Wagiriki nini kiliwakuta? Sasa hivi hamna tena Wagiriki wenye akili kama zamani?

Wagiriki nini kiliwakuta? Sasa hivi hamna tena Wagiriki wenye akili kama zamani?

Sisi uonevu umezidi,yaani ukigundua kitu halafu hujasoma wasomi lazima wakuwekee zengwe.
Ila ushauri wangu Kwa wagunduzi wanapogundua kitu wakitupie moja Kwa moja kwenye mitandao ya jamii
Nalog off
Mkuu
Autodidact ni watu wenye uwezo wa kujifunza vitu wa pekee yao (self-taught), kuna watu wamejaliwa kipaji hichi cha kujifunza wao pekee yao. Watu hawa hua hawahitaji mwalimu awasimamie au kuwafunza vitu ili waelewe bali wanachohitaji ni kujua is where to find right material for them to read…Watu hawa ukilazimisha wafundishwe na mwalimu kamwe hawawezi kuelewa, wataishia kufeli tu.

Mara nyingi watu wenye low latent Inhibition ndio hua na hali hii pia ya Autodidactism, wanasayansi wengi hawakupita vyuoni bali walitumia LLI yao kujifunza vitu na kugundua mambo mengi mapya..!

Baadhi ya watu maarufu ambao walikua ni autodidact ni galileo, Da vinci, Euclid, Socrates, Plato, Pythogras, nk.. zaidi unaweza kutizama orodha hapa

Hebu niambie ni chuo gani alisomea Archimedes,Da Vinci nk.
Basi tu waafrika tumelaanika kwa matendo yetu
 
Mimi jameni Nina waswasi na huu weusi wetu... Haiwezkan kila shida zetu! Kutengwa! Uchawi(kuna mtu uchiz aliupatia eapoti alkuw anaend ulaya scholarship) had Leo anaokot makopo pale mnaz mmoja. Umaskin w kutupwa alaf tuna 60 year tok uhur na bado mpaka Leo tunalaum wazungu [emoji28]
Tusbirin kufa tu tutengenezew mpak elimu na historia yetu wenyew.. watu weusi dah! Mi siamin Kam wamisri hao w miaka hiyo ni weusi mkuu
 
Ku a muda natamani tukae tupige historia za Mesopotamia, Misri, Israel,Norway, Greece, basi tu hua Napenda sana masuala ya historia na deity mbalimbali...
Ila misri kwakua ni hapahapa Afrika napenda Zaid.

wakati mfamle Themistocles wa Jiji la Athens (Ugirki) anahangaika kuhamasisha wafalme wa majiji mengine kama Queen Gogo, King Leonidas waungane wawe taifa moja wao wamisri walikua wanafanya vumbuzi kubwa kubwa zilizoacha ulimwengu kinywa wazi. Nitaorodhesha baadhi ya mambo machache ambayo yamegunduliwa na wamisri weusi kipindi hiko hata Amerika kunakaa nyani na sokwe ,Red Indian na Wamaya

Baadhi ya vitu vilivyogunduiwa na wamisri

Mathematics
Wakati wanasayansi kutoka ugiriki kama Euclid,Pythogras,Archimedes na ugiriki kwa ujumla wakipewa heshima ya kuvumbua hisabati lakini ukweli mchungu ni kwamba wamisri ndio wamegundua hisabati. Geometry,survey,vyote hvyo vimegunduliwa Misri.

Maandishi
Wamisri ndio waliogundua mfumo wa kuweka lugha yao katika maandishi, walikua na mfumo wao wa maandishi unaitwa pictograms, kutokana na picha hizo ndipo kulipozaliwa herufi mbalimbali lakini hii iliendelezwa zaidi na wagiriki’

Dawa ya meno
Kama meno yako ni meupe na masafi basi nenda katambikie kuheshimu mizimu ya mababu zenu wa kimisri maana bila wao tusingepata dawa ya meno.

