Wahamiaji: Safari toka Congo kupitia Brazil mpaka Canada kwa miguu

Wahamiaji: Safari toka Congo kupitia Brazil mpaka Canada kwa miguu

Nionavyo kwa hakininavyokuwa hawa wzungu watakuja kuwapa sumu wasumbufu sisi
 
Waafrika tu wajinga sana. Mimali yote iliyopo Congo tunaiwacha tunaenda kuwa watumwa Canada?

Afrika raia kuwa na leseni ya madini ngumu sana. Ilitakiwa zitungwe sheria raia kuweza kuingia mkataba mzuri wa 50 / 50 wa vitofali vya dhahabu, carats za almasi, tanzanite n.k badala ya kama huyu waziri kuwanyanganya raia umiliki ardhi yenye madini

23 March 2024
Dodoma, Tanzania

Mavunde aagiza leseni 2640 zifutwe '"kuna watu wameshikilia hekari 16 milioni"​


1711201173376.png


Waziri wa Madini Athony Mavunde amemuelekeza katibu mtendaji wa Tume ya Madini kufuta maombi na leseni za uchimbaji wa madini 2640 ili kupisha waombaji wengine kutokana na maeneo hayo kuhodhiwa kinyume na utaratibu.

Waziri Anthony Mavunde ameyasema hayo leo Ijumaa, Machi 23, 2024 jijini Dodoma ambapo amesema kumekuwa na baadhi ya wamiliki wa akaunti za uombaji wa leseni ambao wamekuwa wakiomba maeneo mengi na kutoyalipia kwa lengo la kuyahodhi.

Waziri Mavunde ametoa mfano wa watu 6 ambao wamehodhi kinyume na utaratibu eneo la uchimbaji lenye uubwa wa hekari zaidi ya 13 milioni ambalo ni sawa na mikoa mitatu ya Kilimanjaro.Akitoa Mfano Mwingine Waziri mavunde amesema kuna mtu mwingine ambaye ameomba leseni ya zaidi ya mia tisa ambazo ukubwa wa eneo linaloombwa ni sawa na mikoa miwili ya Kilimanjaro.
 
09 April 2024
Mexico City

NUEVA WAKANDA MEXICO CITY
Wahamiaji kutoka Haiti wakiwa jijini Mexico City nchini Mexico kuelekea mataifa ya Marekani ya Kaskazini yaani nchi za Marekani na Canada


View: https://m.youtube.com/watch?v=Bx8p-tp3Iqs
Wahamiaji hao waliokatiza msitu mnene hatari wa Darien Gap uliopo mpakani mwa nchi za Colombia na Panama na kuwasili Mexico njiani kuelekea kaskazini. Makazi yao ya muda yamepachikwa jina Wakanda Mpya - Nueva Wakanda.

Mbali ya wahamiaji hao walioongezeka kutoka Haiti kutokana na hali ya kukosekana usalama pia umasikini. Kuna wahamiaji kutoka Venezuela, Colombia, Honduras n.k wote wakiwa njiani nchini Mexico kuelekea Marekani ya Kaskazini
Source : Luisito Comunica
 
Julai 2024
Waziri wa Usalama wa Ndani na Uhamiaji wa taifa la Marekani akijibu maswali ya maseneta wa bunge kuhusu masuala ya wahamiaji wanaoingia Marekani, kwa kupitia mpaka wa kusini baina ya Mexico na US wakati akihojiwa na kamati ya baraza la Seneti la Marekani


View: https://m.youtube.com/watch?v=9H8QwrxscGs
Wakimbizi na wahamiaji kutoka Nicaragua, Venezuelan, Cuba, Congo, Haiti, China, Iran, Afghanistan, Congo, Nchi za Mashariki ya Kati n.k kwa maelfu wakielekea border ya ... biashara haramu ya usafirishaji binadamu
 
Hao wazamiaji kwa nini wasizamie uarabuni, Iran au Russia.?
 
