Pre GE2025 Wafuasi CHADEMA wavamia nyumbani kwa Mbowe kumlazimisha achukue Fomu ya kugombea Uenyekiti

Pre GE2025 Wafuasi CHADEMA wavamia nyumbani kwa Mbowe kumlazimisha achukue Fomu ya kugombea Uenyekiti

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kundi kubwa la vijana wamejazana Nyumbani Kwa Freeman Mbowe mikocheni

Baadhi ya majirani wamepiga Simu polisi Ili kuomba Ulinzi wa Makazi yao

Niko hapa Chato ngoja nielekee nikashuhudie kinachojiri 🐼

==

Mamia ya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wamefika nyumbani kwa Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe, wakimtaka achukue fomu kwaajili ya kutetea nafasi yake ya uenyekiti.

View attachment 3179505
View attachment 3179513View attachment 3179514View attachment 3179516
Nadhani siasa hizi zimezoeleka zaidi kufanywa na wanaCCM tangu enzi za akina Kingunge (Castory) Ngombale Mwiru. Hivyo kuanza kutumiwa na Mbowe 2024 ni kumrudisha nyuma.

Mbowe ahitaji tena kufanya mambo haya, kwa kuwa nchi nzima inajua ana dhamira ya kuwa Mwenyekiti wa Chadema hadi atakapofia kwenye kiti, haijalishi ni mwaka gani itakuwa.

Jana usiku Mbowe alikuwa na kikao kirefu na waandishi wanne wa habari, wa Global TV, Mwananchi, ITV na Radio One (mmoja bado sijajua wa chombo gani).

Kikao cha kugawana majukumu ya kualika wanahabari kwa siri, ambapo Hussen wa Global TV alipewa kazi ya kualika kwa siri waandishi wa Online TV's, kuwa waandishi wafike kwa Mbowe leo saa nne asubuhi.

Wengine wakipewa jukumu la kualika wanahabari wa radio, vituo vya TV na magazeti. Sasa yote haya ni ya nini? Hakuna jipya kwenye suala la Mbowe kugombea uenyekiti Chadema wala kuwa Mwenyekiti

Haikuhitaji mbinu hizi za kale za siasa za mapenzi ya uongo-uongo ya wananchi kwa mwanasiasa.

Ova
 

Attachments

  • IMG_20241218_144717.jpg
    IMG_20241218_144717.jpg
    192.8 KB · Views: 2
Kweli ni mwamba, aliwapiga chenga Polisi kwenda kwenye maandamano lakini wanachama wake wamemkuta bila taarifa. Safi sana!
 
Nadhani siasa hizi zimezoeleka zaidi kufanywa na wanaCCM tangu enzi za akina Kingunge (Castory) Ngombale Mwiru. Hivyo kuanza kutumiwa na Mbowe 2024 ni kumrudisha nyuma.

Mbowe ahitaji tena kufanya mambo haya, kwa kuwa nchi nzima inajua ana dhamira ya kuwa Mwenyekiti wa Chadema hadi atakapofia kwenye kiti, haijalishi ni mwaka gani itakuwa.

Jana usiku Mbowe alikuwa na kikao kirefu na waandishi wanne wa habari, wa Global TV, Mwananchi, ITV na Radio One (mmoja bado sijajua wa chombo gani).

Kikao cha kugawana majukumu ya kualika wanahabari kwa siri, ambapo Hussen wa Global TV alipewa kazi ya kualika kwa siri waandishi wa Online TV's, kuwa waandishi wafike kwa Mbowe leo saa nne asubuhi.

Wengine wakipewa jukumu la kualika wanahabari wa radio, vituo vya TV na magazeti. Sasa yote haya ni ya nini? Hakuna jipya kwenye suala la Mbowe kugombea uenyekiti Chadema wala kuwa Mwenyekiti

Haikuhitaji mbinu hizi za kale za siasa za mapenzi ya uongo-uongo ya wananchi kwa mwanasiasa.