Wigi, Make-Up na Vipodozi
Mnasikia kua mwanamke mzuri zaidi duniani ni Cleopatra, basi uzuri wake ulichagizwa na vipodozi na make ups za kutosha. Wewe dada waheshimu sana wamisri maana bila wao sijui ingekuaje, miaka hiyo hata Yakobo hajahamia misri..watu wa misri walikua washagundua kuvaa mawigi,kutengeneza vipodozi na kufanya make up. Wanja na kuchonga nyusi kumeanzia huko misri, mafarao ilikua sifa kwao kupaka wanja na make up..nyusi wananyoa zote. Ikumbukwe kwamba wamisri walikua hawapaki wanja kama urembo ila ilikua ni kwa ajili ya imani zao pia waliamini kufanyia macho urembo kulikua kunawasaidia kuwakinga na magonjwa ya macho.

Wino Mweusi, Karatasi na Meza
Juhudi za watu weusi ndio zinafanya wazungu waweze kukaa na kuandika propaganda zao kuhusu watu weusi.wamisri ndio wamegundua wino mweusi kwa ajili ya kuandikia na kutengeneza meza. Wakati wazungu na watu wa jamii zingine wakitumia mbao,mawe na ngozi katika kuandika Wao wamisri walivumbua Karatasi za kuandikia zilikua zinaitwa “papylus sheets”. Baadae wagiriki waliziboresha na kuziita paper kutokana na neno Papyrus.

Mashine za kuvuna na kusaga nafaka na kilimo cha umwagiliaji
Wao ndio walivumbua mashine za kuvuna na kusaga/kukoboa nafaka hasa ngano, miaka hii Israel ndio inasifika kwa kilimo cha umwagiliaji na kua sehemu ya tafiti za kilimo cha umwagiliaji duniani lakini ukweli ni kwamba misri ya kale ndio ilianza kugunda kilimo cha umwagiliaji. Wamisr wa kale walijenga mifereji mingi kusambaza maji kutoka mto nile kupeleka mashambani.

Majira na Kalenda
Wakati red Indians wa marekani wakiokota matunda nan a kuwinda wadudu kama mlo wa siku kwenye misitu mikubwa iliyokuwepo Newyork miaka ya 1300AD, Miaka karibia elfu kadhaa iliyopita kabla ya Kristo wazee wa Afrika kutoka misri walikua wameshagundua jinsi ya kutambua saa za siku na kutengeneza kalenda ya kuonyesha majira ya mwaka. Kalenda yao ilikua na miezi 12 na siku 365, kila mwezi ulikua na siku 30…lakini pia walikua washatengeneza saa zao za asili ajili ya kupima masaa ya siku.

Kufuli
Wamisri ndio watu wa kwanza kuvumbua kufuli, unambiwa funguo za kufuli zao zilikua zinauweza kua na urefu wa futi 2. Lakini hawa mababu pia sometimes kwenye IT tunawataja kama watu wa kwanza kutengeneza codes, maana ile milango ya Pyramids kuna mingine haifunguliwi na funguo ila ni codes Fulani walizoziweka miaka zaidi ya elfu 5 iliyopita. Hivyo hata coding tunaweza sema imeanzia misri.

Polisi na Serikali
Kama ulikua hujui basi ndio hivyo polisi zimeanzishwa kwa mara ya kwanza misri, polisi walikua wanatumia siraha na mbwa katika kufanya doria zao. Hakuna maskini wala tajiri aliyekua juu ya sharia halafu adhabu zao ilikua kukupa kichapo, kukuhasi,kukata pua na maskio halafu ukifa ulikua huzikwi unatupwa kama mzoga. Wamisri walikua wanaamini kwamba ukizikwa kwa heshima basi kunauwezekano mkubwa wa kwenda kwenye maisha ya baadae/mbinguni/Afterlife. Mifumo hii ya serikali zetu duniani unazoziona sasa imetengenezwa na wamisri ndio maana Yosef mtoto wa Israel alikua waziri mkuu kipindi kile. Yaani wakati Abrahm Lincoln anatunga definition ya Democracy huko misri wao walikua washamaliza kia kitu kuhusu mifumo-endeshi ya serikali (ujamaa,Udikteta,ubepari nk nk)

Egyptian Hieroglyphics (Aka Emoji za Misri[emoji38])

View attachment 1902031
Hii ni michoro adhimu kabisa iliyobuniwa na wazee wa kiafrika ili kuwasiliana, pia zilikua zinatumika kueleza matukio yaliyopita na yajayo..so ilitumika kuweka rekodi za jamii ya watu wa misri. Unaweza kuona mchorouiliochorwa miaka zaidi ya elfu tano iliyopita ukionyesha image ya aeroplane ni ile ie iliyochorwa na Davinci miaka ya 1600sBC
Hapo kwenye maandishi umenena vyema.
Hope hata Yale mapango yetu ya Tanzania yakiyochorwa maandishi na picha ambazo watz tumeshindwa kuyatafsiri yana maana ndani yake.

