Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Carlos The Jackal

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2017
Posts
25,725
Reaction score
78,589

Ila nchi hii ina viongozi wa ajabu sana, hapo unakuta waziri anayehusika kwa kushirikiana na timu Msoga, kwakua tu stendi ina jina la Magufuli, basi kubadilisha jina, ikashindikana baada ya mchezo wao kuwekwa mitandaoni.

Wameona waje na mbinu ya kutofanya ulazima kwa wamiliki wa ma bus kuhakikisha wanashushia abiria na mizigo yao pale stendi...... Ili stendi ijifie yenyewe taratibu..... Jambo la aibu na linalopaswa kukemewa na jambo hili linaendelea kuonyesha kwa namna gani nchi hii inaongozwa wajinga waliopewa nafasi. Hivi JPM angekua hai, kuna mmiliki wa mabasi angeivimbia serikali namna hiii?

Halafu hapo kuna dola, dola hiii hiii tunayosema kila siku iko mafunzoni kuhakikisha jicho lake linamulika kwa maslahi mapana ya taifa. Nadhani moja ya sehemu inayohitaji kufumuliwa ni mfumo mzima wa dola, umejaa wapigania matumbo tu .

Enyi wavivu, wazembe, wala rushwa na mafisadi wakubwa, jina la John Pombe Magufuli, hili halitakaa kufutika mioyoni wa taifa hili, historia itayasahau majina yenu pale tu mtakapokufa, lakini haitokaa kumsahau JPM.
 
Siku zote biashara haitakiwi kutegemea Stendi, bali stendi ndio inapaswa kutegemea biashara yako, shida ni hawa wafanyabiashara walidanganywa na ccm

Nimepita hapo stendi zaidi ya mara 50 lakini sikuwahi kununua chochote, hii ni kwa sababu si lazima abiria kununua kitu hapo stendi, sasa wanacholilia ni nini?
 
Ila Nchi hii Ina viongozi wendawazimu sana , Hapo unakuta Waziri anayehusika Kwa kushirikiana na Timu Msoga, kwakua tu Stendi Ina Jina la MAGUFULI, basi kubadilisha jina ,ikashindikana baada ya mchezo wao kuwekwa mitandaoni.
Bro naomba nitofautiane nawe kidogo. Jifikirie wewe ni abiria unaishi Upanga. Huna gari unategemea mwendokasi au daladala. Gari inaofisi tuseme Kigogo au Mnazi mmoja. Inakuja inakuacha Magufuli halafu wewe utafute usafiri kwenda Upanga.

Hapo hapo yenyewe inaenda tupu mpaka Mnazi mmoja. Ukitoka hapo stendi na mabegi yako mara uburute, ukabwe na kudondoka. Huu ni ukiritimba mkubwa mno. Au uneshafika level za kutembelea V8 linalowekwa mafuta na wananchi? Eti Daktari maana duh!
 
Ila Nchi hii Ina viongozi wendawazimu sana , Hapo unakuta Waziri anayehusika Kwa kushirikiana na Timu Msoga, kwakua tu Stendi Ina Jina la MAGUFULI, basi kubadilisha jina ,ikashindikana baada ya mchezo wao kuwekwa mitandaoni.
utu.be/5e3teIkFNWM?si=BI4o28LkFb0jRQ9H[/URL]
Nyie ndo wajinga ile ni stand na sio soko kama wanataka wafanye biashara wabadili liwe soko na watoe ushuru wa kuingia watu free
 
Abiria wanaingia hiyo Stendi wakiwa wameshiba ama wamechoka, unataka wanunue nini saa 10 alfajiri? wakinunua mavyakula hovyo watachimba dawa njia nzima

Wakifika jioni wamechoka na kwao ni hapo kimara tu sasa wananunua nini hapo stendi ambacho nyumbani kwao hakipo? Wauzaji wenyewe afya zao ni mashaka matupu, unanunua ili ukaharishe?
 
Binafsi nashauri hi!! Bus lazima ipite stendi husika, then inaweza kuendelea na ruti za ofsini kwake. Kutokupita kabisa si suala la kushabikia, huko ni kutumia pesa za watanzania ovyo. Na vitu kama stendi vinawapa ajira watanzania wengi sasa mkigeuza kuwa magofu wale walioko pale wakaibe??
 
Ila Nchi hii Ina viongozi wa ajabu sana, Hapo unakuta Waziri anayehusika Kwa kushirikiana na Timu Msoga, kwakua tu Stendi Ina Jina la MAGUFULI, basi kubadilisha jina, ikashindikana baada ya mchezo wao kuwekwa mitandaoni.
Bro tafuta location nyingine ya biashara. mtu anatokea Tanga/Arusha/Moshi amepita bagamoyo aje ashukie Magufuli?

Acha kukariri stand yaweza kuwa mahala popote abiria wanapopatikana na kuyafikia mabasi kirahisi.
 
Sgr nayo iwe inafuata abiria. Mkuu utaratibu lazima uwepo na upo kila nchi. Hiyo ya mabus kufata abiria sio sahihi ni kulazimisha tu
Hao SGR watafika tuu huko wakiongeza route atleast iwe nchi nzima wataanzisha magari ya kuwafuata abiria kuwaleta kituo cha treni.

Sasa mtu yupo Kigamboni kimbiji huko aje alale Guest ili awahi gari mbezi?
 
