Uchaguzi 2020 Wagombea wa Urais kutoka upinzani kimsingi wanaruhusiwa kutoa ahadi za miradi na misaada mbalimbali nchini, kama anavyofanya Magufuli

Uchaguzi 2020 Wagombea wa Urais kutoka upinzani kimsingi wanaruhusiwa kutoa ahadi za miradi na misaada mbalimbali nchini, kama anavyofanya Magufuli

Hiyo ya kumzuia rais aliyepo madarakani asitoe ahadi ambayo haiwezi kutekelezwa baada ya Oktoba ni kwa mujibu wa Ibara gani ya katiba ya JMT? Au sheria gani? Na hiyo ya kutaka wagombea wa upinzani kutoa ahadi kabla hata kampeni kuanza ni kwa mujibu wa ibara gani? Au mkichwa hakuna?
Nimekuuliza swali rahisi sana. Ikiwa Magufuli atashindwa uchaguzi hizo ahadi zitatekelezwa? Bila shaka hapana.

Kwa hiyo ili walengwa wafaidike na hiyo ahadi si itabidi wampigie kura JPM? Hapo ndipo rushwa inakuja.

Kwa hiyo kama anaahidi kufanya hayo kwa kutumia madaraka yake akiwa raisi baada ya uchaguzi, ni wazi wagombea wengine wana haki ya kufanya hivyo hivyo, kwa kuwa hatujui nani atakuwa raisi.
 
Nimekuuliza swali rahisi sana. Ikiwa Magufuli atashindwa uchaguzi hizo ahadi zitatekelezwa? Bila shaka hapana.

Kwa hiyo ili walengwa wafaidike na hiyo ahadi si itabidi wampigie kura JPM? Hapo ndipo rushwa inakuja.

Kwa hiyo kama anaahidi kufanya hayo kwa kutumia madaraka yake akiwa raisi baada ya uchaguzi, ni wazi wagombea wengine wana haki ya kufanya hivyo hivyo, kwa kuwa hatujui nani atakuwa raisi.
Wagombea wengine wana haki kwa mujibu wa ibara gani ya katiba ya JMT? Bichwa kubwa limejaa maji.
 
Wagombea wengine wana haki kwa mujibu wa ibara gani ya katiba ya JMT? Bichwa kubwa limejaa maji.
Kwani JPM ana haki ya kuahidi vitu beyond Oct 2020 kwa mujibu wa Ibara gani ya Katiba? Inayompa raisi mstaafu mamlaka ya kuamrisha matumizi ya fedha za serikali?
 
Hii safari yake ilikuwa ni ya kampeni au ya kiofisi.

Nani Rais wa JMT sasa na wakati wa kampeni wa uchaguzi.

Hii ni staili yake ya uongozi aliyo ianza tangu 2015 alipochaguliwa kuwa Rais.

Miaka ya nyuma haikuwa rushwa, ila inageuka kuwa rushwa kwa vile ni kipindi cha uchaguzi.
 
Kwani JPM ana haki ya kuahidi vitu beyond Oct 2020 kwa mujibu wa Ibara gani ya Katiba? Inayompa raisi mstaafu mamlaka ya kuamrisha matumizi ya fedha za serikali?
Soma ibara ya 42(3)(a) wa katiba ya JMT ndio upate jibu, we bichwa maji unayelopoka upuuzi na kuhoji ujinga.
 
KUnunua jogoo kwa laki sio tatizo, kwa sababu inawezekana kabisa ilikuwa ni katika suala la uchangishaji. Kwani hujaona minada ya ushangishaji watu wananua vitu mara 10 ya bei yake? Hiyo ni kufanya tukio lifurahishe. Sasa huyo mtu aliyemuuzia JPM jogoo ilikuwa katika mazingira gani?

Believe me, mio sio blind supporter wa Magufuli au mtu yeyeote, so huwa napenda nisimamie ukweli
Kiukweli ili tufaidi inatakiwa kuwe na usawa na haki ktk huu uchaguzi na sio hizi pendeleo zinazoonekana waziwazi za vyombo vya habari.
 
Yaani huelewi kabisa! Tatizo watu wenye vichwa vigumu kuelewa ndio mnaopiga kelele kuliko wengine!
Ukiona maana CCM kakuelewa kwenye mada za maana kama hi nenda fasta msikitini ama Kanisani ukatoe sadaka ya shukurani.
Hawa jamaa Ni mambumbumbu hatari ndio maana wao hata wakiambiwa na jiwe kwenye mkutano "mabwege nyie"wata Sema "Sema babaaa"
 
Kutoa ahadi ni hujuma ki falsafa. Kazi za maendeleo ni za kitaifa, na chama kitakachounda serikali ndicho kitatekeleza mpango wa maendeleo kwa taifa.

CCM wanagombea kiti lakini wao ndio wanacho na wanakikalia.

Walipaswa kiti wakikabidhi kwa ma judge kisha mechi ipigwe fairly, chukua mfano mchezo wa ngumi, mkanda unaopiganiwa huwa chini ya shirikisho mpaka baada ya mechi, na huukabidhi kwa mshindi.

Ccm wanatembea na mkanda wao, na kuhaidi maendeleo chama kikiingia madarakani kitafanya yote hayo, maana kitakuwa na mamlaka na makusanyo ya kofi za watanzania, na credit ya kukopa pia huipokea wanapounda serikali.

Chaguzi za aina hii haziko fair, maendeleo yaliyofanywa na serikali iliyopita siyo mali ya chama kilichokuwepo madarakani ni mali ya watanzania wote.

Kwa maoni yangu vyama vinadi sera zao kiuchumi, kisheria na kimuundo na mfumo sio ahadi za majengo na mabarabara.
 
Hadi sasa sijaona ahadai za miundo mbinu za maana kutoka wagombea wa uraisi wa vyama vya upinzani. Kwa nini?
 
Back
Top Bottom