Kuna Yale maandishi/michoro ya kule kondoa sijui Kolo pana Elimu ya kale pale.
Yes pamoja na kusoma sayansi but napenda historia nimefatilia maandishi yakale ktk vitabu vya zamani Sana nimebahatika kupata kalamu za kizamani zipatazo 100+
JPEG_20210822_092124_8694214751192092198.jpg
JPEG_20210822_092200_3616396696848462496.jpg
 
Mbona jibu ni simple, empire zina raise and fall. zikifa zinaacha baadhi ya alama zake. Hizi alama ni kama majengo monument : pyramid, great wall, hanging garden, aztec, na utamaduni. Katika utamaduni na ustaarabu wa kijiongoza hapa ugiriki ndipo utakapo mwona. Demokrasia ilizaliwa athen, olympic tornament zilianza huko kwao katika milima mount olympia.
Na inapoanguka empire moja nyingine inasimama it just a circle ulimwengu unapitia we have to accept. Alipotoka ugiriki alikuja Rome alikaa ambaye alikop tamaduni karibia zote za ugiriki kasoro jeshi.
 
Hii kwako mr Da'Vinci na kwa wengine wenye mitazamo eti wamisri walikuwa weusi tii. sijui ni misingi gani mnabase your claim. Nadhani mnatumia misingi ya ubara na urangi, eti kwa kuwa misri ipo pamoja na bara la Afrika, eti kama njia ya kuonyeaha mtu mweusi nae yumo. Si sawa kufanya hivyo tafuta ukweli na ukweli atakuweka huru.
Mimi napinga kuwa wamisri wa kale walikuwa weusi kwa kutumia kanuni za kigeographia. Yatupasa kujua watu katika sayari yetu hapo kale walikuwa wametenganishwa kwa namna mbalimbali: kuna bahari,kuna mito, kuna mabonde ya ufa, kuna milima, na pia kuna majangwa. Hili la mwisho jangwa watu huwa hawazingatii kabisa lakini sisi waafrika rangi nyeusi twapaswa kujua the great sahara desert kama moja wapo wa ukinzani uliotukinga na maendeleo kwa miaka mingi hapo nyuma.
Ukitazama ramani yako chini ya jangwa la sahara ndio kuna watu weusi juu yake kuna watu rangi nyeupe. Ukiuliza kwa nini ni kwa sababu ilikuwa haiwezekani enzi hizo weupe kushuka chini na weusi kwenda juuu. In short wamisri wenyewe walishindwa kufwatilia chanzo cha mto nile kutokana na ukakasi uliletwa na jangwa. Imagine wamisri wangefika Victoria si wangetuabudu kama miungu wao na kutupa ujuzi wao wote. Mbali na kuwa kizuizi kikuu pia ilipelekea kusini kutokupata farasi na farasi ndio ilikuwa yaendesha uchumi kipindi hicho. Sasa tunapata taabu sana kwa sababu kuna baadhi ya stage wafrika weusi hatujapitia katika maendeleo yetu.
 
Aliekwambia hakina faida nani?
Hii formula inaelezea nature.
Huwezi jenga jengo kubwa bila kutumia hio formula.
Hio formula ina maximum na minimum, kwa mantiki hio kila chenye maximum na minimum kinatumia hio formula.
Hio formula inakuwa extended na polynomial function which express something in higher degree
Angalia majengo kama viwanja vya mpira, vinatumia tafsiri ya hizo equations.
Waafrika tupo gizani sana na ndio mana hatugundui vitu.
Ukiichunguza formua ya Albert Einstein
F(C) =MC^2 ampapo C is function of f utaona hio ni kanuni ya algebraic equation of second order degree(C^2) ya ax^1 + bx^2 + c ambayo solution yake ndio hio uliondika x= -b +-√(b^2-4ac)/2a

Hii ina mana kwamba nature of energy is quadraticslly formed entity.
Sisi waafrika tunakariri hisabati na sayandi badaka ya kekewa ma jinsi uhusiano wanature na hizo kanunui.
Mpaka leo eti waafrika hatuwezi unda ndege wakati formula zipo vitabuni na hata ndege za wazungu tunazo, tunaweza kufanya reverse engineering tukapata majibu.
We lack curioucity! Then tuna conclude eti formula hazina kazi/ faida.
Wewe umegundua nini mpaka sasa?
 