Utaratibu ni ustaarabu, wafuate utaratibu ma bus yote yapakie na kushusha abiria ndani ya stand ya ma bus na siyo vinginevyo. Kila siku tunalalamikia teuzi za rais, ni kwa sababu ya upuuzi kama huu.

Mkuu wa mkoa yupo, Mkuu wa wilaya yupo, Mkurugenzi yupo, afisa biashara wa mkoa na wilaya wapo, wachumi wa mkoa na wilaya wapo, Askari polisi na askari wa usalama barabarani wapo, kwanini bus lipakie abiria nje au kushusha abiria nje ya stand iliyojengwa kwa madhumuni hayo?

Wahusika wasimamie au watumbuliwe waje wengine wenye nia na kazi hizo.

Hapo nyuma tulilalamikia ndege binafsi kutua kila mahali biula taarifa wala ukaguzi, viwanja vya ndege vimepanuliwa na mamlaka husika walisimamia hili, bandari bubu zilizokuwa zikiingiza vitu vya magendo kama sukari na bidhaa zingine, tulilalamika mamlaka zikashughulikia, sasa kwanini hawa wa mamlaka za usafirishaji wasishughulikie hili la buses na abiria?

Tusipende vitu vya shaghalabaghala, tujenge tabia za kufuata taratibu sisi wenyewe, tunaposhindwa mamlaka husika zisimamie turudi kwenye mstari ndiyo majukumu yao. Na kama waliopewa dhamana hizo wameshindwa na watumbuliwe tu.

Na kama hii ndiyo sababu ya kutumbua watu basi atumbue asubui na jioni na ikiwezekana kila siku mpaka tupate watendaji wanaoelewa majukumu yao.

Nchi zilizoendelea zinatushinda kwasababu wao raia wao kwanza wanapenda utaratibu, na mamlaka zao zina enforce sheria zilizowekwa. Kama ni kutupa uchafu kwenye ndoo wote watatupa uchafu kwenye ndoo, na atakayefanya tofauti anachukuliwa hatua, hapa kwetu watu wanatetea ujinga.

Stand imejengwa kwa madhumuni gani, ikiwa kila mtu atafanya anavyopenda? Miafrika tuone aibu, hivi ni vitu vidogo tujielekeze wenyewe, tusisubiri kusukumwa.

Vijana wanakimbilia south Afrika na Ulaya, au Amerika kupata fursa, sasa bila utaratibu huku nani angeenda?

Nasi tujifunze matumizi mazuri ya akili na vitu , Stand ya bus, ma bus yote yangie stand, na abiria wote washukie stand na kupanda ma bus stand, kama ilivyo kwa ndege, habiria hupanda na kushukia airport na buses iwe hivyo.



Tuache hizi tabia tuendelee.
 
Maana ya Stend ni nini? Kahiyo abiria wote walazimishwe kushuka hapo Stendi ili wafanyabiashara wafanye biashara? Hiyo ni sehemu ya biashara?

Kwahiyo abiria wakiamua wanakuja kufuatwa na vyombo vya usafiri binafsi pia mtaanza kulia kuwa hakuna abiria kupanda gari binafsi bali ni bodaboda na taxi za stendi?

Iwapo makampuni wakaanzisha huduma ya kubeba abiria walioshuka kutoka kwenye mabasi yao bure kuelekea njia ya katikati ya mji pia mtaanza kulalamika?

Acheni lawama, wahimize serikali watengeneze njia nzuri kwa kila mwananchi kunufaika bila kutumia matatizo ya mwingine kama sehemu ya kuponea kwake....mbona Airport abiria wananunua kitu wakipenda na wala hawalazimishwi? Shida mnafanya vitu kiholela sana ndiyo maana hayo majengo mnayaaribu kabla ya kuanza kutumika.

Majengo mengi ya stendi watu wamejianzishia maduka uchwara tofauti na ubunifu ilivyokuwa awali.
 
Kwa hiyo na ndege zifuate abiria walipo? Kuna haja gani ya kutumia pesa nyingi kujenga stendi??
NB: Arusha mbaki na stendi yenu maana tumeona hazina umhimu.
Wanashauri ujinga fikiria mtu anaishi Boko au Mwenge basi Lina Toka Arusha au Moshi au Tanga linalopita Njia hiyo Kwa hiyo linapita hapo Boko na hapo Mwenge linakwenda na abiria Hadi stendi ya Magufuli linawashusha kule waanze kutafuta usafiri wa kurudi Mwenge na Boko basi linarudi tupu hata kama linapaki Mwenge au boko si.biashara kichaa hiyo

Au mtu anaishi mbagala anatoka Lindi na Mtwara basi linafika mbagala linapitiliza mbagala na huyo abiria Hadi stendi ya magufuli linamshusha atafute usafiri wa kurudi mbagala basi linarudi mbagala tupu hata kama linapaki mbagala huo ni wendawazimu

Hakuna abiria atakubali Hilo
 
Waridhike na wanachopata wasilazimishe biashara

Abiria ndio mwamuzi wa Nini anakitaka sio mwenye Basi,Wala mmachinga stendi ya Magufuli

Wasikilize abiria Serikali isipoteze muda kusikiliza Hao wengine isikilize abiria wanataka Nini?nkodi ziko kwenye tiketi wanazokata
 
Back
Top Bottom