Waislamu kumbukeni kujenga nyumba nzuri ya imamu karibu na msikiti. Pia maimamu na mashehe wawe na mishahara kama wakristo kwa wachungaji

Tembea uone. Kuna umuhimu wa philosophy na theology katika kuwa kiongozi wa dini. Ndio maana ukifuata uislamu kwa asilimia mia moja hauwezi kutoboa hapa duniani. Unajua kuwa uislamu unakataza hadi teknolojia. Ndio maana uarabuni kote wenye taaluma ni watu ambao sio waarabu. Waarabu wamebaki kama wamiliki wa biashara na wananchi tu.
 
Kuna madrassa ada ya mwezi wanachaji buku lakini pia wazazi wanalimbikiza malipo.

Huwa najiuliza inakuaje mtu analipa school fees million halafu madrassa buku tu shida kulipa.

Hivi hamjisikii vibaya mnavyoona maustaadhi wana hali mbaya kiuchumi?
 
Kuna Vitu ulitakiwa uvisome kati ya hizo dini mbili na utofauti wake .Imam Sio kazi ya kudumu na yeyote aliekamilika kwa mujibu wa uislam anaweza kusalisha muda wa sala unapowadia hata Huyo Imam akiwa hayupo sasa hao woote nao walipwe?na pia kutokana na mafundisho ya Mohamad s.a.w Ni kuwa yeye mwenyewe alikuwa na kazi nyingine tofauti na kufundisha dini na Ndo pia aliacha mafundisho kwa waislam pindi wanapomaliza kusali watawanyike kwenye tumbo la dunia kutafuta mkate wao wa kila siku.......sasa Huyo imam mshahara wa nini.?japo kisasa Ndo Kuna baadhi ya misikiti wanaajir na mengine wanatoa posho ya kujikimu Ila Sio mafundisho tuliyoyapokea


na Hata hao wakristo wanapomlipa padri au mchungaji Sio mafundisho na Sijui wamelitoa wapi Hili jambo....nyie Ni kondoo mnachungwa iweje mumlipe anaewachunga wakati yupo Baba alietoa hiyo kazi ya kuwachunga.Huyo mchungaji alipwe na aliemtuma awachunge na Sio nyie kondoo mumlipe
 
Ilibidi ujifunze Hata kidogo kuhusu uislam ili uwe na hoja ktk hili

Kusalisha Sio lazima kwa imam....yeyote atakaekuwa hapo muda wa sala umefika atasalisha Ila awe tuu amefikia na kukidhi vigezo vya sala

Hizo ndoa anazofungisha anavuna thawabu kuubwa kuliko hizo pesa anazolipwa japo anapofungisha ndoa hulipwa na hao anaowafungisha

Sala ya maiti Ni km nilivyokuelekeza hapo juu yeyote anaweza kuisalisha akitimia kwenye vigezo na Hata kwenye mazishi mnaweza kuzika Bila kuwa na Imam wala Sheikh kikubwa ni.kujua na kufuata hukmu za maiti


Na Ndo Maana Haya Mambo yanafundishwa kuanzia kwa watoto wadogo ili kujenga uelewa wa dini na taratibu zake
 

Watachinjana na kuuna sana bora wabaki hivyo hivyo mana ndugu zetu hawana subra wala kusamehe,unakumbuka ya juzi bukoba jamaa alitaka kumchinja imamu kisa kuondolewa kazi ya kibarua akaishia kumkata kiganja na yeye kuuwawa na haya aliyafanya mchana kweupe tena msikitini siku ya ijumaa.

Shida nyingine hawa ndugu wana tamaa na hawana misingi ya usimamizi wa raslmali watauza wote kama walivyouza ardhi zao kisha kuanza kujiliza wamedhurumiwa. Playing victms.
 
Hivi ndugu zetu katika imaan, huwa mnajenga hata nyumba zenu za ibada kweli kupitia michango yenu ya hali na mali!

Au ndiyo mpaka wajitokeze wadau kama akina Muammar Gaddaf (RIP), Mfalme wa sita wa Morocco, Magufuli na Waumini Wakatoliki kule Chamwino, nk. kuwajengea!
 
je Hali nzuri yake imekuja kwa kulipwa na Waislamu, ama hali nzuri yake imekuja kwa shughuli zake binafsi nje ya msikiti ?

Halafu mbona mashehe wa wilaya mkoa na walioko bakwata wanalipwa mshahara na sirikali,na pia wakihudhuria vikao au mikutano ya sirikali hupewa bahasha nyeupe.
 

Ngoja nije chumbani unieleze kwa kina huku unaniandalia kahawa na tende mujarab
 
Kwanza unatakiwa ujuwe imamu ni nani tafsir yake ,pili imamu anaweza kuwa mtu yoyote ilikuongoza swala baada ya hapo anakuwa na shughuli zake za utafutaji kama kawaida ,siyo kuwa imamu anatakuwa kushinda msikitin haiko hivyo

Mbona kuna watu wanalala na kushinda msikitini.
 
Maimamu hushinda misikitini huko ndani kunamajini ambayo huwapa stahiki yao ya kila siku.
 
Sasa wale si wanachumia matumbo ebu usiwalinganishe na watu wanaopambania Pepo yakhe.

Kila mtu ni mchumia tumbo ndiomana wanagombania miskiti na kuuza ardhi za taasisi za kiislam,yote hayo ni maslah binafsi ila katika angle tofauti
 
USHAURI KIDOGO:
Umeona mbali sana aisee.
Sasa unaonaje ukaenda kwenye huo Msikiti wa huyo Imam ukawaambia,
Tena uwakute wapo wengi wakusikie vizuri namaanisha kama Ijumaa moja hivi.

Utatisha Jombaa.
Mavii aende haone kilichomtoa kanga manyoya[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Swadaktaaa!!!!
 
Kuna madrassa ada ya mwezi wanachaji buku lakini pia wazazi wanalimbikiza malipo.

Huwa najiuliza inakuaje mtu analipa school fees million halafu madrassa buku tu shida kulipa.

Hivi hamjisikii vibaya mnavyoona maustaadhi wana hali mbaya kiuchumi?
Pale tabata shule,Kuna hotel Kwa nyuma Pana msikiti,baada ya swala ya ijumaa imam kafunga msikiti asitoke mtu analalamika malipo ya sh 50,000 ya mfanya usafi.Hizo 50000 kachangisha wiki tatu hazikupatikana🤣

Imam analalamika mnasomesha watoto wenu shule za bei kuubwa,msikiti hamjali🤣
 
Una hoja..!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…