Wahenga wa kike: Mnakumbuka nguo za redimedi, sare sare, moka bila kisahau fukufuku

Wahenga wa kike: Mnakumbuka nguo za redimedi, sare sare, moka bila kisahau fukufuku

Wahenga wa kike mnakumbuka haya!

Magauni ya redimedi!

Nguo za sare sare(sare sare maua asiyejua kuchagua kabila lake mzegua[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3])

Moka nyeupe kwa nyeusi!

Soksi nyeupe zina maresi kwa juuu zikilegea ni balaaaa!

Vimkoba vilivyokuwa vinakuja na redimedi na kofia zake zina maua na kambaa ya kubana shingoni.

Baada ya kuvaa redimedi sikukuu unajipaka wanja alafu unaweka vidoti vitatu mashavuni na kwenye utosi usoni.

Ukinunua pichu mpya lazima uwaonyeshe mashosti zako [emoji3][emoji3][emoji3]

Siku mkipika wali nyamaa sasa swali la kuwauliza mashost zako
( Otea kwetu leo tumepika nini?)agggh ilikuwa rahaaaaa sana.

Shunie karibu uchukue fukufuku .



Mrs Jr (Malikia wa Ulozi)
picha bana!!
 
Fashion zinajirudia tu, nikiziangalia picha za dingi yangu za miaka hiyo, amepigilia mbano(modo) ya hatare utasema Peter Tosh au Bob, nami ktk ubro men nimezipiga hizohizo, ukiniona utadhani nilizivaa kwa sabuni.
 
Halafu kwa wanaume kuna vitu walikuwa wanavaa, wenyewe wanaviita VIP
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28], mhenga wa kiume anaweza nisaidia kwa hili.
 
Hahahha! Aisee nakumbuka nguo ilikuwa yanunuliwa mapema kabla ya sikukuu, basi kufika sikukuu ishachafuka kwa kujaribisha,,

Hapo unakuwa wataka marafiki zako waione, halafu ushajua mama kaiweka wapi.. Una mvizia mama yupo nje, unaivaa halafu
unawaambia marafiki zako wakae mkao wa kula,,hahahaha! Wanakaa mlangoni halafu unakuwa unajipitisha ili wakuone..Hahahaha
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]mm nilikuwa nafichiwa ndani
 
Ukiona gauni la mwenzio zuri unaenda kumwambia mamako na mi nataka kama la vero,utalia mpaka litaletwa,ila sasa mama angu ni kiboko,siku nyingine hataki huo upuuzi,ukililia nguo utachapwa mpaka uone moto(nadhani hapa pengine anakua hana hela[emoji23] maana siku nyingine nikilia napata)
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]heshima kwa wamama wote wa kwangu mkali ananunua kimya kimya anaficha na alikuwa anajua saiz zetu vizur sana ila anaficha sjui kwann
 
Hahahahahahah daaaah nimecheeeka hiyo ya kujipitisha,nilikua nawaambia wenzangu,kaeni hapa nikawaoneshe nguo nimeletewa naenda navaa af natoka nasimama mlangoni,watanishika shika kunisfia mpaka ichafuke
Ukisikia mama anarud ndukiii mpaka ndani
 
Yaaaani kama ulikuwepo hahaha lilikua la blue bahari,afu hizo nguo mama mpaka leo zake kazitunza,ila zangu uwii nilikua sizipendi nazichukia akazigawa
Wamam jaman resi material mama angu anayo mpaka leo
 
Hahahaha! Ilikuwa raha sana.
Ilikuwa inachanganywa, suruali rangi moja halafu blauzi inakuwa ya maua maua, blauzi inakuwa na mipasuo pembeni.
Wahindi style na kiatu cha kamongooo agggh
 
Hapo kwenye Mokasi ni za kiume za kike zilikuwa zinaitwa Skuna, sisi wanaume tulikuwa tuna suruali za Tokyo. Yaani ukivaa Tokyo we mkali, zilikuwa zina mikanda yake noma sana aisee, wadudu maarufu enzi hizo, ni panzi, fukufuku, dondora kwenye mipera, na wale wanaopatikana kwenye michongoma wana pembe kama za ngombe walikuwa wanacbezeshwa kwa kujizungusha chini pembe zao, mwisho kabisa walikwepo bruce lee walikuwa wana mapigo ya kibruce maarufu kama vunjajungu, hahahahahahahaaa nimecheka sana kwa kukumbuka enzi za wakati huo wa kucheza majoka style ni kuchezesha mabega, kwenda kibisa, na mazingaombe ya mashuleni hatari sana wakina power mabula.
Niishie hapo.
Umenichekesha kwenye dondola jaman ukienda kula maperaa au zambarau lazima ukung'utwe na dondolaaaa hahahahahhaha
 
Back
Top Bottom