Uchaguzi 2020 Wagombea CHADEMA nafasi ya Rais, Lissu ana nafasi kubwa ya kutoa ushindani mkali

Uchaguzi 2020 Wagombea CHADEMA nafasi ya Rais, Lissu ana nafasi kubwa ya kutoa ushindani mkali

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
20,654
Reaction score
35,887
Heshima kwenu wanajamvi,

Leo nimeona ni vyema na haki tukawajadili wagombea nafasi ya Rais wa JMT kutokea chama cha CDM.

Nadhani nianze na Mheshimiwa Lissu si kwa bahati mbaya la hasha, nimeanza na Lissu kwasababu ni mgombea pekee mwenye mvuto kwa wananchi lakini pia ni mgombea mwenye uwezo mkubwa wa kujieleza na kueleweka kwa wananchi.

Namebahatika kusoma maandiko mbalimbali ya Mhe Lissu tangu akiwa mwanasheria aliyejikita zaidi katika masuala ya mazingira hasa migodi ya dhahabu maeneo ya Kanda ya Ziwa (Shinyanga, Mwanza na Mara) Mhe Lissu ni mtu mwenye uwezo mkubwa wa kujenga na kupangilia hoja zake, anaeleweka kwa urahisi kwakuwa kila wakati jambo analolisimamia anakuwa analifahamu ndani nje. Ni aina ya watu ambao hawapendi kubahatisha jambo.

Mhe Lissu si mtu wa kukurupuka hata alipochaguliwa katika nafasi ya ubunge. Bunge letu hasa mawazi na Mwanasheria Mkuu wa Serekali walikumbana na hoja nzito zilizosheheni utafiti wa kutosha. Kwa hakika Bunge la JMT lilikosa mtu mahiri sana na pengo lake mpaka leo sijaona Mbunge angalau mmoja ambaye labda alifikia 50% ya kiwango cha Mh. Lissu. Hii aibu kubwa sana hasa kwa waheshimiwa wabunge waliomaliza muda wao.

Kuna kipindi wananchi walipenda kusikiliza michango ya wabunge mbalimbali kwakuwa waliamini walikuwa wakiwasemea na kuwawakilisha vyema.Michango ya mwisho ya bunge letu la bajeti ilikosa watu aina ya Mh Lissu badala yake tulijikuta tukiambulia michango ya ajabu kutoka kwa wabunge kama Mh Lugola, Mh Msukuma, Mh Lusinde, Mh Silinde, Mh Lijualika na nk ambao badala ya kujadili bajeti ya wananchi walizama zaidi katika kumshambulia KUB Mh Mbowe. Bahati mbaya zaidi hata Mh Job Ndugai naye alijiingiza katika mambo yanayofanana na hayo.

Mh Lissu anatosha kugombea uRais kwa tiketi ya CHADEMA ingawa kushinda ni vigumu sana lakini anaweza kusababisha kupatikana wabunge wengi wa Upinzani.Mh Lissu atahitaji msaada mkubwa sana kutoka chama chake ambacho uchaguzi uliopita kilifanya makosa makubwa ya kuwakaribisha wagombea walioshindwa kupata nafasi za uongozi ndani ya CCM. Kosa la kumkaribisha Mh Lowassa na kumwacha Mh Balozi Dr Slaa kuliondoa identity ya chama kupinga ufisadi. Ajenda hii ilitekwa na Mh Dr Magufuli ingawa utekelezaji umegubikwa na shaka shaka kubwa.

Ningekuwa na mamlaka ndani ya CHADEMA Mh Lissu angepitishwa mapema asubuhi bila kupoteza muda.Nafikiri ni muda muafaka haswa ndani ya CHADEMA kuacha kupoteza muda Mh Lissu anauzika kirahis zaidi ukilinganisha na wagombea wengine hasa katika majira haya yanayo hitaji mtu wa kushindana na Mh Magufuli ambaye katika kipindi cha miaka mitano amehakikisha upinzani haupati nafasi ya kusikika huku yeye binafsi akitumia vyombo vya habari sana.
 
Napendekeza CDM wampitishe Leonard Toja Manyama. Huyu jamaa amejipanga. Niamini nikuvushe
 
Lissu anafaa Ila tuache Demokrasia ichukue mkondo wake.Ikibidi wanatakiwa wagombea wawekewe mdahalo wa wazi na ijulikane ipi mbichi na ipi imeiva japo naamini vyombo ya habari haviwezi kurusha live tukio kubwa Kama Hilo.

