Wafanyabiashara wanaochukua bidhaa Afrika Kusini na Uganda

Wafanyabiashara wanaochukua bidhaa Afrika Kusini na Uganda

Mkuu hongera sana kwa kutoa information zenye faida na kujibu maswali yenye vision.
Ila bado niko na maswali zaidi ya kuuliza japo wadau wengine wameshauliza.
1.Je kwa mtu anayeanza biashara hii ya chocolate na cosmetics inatakiwa minimum capital iwe kiasi gani?
2.Je mtu anaweza akaanza kwa kwenda kufuata mzigo South Africa bila kuandaa soko maalumu Tanzania?Je hizi bidhaa ni hot cake kiasi kwamba hata nisipoandaa soko nikija nazo nitakuwa na uhakika wa kuziuza on time?
3.Je usalama uko vipi South Africa kwa mfanyabiashara anayekwenda kuchukua mzigo?
4.Je kuna cargo agents ambao wanaweza kuzisafirisha bidhaa hizo kwa ndege ili mtu akienda kukusanya mzigo anamkabidhi Cargo agent kisha anarudi kwa bus wakati mzigo wake umeshatangulia kwa ndege?
Mkuu biashara nadhani ni matangazo yako pia ili uweze kufanya biashara ya uhakika na pia na uharaka zaidi ila usikope hela za Bank harafu upeleke SA kununua mzigo maana pana mipaka mingi muda mwingine utashindwa kulipa marejesho kwa sababu mzigo haujafika kwa wakati..
Chochote ni bidhaa zenye uzito kidogo hautapata faida ukipakia kwenye ndege waliofanikiwa ni wale wenye Canter yake harafu anaenda kupakia mwenyewe mzigo akiwa na dereva wake na yeye pia anaendesha wakifika Tanzania wanazunguka mkoa kwa mkoa wanamalizia Dodoma tuu hapo...
Kwa mazingira ya wafanyabiashara usalama upo ndio maana watu wengi wanafata bidhaa JHb na pia yapo maeneo yenye hotel salama unafanya biashara zako na kurudi salama kabisa..
Sijaelewa mnaposema mtaji kiasi gani maana wapo wanaohitaji kubeba box zake 200 za Chochote au Kontena zima au fusso ukajaze hapo ndio wewe useme nikiwa na kiasi gani ntanunua mzigo wa kiasi gani mpaka naufikisha Tanzania kwa kulipa kila kitu...Mtaji mkubwa sio solution ya biashara wewe na mbio zako kukimbia na kuuza kwa haraka na kutokopesha mali kwa watu wasio waaminifu bora ubaki na mali yako kuliko kutake risk kwa watu wataokukwamisha...
Chocolate ina soko sana Tanzania hivi vitu ukiambiwa jaribu kwenda kwenye supermarket yeyote ulio jirani yako yenye hizo bidhaa uliza kama unaweza ukawapa uone muitikio wao na aina za Chocolate maana zipo aina tofauti tofauti ni wengi wanafanya hii biashara na msitegemee watakuja kuwaambia hapa hata kama wapo humu...mimi niliwahi pata order kipindi fulani niliona ina faida na SA vipo vingi mpaka oil ya Castrol pia pale pana kiwanda na wana bei nzuri ambayo ukileta Tanzania unauza kwa jumla vizuri tuu na huku umelipia kodi kwa hizo biashara za nje sumu yake ni kukwepa kodi ukikwepa Kodi harafu TRA wakachukua mzigo hautaweza kuja kusimama ni kupambana kulipa kodi ili usisumbuliwe na wahuni Road au unapouza bidhaa zako...
Bidhaa za SA nyingi zinajitajika sana nchi zetu hizi unaweza kwenda sokoni ukauliza bidhaa ambazo ni adimu harafu ukakimbia kama unataka kuuza kwa haraka hasa hasa ni Kariakoo ndio wanajua bidhaa zilizopo sokoni au hakuna...
 