Nyie endeleeni kusema nani kagundua na hajagundua,, Alafu mbona siwaelewi mara tusimtukuze mzungu,, wakati vitu vyote unavyotumia ametengeneza White people,, white people atabaka kuwa hivyo hivyo na black people mtabaki na akili zetu nyeusi tiii kama rami au oili chafu,,
 
Hii kwako mr Da'Vinci na kwa wengine wenye mitazamo eti wamisri walikuwa weusi tii. sijui ni misingi gani mnabase your claim. Nadhani mnatumia misingi ya ubara na urangi, eti kwa kuwa misri ipo pamoja na bara la Afrika, eti kama njia ya kuonyeaha mtu mweusi nae yumo. Si sawa kufanya hivyo tafuta ukweli na ukweli atakuweka huru.
Mimi napinga kuwa wamisri wa kale walikuwa weusi kwa kutumia kanuni za kigeographia. Yatupasa kujua watu katika sayari yetu hapo kale walikuwa wametenganishwa kwa namna mbalimbali: kuna bahari,kuna mito, kuna mabonde ya ufa, kuna milima, na pia kuna majangwa. Hili la mwisho jangwa watu huwa hawazingatii kabisa lakini sisi waafrika rangi nyeusi twapaswa kujua the great sahara desert kama moja wapo wa ukinzani uliotukinga na maendeleo kwa miaka mingi hapo nyuma.
Ukitazama ramani yako chini ya jangwa la sahara ndio kuna watu weusi juu yake kuna watu rangi nyeupe. Ukiuliza kwa nini ni kwa sababu ilikuwa haiwezekani enzi hizo weupe kushuka chini na weusi kwenda juuu. In short wamisri wenyewe walishindwa kufwatilia chanzo cha mto nile kutokana na ukakasi uliletwa na jangwa. Imagine wamisri wangefika Victoria si wangetuabudu kama miungu wao na kutupa ujuzi wao wote. Mbali na kuwa kizuizi kikuu pia ilipelekea kusini kutokupata farasi na farasi ndio ilikuwa yaendesha uchumi kipindi hicho. Sasa tunapata taabu sana kwa sababu kuna baadhi ya stage wafrika weusi hatujapitia katika maendeleo yetu.
Maelezo yako mazuri kuna point ndani yake ila bado hujaonyesha ni vipi wamisri enzi hizo hawakua weusi.
Nipe facts mkuu zinazoonyesha wamisri walikua weupe...
Ahsante kwa hoja yako mkuu
 
Hakua smart... Ila kwenye top ten ya watu maarufu yeye ni namba mbili baada ya Yesu.
Kwhy alikuwa average au foolish?
Tuachane Na Hayo sehem Gani hapa Kigoma naweza kupata watoto wa Congo Na Rwanda niwe najisevia?Nataka kuoa huku Na Sina rafiki
 
Maelezo yako mazuri kuna point ndani yake ila bado hujaonyesha ni vipi wamisri enzi hizo hawakua weusi.
Nipe facts mkuu zinazoonyesha wamisri walikua weupe...
Ahsante kwa hoja yako mkuu
Watu weusi ni watu gani? Watu wote wa Afrika siyo jamii moja, kuna jamii nyingi tofauti ambazo hazina uhusiano wa kinasaba.
 
Mbona jibu ni simple, empire zina raise and fall. zikifa zinaacha baadhi ya alama zake. Hizi alama ni kama majengo monument : pyramid, great wall, hanging garden, aztec, na utamaduni. Katika utamaduni na ustaarabu wa kijiongoza hapa ugiriki ndipo utakapo mwona. Demokrasia ilizaliwa athen, olympic tornament zilianza huko kwao katika milima mount olympia.
Na inapoanguka empire moja nyingine inasimama it just a circle ulimwengu unapitia we have to accept. Alipotoka ugiriki alikuja Rome alikaa ambaye alikop tamaduni karibia zote za ugiriki kasoro jeshi.