Lkin pia lazima tuwaheshimu wengine mfano Nyalandu yuko vizuri Ila mfumo wa CCM ulishamchafua. Msigwa Bado kidogo. Mbowe anaweza vizuri tu kuongoza nchi Ila sio kwa kushindana na Huyu Meko. Lissu anatosha lakini hata asipopitishwa yeye lengo letu ni kuiondoa CCM hivyo yeyote atakayepita atapewa msaada.
 
Suala la Lissu kukubalika na sisi wapiga kura wa upinzani wala halina mjadala. Tuko tayari kulipa gharama za kumchagua Lisu kuwa mgombea wa cdm. Naujua uwezo wa Lissu hasa kuelekea ccm inayotoka kuchezea katiba, ili kumuongezea muda Lissu wa kukaa madarakani.
 
Hivi kuna mtu anaamini Lissu atarudi Tanzania?
 
Ndugu; Tundu Lissu katia nia kugombea Urais wa JMT kwa tiketi ya CHADEMA na siyo CDM....

Katika orodha ya msajili wa vyama vya siasa Tanzania, hakuna chama chenye jina la "CDM"....

CHADEMA ni abbreviation ya maneno " CHAMA CHA DEMEKRASIA NA MAENDELEO" = CHADEMA. Sasa CDM sijui kirefu chake kitakuwa nini....

Kwa hiyo tunapotaja chama fulani cha siasa katika mijadala yetu, ni vyema tukakitaja kwa jina lake halisi ili kutokuleta confusion kwa wanaojifunza mambo haya kupitia jukwaa hili lililo kisima cha elimu ya uraia na mambo mengine.....
 
Lissu anafaa Ila tuache Demokrasia ichukue mkondo wake.Ikibidi wanatakiwa wagombea wawekewe mdahalo wa wazi na ijulikane ipi mbichi na ipi imeiva japo naamini vyombo ya habari haviwezi kurusha live tukio kubwa Kama Hilo.

Lkin pia lazima tuwaheshimu wengine mfano Nyalandu yuko vizuri Ila mfumo wa CCM ulishamchafua. Msigwa Bado kidogo. Mbowe anaweza vizuri tu kuongoza nchi Ila sio kwa kushindana na Huyu Meko. Lissu anatosha lakini hata asipopitishwa yeye lengo letu ni kuiondoa CCM hivyo yeyote atakayepita atapewa msaada.

Ni obvious itakuwa hivyo....

Ila wachujwe kwanza tubaki na TOP THREE ama FIVE tu na kisha hao ndiyo wafanye mdahalo wa wazi....

Hoja ama maswali ya mdahalo yalenge kuwapima wagombea wote uwezo wao wa kujieleza na ufahamu wao katika nyanja hizi;

å Uchumi
å Siasa za ndani na kimataifa
å Diplomasia ya ndani na kimataifa
å Utamaduni

Hii itasaidia na kuepusha taifa kumpa uongozi wa juu wa nchi watu dizaini ya John Pombe Magufuli wa CCM ambao wanalitea fedheha na aibu tu taifa letu nzuri la Tanzania....
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Leo nimeona ni vyema na haki tukawajadili wagombea nafasi ya Rais wa JMT kutokea chama cha CDM.

Nadhani nianze na Mheshimiwa Lissu si kwa bahati mbaya la hasha, nimeanza na Lissu kwasababu ni mgombea pekee mwenye mvuto kwa wananchi lakini pia ni mgombea mwenye uwezo mkubwa wa kujieleza na kueleweka kwa wananchi.

Namebahatika kusoma maandiko mbalimbali ya Mhe Lissu tangu akiwa mwanasheria aliyejikita zaidi katika masuala ya mazingira hasa migodi ya dhahabu maeneo ya Kanda ya Ziwa (Shinyanga, Mwanza na Mara) Mhe Lissu ni mtu mwenye uwezo mkubwa wa kujenga na kupangilia hoja zake, anaeleweka kwa urahisi kwakuwa kila wakati jambo analolisimamia anakuwa analifahamu ndani nje. Ni aina ya watu ambao hawapendi kubahatisha jambo.

Mhe Lissu si mtu wa kukurupuka hata alipochaguliwa katika nafasi ya ubunge. Bunge letu hasa mawazi na Mwanasheria Mkuu wa Serekali walikumbana na hoja nzito zilizosheheni utafiti wa kutosha. Kwa hakika Bunge la JMT lilikosa mtu mahiri sana na pengo lake mpaka leo sijaona Mbunge angalau mmoja ambaye labda alifikia 50% ya kiwango cha Mh. Lissu. Hii aibu kubwa sana hasa kwa waheshimiwa wabunge waliomaliza muda wao.

