Wagiriki nini kiliwakuta? Sasa hivi hamna tena Wagiriki wenye akili kama zamani?

Wagiriki nini kiliwakuta? Sasa hivi hamna tena Wagiriki wenye akili kama zamani?

Mkuu ukiachana na imani(Si kwamba nakejeri) Yesu alikuwa na uwezo gani mpaka wewe kumchukulia moja ya Watu wenye akili Zaidi.
Yesu anamzidi hata Isaac Newton kweli.
Japo aliishi miaka 33 na kufanya kazi yake kama rabi kwa mmuda wa miaka 3 aliweza kufanya mengi makubwa ambapo mpaka leo hii ulimwengu hautamsahau kamwe.

kafariki takribani miaka 2000 iliyopita lakini kila siku wafuasi wake wanazidi kuongezeka, hzamani kulikuwa na watu mashuhuri na maarufu wengi sana waliofanya mambo mengi kama vile Mose, Imhotep, Caesar Augustus, Archimedes, Pharaoh Rammiress II, Socrates, Spartacus, Leonidas, Plato, Alexander the Great, Aristottle, Ibrahim, Nebucadnezar na wengineo wengi. Lakini ndani ya miaka mitatu tu aliweza kuvunja rekodi za watu wote hao mashuhuli na kubaki yeye ndiyo kinara.

Miaka imepita lakini mpaka leo hakuna mtu ambaye ameweza kuvunja rekodi yake, anafahamika kama mwanafalsafa, mtabiri na mwanasayansi nguli aliyewahi kuishi na hatokuja kutokea kama yeye.

Vitabu vyenye mafundisho yake ndio vinaongoza kuuza kuliko vyote, ni binaadamu ambae jina lake linazidi kukua kila siku badala ya kufifia japo ni miaka 2000 imepita. Wafuasi wake wengi wamekuja kuwa ni watu mashuhuri na wanafalsafa wakubwa kama vile Paulo, Thomas aquinus, Francis of Assis, Ignatus Luyola, St Luke, Francis Xvery, John Paul II, nk.
 
Wapo, ila siku hizi hawana promo tena, kila zama na zama zake...
 
Ku a muda natamani tukae tupige historia za Mesopotamia, Misri, Israel,Norway, Greece, basi tu hua Napenda sana masuala ya historia na deity mbalimbali...
Ila misri kwakua ni hapahapa Afrika napenda Zaid.

wakati mfamle Themistocles wa Jiji la Athens (Ugirki) anahangaika kuhamasisha wafalme wa majiji mengine kama Queen Gogo, King Leonidas waungane wawe taifa moja wao wamisri walikua wanafanya vumbuzi kubwa kubwa zilizoacha ulimwengu kinywa wazi. Nitaorodhesha baadhi ya mambo machache ambayo yamegunduliwa na wamisri weusi kipindi hiko hata Amerika kunakaa nyani na sokwe ,Red Indian na Wamaya

Baadhi ya vitu vilivyogunduiwa na wamisri

Mathematics
Wakati wanasayansi kutoka ugiriki kama Euclid,Pythogras,Archimedes na ugiriki kwa ujumla wakipewa heshima ya kuvumbua hisabati lakini ukweli mchungu ni kwamba wamisri ndio wamegundua hisabati. Geometry,survey,vyote hvyo vimegunduliwa Misri.

Maandishi
Wamisri ndio waliogundua mfumo wa kuweka lugha yao katika maandishi, walikua na mfumo wao wa maandishi unaitwa pictograms, kutokana na picha hizo ndipo kulipozaliwa herufi mbalimbali lakini hii iliendelezwa zaidi na wagiriki’

Dawa ya meno
Kama meno yako ni meupe na masafi basi nenda katambikie kuheshimu mizimu ya mababu zenu wa kimisri maana bila wao tusingepata dawa ya meno.