Noma sana, ila wazungu wakiacha kufyonza raslimali za Wafrika kama vile makinikia na kuacha tunufaike kwa raslimali zetu hawatatuona huko kwao, lakini kwa hili la wao kujenga mataifa yao yanapendeza kwa kutumia raslimali zetu, tutawafuata hadi wakome, huko huko tena tunazaliana tukifika, mama anafyatua watoto kumi huko kwao na kunyonyesha nyonyesha barabarani....
🤣🤣🤣🤣 Hiyo kunyonyesha barabarani huwa Inanikera Sana
 


Ungana nasi kwa kutazama video hii kufuatilia mguu kwa mguu toka wakiwasili jijini Sao Paolo Brazil wakijifanya raia wa Angola ktk utalii Brazil kisha wanaanza safari kwenda Canada.

Safari hii ya 'Wakongomani' toka Congo na nchi za Maziwa Makuu pia Afrika ya Mashariki wanaoingia Brazil bila viza kisha wanakutana na wahamiaji wengine toka nchi za China, Morocco, Mali, Senegal, Somalia, Nepal, Nigeria and Bangladeshi kwa miezi mitano wanakatiza mito misitu na barabara ktk nchi kumi za bara la Marekani ya Kusini kabla ya kuingia Marekani nia ni kufika nchini Canada.

Safari hii ya kilometa 20,000 wanakutana wa wahamiaji wengine toka nchi za Caribbean na Latino America ambao pia lengo lao ni kufika Marekani na Canada. Wakongomani lengo ni kufika jimbo la Quebec Canada linalotumia lugha ya Kifaransa kama Congo.

Safari hii inajumuisha kutembea kwa miguu, kupanda basi, taxi, punda, boti , ngalawa na kushirikisha wenyeji wa nchi hizo za Latin America ktk kuonesha njia za vichochoro vijijini zisizo ktk ramani za GPS maana wahamiaji wanatumia simu janja smart phone kutafuta welekeo kupuguza malipo kwa wavushaji watu kwa magendo pale inapowezekana.

Njiani katika njia za panya zilizobatizwa "Njia ya Kuzimu" kukwepa askari wa uhamiaji, kunaonekana utelezi utokanao na mvua zisizokoma za misitu minene ya tropiki, matope yafikayo ugokoni, makaburi yasiyo na jina wala alama za imani zao kwani hao wahamiaji waliopoteza maisha na sasa wamelala udongoni hata kaburini utambulisho wao haujulikani.

Nchi nyingi kama Colombia, Ecuador na Panama wameongeza vikwazo ktk vituo vya mipaka rasmi kutokana na mbinyo toka serikali ya Marekani. Hivyo wahamiaji na watu wote wanaojihusisha na biashara ya kusafirisha watu hutumia njia za vichochoroni kukwepa askari hao.

Pamoja na hayo bado kuna ongozeko kubwa la wahamiaji wanaoelekea Marekani ya Kaskazini wakiwa na imani ya kutafuta fursa na maisha bora zaidi. Wenyeji wa vijiji vya ndani ndani Colombia na Ecuador wanashangazwa na ari bila kusahau hamasa ya kusonga mbele ya hawa wageni toka nchi za mbali.

Watu watajiuliza unawezaje kukatiza nchi zaidi ya 10 salama bila kudhuriwa na wenyeji au magenge ya kutorosha watu mipakani.

Sababu ni kuwa hii ni biashara kubwa inayoingiza kipato na makundi ya waliokuwa wanasafirisha madawa ya kulevya sasa wamejiingiza ktk biashara hii ya kusafirisha watu. Hivyo wakubwa wa magenge haya hawataki kusikia mtu kakabwa au kina mama kubaka n.k na kuwataka wote wanaojihusisha na biashara hii ya kuvusha watu kimagendo mipakani kuwalipa 'kodi' ma drug lords na pia kuhakikisha wageni hao wanamaliza safari salama ili njia zao ziendelee kuaminiwa na maelfu ya wageni hawa waendao Marekani ya Kaskazini. Yeyote atakaye mdhuru mgeni huadhibiwa kwa adhabu kali na wababe hawa wa biashara hii ya kusafirisha wageni.

Canada has become the new El Dorado for many African migrants, who have seen Europe and the United States close their borders.

But they face a dangerous journey across South and North America. Every year, some of them die on their way to a better life, amid widespread indifference to their plight.

