take home inakuwa laki 2 ss uyo si bora boda boda anakuwa ana maisha mazuri
Hivi mfanyakazi yupi huyo anayeishi maisha magumu mbona mimi alhamdulillah mtelezo tu
 
Makundi yapo mengi

Waajiriwa
Waliojiajiri
Wafanyabiashara
Waliowekeza

Hawa wote wanautofauti wake!!
 
Ni ukweli usiopingika kwamba wafanyabiashara wana pesa nyingi, hata ukiangalia top 20 ya matajiri hapa Tz utawakuta wafanyabiashara wamejaa wao hasa wahindi , wasarabu na wasomali, hata baada ya hapo kuna watanzania wenye asili zetu wanaofanya biasbara.

Lakini katika kigezo cha idadi ya watanzania wanaoishi maisha standard idadi kubwa ni waajiriwa hasa wa serikalini, Ni kweli wafanyabiashara ni wengi kuzidi waajiriwa lakini kuna wafanyabiashara wachache ndio wenye mafanikio, excuse ya kusema serikalini wapo wanaopiga pesa haina mantiki sababu hata kwenye biashara kuna wanaopiga pesa kwa njia nyeusi kuzidi hata waajiriwa wapigaji.

Ukienda mitaa ambayo inasifika angalau wanaishi watu wenye maisha standard basi utakuta wengi ni waajiriwa

Ukienda shule binafsi private hizi ada milioni + utawakuta wanafunzi wengi wazazi ni waajiriwa

Ajira kipato ni cha uhakika kwa muda mrefu, pia kuna kuongezewa mishahara na kupanda madaraja, Biashara upepo unaweza badilika aidha kwa ushindani, madeni, wenye mitaji mirefu kuua soko, n.k. Kufirisika kwenye biashara ni suala la kawaida, wengi walioshindwa kumaliza ujenzi na kuacha mapagala huwa ni wafanyabiashara,

Wafanyabiashara wengi wa Tz wamebanwa sana hawana muda wa kutosha kupumzika na familia zao ama kufatilia mienendo ya watoto, wengi huondoka alfajiri hurudi usiku wakiwa wamechoka, waajiriwa wengi hawajabanwa hata makazini kuna muda hutoka kufanya mambo mengine, kazi zinaisha jioni, weekemd kuna mapumziko, sikukuu kibao za kiserikali na kidini, likizo, n.k.
Hila hii agenda ya wafanyabiashara na wachuuzi iwekwe wazi!
(wajasiriamali,wafanyabiashara,wakulima,mawinga,madalali na machinga)
Ukifikia level ya kuitwa mfanyabiashara unatakiwa huwe umeajiri! Mfanyabiashara kazi yake kuongoza na kusimamia mwenendo wa biashara! Sio mtu wa 💯 kuwa sehemu ya biashara!
 

Attachments

  • 1712677793297.gif
    1712677793297.gif
    42 bytes · Views: 9
Back
Top Bottom