Wigi, Make-Up na Vipodozi
Mnasikia kua mwanamke mzuri zaidi duniani ni Cleopatra, basi uzuri wake ulichagizwa na vipodozi na make ups za kutosha. Wewe dada waheshimu sana wamisri maana bila wao sijui ingekuaje, miaka hiyo hata Yakobo hajahamia misri..watu wa misri walikua washagundua kuvaa mawigi,kutengeneza vipodozi na kufanya make up. Wanja na kuchonga nyusi kumeanzia huko misri, mafarao ilikua sifa kwao kupaka wanja na make up..nyusi wananyoa zote. Ikumbukwe kwamba wamisri walikua hawapaki wanja kama urembo ila ilikua ni kwa ajili ya imani zao pia waliamini kufanyia macho urembo kulikua kunawasaidia kuwakinga na magonjwa ya macho.

Wino Mweusi, Karatasi na Meza
Juhudi za watu weusi ndio zinafanya wazungu waweze kukaa na kuandika propaganda zao kuhusu watu weusi.wamisri ndio wamegundua wino mweusi kwa ajili ya kuandikia na kutengeneza meza. Wakati wazungu na watu wa jamii zingine wakitumia mbao,mawe na ngozi katika kuandika Wao wamisri walivumbua Karatasi za kuandikia zilikua zinaitwa “papylus sheets”. Baadae wagiriki waliziboresha na kuziita paper kutokana na neno Papyrus.

Mashine za kuvuna na kusaga nafaka na kilimo cha umwagiliaji
Wao ndio walivumbua mashine za kuvuna na kusaga/kukoboa nafaka hasa ngano, miaka hii Israel ndio inasifika kwa kilimo cha umwagiliaji na kua sehemu ya tafiti za kilimo cha umwagiliaji duniani lakini ukweli ni kwamba misri ya kale ndio ilianza kugunda kilimo cha umwagiliaji. Wamisr wa kale walijenga mifereji mingi kusambaza maji kutoka mto nile kupeleka mashambani.

Majira na Kalenda
Wakati red Indians wa marekani wakiokota matunda nan a kuwinda wadudu kama mlo wa siku kwenye misitu mikubwa iliyokuwepo Newyork miaka ya 1300AD, Miaka karibia elfu kadhaa iliyopita kabla ya Kristo wazee wa Afrika kutoka misri walikua wameshagundua jinsi ya kutambua saa za siku na kutengeneza kalenda ya kuonyesha majira ya mwaka. Kalenda yao ilikua na miezi 12 na siku 365, kila mwezi ulikua na siku 30…lakini pia walikua washatengeneza saa zao za asili ajili ya kupima masaa ya siku.

Kufuli
Wamisri ndio watu wa kwanza kuvumbua kufuli, unambiwa funguo za kufuli zao zilikua zinauweza kua na urefu wa futi 2. Lakini hawa mababu pia sometimes kwenye IT tunawataja kama watu wa kwanza kutengeneza codes, maana ile milango ya Pyramids kuna mingine haifunguliwi na funguo ila ni codes Fulani walizoziweka miaka zaidi ya elfu 5 iliyopita. Hivyo hata coding tunaweza sema imeanzia misri.

Polisi na Serikali
Kama ulikua hujui basi ndio hivyo polisi zimeanzishwa kwa mara ya kwanza misri, polisi walikua wanatumia siraha na mbwa katika kufanya doria zao. Hakuna maskini wala tajiri aliyekua juu ya sharia halafu adhabu zao ilikua kukupa kichapo, kukuhasi,kukata pua na maskio halafu ukifa ulikua huzikwi unatupwa kama mzoga. Wamisri walikua wanaamini kwamba ukizikwa kwa heshima basi kunauwezekano mkubwa wa kwenda kwenye maisha ya baadae/mbinguni/Afterlife. Mifumo hii ya serikali zetu duniani unazoziona sasa imetengenezwa na wamisri ndio maana Yosef mtoto wa Israel alikua waziri mkuu kipindi kile. Yaani wakati Abrahm Lincoln anatunga definition ya Democracy huko misri wao walikua washamaliza kia kitu kuhusu mifumo-endeshi ya serikali (ujamaa,Udikteta,ubepari nk nk)

Egyptian Hieroglyphics (Aka Emoji za Misri😆)

View attachment 1902031
Hii ni michoro adhimu kabisa iliyobuniwa na wazee wa kiafrika ili kuwasiliana, pia zilikua zinatumika kueleza matukio yaliyopita na yajayo..so ilitumika kuweka rekodi za jamii ya watu wa misri. Unaweza kuona mchorouiliochorwa miaka zaidi ya elfu tano iliyopita ukionyesha image ya aeroplane ni ile ie iliyochorwa na Davinci miaka ya 1600sBC
Heshima yako mkuu!
Kwa historia ulipaswa upewe PHD ya heshima ila nashangaa wamempatia mh Kasheku Musukuma wanawaacha watu wanaostahili.
 
