Wafanyabiashara wa mboga ilala waingia hasara baada ya mboga zao kushikiliwa na mamlaka ya vipimo.

Wafanyabiashara wa mboga ilala waingia hasara baada ya mboga zao kushikiliwa na mamlaka ya vipimo.

Koffi Annan

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2018
Posts
1,771
Reaction score
5,087
Wafanyabiashara wa mbogamboga Soko la Ilala wamelia kupata hasara baada ya gari iliyokuwa imebeba mizigo yao kutoka Gairo mkoani Morogoro kukamatwa nje ya soko hilo.
Mwenyekiti wa Wafanyabiashara hao, Thomas Hezron amesema gari hiyo ilikamatwa na mawakala wa vipimo kwa mazao ya shamba mkoa wa Ilala baada ya kuonekana kwamba uzito kwa kila gunia kuzidi, leo jijini hapa.
"Kwa kawaida mizigo yetu tunauza kwa fungu na sio kwa kilo, sasa tumeshangaa kuambiwa mizigo yetu imezidi uzito," amesema Hezron.

Hezron amesema walipata ridhaa ya kupewa mizigo yao saa mbili asubuhi muda ambao hawawezi tena kupata wateja kwani huwa wanafanya biashara hiyo kuanzia saa 9 usiku mpaka saa 12 asubuhi.
Hata hivyo wafanyabiashara hao waligomea kushusha mizigo yao hata baada ya Mamlaka ya Vipimo kuiachia gari hiyo huku wengine wakidai kulipwa fidia na mamlaka hiyo kwa kuchelewesha kuruhusu mzigo na kusababisha hasara hiyo.
Naye Fatihia Kawiche ambaye ni mfanyabiashara wa mbogamboga katika soko hilo amesema hawajui hatima yao kwani mboga zao hazina wateja tena na hawajui pa kizipeleka.
"Mimi nina mtoto wa miezi 10, nimemuacha nyumbani saa saba usiku, nikijua nitakuja hapa nifanye biashara na kurudi nyumbani, lakini mpaka sasa sielewi hatima yangu," amesema Kiwiche.
Kiwiche amesema walifika ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kuambiwa warudi katika ofisi za Vipimo vya Mazao ya Shamba hapo Ilala ili kuruhusiwa kupewa mizigo lakini amesema uamuzi huo ulikuwa hauna msaada tena kwani tayari ni hasara kwao.
Martha Samburu, mfanyabiashara wa soko amesema utaratibu wa kupima mboga katika mizani ni mpya na yeye ameshangaa kuona utaratibu huo.
"Nina miaka 30 katika kazi hii, lakini sijawahi kuona utaratibu huu. Sijawahi kuona gunia la mboga kupimwa uzito, na hatujawahi kupewa taarifa hizi wala elimu yoyote, lakini leo kwa ghafla wameamua kufanya hivyo," amesema Samburu.

Crédit: Instagram
 
Nawaomba wasitupe au kuruhusu mboga hizi kuharibika,pls wazipeleke kwa charity house yoyote inayo deal na poor of the poorest
 
Kila wakati huwa nalalamika humu ya kuwa serikali huwa inakurupuka kwa maamuzi yenye hasara tu na kuumiza watu

Viongozi wote akili yao moja tu ni kuamka asubuhi na kutoa amri tu hata kama ilitungwa je wananchi wote wanaijua?

Hasara ambayo ingeweza kuzuilika, hata kama sheria ipo wangesema kuanzia siku fulani tuaanza rasmi

Sheria mbovu za kukurupuka kama yule mama aliesema marufuku Kuachana
Yaani sheria katoka nayo nyumbani
 
Mimi kuna trafiki mmoja juzi alikamata gari yangu school bus na kuipiga faini kwa kukosa reflector nikajiuliza school bus inatembea usiku?

Lakini alikomaa na kuandika faini.
Wafanyakazi wengi wa serikali hekima hawana wamejaa ubabe wa kindezi sana wanaumizwa wananchi.

Ningekuwa na mamlaka hao waliokamatwa mboga za watu wangekuwa hiyo hasara toka kwenye mishahara yao au waende wakauze mali zao hata kudanga ni sawa tu kikubwa pesa ilipwe.
 
Mimi kuna trafiki mmoja juzi alikamata gari yangu school bus na kuipiga faini kwa kukosa reflector nikajiuliza school bus inatembea usiku?

Lakini alikomaa na kuandika faini.
Wafanyakazi wengi wa serikali hekima hawana wamejaa ubabe wa kindezi sana wanaumizwa wananchi.

Ningekuwa na mamlaka hao waliokamatwa mboga za watu wangekuwa hiyo hasara toka kwenye mishahara yao au waende wakauze mali zao hata kudanga ni sawa tu kikubwa pesa ilipwe.
Mkuu kwanini ikose reflekta?
Ila pole
 
Kwasababu sikuona umuhimu wake coz haitembei usiku,mchana reflector ina kazi gani?
School bus zinaanza. kuzunguka 0400hrs huoni haja ya reflector bado?
kuna muda wanafunzi wanafanya tours na activity mbalimbali unasubiri ruti ya usiku ndio uweke reflector?

ANY WAYS SIUNGI MKONO UNYANYASAJI WA WATUMISHI WA UMMA BUT NA SISI RAIA TUNA MAMBO YETU SIYO
 
Ripoti ya cag inasema tanesco wameleta mashine za luku bila wakala wa vipimo kuthibisha lakini wanawaacha na kuhangaika na wauza mboga
 
School bus zinaanza. kuzunguka 0400hrs huoni haja ya reflector bado?
kuna muda wanafunzi wanafanya tours na activity mbalimbali unasubiri ruti ya usiku ndio uweke reflector?

ANY WAYS SIUNGI MKONO UNYANYASAJI WA WATUMISHI WA UMMA BUT NA SISI RAIA TUNA MAMBO YETU SIYO
School bus ya kwangu ni ya nursery school inaanza kazi 06:30 kwa asubuhi na kumaliza 17:00 jioni na huyo trafiki anajua RUTI ya hiyo gari sema tu alitaka ya kubrashia viatu kaona hapewi kaamua kuandika cheti kihuni.
Watoto wadogo chini ya miaka 6 hawana tours wala excursions ya usiku.
 
School bus ya kwangu ni ya nursery school inaanza kazi 06:30 kwa asubuhi na kumaliza 17:00 jioni na huyo trafiki anajua RUTI ya hiyo gari sema tu alitaka ya kubrashia viatu kaona hapewi kaamua kuandika cheti kihuni.
Watoto wadogo chini ya miaka 6 hawana tours wala excursions ya usiku.
hiyo faini umejitakia mwenyewe kama ni hiace au coaster reflector lazima labda kama unabebea wanafunzi na passo
 
Back
Top Bottom