Wafugaji wa mbwa kibiashara au ulinzi tukutane hapa

wewe umefuga kweli mkuu, gs pure kwa sasa bongo wapo wachache sana Dar, Arusha na Mwanza japo ni wachache kweli kweli.
Trainer, madaktari na madalali wa mbwa ni majambazi kaa nayo mbali
GSD pure wapo ndugu kikubwa uende kwa mtu aliyenao yy mwenyewe sio kupitia kwa madalali, na uweze kutambua pure yupo vipi maana hawa gsd huwa wanachanganya sana,na uwe unajua unataka show line au worlk line, kwenye kuwatambua na kupata aliye register ndio challenge kubwa kwa hasa asiyejua gsd ni nini.
 
Ili uweze kupata mtokeo bora yakupasa kupata gsd kwa gsd utafurahia hutajuta, hapo bado utapata cross halafu itakufisha moyo kwamba hujapata gsd uliyokuwa unahitaji, hizo breed za kwetu ni nzuri pia kikubwa ni ww jinsi gani unamtunza. Hao nimekuwekea picha hapo ni wakwangu
 
mkuu, atakayezaliwa anaweza kufanana na babake kwa vitu vingi lakini hawezi kuwa pure breed sababu tayari huyo uliyonayo ni cross breed.
si lazima uwe na cross breed andapo lengo lako ni ulinzi na sio biashara.
 
@steven nguma hao wako naona ni cross breed ya gs
 
@steven nguma hao wako naona ni cross breed ya gs
Sina uhakika ila nimesema itakuwa vizuri kama mtu anaetaka kufuga hasa gsd wanasumbuwa sana kwenye kupata pure sana sana mtu anakuuzia cross mwisho hamu ya kufuga inamwisha hizo kesi nazijua ni nyingi sana kwakweli.
 
tatizo kubwa la kutokuwa na mbegu pure;
1. kukosa ufahamu sahihi wa kuwatambua gsd
2. kutokufika bei
 
kweli
Sina uhakika ila nimesema itakuwa vizuri kama mtu anaetaka kufuga hasa gsd wanasumbuwa sana kwenye kupata pure sana sana mtu anakuuzia cross mwisho hamu ya kufuga inamwisha hizo kesi nazijua ni nyingi sana kwakweli.
 
Mkuu inaonekana unajua kweli ufugaji wa mbwa. Maana kwa mfano mdogo tu aina ya uvishaji wa chain za mbwa wa kuzunguka kwenye shoulder. Ule uvishaji wa wa chain kavu shingoni bila hata mkanda kwa kiasi fulani huumiza na kuwatesa hawa viumbe
 
Huyu ndie alitumika kwenye operation Neptune Spear inaelekea akipewa mafunzo anakuwa master hasa .
 
Vp huyu ni "Malinwaa"? Ana umri wa miezi 7 na nusu (kadi ya usajili na tiba). Maana nilimnunua tu 'mahala' akiwa na miezi miwili nikijua ni ni GS! Ila kwa maelezo yenu humu naona ni 'Malinwaaa'. (Sio mtaalam). View attachment VID20181007135046.mp4
 
Tutafutane kaka hii tasnia ya mbwa inatuhitaji sana maana huwa kunaupotoshaji sana ktk ufugaji, kama unakumbuka ule wa mkuki pale saba saba tuliukemea sana.
mkuu mwanzoni nililzwa sana tena wengine ni askari wa kikosi cha farasi, niliuziwa makoko yafananayo na gs, lkn sasa kunidanganya ni mwiko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…