Kuna kipindi wananchi walipenda kusikiliza michango ya wabunge mbalimbali kwakuwa waliamini walikuwa wakiwasemea na kuwawakilisha vyema.Michango ya mwisho ya bunge letu la bajeti ilikosa watu aina ya Mh Lissu badala yake tulijikuta tukiambulia michango ya ajabu kutoka kwa wabunge kama Mh Lugola, Mh Msukuma, Mh Lusinde, Mh Silinde, Mh Lijualika na nk ambao badala ya kujadili bajeti ya wananchi walizama zaidi katika kumshambulia KUB Mh Mbowe. Bahati mbaya zaidi hata Mh Job Ndugai naye alijiingiza katika mambo yanayofanana na hayo.

Mh Lissu anatosha kugombea uRais kwa tiketi ya CHADEMA ingawa kushinda ni vigumu sana lakini anaweza kusababisha kupatikana wabunge wengi wa Upinzani.Mh Lissu atahitaji msaada mkubwa sana kutoka chama chake ambacho uchaguzi uliopita kilifanya makosa makubwa ya kuwakaribisha wagombea walioshindwa kupata nafasi za uongozi ndani ya CCM. Kosa la kumkaribisha Mh Lowassa na kumwacha Mh Balozi Dr Slaa kuliondoa identity ya chama kupinga ufisadi. Ajenda hii ilitekwa na Mh Dr Magufuli ingawa utekelezaji umegubikwa na shaka shaka kubwa.

Ningekuwa na mamlaka ndani ya CHADEMA Mh Lissu angepitishwa mapema asubuhi bila kupoteza muda.Nafikiri ni muda muafaka haswa ndani ya CHADEMA kuacha kupoteza muda Mh Lissu anauzika kirahis zaidi ukilinganisha na wagombea wengine hasa katika majira haya yanayo hitaji mtu wa kushindana na Mh Magufuli ambaye katika kipindi cha miaka mitano amehakikisha upinzani haupati nafasi ya kusikika huku yeye binafsi akitumia vyombo vya habari sana.
Lissu anampita jiwe kwa mbali sana katika kuwa presidential material, anafaa sana na tumwuunge mkono shujaa Lissu.
 
Heshima kwenu wanajamvi.

Ningekuwa na mamlaka ndani ya CHADEMA Mh Lissu angepitishwa mapema asubuhi bila kupoteza muda.Nafikiri ni muda muafaka haswa ndani ya CHADEMA kuacha kupoteza muda Mh Lissu anauzika kirahis zaidi ukilinganisha na wagombea wengine hasa katika majira haya yanayo hitaji mtu wa kushindana na Mh Magufuli ambaye katika kipindi cha miaka mitano amehakikisha upinzani haupati nafasi ya kusikika huku yeye binafsi akitumia vyombo vya habari sana.
Mkuu Ngongo, kwanza naunga mkono hoja ya presidential candidature ya Tundu Lissu kwasababu ni presidential material, hata mimi nilishauri
Elections 2020 - Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha Uwezo Zaidi ya Magufuli!

Ila baada ya kuanza kufunguka funguka huko Ughaibuni, niliingia mashaka kama atarejea home
Kwa mliomsikia Tundu Lissu kwenye Hard Talk, unadhani atarejea nchini? Mimi sina hakika na akirejea, atakuwa ni shujaa kuliko hata Nelson Mandela!

Tundu Lissu akatoa conditions to be met kabla ya kurejea, na mimi nikashauri
Kamanda Lissu, Usisubiri Jibu la IGP Kuhusu Usalama Wako, Aliyekulinda na Shambulio Lile Yupo, Yeye Aweza, na Ataendelea Kukulinda, Welcome Back Home!

Na alipoamua kugombea kutokea Ughaibuni nika comment
Elections 2020 - Je, kuna uwezekano kutangaza nia kugombea Urais kupitia CHADEMA kwa baadhi, kunatumika kama kichaka cha kujifichia aibu ya kushindwa ubunge?.

Na mwisho nikawatajia mgombea urais wa Chadema, sio Lissu!.

Elections 2020 - Jicho la Tatu: Mgombea Urais CHADEMA ni Freeman Mbowe! Tundu Lissu Pacemaker! Nyalandu ni Serious Contender, Msigwa anatania, Dkt. Mayrose Majinge...

P
 
Back
Top Bottom