For five months, our reporters followed Rosette and her family from DR Congo on this long, dangerous odyssey across ten countries. In the space of five months, Rosette and her family have travelled more than 20,000 kilometres – risking their lives.

First, they fled DR Congo for Brazil. Then, from Sao Paulo, where they arrived on a tourist visa, they crossed South America – including the perilous Colombian jungle – before reaching the United States and finally their Canadian El Dorado.

They traversed ten countries in total, in the hands of powerful clandestine networks of people smugglers and cartels, and corrupt policemen or soldiers who control the borders.

They often crossed paths with cocaine smugglers heading for North America. ►► Now hiring! Unemployment in Quebec hits record low During the five months that we spent with Rosette, her husband Godet and their daughters Maria and Pauline, we saw many other migrants heading north to Canada.

On this route, where a human life is worth just a few handfuls of dollars, Congolese, Malians, Senegalese, Nepalese and Bangladeshis try to blend in with the flow of South American and Caribbean migrants.

But some will never reach their destination. We spent longer on the most dangerous stage of the journey: a vast stretch of jungle called the Darien Gap, the only way of getting from Colombia to Panama.

Finally, we reached the Canadian border, which is seeing an unprecedented wave of illegal migrants crossing daily to seek asylum, all of them desperate for better lives. Report by François Rihouay. A Keep In News production with teams from France 24, Radio Canada, and RCN (Colombia).

Source: France 24

Duh!!! Hao watoto wadogo wanatia huruma aisee.
Mungu awasaidie sana
 
10 Agosti 2023
Sao Paulo, Brazil

Wazamiaji stowaway wajipigilia kwenye rudder ya Meli "the Ken Wave' waibukia Brazil.

Wazamiaji waliosafiri juu ya mkono wa usukani wa meli (mkombo) wakipewa maji na polisi wa majini Brazil


Muda kidogo baada ya saa sita usiku tarehe 27 Juni, Bw. Roman Ebimene Friday alikusanya chakula alichokuwa akikusanya kwa miezi michache na kuanza gizani kuelekea bandari kubwa ya kibiashara katika jiji la Lagos, Nigeria.

Mapema siku hiyo, Ijumaa alikuwa ameiona meli kubwa yenye urefu wa futi 620 (m 190) ikiwa imetia nanga kwenye bandari hiyo na kuamua kuwa ndiyo ingekuwa meli ya kumpeleka Ulaya.

Bw. Friday alikuwa amelenga sehemu ya nje ya usukani wa meli ya mafuta inayoogoza mwelekeo wa meli yoyote kwa kuwa ktk meli kubwa kiasi hicho kulikuwa na nafasi ya kizimba cha futi 6 kwa sita.

Akamuomba mvuvi mmoja kumfikisha melini kwa kificho kutokea baharini. "Alikuwa mtu mtakatifu mtu wa Mungu , mvuvi yule," Friday alikumbuka. "Hakuomba pesa. Aliona kwamba nilitaka kuondoka kutafuta kutoka kimaisha ulaya hakuwa na noma yoyote ."

Mvuvi huyo aliiegemeza ngalawa kwenye usukani wa meli ya the Ken Wave na kisha Bw. Friday , 35, alijiinua kuingia eneo la chuma hicho huku akibeba mfuko wake wa chakula nyuma yake kwenye kamba. Alipojiweka sawa aliona, kwa mshangao, nyuso tatu gizani. Alikuwa wa mwisho kati ya wanaume wanne waliokuwa na wazo moja. "Niliogopa, mwanzoni," Bw. Friday alisema. “Lakini walikuwa mabraza Waafrika weusi, ndugu zangu.

Kwa kuogopa kukamatwa, wanaume hao wanne walikaa kimya kwenye usukani kwa saa 15 zilizofuata. Saa kumi na moja jioni, walihisi injini kubwa za meli zikitetemema. Wote kwa dini zao walipiga kelele kwa maneno machache ya sala . Wote walikuwa wanalenga kufika Ulaya. Walitarajia kuwa wasafiri kwa muda wa wiki moja.
View attachment 2715377
Meli hiyo, iitwayo Ken Wave, ilijisukuma kutoka bandarini Lagos na kuelekea baharini bahari kuu - mwanzo wa safari ya hatari ya wiki mbili ya bahari ambayo ingewaleta karibu kifo.