Kwa maana hiyo wewe hata Socrates na Aristotle hukuwahi kuwasikia?

duuuu aisee kazi Ipo Plato ni mwanafalsafa mgiriki aliishi miaka mingi nyuma kabla ya Yesu na sio Ponsio Pilato mrumi ndugu!
Wayahudi tangu walipodai watawaliwe na wafalme ukirejea 1sam 8:1-9,Mungu aliruhusu wafalme wawatawale wakianzia na Saul, Daud na baadaye Sulemani.Hawa wote walianza kazi zao vizuri lakini polepole mwishoni mwa kazi zao hawakuweza kuendelea kuyashika maagizo ya Bwana na hivyo wakalifanya taifa zima kupotea njia.Mambo kama haya ndiyo hatimaye yanawapeleka waisrael utumwani mnamo mwaka 587 KK.

Ilipofika mwaka 63 KK nchi ya wayahudi ikiwa chini ya utawala wa Aristobulus II, ilitekwa na warumi waliokuwa wakiongozwa na Pompey.Warumi hawa waliitawala nchi ya wayahudi kutoka Roma.Wafalme walioitwa Makaisari walikaa Roma na nchi zote walizoziteka walizigawa katika mikoa ambayo iliwekwa chini ya magavana. Hawa magavana waliweka wafalme wa kienyeji. Kumbe, hawa wafalme wa kienyeji walitawala chini ya gavana wa kirumi.Ni kama kwa mfano jinsi wakoloni hapa nchini kwetu walivyoteua machifu kuongoza badala yao enzi za ukoloni.Hapa naweza kukutajia magavana wachache kati ya wengi wanaojulikana kama Ponsio Pilato,Titus,Felix,Festus n.k
Kumbe jina Herode ni jina la ukoo uliotawala nchi ya Palestina kwa muda wa miaka 47 kabla ya Kristo na miaka 79 baada ya kuzaliwa Kristo.Hawa niliowataja walikuwa wafalme wa kienyeji waliowekwa kutawala badala ya Warumi na kwa kweli hao ndio waliotumia jina Herode.

Pia, watawala hawa yaani maherode, walitoka katika shina moja yaani baba yao alikuwa anaitwa Antipater mtawala wa Idumea, kusini mwa nchi ya Palestina ambaye alikuwa amechaguliwa na Warumi kutawala eneo hilo. Huyu alipata kuzaa mtoto mmoja anayejulikana kama Herode Mkubwa.Huyu Herode Mkubwa,alipewa nafasi ya kutoka katika nchi yake kuja Palestina kwa Wayahudi na kutawala katika mkoa wa Galilaya baada ya kifo cha baba yake na ingawa mwenyewe hakuwa myahudi akatawala tangu mwaka 37-4KK.Wayahudi hawakumpenda mtu huyu kutokana na sababu mbili kuu. Kwanza ni kwa sababu hakuwa myahudi hivyo walijisikia vibaya kutawaliwa na mtu ambaye hakutoka katika taifa lao. Sababu ya pili ya kutompenda ni kwamba Herode huyu alikuwa ni katili sana.

Ukatili huu unatokana na ukweli kwamba aliyapata madaraka kwa ujanja. Herode huyu alijua kwamba wengi hawampendi hivyo akajitahidi kuhakikisha kuwa wote wanaompinga anawaangamiza rej Lk 19:27.Tunaambiwa kwamba aliwaua hata ndugu zake na watoto wake mfano akina Antipater, Alexander na Aristobulus walioonekana vinara wa kumpinga. Ukisoma pia Mt 2:16-18 pale wanatajwa watoto mashahidi waliouawa katika harakati za kuhakikisha kwamba mtoto Yesu anauawa pia ingawa hakufanikiwa kumuua Yesu kwani tayari alikuwa ametoroshwa toka Bethlehemu.