Soko lipo Arusha kwenye Camp zao za watalii wanahitaji mpaka vitunguu na mayai ya SA...sema matunda yanhitaji uwe na storage ya Freezer ambalo uwe na umeme na Generator ili uweze kufanya biashara ya uhakika ila vitu kutoka SA ni chocolate pamoja na pipi zao zinapatikana karibu na Cash n carry hapo JHb maeneo ya viwandani pamoja na mafuta ya kupakaa Cosmetics naona hii ndio biashara isiyo na mawazo mengi kuliko mambo ya matunda...
ila mkuu nikiwa na milion 16 siwezi kupata gari kali la kutembelea huko south Africa ?
 
ila mkuu nikiwa na milion 16 siwezi kupata gari kali la kutembelea huko south Africa ?
Mkuu magari angalia Kodi yake kununua unaweza kupata kali sana ila kikokoteo cha TRA kikakushangaza...mara nyingi ukiwa na pesa kidogo zingatia mwaka na aina za gari zenye kodi ndogo unatembea kweli kwenye mtandao wao uone utafiti wapi...
 
Mkuu magari angalia Kodi yake kununua unaweza kupata kali sana ila kikokoteo cha TRA kikakushangaza...mara nyingi ukiwa na pesa kidogo zingatia mwaka na aina za gari zenye kodi ndogo unatembea kweli kwenye mtandao wao uone utafiti wapi...
Sasa mkuu ni zipi sites zao hao wauza magari? Na vipi naweza kuangalia kodi ya TRA?
 
Habari za leo wakuu .mimi ni mfanyabiashara.nahitaji kuanzishq biashra ya matunda ku import from South Africa to Tz. Especially apples, zabibu kijani na nyekudu (seedless grapes) makungwa na mengine..naomba kujuwa kampuni au process ya kuagiza APPLE kutoka South Africa to Tz online Ili yanifikie .

Au kama ni kwenda yako wapi South..
na atleast niwe na mtaji wa sh. Ngapi kuanzia?
process ni ipi ili niweze kufanikiwa.
Naanzia wapi .bado niko gizani
Maana ukinnunua kwa hapa haluna faida.

Shukurani sana wadau
Good luck , ila ninachofahamu matunda hasa garapes kutoka south africs zinahitaji cold chain trucks . kukodi refrigerated truck kutoka cape town hadi dar es salaam ni pesa nyingi sana. Refrigerated container is even more.
Usijaribu kununua matunda hayo Johannesburg market , hapo yanakuwa yameshafika kwa dalali wa kwanza au wa pili. Shambani kunapolimwa apples na zabibu ni western cape , nenda huko upate fresh products kwa bei elekezi.
Nilifanya hiyo biashara( apples) 15 years back ilikuwa inalipa haswa ,japo sikuwahi kufikia level ya kusafirisha container zima
 
Mkuu chocolate karibu nyingi unazoziona kwenye Supermarket za Tanzania zinatoka SA au UK na ukipata vibali hata ulipe kodi unapata faida naona wengi wanabeba kutokana na bei ya SA maana kule 15% kodi unaridishiwa ila mpaka mzigo upite Tunduma pana mchakato ila wapo watu SA ukiamua wanakurudishia kiasi cha VAT maana mzigo ni wa Export kiasi kingine wanafatilia wao na ndio maisha yao...
Chocolate zipo Jumbo,Cash n carry na maduka makubwa yote yalio karibu na hapo..
Jumbo na cash n carry !! South africa kitambo sana . nilikuwa nanunua sweets kuja kuuza jo berg down town.
On a serious note Isanga family umejua kukomaa na south Africa , mimi nilikinai matukio ya kule mapema sana
 
Sasa mkuu ni zipi sites zao hao wauza magari? Na vipi naweza kuangalia kodi ya TRA?
Metal car rebuild.co.za
We buyscar.co.za
Gumtree.co.za
Citydeep auto.co.za
Smd auction
Midlands auction
Car salvage.co.za
Unachagua aina ya gari hapo unayotaka kikubwa kununua uwepo SA usilipe ukiwa Tanzania wahuni wanaingilia sana account zao hazina ulinzi wa kutosha ukinunua mara moja trip zinazofatia unaweza kununua ukiwa Tabora na malipo unafanya na unamlipa dereva analeta gari yako kwa jina lako...
Code yao ni co.za rate mara nyingi imekomaa 1 rand kwa Tsh 140 mpaka 150...zidisha na bei unayoiona hapo...
 
