Wahalifu waliowatumbukiza Wazazi kwenye shimo la choo kisha kuondoka na mtoto wakamatwa

Wahalifu waliowatumbukiza Wazazi kwenye shimo la choo kisha kuondoka na mtoto wakamatwa

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani limefanikiwa kumpata mtoto mwenye umri wa miezi sita aliyechukuliwa na watu wasiojulikana, baada ya kuvamia nyumba ya Melksedek Mrema na mkewe Joan Gabriel, ambao nao wakati wa tukio hilo walitupwa kwenye mashimo ya choo, kabla ya watuhumiwa kuondoka na mtoto huyo.

Soma pia: Kibaha: Waiba gari, kichanga na kuwatumbukiza wazazi kwenye shimo la choo

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Salim Morcane amesema majira ya saa 9.00 usiku wa kuamkia leo Januari 24, 2025, katika eneo la Kimalamisale, mtaa wa Serengeti B uliopo Kata ya Dutumi, Kibaha vijijini waliwakamata wanaume watatu na mwanamke mmoja aliyekutwa na mtoto huyo wa kike na gari Toyota IST.

Amesema baada ya kumpata mtoto, walimpeleka katika Hospitali ya Tumbi kwa uchunguzi Zaidi, kisha atakabidhiwa kwa wazazi lakini kwa sasa yupo sehemu salama zaidi.

Watuhumiwa wote wapo kituo cha polisi na uchunguzi unaendelea.
Screenshot 2025-01-24 152640.png
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani limefanikiwa kumpata mtoto mwenye umri wa miezi sita aliyechukuliwa na watu wasiojulikana, baada ya kuvamia nyumba ya Melksedek Mrema na mkewe Joan Gabriel, ambao nao wakati wa tukio hilo walitupwa kwenye mashimo ya choo, kabla ya watuhumiwa kuondoka na mtoto huyo.

Soma pia: Kibaha: Waiba gari, kichanga na kuwatumbukiza wazazi kwenye shimo la choo

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Salim Morcane amesema majira ya saa 9.00 usiku wa kuamkia leo Januari 24, 2025, katika eneo la Kimalamisale, mtaa wa Serengeti B uliopo Kata ya Dutumi, Kibaha vijijini waliwakamata wanaume watatu na mwanamke mmoja aliyekutwa na mtoto huyo wa kike na gari Toyota IST.

Amesema baada ya kumpata mtoto, walimpeleka katika Hospitali ya Tumbi kwa uchunguzi Zaidi, kisha atakabidhiwa kwa wazazi lakini kwa sasa yupo sehemu salama zaidi.

Watuhumiwa wote wapo kituo cha polisi na uchunguzi unaendelea.
View attachment 3212482
Shukrani Kwa polisi, kazi nzuri wamefanya
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani limefanikiwa kumpata mtoto mwenye umri wa miezi sita aliyechukuliwa na watu wasiojulikana, baada ya kuvamia nyumba ya Melksedek Mrema na mkewe Joan Gabriel, ambao nao wakati wa tukio hilo walitupwa kwenye mashimo ya choo, kabla ya watuhumiwa kuondoka na mtoto huyo.

Soma pia: Kibaha: Waiba gari, kichanga na kuwatumbukiza wazazi kwenye shimo la choo

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Salim Morcane amesema majira ya saa 9.00 usiku wa kuamkia leo Januari 24, 2025, katika eneo la Kimalamisale, mtaa wa Serengeti B uliopo Kata ya Dutumi, Kibaha vijijini waliwakamata wanaume watatu na mwanamke mmoja aliyekutwa na mtoto huyo wa kike na gari Toyota IST.

Amesema baada ya kumpata mtoto, walimpeleka katika Hospitali ya Tumbi kwa uchunguzi Zaidi, kisha atakabidhiwa kwa wazazi lakini kwa sasa yupo sehemu salama zaidi.

Watuhumiwa wote wapo kituo cha polisi na uchunguzi unaendelea.
View attachment 3212482
Hii ndiyo maana ya ulinzi wa Rai na Mali zao.
 