Ova
Inaonekana hicho Chama hakina nia ya mabadiriko ya kweli, kina kuwa ni mali ya mtu binafsi sio tena Taasisi

Sijaona utofauti wake na CCM hadi sasa
 
Baada ya miaka mingi kupita, leo Wacha na Mimi nichangie kidogo kuhusu yanayoendelea Chadema.

Ukitaka mabadiliko lazima uoneshe Nia ya kubadilika na si kuendelea kufanya mambo Yale yale. Wananchi wengi wamekatishwa tamaa na namna upinzani unavyokabiliana na serikali dhalimu ya CCM.

Kuna matukio mengi yamefanyika kutoka mwaka 2015 Mpaka leo ambayo yamerudisha nyuma Ari na morali ya wananchi kushiriki katika demokrasia na kwa kiasi kikubwa wamekata tamaa.

Mtu mmoja ambaye walau ameonesha kuwa na msimamo wa kukabiliana na hali tangu kipindi hicho kwa mtazamo wangu ni TAL. Huyu mtu hakika anaonesha wazi wazi ana Nia thabiti ya kuleta mabadiliko kwani Hana hata chembe ya hofu kwa Yale anayoamini yanaweza kuleta haki.

Nilidhani CDM wameliona hili kama sie watu ambao tupo nje ya CDM vile ambavyo tumeweza kuona. Nashangaa ndani ya CDM hawataki mabadiliko ilhali wanataka mabadiliko ndani ya nchi, hapa tunashangazwa wengi.

Haileti picha nzuri kuona TAL anapingwa wazi wazi na kuanza kuonekana kama ni mtu Baki wakati ameweka rehani uhai wake kusaidia vugu vugu la mabadiliko kupitia CDM.

Wengi tungependa ashike nafasi ya kuu pale CDM tuone namna Gani ataleta mbinu mpya za kukabiliana na CCM.

Mbowe amepata muda wa kutosha na kwa kweli mbinu zake hazijatosha kabisa kukabiliana na CCM ambao wanatumia Dola kuendelea kubaki madarakani.

CDM msichezee fursa hii tena, manalo jukumu la kuonesha Jamii kuwa mnaweza kubadilika kulingana na mazingira na kusaidia Jamii ya Tanzania ambayo imebaki bila msaada kwa ukoloni wa CCM.

Ahsante
Mtu anaeweza kuleta mabadiliko chanya CDM ni John Heche, siyo Lissu.

Lissu aungane na akina Kibatala kusaidia chama kisheria.
 
Kama kweli Mbowe anataka kulinda heshima yake na ushawishi angeachana na habari za kuendelea kuwa mwenyekiti wa hicho chama.


Ikiwa Tundulissu atakubali kumuachia Mbowe uenyekiti wa Chadema kutakuwa hakuna sababu yeye kuendelea Kuwa Chadema.


Machaguo ni mawili kukiua chama Kwa kumrudisha Mbowe au kumpatia Lissu hiyo nafasi ya uenyekiti.

Sioni sababu zozote za Muhimu za Mbowe kuendelea kuwa Mwenyekiti.
 
Kundi kubwa la vijana wamejazana Nyumbani Kwa Freeman Mbowe mikocheni

Baadhi ya majirani wamepiga Simu polisi Ili kuomba Ulinzi wa Makazi yao

Niko hapa Chato ngoja nielekee nikashuhudie kinachojiri 🐼

==

Mamia ya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wamefika nyumbani kwa Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe, wakimtaka achukue fomu kwaajili ya kutetea nafasi yake ya uenyekiti.

View attachment 3179505
View attachment 3179513View attachment 3179514View attachment 3179516
hao ni ccm siyo chadema maana ccm ndiyo wanataka mbowe agombee uenyekiti wanamuogopa LISSU
 
Mtu anaeweza kuleta mabadiliko chanya CDM ni John Heche, siyo Lissu.

Lissu aungane na akina Kibatala kusaidia chama kisheria.
Heche pamoja na kusoma Mlimani bado mshamba mshamba

Chadema ni chama Cha swaga 😄😄
 
Hapo ndio utajua yupo upande gani.
Maana hiyo ndio aina ya michakato upande ulee!
 
Back
Top Bottom