Good luck , ila ninachofahamu matunda hasa garapes kutoka south africs zinahitaji cold chain trucks . kukodi refrigerated truck kutoka cape town hadi dar es salaam ni pesa nyingi sana. Refrigerated container is even more.
Usijaribu kununua matunda hayo Johannesburg market , hapo yanakuwa yameshafika kwa dalali wa kwanza au wa pili. Shambani kunapolimwa apples na zabibu ni western cape , nenda huko upate fresh products kwa bei elekezi.
Nilifanya hiyo biashara( apples) 15 years back ilikuwa inalipa haswa ,japo sikuwahi kufikia level ya kusafirisha container zima
Niko western cape hapa hebu tupeane hiyo ideas za biashara apples na grapes kwaujumla
 
Good luck , ila ninachofahamu matunda hasa garapes kutoka south africs zinahitaji cold chain trucks . kukodi refrigerated truck kutoka cape town hadi dar es salaam ni pesa nyingi sana. Refrigerated container is even more.
Usijaribu kununua matunda hayo Johannesburg market , hapo yanakuwa yameshafika kwa dalali wa kwanza au wa pili. Shambani kunapolimwa apples na zabibu ni western cape , nenda huko upate fresh products kwa bei elekezi.
Nilifanya hiyo biashara( apples) 15 years back ilikuwa inalipa haswa ,japo sikuwahi kufikia level ya kusafirisha container zima
Mkuu mi nipo hapa capetown,na ninatamani kuanza hiyo biashara ila sijui nianzie wapi mpaka nihakikishe mzigo unafika tz na masoko
 
Kwa Kampala Uganda;
wengi wa TZ hufuata nguo hasa za kike, na viatu. Maduka mengi ya nguo yapo Kampala maeneo yanayozungukia New & Old Kampala Taxi Park hasa mitaa ya Nakivubo, Namgoba, Namirembe n.k.
Usafiri ni kwa basi na kampuni mashuhuri ni FRIENDS Express ambao wana route ya DSM-KPLA, MZA-KPLA. Kutokea Dsm-Kampala ni kama 80,000/= na kutokea Mza-Kampala ni 40,000/=.
Usafiri wa mizigo ni kutumia basi, na kutoka DSM-KPLA ni siku 2, na kutokea Mza-KPLA ni masaa kama 14.
Usumbufu upo mpakani hasa kama ni mgeni kwa kuwa kodi ya mpakani sharti upatane na kondakta kulingana na atavyokukadiria mkiwa pale Terminal kabla ya safari. Ukileta ujuaji zaidi sharti akuchomeshe kwa maafisa wa TRA pale Mutukula, ila ukipatana nae wewe hata hutazungumza na maafisa wa TRA.
Sehemu za kulala kama upo na mwenyeji zipo affordable kwa maana kwamba mnaweza kuchangia chumba kimoja (hawana usumbufu wa kuzuia kulala jinsia moja) na vyumba vya watoto wa wakulima vipo vya hadi 30,000 Tsh kwa kuchangia wawili.
Passport ya dharura inaweza kutumika kuingia na kutoka UG.
Ni vizuri unapoenda kwa mara ya kwanza kupata mwenyeji ili kukufahamisha mambo mengine machache na hasa ukadiriaji wa kodi wa kondaktaz.
Epuka kuzoena na mtu usiyemjua uwapo UG na kumkaribisha kwa room yako labda tu kama unatoka naye huko unakotoka.
Kushare Chumba sishauri hata kidogo hakuna mfanya biashara anayeshindwa kulipa elfu 30.Hila ushauri wako wa kibiashara ni mzuri.
 
