Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Pikipiki zina vituo vyake vilivyosajiliwa ndiyo. Na namna ya bus huwa ni stendi ya bus mengineyo ni kumsaidia abiria tu lakini kituo cha bus huwa ni stendi na si ofsini kwao. Bus ni mhimu kushusha abiria stendi ili hiace nazo zile vichwa, tudigeuze bus kufanya kazi za daladala
 
Kuna Ile stendi ya Kibaha maili Moja,hamna biashara zinafanyika mle ndani ingawa madhumuni ya kujengwa ile stendi ilikuwa na biashara ifanyike pale.Basi zinaingia kulipa ushuru tu,lkn wakati ule stendi Iko pale maili moja mjini ilikuwa imechangamka na watu walifanya biashara kwa kuwa kulikuwa na mchangamano wa watu.
 
Tatizo ni ushamba na kufanya mambo kwa sifa bila uhalisia. Darhaihitaji stand moja kubwa, bali inahitaji stand nyingi ndogo ndogo.
Huo ujenzi ulikuwa ni ufisadi tu.
Stendi ndogondogo ni za daladala na si bus!! Shida yenu mnafikiria bus kuwafikisha nyumbani, bus zinapiga ruti ndefu zikikufikisha kituo husika shuka ukapande hiace zinazoenda mtaani kwenu. Tusigeuze kazi ya daladala kufanywa na bus
 
Lakini pia ni nzuri wao kuuza pipi, vituo kama hivyo vilistahili kuwa fursa kwa vijana na mama zetu kujipatia kipato. Kama una kazi maalum usione wanaolalamikia hili kama wakosefu, iliwasaidia mkono kwenda kinywani
 
Yani mimi naishi Kigamboni, mwenye bus ameamua kunichukua na kunirudisha kigamboni halafu wewe mpuuzi unayetaka kupiga debe hapo stand unalalamika.
Badala ya kurahisisha maisha tunakomaa kuyafanya magumu.
Hao wezi wakalime na waliokodi fremu hawajafungiwa na bolt hapo wakatafute maeneo mengine.
 
Na mikoa karibia yote kila wilaya ina stendi yake, Dar es Salaam ilipaswa kila wilaya kuwa na stendi hata tatu.
Dar si ni kama wilaya ya ulambo tu kwa ukubwa!! Watu wa dar mkishuka stend kufika unakolalamikia ni mbali nauli buku 2 imezidi sana. Kuna watu tunashushwa stend ulambo kufika nyumbani elfu 8, halafu mnataka stendi kila wilaya wakati kigoma hata lami ni shida.
 
🀣 🀣 🀣
 
Maana ya bus sio stendi tu, stendi imewekwa mahususi kwa ajili ya kumsaidia abiria kwanza, kwa hiyo kama inageuka mateso kwa mlengwa namba moja ambaye ni abiria inakuwa haina maana hiyo stendi. Stendi sio kwa ajili ya daladala kula vichwa au wauza crisps na lambalamba wanufaike. Pia kuna nchi nyingi tu mabasi huwa yanaanzia safari kwenye ofisi zao au miji ina stendi private, tatizo la Watanzania wengi ni kukosa exposure.
 
Usipende kuiga kila kitu eti exposure!! Wenzio miundombinu iko imara hukuti msongamano wa magari hivyo, hiace zenyewe zinaweka jam mjini ndo tuongezee na bus kusupply abiria mtaani eti kisa nchi nyingne wanafanya hvyo.
 
πŸ™‹β€β™‚οΈπŸ“βœοΈπŸ‘πŸ‘ŒπŸ‘πŸ‘ŠπŸ€πŸ™
 
πŸ™‹β€β™‚οΈπŸ“βœοΈπŸ‘πŸ‘ŒπŸ‘πŸ‘ŠπŸ€πŸ™
 
Kwa hiyo na ndege zifuate abiria walipo? Kuna haja gani ya kutumia pesa nyingi kujenga stendi??
NB: Arusha mbaki na stendi yenu maana tumeona hazina umhimu.
Usifaninishe ndege na bus mwisho utasema kwanini treni zisiwafate walipo ..kama ndege ingeweza kutua shekilango wangetua .. mimi mkaZi wa kigamboni .. unanilazimisha nitoke kigamboni hadi Magufuli stand for whom convenience?! Jamaa muuza mikate au tax driver ?! Vipi kuhusu mimi ?! Ile stand imejengwa kwa kodi zetu hakuna hasara ile stand ni huduma kama wilaya inategemea mapato basi hapo ndipo wanapokosea .. nitoke Mbagala hadi Magufuli stand nawaunga mkono wenye mabus kwa kuturahisishia..ile stand ibaki kwa huduma tu ambayo kwa mwenye kutaka kupanda na kushuka pale ... Mwisho mtakuja kusema hata kibaha wasishushwe abiria wote hadi Magufuli stand alafu aanze safari ya kibaha na daladala
 
Bus ni mhimu kushusha abiria stendi ili hiace nazo zile vichwa, tudigeuze bus kufanya kazi za daladala
Basi mpya za mwendokasi zimeshakuja?
Halafu daladala pia zinatakiwa ziwe zinapakiza abiria level seats tu, Abiria waliopo hata hamuwezi kuwahudumia vizuri, hiki kinachofanyika sasa kwenye dalala kupakiza abiria kwa kushindilia kama nyanya kwenye tenga ni wendawazimu halafu na bado mna tamaa ya fisi kuchukua hata wachache wanaobebwa na mabasi.
 
Imejengwa kwa mikopo yenye riba nafuu siyo pesa zako. Tunasubiri ushuke pale tupate kodi tukalipe deni. Nafananisha ndege na bus kwa kuwa vyote vina vituo maalumu vya kupakia na kushusha, hata hiace zina vituo maalumu vya kupakia na kushusha. Bus zingekuwa na msaada huo zisingelalamika kuomba kupandisha nauli, mafuta yakishuka mbona hawaombi kushusha nauli?? Ni uhuni tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…