Wagombea Ubunge wa CHADEMA wanapata wakati mgumu kuomba kura

Wagombea Ubunge wa CHADEMA wanapata wakati mgumu kuomba kura

ZeMarcopolo

Platinum Member
Joined
May 11, 2008
Posts
14,040
Reaction score
7,303
Mgombea Urais wa CHADEMA mwaka huu amekuwa akipinga jitihada za serikali kusambaza umeme, maji vijijini na mijini, kuboresha huduma za afya, elimu na ofisi za umma, kuimarisha miundombinu na huduma za usafiri wa majini, anga na nchi kavu.

Kutokana na kauli za mgombea huyo wa Urais, wagombea wa Ubunge wa CHADEMA wamekosa ahadi za kuwapa wapiga kura. Yale yote yanayopingwa na mgombea wa chama chao, ndio kero za wapiga kura wa Ubunge na Udiwani.

Kila wanapopita wanajikuta wanalazimika kuahidi kuboresha huduma za afya, lakini kwa vile chama chao kinapinga, wananchi wanashindwa kuwaelewa. Wakijaribu kuahidi kuboresha elimu wanajikuta katika hali hiyohiyo ya kukosa hoja mbadala.

Kwa hali iliyopo huku mitaani, wabunge wengi wa CHADEMA watashindwa kurudi bungeni. Vilevile, chadema itashindwa kupata wabunge kwenye majimbo mengine yasiyokuwa na wabunge wa CHADEMA.

Imeshakuwa bayana kuwa kitendo cha mgombea Urais wa Chadema kuacha kunadi ilani ya chama chake na kujiamulia kupinga maendeleo kitakigharimu chama hicho.
 
CCM mpya chini ya Bashiru na Chakubanga mbona imeacha kuongelea mambo ya madege na madaraja? Walidhani mwanzoni kuwa wananchi watakula madaraja? Sasa kama wanajua kusoma alama za nayakati wasome. Huu uchaguzi waki mess up wanakwenda kupigwa vikwazo siyo vya dunia hii. Yaani sisi
 
CCM mpya chini ya Bashiru na Chakubanga mbona imeacha kuongelea mambo ya madege na madaraja? Walidhani mwanzoni kuwa wananchi watakula madaraja? Sasa kama wanajua kusoma alama za nayakati wasome. Huu uchaguzi waki mess up wanakwenda kupigwa vikwazo siyo vya dunia hii.. Yaani sisi

Hizi siasa za kupinga maendeleo zinawapa wakati mgumu wagombea wa ubunge na udiwani wa Chadema.

Mgombea udiwani hawezi kuahidi kuongeza mshahara wa watumishi. Ahadi za diwani na mbunge ni miundombinu, umeme, maji, kilimo, shule, afya. Sasa hivi vitu vyote Chadema inavipinga!
 
Kama wagombea wa Chadema wameshindwa kuomba kura nyinyi CCM kinachowafanya mpige magoti ni nini ?
IMG_20201002_000058.jpg
IMG_20200930_083838.jpg
IMG_20200930_083832.jpg
Screenshot_20200930-082754.png
 
Kama wagombea wa Chadema wameshindwa kuomba kura nyinyi CCM kinachowafanya msombe watu kwenye malori , trekta , boti kujaza uwanja nini ?
IMG_20201002_161854.jpg
IMG_20201003_165209_8.jpg
IMG_20201003_164520_7.jpg
IMG_20201002_161846.jpg
IMG_20201002_161835.jpg
 
Hizi siasa za kupinga maendeleo zinawapa wakati mgumu wagombea wa ubunge na udiwani wa Chadema.

Mgombea udiwani hawezi kuahidi kuongeza mshahara wa watumishi. Ahadi za diwani na mbunge ni miundombinu, umeme, maji, kilimo, shule, afya. Sasa hivi vitu vyote Chadema inavipinga!
Tatizo lako ni elimu 2 inakusumbua, hv unaelewa majukumu ya mbunge na diwani kweli? majukumu ya halmashauri,manispaa au serikali kuu kweli? shame mtu kama ww kuwa humu.
 
Tatizo lako ni elimu 2 inakusumbua, hv unaelewa majukumu ya mbunge na diwani kweli? majukumu ya halmashauri,manispaa au serikali kuu kweli? shame mtu kama ww kuwa humu
Mkuu, wagombea wanahangaika huku mitaani jinsi ya kuomba kura. Je, una ushauri wowote kwao? Watoe ahadi gani kwa wapiga kura?
 
Kama wagombea wa Chadema wameshindwa kuomba kura nyinyi CCM kinachowafanya mkimbilie kwa waganga na Masheikh Ni nini?
IMG_20201004_080516.jpg
IMG_20201004_080507.jpg
 
Naona silaha zinarudi sasa ...[emoji41]
Mkuu, nilikumiss sana. Nakumbuka Mbowe na Lissu walikuumiza sana jinsi walivyomsaliti Dr Slaa. Tunashukuru Mungu nchi yetu ina uongozi imara. Tunaendelea kupiga hatua za maendeleo.
 
Back
Top Bottom