Ok, Ahsante kwa ufafanuzi.
Ila wababeli walikua watabe sana aisee enzi hizo.
Sisi tule bata au tuhonge hatutafikia alivyofanya Nebuchadnezzar.
Nebuchadnezzar alifanya sherehe kwa miezi mitatu yaani wanasherehekea wanalala wanaamka wanasherehekea wanalala kila siku hafi miezi mitatu full pombe,nyama na Chakula. Sijui hali yao ilikuaje baada ya hapo maana ndio sherehe iliyofanyika muda mrefu zaidi kama kumbukumbu zangu ziko sawa ndipo Nebuchadnezzar alipotumia vikombe vya hekalu la Mungu kunywea pombe mkono ukatokea ukaandika ukutani (sina uhakika kama ni Nebuchadnezzar)

Akamuhonga mke wake bustani yenye kila ua lililopatikana enzi zile
Zaid ya biblia ni kitabu gani nisome niweze kupata hii historia ya kale mkuu?
 
Ukiniambia nitaje Binaadamu watano wenye akili zaidi duniani nitataja hawa.
1. Imhotep
2.Leonado da Vinci
3. Yesu
4. Nikola Tesla
5. plato

Imhotep ndio baba wa gunduzi zote kunzia hesabu za Geometry, Upasuaji wa ubongo, pyramids na Maze Tombs zilizojengwa Misri katengeneza yeye. Huyu jamaa wagiriki wanamuabudu kama Mungu wa tiba na madawa maana alikua daktari wa kila kitu. Alikua Polymath kwelikweli kuliko hata Da'Vinci. Michoro yote ya Misri katengeneza yeye.



Alikuwa mtu mweusi ..
Egyptian wote walikuwa blacks
Hadi kina Ramses..
 
Zaid ya biblia ni kitabu gani nisome niweze kupata hii historia ya kale mkuu?
Mkuu huu uzi una mwendelezo wake, nilijikita zaidi kwenye anguko la misri. Ngoja nikutag huko
 
Mkuu ukiachana na imani(Si kwamba nakejeri) Yesu alikuwa na uwezo gani mpaka wewe kumchukulia moja ya Watu wenye akili Zaidi.
Yesu anamzidi hata Isaac Newton kweli.
1.Alitembea Juu ya Maji.
2.Alimfufua Lazaro.
3.Alilisha watu elfu tano kwa Samaki wawili na Mikate Mitano na Mabaki ya samaki na mikate yakajaza vikapu 12.
4.Aliponya Vipofu,wakaona na Viziwi Wakasikia.
5.Aligeuza Maji kuwa Pombe kwenye harusi kule kana.
6.Alipokata roho pazia la hekalu lilipasuka na Wafu wakafufuka.
7.Mwenyewe alifufuka.

Sio isaack Newton tu bali hakuna mwanasayansi yeyote anayeweza kuikaribia hiyo CV.
 
Zaid ya biblia ni kitabu gani nisome niweze kupata hii historia ya kale mkuu?
Tembelea Maktaba za Kale hasa middle East utapata vitabu vingi tu mfano injili ya Nicodemu.
Hivi vichache walivikusanya watu wa dini na kuamua kuvitengenezea Kitabu kimoja kiitwacho Biblia.Sio Vitabu vyote vilivyoandika historia ya Yesu viliunganishwa kwenye Biblia.
 
Hivi unajua sehemu kama Egypt, Mesopotamia, Crete, Syria, Anatolia, Iran, and the Indus Valley walipata civilization kabla hata ya wagiriki....