Huku wakiona mataa ya majengo marefu ya jiji la Lagos taa zake zikizidi kufifia kutokana na jinsi safari ya meli iliendelea kuingia bahari kuu , wanaume hao walijaribu na kushindwa kupata nafasi nzuri kwenye sehemu hiyo ya usukani, ambao ulisogea kila mara ilipokuwa ikiongoza meli. Kulikuwa na nafasi ndogo sana ya kusimama, na mahali pekee pa kulala palikuwa katika mojawapo ya vitanda vilivyotengenezwa kwa kamba za plastiki viwili vidogo vilivyofungwa kwa hatari juu ya maji, na wazamiaji walio tangulia, Bw. Friday anaamini wakati akiviangalia.

Inaweza kuwa vigumu kuelewa sababu ni nini kinachomsukuma mtu kuhatarisha maisha yake kwa kujipigilia katika usukani wa meli au mashua yenye misukosuko katika Bahari ya Mediterania. Lakini uamuzi unakuja rahisi wakati tayari umepoteza matumaini, Bw. Friday alisema.
View attachment 2715395
"Nchini Nigeria hakuna kazi, hakuna pesa na hakuna njia ya mimi kuwalisha wadogo zangu na mama yangu," alisema. "Mimi ni mtoto wa kwanza wa kiume na baba yangu alifariki miaka 20 iliyopita, hivyo napaswa kutunza familia yangu, lakini siwezi."

Walikuwa wamejipigilia kwenye meli ilipokuwa imefungwa kamba katika gati ya bandari umbali wa maili 3,500 - huko kwao Lagos, jiji lenye watu wengi zaidi katika taifa la Afrika Magharibi la Nigeria.

Wakisimulia safari yao ya kutisha kwenye gazeti la The New York Times la Marekani , walisema walitumia siku 14 kuvuka Bahari ya Atlantiki, wakiwa wameegemea chuma baridi cha usukani, wakiwa na hofu ya kuanguka kwenye maji yanayotembea kwa kasi chini ya miguu yao. Wakati mwingine, waliona papa. "Tuliogopa sana, tuliendelea tu kusali," alisema mmoja wa wanaume hao, Bw. Roman Ebimene Friday


Kwa njia fulani, njia za meli ni salama zaidi kuliko zile zinazovuka sehemu za Sahara kwa miguu au Mediterania kwa boti za mbao zenye misukosuko. Lakini siku ya tano ilipopita, Bw Friday na Bw. Yeye walianza kuhesabu hatari mahususi za hali yao.

Tayari walikuwa dhaifu kutokana na kugawana chakula chao na uchovu wa kukosa usingizi. Walifunga kamba viunoni mwao walipohitaji kukojoa kando ya usukani. Wakati maji yalikuwa magumu, mawimbi yaliwapiga. "Sote tuliogopa mawimbi makubwa," alisema Bw.Yeye. ""

Nyavu za vitanda vya kamba ya plastiki zililegea na ikabidi zifungwe tena kwa njia isiyo ya ustadi. Walilala tena ndani ya nyavu lakini Bw. Friday alikumbwa na ndoto kila mara aliota tu kuamshwa na hisia ya ghafla ya kuanguka na kupigwa na baridi chini. "Neti ikipasuka, unaingia moja kwa moja kwenye maji na umekwenda," alisema. Na kweli ulikuwa umeenda. Hakuna nafasi ya kuokoa baharini wakati hakuna anayejua kuwa umepotea



"Sijawahi kuona bahari hapo awali lakini nilikuwa nikitazama filamu kuhusu dhoruba na niliona meli kubwa zikitikiswa kutoka upande hadi upande kwa mawimbi." Usingizi ulikuwa hauwezekani kabisa. "Unajaribu hata kufumba macho yako," Friday alisema. "Usukani hugeuka saa 24 kwa siku, siku saba kwa wiki, unapaswa kuwa macho kila wakati."

