Sijui ni kwanini Watani zangu wengi ni Watu wenye majanga majanga hivi hadi najuta hawa Wazee wetu wa Kale walifikiria nini hadi kutufanya Sisi watu wa Mkoa wa Mara tukawa tukawana na Ujomba na Ushangazi ( Utani ) na haya makabila ya Waha, Wahaya, Wanyiramba, Wanyaturu na Warangi kwani kiukweli wanatutia mno aibu Sisi.
katika hali isiyokuwa ya kawaida kabisa bila ya Wao kujua kuwa waliyekaa nae jirani hapo ni GENTAMYCINE akina Dada fulani mmoja wao akiwa ni Mfanyakazi wa Ndege ile yenye nembo ya Ndege huku mwingine akiwa ni Mfanyakazi wa Ndege moja yenye nembo ya Twiga jana usiku walikuwa wanajadiliana masuala yao ya Kazi ila wote wawili walielezea sana ' changamoto ' zao ambazo huwa wanazipata kutoka kwa abiria hasa wa Kabila la Waha kutoka Mkoani Kigoma.
Zifuatazo ni nukuu mbili tofauti tofauti za hao akina Dada ambao ni Wahudumu wa ndani ya Ndege ya hayo Makampuni mawili maarufu ya Ndege hapa nchini Tanzania na naziweka kama ambavyo nimewasikia mwenywe jana wakitiririka na kuserereka nazo tena kwa hasira kabisa...
Dada wa Shirika la Ndege lenye nembo ya ' Ndege '....." Yaani Shosti nashukuru Mungu Kazi zinaenda tu vizuri na mambo siyo mabaya ila kuna hawa Abiria wa Kigoma hasa wa Kabila hili la Waha sijui kwanini hawastaarabiki kwani wenzao hupanda ndani ya Ndege na Vitabu vya Kujisomea au Magazeti lakini cha kushangaza wao kila wakipanda humu wanapanda na mifuko ya Wali na Samaki halafu Ndege ikishaanza tu kuruka wanaito hiyo mifuko ya Vyakula na kuanza kula wakati Sisi mule huwa tunatoa Vyakula vyetu....."
Dada wa Shirika la Ndege lenye nembo ya ' Twiga '....." Si bora nyie huko Kwenu wakishaingia na hiyo mifuko ya Vyakula wanaitoa na kuanza kula. Huku katika Ndege yetu hawa Waha kiukweli wametuchosha kwani huku wakishaanza kula tu hivyo Vyakula vyao huanza kubishana yaani utakuta mmoja amekaa kule First Class anaanzisha ligi / ubishani na abiria wa Economy huku Chakula kikiwa mdomoni na miba ya Samaki wao wale ikiwadondoka midomoni. Halafu wana tatizo moja sugu sana kwani wakishakula, kushiba na kumaliza ubishani wao ambao ni asili yao hulala ghafla na kuanza Kuwajambia hovyo abiria wengine hali ambayo huwa inatupa sana wakati mgumu Sisi wahudumu....."
Haya naamini kabisa kwamba humu Jamvini JF Watani zangu ' Waha ' mpo wengi hivyo haraka sana naomba mjitokeze kujibu hizi ' Shutuma ' la sivyo hawa Dada zenu tuliwaoa huku Mkoani Mara ( Musoma ) sasa hivi tuwaacha na kuwapa ' talaka ' ili warudi huko Kwenu Mkoani Kigoma mfundishane vizuri ' maadili '. Na hivi mnavyotupenda Wanaume wa Mkoa wa Mara ( Musoma ) sijui kama tukiwaacha mtapata tena Waume wa Kuwaoa.
Waha na wana Mkoa Kigoma badilikeni upesi!
Nawasilisha.