Pia wachina waligundua mengi na kusafiri hata kabla ya wengi ambao ndio wamekuwa accredited na ugunduzi huo...

Kwa ufupi ni utamaduni, kukiwa na utamaduni wa kuhoji na watu kupenda kujifunza basi jamii itagundua vitu na kuendelea (Binadamu wanazaliwa wakiwa a Blank Slate) Tabula Rasa ila jamii inayowazunguka ndio inawajengea wawe watu wa aina gani...

Iran ilikuwa imepiga hatua sana, lakini kuingia mambo ya imani all was destroyed in few years. Wachina walikuwa wamesafiri duniani kote tangia zamani ila Mfalme wao kupiga marufuku culture za nje ikawapunguzia kasi...

Kwahio na sisi hizi indoctrination kwamba kila kitu tumepewa au kila kitu kina sababu, hakuna kuhoji wala kutafuta ukweli usishangae miaka milioni moja ijayo tukawa bado tunapiga ramli na kudhani ni Jirani yetu katuloga, au tukiugua ni Mungu amependa.
Wachina noma, marcopolo baada ya kurudi kwao akawa anawasimulia kuhusu china nyumba, matumizi ya pesa, icecream na mengine lakini wakawa hawaamini maana ilikuwa ni mbele ya wakati na hawakuwahi sikia vitu kama hivyo
 
Wachina noma, marcopolo baada ya kurudi kwao akawa anawasimulia kuhusu china nyumba, matumizi ya pesa, icecream na mengine lakini wakawa hawaamini maana ilikuwa ni mbele ya wakati na hawakuwahi sikia vitu kama hivyo
Umemtaja Marco Polo umenikumbusha huyu jamaa na Silk road. Wachina wamemtemgenezea muvi nyingi sana..Ila Japan na England naziheshimu sana hizi nchi, ni visiwa tu ila mambo yake noma sana. Sasa hivi ndio wamepunguza makali
 
1.Alitembea Juu ya Maji.
2.Alimfufua Lazaro.
3.Alilisha watu elfu tano kwa Samaki wawili na Mikate Mitano na Mabaki ya samaki na mikate yakajaza vikapu 12.
4.Aliponya Vipofu,wakaona na Viziwi Wakasikia.
5.Aligeuza Maji kuwa Pombe kwenye harusi kule kana.
6.Alipokata roho pazia la hekalu lilipasuka na Wafu wakafufuka.
7.Mwenyewe alifufuka.

Sio isaack Newton tu bali hakuna mwanasayansi yeyote anayeweza kuikaribia hiyo CV.
Asante kwa ufafanuzi Mzuri.
Lakini kulingana na sifa ulizi taja yesu naona mengi alifanya Mazingaombwe (Miujiza) wala hakuna ugunduzi alio ufanya. Maana angefanya ugunduzi mpaka sasa alichokuwa akifanya angeacha walau Formula ili na wengine wakifanye.

Je, kama yesu alifanya hayo yote na hakuna alio waachia urithi (kuendeleza) miujiza hiyo nitakuwa ninakosea kusema alikuwa Mbinafsi? NB: si kwamba nakufuru ila ni mawazo tu.

Hitimisho kulingana na Miujiza ya Yesu hatolinganishwa na watu wasio na miujiza kama akina Galilei Galileo, Newton, Aristottle, Faraday, Archimedes, n.k hivyo alipaswa kushindanishwa na watenda miujiza wenzake kama Ngh'wana Malunde (Wa kabila la kisukuma).
 
Japo aliishi miaka 33 na kufanya kazi yake kama rabi kwa mmuda wa miaka 3 aliweza kufanya mengi makubwa ambapo mpaka leo hii ulimwengu hautamsahau kamwe.

kafariki takribani miaka 2000 iliyopita lakini kila siku wafuasi wake wanazidi kuongezeka, hzamani kulikuwa na watu mashuhuri na maarufu wengi sana waliofanya mambo mengi kama vile Mose, Imhotep, Caesar Augustus, Archimedes, Pharaoh Rammiress II, Socrates, Spartacus, Leonidas, Plato, Alexander the Great, Aristottle, Ibrahim, Nebucadnezar na wengineo wengi. Lakini ndani ya miaka mitatu tu aliweza kuvunja rekodi za watu wote hao mashuhuli na kubaki yeye ndiyo kinara.