Wakiwa na wenzao wawili, William na Zeze, walipita siku chache za kwanza kwenye meli katika mchanganyiko wa kuchoka, usumbufu, na woga, wakizungumza kidogo tu, wakiomba mara kwa mara na kujaribu kukesha, huku meli the Ken Wave - Wimbi la Ken lijisukuma ndani ya eneo kubwa. eneo la Atlantiki ya kusini kwa safari ya maili 3,500 kwenda Brazili.

Siku ya tisa, walisema waliishiwa chakula na maji. "Tulilamba colgate dawa ya meno na kunywa maji ya bahari ili tu kuwa na nguvu," Bw. Friday alisema katika mahojiano ya simu kutoka kwa makao yao mapya huko mji wa São Paulo, Brazili, alipokuwa akiishi.

Baada ya siku 14 wakiwa baharini waliona boti ya polisi marine ikiwafuta.

"Tulipowajulisha kuwa sisi ni polisi wa shirikisho la Brazili, walikumbwa bumbuazi na kuuliza 'Je, tuko Brazili?'" Rogerio Lages, mkuu wa kitengo cha wanamaji cha polisi wa shirikisho katika jimbo la Espírito Santo, ambako meli hiyo ya mizigo imetiwa nanga.


Kikosi chake cha polisi maji kiliitwa kwenye bandari ya Vitória, kama maili 350 kaskazini mwa Rio de Janeiro, mnamo Julai 10 baada ya mashua iliyokuwa inawasafirisha wafanyakazi wapya hadi kwenye meli iliyobatizwa jina the Ken Wave 'Wimbi la Ken' kuwaona wahamiaji kwenye usukani, wakiomba msaada.

Wawili kati ya wanaume hao waliomba kurejeshwa Nigeria, mamlaka ya Brazil ilisema, lakini Bw. Friday na stowaway wa nne, Bw. Thankgod Opemipo Matthew Yeye, waliamua kusalia na wametuma maombi ya kuwa mkimbizi.

View attachment 2715360
Picha: wakiwa wameketi kwenye benchi ya bustani nje ya kanisa la Jeshi la Wokovu . Bw. Thankgod Opemipo Matthew Yeye, kushoto, na Bw. Roman Ebimene Ijumaa mjini São Paulo Brazil mwezi uliopita. Wameamua kusalia Brazili na wametuma maombi ya kuwa mkimbizi

Bw. Friday, 35, ambaye anatoka Bayelsa, jimbo katika Delta ya Niger, eneo lililochafuliwa la petroli, alisema alikuwa akitafuta kazi huko Lagos kwa karibu miaka miwili, akitumai kusaidia mama yake mjane na wadogo zake watatu.

Alikuwa na pesa kidogo sana, alisema aliishi na usiku kulala chini ya madaraja ya mji mkubwa wa Lagos Nigeria huku
"Ninafikiria sana jinsi ya kuwa mtu bora zaidi kimaisha ," Bw. Friday alisema, akielezea kwa nini aliondoka Nigeria, "kwa hivyo nilichagua njia hii kufanya maisha bora ya baadaye na kuweka msingi kwa ndugu zangu wadogo."

Aliyesimama karibu na Bw. Friday kwenye usukani wa meli ya alikuwa Bw. Thanksgod Opemipo Matthew Yeye, mchungaji wa madhehebu ya kanisa la Pentekoste, mfanyabiashara na baba wa watoto wawili ambao shamba la karanga na michikichi lilisombwa na mafuriko yaliyoikumba Nigeria mwaka jana. Hakukuwa na kurudi nyuma au bima ya kufidia hasara.

"Biashara yangu iliharibiwa na familia yangu ikakosa makazi. Na huo ndio ulikuwa mwanzo wa uamuzi wangu wa kuondoka," alisema.

Uamuzi wa mchungaji wa kanisa Bw. Yeye ulikuwa wa mwisho baada ya uchaguzi wa rais wa hivi majuzi, ambao ulikumbwa na hitilafu na madai ya wizi wa kura. "Uchaguzi umekuwa tumaini letu," alisema. "Lakini tunaifahamu vyema Nigeria, tunajua mfumo huo ni mbovu." Kwa hiyo, bila kuwaambia familia yake, aliondoka nyumbani kwa dada yake usiku na kuelekea bandarini, ambako alijua kwamba meli kubwa ya the Ken Wave- Wimbi la Ken lilikuwa likingoja kuondoka.

