Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
unaweza wafuga aina zotehizo za mbwa..kwa mfano nina eneo kubwa sana naona mbwa wawili hawatoshi nahitaji mbwa kuanzia 6 kwenda mbele..
swali langu ni: naweza fuga aina tofauti za mbwa nikafuga German wawili,belgian tuveren wawili,nk yani nichanganye aina na wote niwafungulie eneo moja??
Kuna madhara ki afya na je wanapatana au ndio isije kua kama ya KUKU kudonoana maana hamna kitu sipendi kama kuona kidonda kwa mbwa au mnyama yeyote ana kidonda.
Mie nafugaga hii mijibwa ya uswazi (koko)
Yenyewe hayana gharama ya misosi maana yanakula chochote yanachokiona hata mavi ya walevi.!
Halafu wakiwa wengi huwa tunaua kisha tunawachuna na kuwapelekea wauza supu wa bar wao huchanganya na nyama ya mbuzi ili kuleta kale kaharufu ka kimbuzimbuzi kisha hupikwa supu na kuuziwa wateja.
Haya gharama lakini yana hasara, ysnakula na hayazalishi kipato chochote, huu uzi unahusu UFUGAJI WA MBWA KIBIASHARA
Hutaki mbwa wa nyama upewe?Lee hii thread ulishawahi kuiona inakuhusu na ma mbwa wako
Naona unatubadilishia tu I'dHutaki mbwa wa nyama upewe?
unaweza wafuga aina zotehizo za mbwa..kwa mfano nina eneo kubwa sana naona mbwa wawili hawatoshi nahitaji mbwa kuanzia 6 kwenda mbele..
swali langu ni: naweza fuga aina tofauti za mbwa nikafuga German wawili,belgian tuveren wawili,nk yani nichanganye aina na wote niwafungulie eneo moja??
Kuna madhara ki afya na je wanapatana au ndio isije kua kama ya KUKU kudonoana maana hamna kitu sipendi kama kuona kidonda kwa mbwa au mnyama yeyote ana kidonda.
Mkuu vipi hao puppies bado wapo? How much?Habari wadau puppy wanauzwa wana umri wa mwezi 1na siku 4 wamepata chanjo Dhlp na kadi zao zipo.Pichani ni mama yao na baba yaoView attachment 1065984View attachment 1065985View attachment 1065987View attachment 1065988View attachment 1065989View attachment 1065990View attachment 1065991
Sent using Jamii Forums mobile app
Aisee, siyo kitu kizuri lakini.
Kuwa na aina tofauti tofauti za mbwa siyo vizuri sana.
Changamoto inakuwa katika swala la kupandana.
Utatakiwe uwe makini sana majike yanapokuwa kwenye ‘Heat’.
Ili jike la GS mfano lisije likapandwa na dume la Rottweiller nakadhalika nakadhalika.
Ukifanya hiyo cross-breedings utakuwa unapata watoto wa mbwa wenye sura za ajabu ajabu mno.
Wewe fikiria mfano upandishe kati ya Boreboel na German Shepherd.
Je, puppies watakuwa na sura gani??!! Na nakuhakikisha kila mnunuzi wa mbwa atakuwa anakukimbia.
Ushauri: Fuga aina moja tu ya breed. Usichanganye breed nyingi katika eneo moja la kufugia.
Ukiamua kufuga zaidi ya breed moja kwenye eneo moja ina bidi ugeuke kuwa Watchman majike yanapoingia kwenye heat. Hii inaitwa kupiga chabo.
Matokeo yake utajikuta unakuwa unanuka harufu kama ya kiwonder cha Tanuru dogo la mikate.
Ila kama utakuwa na huo uwezo wa kusimamia, unaweza kufuga hizo breeds tofauti tofauti. Ila nikujipatia pressure tu bila sababu ya msingi.
Tafuta breed moja tu unayoipenda sana katika moyo wako ufuge.
Na ukweli ni kwamba hata ukiwa nao wengi wa aina moja, wakati wa kupandana inafaa uruhusu wazazi wenye ubora ndo wapandane ili angalau uweze kupata puppies wenye ubora mkubwa na mzuri.
Unapatikana wapi mkuu nikitaka Germanhao mbwa walipigwa marufu nchi nyingi ninavyosikiaga, ni hatari sana.
Kuhusu kufuga koko ni hasara sana kwani huwezi hata kuuza akizaa.
Mimi nilianza kwa kufuga koko nikahamia German na belgian shephard sijawahi kujuta
Ukiepeleka polisi hawawezi kukufundishia mbwa wako? Hakuna manual ya jinsi ya kunfundisha mmbwa unavotaka??G.S Kupata pure kazi saaana na ni ghali mi nilipata Zambia, RW ndo nnae mpaka sahivi, GS Aliibiwa hawa watu unaotumia kuwapa train mbwa wengi sio waaminifu haswa wakikuta una pure breed, Fanya kila njia ujue jinsi ya kuwapa train we mwenyew, haya ma pitbull sijakutana nayo pure, nilipata crossbreed, yana nguvu sana ila sasa kama linanguvu halafu zito kuelewa la kazi gani sasa
Mi nadhani familia nzima inapaswa kizoeana na mbwa maana bila hivyo huyo aliyezoena naye asipokuwepo itakuwa shida sanaNgoja niwape kisa kilimtokea family friend mmoja mwaka 2015 msimu wa xmass na mwaka mpya.
Jamaa alikuwa na GS wako nane. Kawaida huwapa msosi kila siku usiku mida ya saa 4 baada ya watu wote kuingia ndani maana ni wakali mno. Na zoezi la chakula kuna shamba boy huwa ndie anawahudumia mbwa.
Sasa shamba boy xmass alienda kwao kula sikukuu. Na family friend yeye ni mtu wa tungi sana huwa anakesha baa na wajomba zangu.
Siku shamba boy alipoondoka jamaa akawa amelewa zake akarudi home akapitiwa akalala (mbwa hawakupewa chakula kama kawaida).
Akaamka asubuhi akaandaa msosi vizuri akafungulia banda la kwanza. (Amewagawa katika mabanda mawili wanne wanne).
Baada ya kufungua banda la kwanza mbwa mmoja akaanza kumkoromea kwa hasira sana kisha akamrudia, wale wengine watatu nao wakamrukia wakaanza kumrarua kwa hasira, wale wengine ndani nao wakapandwa na wazimu mpaka wakavunja banda wakaungana na wenzao.
Mke wa jamaa ni mayowe tu kwa dirishani anashuhudia mumuwe anavyotafunwa bila kuwa na lakufanya. Watoto vilio mpaka majirani wakasogea karibu.
Bahati nzuri kuna mtoto wa jirani ni rafiki wa shamba boy na mara nyingi wakiwa wanalisha mbwa wanakuwa wote hivyo wale mbwa wamemzoea sana.
Basi dogo ndio kuingia pale akawatuliza mbwa na jamaa kukimbizwa hospital ambapo alilazwa miezi mitatu akiwa hana fahamu.
Kusema ukweli yule jamaa kama angekuwa kapuku wala asingepona kwa shambulio lile. Pesa ilimuokoa.
Baada ya kurudi uraiani alikuwa amefungwa POP miguuni wala kutembea bila magongo hawezi. Aliwatandika risasi mbwa wote na mpaka sasa sijui kama anafuga tena.
Mbwa ni Loyal Friend kuliko hata binadamu lakini ni hatari sana pia.
Wafugaji tuzingatie Terms and Conditions
[emoji190] [emoji240]