Kila mtu anayo mazuri na mapungufu. Herode Mkubwa naye kafanya kitu fulani ambacho kiliwafurahisha Wayahudi pamoja na ukatili wake.Yeye ndiye aliyejenga hekalu la Yerusalemu,hekalu lililokuwa kubwa na zuri kiasi kwamba wayahudi hao hao wakawa wanasema kwamba kama mtu alizaliwa hadi akafa bila kuliona hekalu lile,basi mtu huyo atambue kwamba hakuwahi kuona kitu chochote kizuri hapa duniani.Kumbe huyo ndiye Herode aliyetishia maisha ya Yesu maana hakupenda aje mtu yeyote atakayeitwa mfalme tofauti na yeye.Aliposikia kwamba amezaliwa mtoto ambaye ni mfalme alijua mtoto huyo anataka kurithi ufalme wake hivyo alifanya lolote awezalo ili kuhakikisha anammaliza bila kujua kwamba ufalme wa mtoto Yesu haukuwa wa kidunia.
Herode Mkubwa naye alikuwa na watoto. Kabla ya kifo chake aliacha wosia ulioagiza kwamba nchi aliyoitawala igawiwe kati ya watoto wake watatu yaani Archelaus, Herod Antipas na Philip.

Katika mgao huo, Archelaus akawa mtawala wa Yudea na Samaria na kwa kweli hii ni karibu nusu ya nchi yote ya wayahudi kwani alitawala mikoa miwili. Herode huyu ndiye alikuwa mtawala kipindi kile Yoseph na Maria waliporudi kutoka Misri rej Mt 2:22.Hata hivyo alishindwa kumudu uongozi wa mikoa hiyo na hivyo Warumi wakamtoa na kumweka Pontio Pilato kuwa mtawala badala yao. Mtoto wa pili yaani Herode Antipas alipewa kutawala mkoa wa Galilaya tangu mwaka 4KK-39 BK.Huyu alitawala wakati Yesu alipokuwa akitembea huko na huko kuhubiri Lk 3:1,MK 6:4 Zaidi sana,huyu ndiye Herode aliyekemewa na Yohane Mbatizaji alipomwoa Herodia mke wa kaka yake Philip rej Mt 14:1-5,Mk 6:14-29,ndiye anayeitwa na Yesu mbweha Lk 3:32,na Ndiye aliyekutana na Yesu wakati wa mateso Lk 23:7-12. na mwisho ndiye aliyemuua mtume Yakobo na kumfunga mtume Petro Mdo 12:1-5.
 
Yeye ndiye aliyejenga hekalu la Yerusalemu,hekalu lililokuwa kubwa na zuri kiasi kwamba wayahudi hao hao wakawa wanasema kwamba kama mtu alizaliwa hadi akafa bila kuliona hekalu lile,basi mtu huyo atambue kwamba hakuwahi kuona kitu chochote kizuri hapa duniani

Hilo hekalu alilojenga na lile la mfalme Sulemani lipi ni bora zaidi. Naongelea hekalu ambalo Newton alitumia muda mwingi akilifikiria na akifanyia utafiti akizani kuna siri atagundua, hekalu ambalo mpaka leo wayahud wanasali kwenye msingi wake
 
Nyie endeleeni kusema nani kagundua na hajagundua,, Alafu mbona siwaelewi mara tusimtukuze mzungu,, wakati vitu vyote unavyotumia ametengeneza White people,, white people atabaka kuwa hivyo hivyo na black people mtabaki na akili zetu nyeusi tiii kama rami au oili chafu,,
Maelezo yako mazuri kuna point ndani yake ila bado hujaonyesha ni vipi wamisri enzi hizo hawakua weusi.
Nipe facts mkuu zinazoonyesha wamisri walikua weupe...
Ahsante kwa hoja yako mkuu
Watu weusi misri wameingizw nautumwa mkuu.. ndo mana ni minority group pale misri' Kam ulivyo kwao minority in Asia, America n europe' pili, wazawa w misri Kam wangekuwa weusi lazima tuwe n tresi ni Lin hasa muarab aliingia pale na kwa hoja zipi has muarab akatwaa uongoz n uwingi was wat wake kias Cha mzawa kukos madaraka yote mpak kuwa mtumwa
Alaf hizi za michoro kuonekan n pua kubwa sijui au kuonekan miungu yenye rangi nyeus ni hoja zeny dhana ya kuuikweza tu uafrika sabb (north Africa yenyew) tukisem misri weusi lazima tuelezee imekuaje misri na sio north yote!?vip!? na kw nn Libya, Tunisia na moroko Arabs pia!? hao weusi walitolewaje!? .North yote mpak wazawa Afrikan kuw minorities maeneo hayo!?
Toa elimu hiyo mkuu
 
Back
Top Bottom