Miaka imepita lakini mpaka leo hakuna mtu ambaye ameweza kuvunja rekodi yake, anafahamika kama mwanafalsafa, mtabiri na mwanasayansi nguli aliyewahi kuishi na hatokuja kutokea kama yeye.

Vitabu vyenye mafundisho yake ndio vinaongoza kuuza kuliko vyote, ni binaadamu ambae jina lake linazidi kukua kila siku badala ya kufifia japo ni miaka 2000 imepita. Wafuasi wake wengi wamekuja kuwa ni watu mashuhuri na wanafalsafa wakubwa kama vile Paulo, Thomas aquinus, Francis of Assis, Ignatus Luyola, St Luke, Francis Xvery, John Paul II, nk.
Asante, ukiweza pitia kidogo comment #175
Labda utanipa elimu zaidi.
 
Ukiniambia nitaje Binaadamu watano wenye akili zaidi duniani nitataja hawa.
1. Imhotep
2.Leonado da Vinci
3. Yesu
4. Nikola Tesla
5. plato

Imhotep ndio baba wa gunduzi zote kunzia hesabu za Geometry, Upasuaji wa ubongo, pyramids na Maze Tombs zilizojengwa Misri katengeneza yeye. Huyu jamaa wagiriki wanamuabudu kama Mungu wa tiba na madawa maana alikua daktari wa kila kitu. Alikua Polymath kwelikweli kuliko hata Da'Vinci. Michoro yote ya Misri katengeneza yeye.
Hao wengine kazi zao zinagusa jamii yote ila kwa Yesu hapana umemuweka kishabiki tu hana lolote kwa Yesu ana faida gani kwa watu wasiokuwa na dini au ana faida gani au wanaofata dini ya budha au ana faida gani kwa dini za kigiriki utakuja kuona hana faida kihivyo pia hakuna jambo kubwa alilofanya likagusa dunia nzima huyo hawezi kuwa na akili dunia nzima au genisus maana yake ufalme wake Yesu upo kwa wakristo na waislam tu wayahudi hawamtambui kitu wanaona ana laana ya torati
Ila mtu kama tesla kazi yake inaonekana kila mtu Anajua uwe huna dini au unayo itakugusa tu huyo unaweza sema mtu mwenye akili ila sio huyo Yesu wenu ambaye ufalme wake kwenu wakristo na waislam
 
Hao wengine kazi zao zinagusa jamii yote ila kwa Yesu hapana umemuweka kishabiki tu hana lolote kwa Yesu ana faida gani kwa watu wasiokuwa na dini au ana faida gani au wanaofata dini ya budha au ana faida gani kwa dini za kigiriki utakuja kuona hana faida kihivyo pia hakuna jambo kubwa alilofanya likagusa dunia nzima huyo hawezi kuwa na akili dunia nzima au genisus maana yake ufalme wake Yesu upo kwa wakristo na waislam tu wayahudi hawamtambui kitu wanaona ana laana ya torati
Ila mtu kama tesla kazi yake inaonekana kila mtu Anajua uwe huna dini au unayo itakugusa tu huyo unaweza sema mtu mwenye akili ila sio huyo Yesu wenu ambaye ufalme wake kwenu wakristo na waislam
@Iblis Bin Shetan
 
Opium ndiyo hutengeneza anaesthesia au nusu kaputi anayopewa mgonjwa na kuruhusu tiba ya upasuaji iendelee bila mgonjwa kusikia maumivu.
Ahsante kwa kunijuza!
Ila ningependa kuuliza pia, historia inaonyesha kwamba upasuaji ulianzia misri, maana vifaa vya upasuaji vimegunduliwa huko!
Je wao walitumia nini wakati wa kufanya upasuaji?? Au ndio ilikua live bila ganzi, Ningependa kujua historia ya upasuaji maana sifahamu sana maswala ya utabibu
 
Back
Top Bottom