kbm
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 5,224
- 1,677
Serikali kupitia Wizara ya Kazi na ajira iko katika mchakato wa kuanzisha sheria ya mkataba wa wafanyakazi wa majumbani.
Mkataba huo utasimamia na kuteteahaki, maslahi, afya na usalama, mazingira ya utendaji kazi, pamoja na uingizwaji katika makato ya hifadhi ya mifuko ya jamii kwa wafanyakazi hao.
Hatua hiyo imefuata mkutano wa kimataifa wa mkataba namba 189 wa kazi zenye staha kwa wafanyakazi wa majumbani uliofanyika Geneva, Uswis mwaka 2011.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana katika ofisi za Shirika la Kazi la Umoja wa Mataifa (ILO), Mkurugenzi wa Ajira, Ally Msaki, alisema serikali imeandaa mpango kazi kwa kuazna na uzinduzi wa dodoso zitakazotumika kufanyia utafiti wa sheria hiyo.
Alisema utafiti huo utaanza Juni maka huu hadi Julai mwakani na pindi utakapokamilika, itapelekwa bungeni kama muswada na baadayekupitishwa na kuwa sheria.
Kwa mujibu wa ripoti ya takwimu zaILO ya mwaka 2010, bara la Afrika lina wafanyakazi wa ndani milioni tano na asilimia 70, kati yao ni wanawake.
Kadhalika katika takwimu za mwaka huu zinaeleza kuwa wafanyakazi wa ndani Tanzania Bara ni asilimia 1.2 ya soko la ajira na asilimia 0.7 kwa Zanzibar.
Ripoti pia inaeleza kuwa miongoni mwa wafanyakazi hao wa ndani wanafanya kazi katika mazingira magumu pasipo kupewa ujira wao sahihi.
Mkurugenzi wa ILO Kanda ya Afrika Mashariki na Kati, Alexio Musindo, alisema kuanzishwa kwa mkataba namba 189 ya mwaka 2011 kutapelekea kuwapo kwa uhuru wa mfanyakazi wa ndani, masaa ya maalum za kufanya kazi, uboreshwaji wa mazingira ya kazi pamoja na kulipwa kwa wakati.
Alisema mpaka sasa Maurituis pekee ndiyo inayoitumia sheria hiyo.
CHANZO: NIPASHE
Mkataba huo utasimamia na kuteteahaki, maslahi, afya na usalama, mazingira ya utendaji kazi, pamoja na uingizwaji katika makato ya hifadhi ya mifuko ya jamii kwa wafanyakazi hao.
Hatua hiyo imefuata mkutano wa kimataifa wa mkataba namba 189 wa kazi zenye staha kwa wafanyakazi wa majumbani uliofanyika Geneva, Uswis mwaka 2011.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana katika ofisi za Shirika la Kazi la Umoja wa Mataifa (ILO), Mkurugenzi wa Ajira, Ally Msaki, alisema serikali imeandaa mpango kazi kwa kuazna na uzinduzi wa dodoso zitakazotumika kufanyia utafiti wa sheria hiyo.
Alisema utafiti huo utaanza Juni maka huu hadi Julai mwakani na pindi utakapokamilika, itapelekwa bungeni kama muswada na baadayekupitishwa na kuwa sheria.
Kwa mujibu wa ripoti ya takwimu zaILO ya mwaka 2010, bara la Afrika lina wafanyakazi wa ndani milioni tano na asilimia 70, kati yao ni wanawake.
Kadhalika katika takwimu za mwaka huu zinaeleza kuwa wafanyakazi wa ndani Tanzania Bara ni asilimia 1.2 ya soko la ajira na asilimia 0.7 kwa Zanzibar.
Ripoti pia inaeleza kuwa miongoni mwa wafanyakazi hao wa ndani wanafanya kazi katika mazingira magumu pasipo kupewa ujira wao sahihi.
Mkurugenzi wa ILO Kanda ya Afrika Mashariki na Kati, Alexio Musindo, alisema kuanzishwa kwa mkataba namba 189 ya mwaka 2011 kutapelekea kuwapo kwa uhuru wa mfanyakazi wa ndani, masaa ya maalum za kufanya kazi, uboreshwaji wa mazingira ya kazi pamoja na kulipwa kwa wakati.
Alisema mpaka sasa Maurituis pekee ndiyo inayoitumia sheria hiyo.
CHANZO: NIPASHE