Waha acheni uchawi. Muuza sambusa kafungua duka la vifaa vya pikipiki vya jumla

Waha acheni uchawi. Muuza sambusa kafungua duka la vifaa vya pikipiki vya jumla

Nadhani mwenye fikra potofu za kichawi ni wewe na sio Waha na kwa muktadha huo ukikutana na hao Waha lazima utakubali wakupe huo so called uchawi (na kwangu mimi uchawi ni tabia)
 
Kubaguana na kudharauliana ni moja ya sababu inayotufanya tuwe masikini.

Jamaa kaona mwenzake kafanikiwa, badala ya kumdadisi ajue siri ya mafanikio, anakimbilia kusema uchawi.

Yani hapo hata kama Waha wametengeneza network ya kusaidiana, kwa dharau na ubaguzi huu, hatuwezi kujifunza kutoka kwao.
Kweli kabisa
 
Nakubali biashara ni hatua, ila hatua alizopiga huyu muha ni uchawi kabisa. Alikuwa akitembeza sambusa.

Ukihesabu kwenye ile pot yake ni kama sambusa 50-100 kwa siku. Hapo hupata 25k-50k kwa siku, ukiondoa gharama za kuandaa, muda na chakula, lets say kwa siku anapata faida ya 10-20k. Kuumwa na matatizo mengine pia lazima tuyahesabu.

Duka la kawaida la vifaa vya pikipiki ni atound 5ml -10ml. Duka la jumla mtaji wake si chini ya milioni 25.

Sasa kutoka kwenye kutembeza sambusa mpaka kufungua duka la milioni zaidi ya 25 ghafla inawezekana vipi kama si uchawi? Acheni uchawi.

Angepitia hatua kadhaa mpaka kumiliki duka kubwa kiasi hichi sawa, sasa huyu dogo kapotea kuuliza yuko wapi naambiwa yuko Ilala kafungua duka la jumla la vifaa vya pikipiki.

Ikumbukwe kodi ya fremu Ilala lazima uandae kama milioni 5 hivi wakati wa kuanza biashara.
Vina muda bhas
 
Watanzania ndo mana hatufanikiwi..
Sababu na we ni mchawi mloge tu arudi kuuza mbusasa
 
Hoja sio kula kuvaa hoja iko hapa ni waha tu wenye uwezo wa kuicha mke na watoto kwa kipindi kirefu bila hata kuwapigia cm kisa utafutaji hela ya muha ailiwi na ndugu wala mke mtoto

Muha anaweza ugua ndani hoi asiende hositpal hali yakuwa yuko na milioni 3 ndani muha ni mtu anae weza mpiga babake mzazi kisa kamkomesha sh 50000 kashindwa kulipa muha ni mtu anae weza kutembeza miwa machungwa kuuza nadafu akawa analala hanapo kaza tolololi kwa miaka 5 mfululizo

Nenda pale mabibo kuna muha anauza maji na sigara na vocha kaangalie anako lala kwenye banda Miaka 5 katoka kibondo kaacha mke na watoto no kupiga simu no kutuma hela ya matumizi no kutuma ada ya shule waha wengi wao wako hivio utafutaji wa waha ni mgumu sana wamezidi ubahili fikilia mtoto kumjazia watu au kumkwida baba yake kisa hela !!kaishi na waha ujifunze mengi

Utafutaji wao ni wakujima sana uchawi ni sehemu ndogo sana labda huko kwao lakini walipo mjini wauza kahawa mbezi kariakoo wauza viombo mitumba madafu nk hela yao hsiliwi na mtu sio mzazi mke wala mtoto je makabila mengine ya aweza ?? Mimi siwezi
Mkuu una muda mwingi mpk kuyajua yote haya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We kiswahili ulijifunza wap mkuu?!!
Au ndo umeamua kuwa mjinga kwa kujinufaisha ww na lengo lako?!!

Sent using Jamii Forums mobile app
ukitumia akili zako kila saa unaweza data!
kuna wakati ni vizuri kutoa majibu yasiyotarajiwa ili aliyeandika aweze kutoa tafakari ya ndani kuwa hili neno halikuwa sahihi kwa mtoa mada yaani aliua mbu kwa nyundo.
inawezekana mleta mada alileta mada ili tupanue mawazo yetu zaidi hivyo hakukuwa na sababu ya kumtukana kiasi cha kumuweka chini ya miguu ya watu haikukaa sawa sana.
hivyo unapunguza mihemko kwa staili hiyo kwa kuonyesha uwezo wa neno moja linaweza kuwa na maana nyingi kwa kufanya hivyo unaondoa uchungu kwa aliyeumizwa na aliyeumizwa anajifunza upya ya jinsi ya kuwa mvumilivu.
 
Kafanye na wewe huo uchawi utajirike,unaonekana huna kazi na pia ni choka mbaya,ndio maana unafuatilia maisha ya watu,endelea kumfuatilia mpaka siku atakayo kuja kununua mtaa wenu mzima ndio utatoka usingizini.
 
kama pesa ya uchawi ipo kigoma nzima wangekua na maduka ya jumla na matajiri 😅😅😅uza sambusa na wewe nenda kwa mganga ufungue duka la jumla la spea za bajaji kitumbini
 
Back
Top Bottom