Wailboru wenzangu nasikia Mwigulu naye ni Muilboru

Wailboru wenzangu nasikia Mwigulu naye ni Muilboru

Ok nyie iliboru mie chama linalojulikana kichwa cha tanzania,am talking about berlin! Hapo alisomeshwa kichwa namber moja wa tanzania.Pale vilaza hawapiti salama,nature eliminates them

mimi sikuwa huko, nilikuwa kwa makamanda Tabora Boys, nachoweza kusema kwa ndugu zangu wa ilboru, kuhusu Mwigulu, "yule mtoto si rizki".

Wakuu pamoja sana. Ila uzi huu ulikuwa wa wana Ilboru na matendo wanayofanyiwa na mwenzao. Tusiwashangae kwanini mwenzao anafanya vitu visivyoendana na watu waliopitia shule hizo. Hata sisi tunae member hapa anaitwa Rejao siku zote huwa ananishangaza kwa mitazamo yake. Sie tuna uzi wetu hapa mkiutafuata mtaupata.
 
Niameanza nae 1994-97,sijui kwanini kwa sasa amekuwa anaongea kwa jazba bila kutegemea hoja ya nguvu,may be atajirudi
 
Nyie mnaojiita wnailboru acheni majivuno mbona hakuna chochote mnachoonyesha cha ziada katika taifa letu. Mngepata majukwaa ya kisiasa mngejisifia tu kama Mwigulu wote ni walewale tu.
 
huyo nchemba anatuaibisha sana,wana ilboru hatukuwa na swaga za kiivyo,mawenzi moja...chief pia is no more
 
hakuna cha ilboru wala ilbaru hata usome wapi izo n tabia za mtu achen kujiona special nyie
 
Shule yangu Ilboru inasifika sana...
Popote unapoenda inasifika sana.....
Haka kawimbo kaliniacha hoi enzi za Bino pale Ilboru
Hata mimi ni wa enzi za Bino!.
Wengi niliowasikia humu walikuwa yale mabweni ya high class, sijabahatika kumsikia hata mmoja aliyekuwa Oldonyo!. Jamani mimi mwenzeni nilikuwa Oldonyo by choice!, na kitanda changu kilikuwa kwenye hall na sio kule cublicle chembar, nimepiga sana sumu na chui!.

Tukubali tukatae, jamaa ni kichwa!, O-Level alipiga Div 1 kali, A-Level pia akatundika 1, pale UDSM akapata GPA kali na kuunganisha Masters.

Majisifu yake ni ule msemo wa masikini akipata.., kwa vile jamaa katokea Singida, unaweza kukuta kijiji kizima wameishia la 7, hivyo yeye kufika chuo kikuu unaweza kukuta ndio pekee wilaya yake nzima!, sasa kuunganisha na masters, basi ndio anajiona yeye ni mfalme kabisa!. Nadhani anampago wa kupiga Ph.D, basi ndio atatembelea dole gumba kabisa ili apae juu!.
 
Back
Top Bottom