Kwa sasa huduma ya usafiri wa basi kutoka Dar es salaam hadi Afrika kusini inapatikana. kuna kampuni inaitwa mkombe luxury ofisi zao zipo business park shekilango basi kutoka Dar-Es-Salaam hadi Johannesburg, nauli laki tatu
 
Mkuu biashara nadhani ni matangazo yako pia ili uweze kufanya biashara ya uhakika na pia na uharaka zaidi ila usikope hela za Bank harafu upeleke SA kununua mzigo maana pana mipaka mingi muda mwingine utashindwa kulipa marejesho kwa sababu mzigo haujafika kwa wakati..
Chochote ni bidhaa zenye uzito kidogo hautapata faida ukipakia kwenye ndege waliofanikiwa ni wale wenye Canter yake harafu anaenda kupakia mwenyewe mzigo akiwa na dereva wake na yeye pia anaendesha wakifika Tanzania wanazunguka mkoa kwa mkoa wanamalizia Dodoma tuu hapo...
Kwa mazingira ya wafanyabiashara usalama upo ndio maana watu wengi wanafata bidhaa JHb na pia yapo maeneo yenye hotel salama unafanya biashara zako na kurudi salama kabisa..
Sijaelewa mnaposema mtaji kiasi gani maana wapo wanaohitaji kubeba box zake 200 za Chochote au Kontena zima au fusso ukajaze hapo ndio wewe useme nikiwa na kiasi gani ntanunua mzigo wa kiasi gani mpaka naufikisha Tanzania kwa kulipa kila kitu...Mtaji mkubwa sio solution ya biashara wewe na mbio zako kukimbia na kuuza kwa haraka na kutokopesha mali kwa watu wasio waaminifu bora ubaki na mali yako kuliko kutake risk kwa watu wataokukwamisha...
Chocolate ina soko sana Tanzania hivi vitu ukiambiwa jaribu kwenda kwenye supermarket yeyote ulio jirani yako yenye hizo bidhaa uliza kama unaweza ukawapa uone muitikio wao na aina za Chocolate maana zipo aina tofauti tofauti ni wengi wanafanya hii biashara na msitegemee watakuja kuwaambia hapa hata kama wapo humu...mimi niliwahi pata order kipindi fulani niliona ina faida na SA vipo vingi mpaka oil ya Castrol pia pale pana kiwanda na wana bei nzuri ambayo ukileta Tanzania unauza kwa jumla vizuri tuu na huku umelipia kodi kwa hizo biashara za nje sumu yake ni kukwepa kodi ukikwepa Kodi harafu TRA wakachukua mzigo hautaweza kuja kusimama ni kupambana kulipa kodi ili usisumbuliwe na wahuni Road au unapouza bidhaa zako...
Bidhaa za SA nyingi zinajitajika sana nchi zetu hizi unaweza kwenda sokoni ukauliza bidhaa ambazo ni adimu harafu ukakimbia kama unataka kuuza kwa haraka hasa hasa ni Kariakoo ndio wanajua bidhaa zilizopo sokoni au hakuna...
Mkuu kuna swali moja muhimu sana la kumalizia.
Nikienda Johannesburg nikakaa wiki moja je kwenye malazi na chakula inaweza kunigharimu kiasi gani?
 
Mkuu kuna swali moja muhimu sana la kumalizia.
Nikienda Johannesburg nikakaa wiki moja je kwenye malazi na chakula inaweza kunigharimu kiasi gani?
Mbu wa Dengue JHB utafikia maeneo ya Shalom bus ndio pana hotel za bei ya wafanyabiashara au Shopers Plaza kule kwa Wasomali hayo ndio maeneo salama unapotembea kwenda kufanya ununuzi wako tumia Tax hata wazulu ila wale ambao wapo pale Shalom au huko Plaza hawana ujinga wa kufanya uibiwe ndio wapo hapo miaka nenda miaka rudi na hawana bei...
Gharama Lodge huku Kerk Street ni rand 200 mpaka 250 ila kule Plaza ni rand 300 kuendelea sehemu unazonunua bidhaa ni Dragon City au China City na maeneo mengine utaambiwa ukifika kutokana na bidhaa unayotaka kula chakula ni rand 30 hapo hapo Shalom chai rand 12 kumlipa jamaa wa Tax unaweza kuzunguka nae kwa muda fulani unampa rand 300 na umepakia vitu vyako...hata ukiwa SA nicheki hapa nakupa maelezo au kama pana mtu anajua urahisi zaidi atatoa mawe ili tuweze kukimbizana na hili gurudumu...fata oil hizi Castro trip za Mwanzoni usifate bidhaa za kuoza maana utapata tabu kidogo...
 
Back
Top Bottom