Wahenga wenzangu njoo tukumbushane vipindi vilivyobamba RTD enzi hizoo

Wahenga wenzangu njoo tukumbushane vipindi vilivyobamba RTD enzi hizoo

Khantwe

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
59,415
Reaction score
119,473
Jamani kweli siku hazigandi. Nakumbuka enzi hizo hakuna utitiri wa redio stations ukitaka kusikiliza huna option kama kipindi kilichopo hukipendi uzime tu radio.
Hata mfumo wa vipindi ulikuwa tofauti sana na huu wa sasa...enzi hizo vipindi vililenga kutoa elimu zaidi kuliko burudani. Kama kipindi ni cha kutoa elimu kuhusu masuala ya umeme let's say, hakuna porojo ni elimu tu mwanzo mwisho.
Nakumbuka ilikuwa miaka ya tisini mwishoni hivi, kuna vipindi nilikuwa sipitwi kabisa hata kama nilikuwa kucheza muda huo ntafanya juu chini niwepo

Kulikuwa na vipindi vya watoto kimoja nilikuwa kinaitwa Mama na mwana kilikuwa kinarushwa jumamosi saa nane na nusu. Nilikuwa sipitwi kabisa....kulikuwa na hadithi zilikuwa zinasimuliwa naikumbuka moja tu ya Binti Chura.

Kuna kipindi kingine kilikuwa kinaitwa Twende na wakati ulikuwa mchezo wa kuigiza unarushwa kila jumamosi saa mbili na nusu usiku. Nilikuwa nafuatilia hatua kwa hatua maana ulikuwa haurudiwi ukipitwa ndo tuonane next episode.
Karibu mdau tukumbushane wewe ulikuwa unapenda vipindi gani?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mama na mwana.. cha edda sijui naniii pamoja na pwagu na pwaguzi.

Kuna pia mazungumzo baada ya habari. Ukija miaka ya 2000 kuna ule mdundo wa majira aseeh nilikuwa naupenda pamoja na utangazaji wa Ezekiel malongo kwenye mpira.

Kuna kipindi nilikuwa nachukua kanda na tape RTD. Moja ya vipindi nilivyowahi ku-tape ni cha ule mdundo majira na ule wimbo wa tunaye Rais Ben will wa Tanzania.

Ila pia kwa wale wa KBC je huu ni uungwana cha mzee mbotela kiliiteka Kenya kipindi hicho.
 
Jamani kweli siku hazigandi. Nakumbuka enzi hizo hakuna utitiri wa redio stations ukitaka kusikiliza huna option kama kipindi kilichopo hukipendi uzime tu radio.
Hata mfumo wa vipindi ulikuwa tofauti sana na huu wa sasa...enzi hizo vipindi vililenga kutoa elimu zaidi kuliko burudani. Kama kipindi ni cha kutoa elimu kuhusu masuala ya umeme let's say, hakuna porojo ni elimu tu mwanzo mwisho.
Nakumbuka ilikuwa miaka ya tisini mwishoni hivi, kuna vipindi nilikuwa sipitwi kabisa hata kama nilikuwa kucheza muda huo ntafanya juu chini niwepo

Kulikuwa na vipindi vya watoto kimoja nilikuwa kinaitwa Mama na mwana kilikuwa kinarushwa jumamosi saa nane na nusu. Nilikuwa sipitwi kabisa....kulikuwa na hadithi zilikuwa zinasimuliwa naikumbuka moja tu ya Binti Chura.

Kuna kipindi kingine kilikuwa kinaitwa Twende na wakati ulikuwa mchezo wa kuigiza unarushwa kila jumamosi saa mbili na nusu usiku. Nilikuwa nafuatilia hatua kwa hatua maana ulikuwa haurudiwi ukipitwa ndo tuonane next episode.
Karibu mdau tukumbushane wewe ulikuwa unapenda vipindi gani?


Sent using Jamii Forums mobile app

From muhenga/pwagu na pwaguzi.
 
Mama na mwana.. cha edda sijui naniii pamoja na pwagu na pwaguzi.

Kuna pia mazungumzo baada ya habari. Ukija miaka ya 2000 kuna ule mdundo wa majira aseeh nilikuwa naupenda pamoja na utangazaji wa Ezekiel malongo kwenye mpira.

Kuna kipindi nilikuwa nachukua kanda na tape RTD. Moja ya vipindi nilivyowahi ku-tape ni cha ule mdundo majira na ule wimbo wa tunaye Rais Ben will wa Tanzania.

Ila pia kwa wale wa KBC je huu ni uungwana cha mzee mbotela kiliiteka Kenya kipindi hicho.
Alikuwa anaitwa Edda Sanga. Hivi yupo hai huyu mama? Mazungumzo baada ya habari acha kabisa. Nakumbuka karibu na uchaguzi wa 2000 yule baba mazungumzo yake yalijikita kuponda wapinzani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom