Kwa Mungu hakuna huyu mtumishi ndio Bora kuliko wengine. Mungu amempatia kila mmoja karama yake, na huwezi kushindanisha karama na kuanza kuwashindanisha watumishi.
Na mara nyingi tunapotoka kwa kulazimisha kwamba watumishi maarufu ndio waziri kuliko wengine. Mtumishi akisha kuwa na you tube channel au redio basi ndio anaitwa Bora.
Kuna siku nilikuwa nasikiliza Mwalimu Mwakasege, akasema Kuna siku Mchungaji wa Kanisa alimfuata akamwuliza , Kama Mwakasege akiwa kwenye ibada huwa anafuatilia mahubiri ya watumishi wengine. Mwakasege akamjibu kuwa huwa anafuatilia Sana na Kuna mambo mengi anayapata.
Point ya Mwakasege ni kwamba kila mtumishi kawekewa kitu chake tofauti hivyo huwezi kuanza kuwarank huyu ni Bora huyu sio Bora ( hii happy kwa manabii matapeli).
Mimi miaka ya Nyuma nilikuwa najua Askofu Kulola ndio mwanzilishi wa Upentekoste, ila nilipokuja kusoma historia ya Upentekoste nikagundua kumbe kulikuwa Kuna watumishi wakubwa miaka ya nyuma walioanzisha Upentekoste, tatizo hawakuwa maarufu.
Kwa mfano miaka ya 1935 kipindi Cha ukoloni kulikuwa na mwinjilisti mkubwa Sana alihubiri maeneo mengi Sana alikuwa anaitwa Harris Kapiga. Na wengine wengi akiwemo Mzee Andrea shimba ila hawakuwa maarufu. So nashauri tuachane na roho ya mashindano ndani ya kanisa , na kila mmoja afanye kwa kadri alivyopewa na Mungu.