MKUU WA KAYA(MUHAYA) AKITOA MAELEKEZO KWA DADA WA KAZI KABLA YA KUONDOKA NYUMBANI ASUBUHI:
Mimi natoka watu wa sensa wakiulizia nimeenda wapi waambieni nimeenda bank kuchukua milioni thelathini kwa ajili ya ada za kaka zenu wawili wanaosoma PHD uingereza, wakiuliza jumla mu wangapi waambieni tuko nane, ila Bibi mzaa Baba ameenda India kutibiwa na yupo huko mwezi sasa, na imetucost mpaka dakika hii milioni sabini, mama yenu muwaambie yupo site, anasimamia ushushwaji wa vifaa vya ujenzi 'kwa ajili ya finishing' vimetoka China ambavyo vimetugharimu milioni 600, halafu na watoto wengine waliobaki waambieni wameenda kutembea serengeti na rafiki zao wametoka Australia, na wanatumia gari mbili Range Rover na Hummer, kama watahitaji kuongea namimi wapeni namba zangu za Blackberry tu, zile Samsung Galax waambieni huwa natumia kwa family Issues tu ...