Wafanyakazi 12 wa Azam Tv wapata ajali mlima Kitonga. Walikuwa wanaelekea jijini Mbeya kurusha matangazo ya NBC premier league

Magari ya Azam TV na madereva wao wachunguzwe.

Magari yao yanapata ajali mara kwa mara na zinakuwa mbaya na au zinatokea maaeneo hatari.

Kuna uwezekano madereva hawana ujuzi wa 'udereva wa kujihami' ambao kila dereva haswa wa 'Passenger Service Vehicles (PSV)' anatakiwa awe nao.
 
Pole kwao, majeruhi wapone haraka. Tahadhari muhimu na udereva makini unahitajika maeneo hatari.
 
Mkuu, unaweza ku-overtake tu. Usikubali kuweka roho yako rehani kwa kuogopa kuvunja sheria. Mimi nilifanya hivyo mwezi uliopita, hapo hapo Kitonga. Nilikuwa napanda huo mlima, nikiwa na 4X4, mbele yangu kulikuwa na lori ambalo niliona kabisa lina matatizo. Spidi ilikuwa ni ndogo, na kuna wakati linasimama kabisa kwa kushindwa kupanda Mlima, nikaona kabisa hii ni hatari. Nikaamua kulipita, na hata dereva wa lori akanipa ishara nimpite. Kumbe kule mbele kuna trafiki wamepaki gari yao, wakiaangalia watu wanaopiga overtake mlimani. Nilipofika walipo, wakanipiga mkono, nikasimama. Trafiki mmoja wao akaniambia kuwa nimefanya kosa kupiga overtake. nikamwambia hapana, ile ni hatari, lile gari ni bovu, linashindwa kupanda mlima, ni hatari kuwa nyuma yake. Na akitaka, tusubiri pale wote mpaka lifike, alione mwenyewe kwa macho yake. Akaelewa, na kuniruhusu tu niondoke zangu.
 
Tatizo la askari wetu wa barabarani ni uelewa mdogo na kuendekeza rushwa ndogondogo. Kuna sehemu zingine kwa mjibu wa sheria hurusiwi kulipita gari la mbele yako lakini ki usalama unatakiwa kulipita, cha ajabu polisi wetu akiona hivyo ni fursa ya yeye kupata rushwa, hata uongee vipi hakuelewi. Binafsi kitonga huwa naovetake kwa usalama wangu.
 

 
Huu mlima huu!! Nasikia kuna mlima mwingine huko, Ushoto sorry Lushoto nao unatisha.
===
Ugueni poleni majeruhi, na nawaombea kwa Mungu mpone haraka.
 
kampuni kubwa bado mnapandisha watangazaji wenu kwenye magari na madereva wabovu wazembe na ndege mbeya zinaenda kilasiku
 
AZAM acheni kuajiri madereva wa daladala za Buguruni / Kariakoo kwani hawajui kanuni za udereva, wao bora liende mbele tu.
 
Kafara hizo..kufanya kazi kwenye kampuni binafsi kuna mambo mengi sana yakutisha.
 

1. Umewahi kupita Kitonga?

Maana naona ume comment kwa Mbwembwe kabisa!
 
Hao jamaa ni mandezi sana wanavizia kwa juu maana wanajua kwamba lazima uovertake maana malori hayawezi panda mlima huo vizuri...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…