Nigeria imeshuhudia kuhama kwa watu kama Bw. Yeye na Bw. Friday katika miaka ya hivi karibuni, kupitia njia za kawaida na zisizo za kawaida, zinazoendeshwa na kushuka kwa uchumi na kurekodi viwango vya ukosefu wa ajira. Wengi husafiri kuvuka Sahara na Mediterania, ambapo takriban Wanigeria 1,200 wamekufa tayari mwaka huu 2023, kulingana na UN.

Maisha ya kila siku yamekuwa magumu kwa Wanigeria wengi katika miaka ya hivi karibuni huku taifa hilo likipambana na migogoro karibu kila eneo: uasi wa Kiislamu, mfululizo wa utekaji nyara na mapigano mabaya kati ya wakulima na wafugaji kuhusu ardhi katika taifa ambalo idadi ya watu inaongezeka.

Kuna watu wachache Nigeria wenye utajiri katika maeneo kama Lagos, yenye benki zake za uwekezaji, majumba ya starehe ya sanaa na harusi za kifahari za wasomi ambazo huvutia mamia ya wageni. Lakini kwa Wanigeria wengi, ukosefu wa ajira umekithiri, na kusaidia kuchochea msafara mkubwa kukimbilia mabara ya Ulaya, Marekani .

Idadi ya wahamiaji kutoka Nigeria, ambayo ina wakazi wapatao milioni 224, iliongezeka mara tatu kati ya 2009 na 2019, kulingana na Kituo cha Maendeleo ya Ulimwenguni.

Kufikia mwisho wa 2020, Nigeria iliorodheshwa katika nchi 10 zinazo ongoza duniani zenye idadi kubwa ya watu wanaoishi nje ya nchi, kulingana na Takwimu za Umoja wa Mataifa UN .

Wengine huchagua kujificha melini . Mwaka jana, wanaume watatu walipanda usukani kwa mtindo sawa na Bw. Friday na Bw. Yeye, na safari yao iliwachukua maili 2,500 hadi visiwa vya Canary, bahari ya Atlantic mahali pa kuingilia Uhispania. Bw. Friday na Bw. Yeye waliamini wanafuata njia hiyo hiyo ya Uhispania ulaya.


Hivi karibuni Bw. Friday na mchungaji Bw. Yeye walipata vibali vya kazi nchini Brazil na wameanza kuomba kazi.

“Natarajia sana kupata usaili wa kazi,’’ Bw. Yeye alisema. "Nadhani hicho ndicho kitu kinachofuata kwangu sasa. Kwa kweli nahitaji kazi sasa ili kutunza fedha kwa ajili yangu na familia yangu.” Alisema anatumai kupata pesa za kutosha kuleta familia yake Brazil.

Wazamiaji wote wawili wamechukuliwa katika Casa do Migrante, makazi ya wahamiaji huko São Paulo ambapo wanapata ahueni kutoka kwa safari yao. Wamepata usaidizi wa kuwakilisha makaratasi ya uhamiaji, kujiandikisha kwa masomo ya Kireno na kujifunza kuhusu mila na utamaduni wa Brazili.

"Sikuwa hata nikitarajia kwamba ningekuja Brazili, lakini nimejikuta nipo Brazili, na ni mahali pazuri zaidi," Bw. Friday alisema. "Nina furaha sana."

Wala hawakujua mengi kuhusu nchi hiyo mbali na timu yake maarufu ya soka, walisema. Sasa, wanapanga kuifanya ni nchi yao.

“Hadi sasa,’’ Bw. Yeye alisema, “Nimeona kwamba Wabrazili ni watu wenye urafiki na wenye upendo sanaHawa



Hawa wajuba walitisha sana.
 
Vita na ugumu wa maisha vinatufanya binadamu kuhangaika namna hiyo.

Wangebaki huko dunia ya tatu guarantee ya kuteseka na ugumu wa maisha na kufa masikini ni zaidi ya asilimia 90
Hawa ni wasanii wa kawaida wa kingole msiwaamini. Mtakaowafuata mtapotea bure.
 
Back
Top Bottom