Maua yenu polisi. Kwa hili mmenipa raha kwa kumpata huyu mtoto. ninawapongeza sana sana. Na Ahsante Mungu kwa kujibu maombi ya familia na wote waliohusika kuomb huyu mtoto apatikane. Ningefurahi kama jeshi la polisi lingetuonyesha hawa hadharani tuwajue.
 
Melksedek Mrema na mkewe Joan Gabriel, ambao nao wakati wa tukio hilo walitupwa kwenye mashimo ya choo,...
Dah,
Hao wazazi wa mtoto hawatasahau huo msukosuko.
Kutumbukizwa ndani ya chemba za choo si tukio jepesi.
Pongezi kwa Polisi kumpata mtoto akiwa hai
 
Jeshi la polisi sasa hivi linapiga kazi kwelikweli,hii nadhani itakuwa effect ya Bashungwa...
 
Snapinst.app_474912794_1753556498836454_7445847820586496772_n_1080.jpg

Snapinst.app_474783849_623389246830698_5573092660050595506_n_1080.jpg

TAARIFA KWA UMMA

Tarehe 15/01/2025 majira ya saa 1:00 asubuhi huko Galagaza, Kata ya Msangani, Wilaya ya Kibaha Mkoa Pwani. Melkizedeck Sostenes, miaka 28, mfanya biashara mkazi wa Galagaza alivamiwa nyumbani kwake na watu 4 wasiofahamika wakiwa na mapanga na nondo na kuanza kumshambulia kwa kumkata na kitu chenye ncha kali mkono wa kushoto, na kumpiga na mabapa ya panga mgongoni na kumuibia gari dogo aina ya IST lenye namba za usajili T.331 DLZ, Televisheni 1 aina ya Haier nchi 42, Kompyuta mpakato 3 na simu tano za aina mbalimbali.

Kisha kumfunga Kamba na kumtumbukiza kwenye shimo la maji taka na kuwachukua mke wake aitwaye Johana Gabriel pamoja na mtoto wao aitwaye Merysiana Melkzedeck na kuondoka nao kusikojulikana.

Baada ya Jeshi la Polisi kupokea taarifa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani akiambatana na wataalam wa kuchunguza matukio makubwa walifika eneo la tukio na kupata taarifa za kuanza msako wa wahalifu na kuwapata mama na mtoto waliochukuliwa.

Msako ulioanzishwa ulifanikisha kupatikana kwa mke wa Melkizedek majira ya saa 10:00 jioni akiwa ametumbukizwa katika shimo la nyumba ya jirani umbali wa mita 300, ambalo halikuwa limeanza kutumika.

Aidha tarehe 24/01/2025 majira ya saa tisa 9:00 usiku wakiwa wamejificha katika msitu uliopo kati ya eneo la Kimalamisale na Serengeti "B" Kata ya Dutumi, Wilaya ya Kipolisi Mlandizi katika kujaribu kukwepa msako mkali uliokuwa unaendelea, Jeshi la Polisi lilifanikiwa kuwakamata watuhumiwa watatu (3) ambao walihusika katika tukio wakiwa na mtoto wa kike mwenye umri wa miezi saba (7) waliomchukua katika tukio la uvamizi la tarehe 15/01/2025 akiwa hai.

Pia katika eneo hilo Jeshi la Polisi lilifanikiwa kukamata Gari T.331 DLZ aina ya Toyota IST iliyoibwa katika uvamizi huo, Pete ya ndoa ya Johana mke wa Melkizedeki, simu aina ya Redmi na kompyuta mpakato 1. Mtoto aliyepatikana alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Tumbi kwa uchunguzi zaidi juu ya Afya yake.

Taratibu za upelelezi zinaendelea kwa mahojiano ya kina ikiwa ni pamoja na kumtafuta mtuhumiwa mmoja ambaye hajapatikana na watuhumiwa hao na mara baada ya kukamilika watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani kwa hatua Zaidi za kisheria.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linatoa wito kwa wananchi kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu haraka kwa viongozi waliopo maeneo yao na Jeshi la Polisi au chombo chochote cha dola ili hatua za haraka ziweze kuchukuliwa.

Imetolewa na:-
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Pwani
 
Melkizedeki anaendeleaje mkuu
Hao watu wanyongwe kabisa
 
Back
Top Bottom