Utasema vipi Mungu anatupa nafasi ya kuchagua hatima yetu ikiwa hata kuzaliwa hatuchagui, tunajikuta tu tumezaliwa?Mkuu iko hivi Mungu yupo fair Sana
Anatupa nafasi ya Sisi wenyewe kuchagua hatima yetu,Hana upendeleo WA kuteua watu Fulani Tu ndio waje wapate Makao mema
Ndio maana ametufahamisha lipi zuri na lipi Baya,na akatuhimiza kwenda kwenye mazuri na akatutahadharisha na njia mbaya
Then mwisho wa siku ametupa Uhuru WA kuchagua ambao ndio mtihani kwetu,tufaulu au tufeli
Mkuu hii hoja yako nilishaijibu hapo awaliUtasema vipi Mungu anatupa nafasi ya kuchagua hatima yetu ikiwa hata kuzaliwa hatuchagui, tunajikuta tu tumezaliwa?
Huoni kwamba ukishaanza hoja yako na "huwezi kuchagua kuzaliwa" unakubaliana nami kwamba watu hawapewi uchaguzi wa kuzaliwa au kutozaliwa, na hivyo hoja yote ya kwamba wana uhuru wa kuchagua inatoweka?Mkuu hii hoja yako nilishaijibu hapo awali
Lakini ngoja nirudie tena,
Huwezi kuchagua kuzaliwa wakati awali hukuwepo mkuu
Mfano rahisi ni Mimi na wewe sasa hivi tunatembea na mbegu za kizazi chetu katika suruali zetu,je hiki kizazi ambacho hakijatokea au sababu ya kutokea kwake bado haijafanyika Kwa maana bado hatujakutana na mwanamke,je huyu mtoto atachaguaje kuzaliwa wakati bado hajapatikana au hayupo kabisa?
Je, unakubali/unaamini dhana ya sayansi isemayo energy can neither be created nor destroyed ?Ukishakubali kwamba Mungu hana mwanzo wala mwisho, umeshalibatilisha swali la kuuliza injinia kwa yeyote, kwa sababu ushaonesha kwamba inawezekana kilicho complex kikawepo bila ya injinia wake kuhitajika au kukiumba.
Ukikubali Mungu hana mwanzo wala mwisho, halafu ukauliza injinia wa mtu ni nani, umefanya kitu Waingereza wanakiita "You want to eat your cake and still have it". Unataka kuila keki yako uimalize, halafu keki ibakie kuwapo kwenye kisahani chako.
Kwa upande mmoja unakubali kilicho complex si lazima kiwe na muumbaji wala na mwanzo, kwa kusema Mungu hana muumbaji wala mwanzo, halafu kwa upande mwingine unakanusha hilohilo kwa kuhoji mtu kaumbwaje na mwanzo wake ni nini?
This is a contradiction. Chagua upande mmoja. Je, kilicho complex ni lazima kiwe na mwanzo na muumbaji? Au si lazima?
Kama ni lazima kilicho complex kiwe na mwanzo au muumbaji, basi, Mungu hayupo, kwa sababu na yeye atahitaji muumbaji, na akihitaji muumbaji, basi huyo si Mungu.
Kama si lazima kilicho complex kiwe na mwanzo au muumbaji, basi Mungu hahitajiki kama chanzo cha kitu chochote kilicho complex.
Jibu lolote utakalolitoa linatuonesha udhaifu wa hoja ya kuwepo Mungu huyo.
Kwenye swali lako la vitu tusivyoviona lakini vipo, mimi sijawahi kukanusha uwepo wa Mungu kwa sababu haonekani. Nakupa kazi ya kutafuta nilipokanusha uwepo wa Mungu kwa sababu haonekani, hutapata hilo.
Mambo mengi hayaonekani, lakini yapo. Jicho la mtu halioni the electromagnetic spectrum yote, hatuoni heat waves, hatuoni radio waves, hatuoni microwaves, hatuoni ultraviolet waves, tunaona sehemu ndogo tu ya electromagnetic waves, visibke light.
Je, hilo linamaanisha hizo waves zote tusizoziina hazipo? Zipo.
Nimegundua watu wengi wanashindwa kujadiliana kidhahania hapa, kwa sababu hawaelewi hata hoja zangu ni zipi.
Sikatai Mungu yupo kwa sababu haonekani.
Nakataa uwepo wa Mungu muweza yote, mwenye ujuzi wote na upendo wote, kwa sababu uwepo wake ukiulinganisha na uwepo wa dunia hii inayoruhusu mabaya mengi sana kwa vinavyoitwa viumbe wake unatengeneza logical inconsistency, unatengeneza contradiction.
Uwepo wa Mungu huyo ni sawasawa na uwepo wa pembetatu ambayo hapohapo ni duara katika Euclidean geometry. Au uwepo binti mwenye miezi 6 leo, ambaye ni mama mzazi wa mwanamme mwenye miaka 30 leo, au kuambiwa kwamba 10 ni square root ya 2.
Haya mambo yote matatu niliyoyataja hapo juu naweza kuyakanusha na kusema si kweli.
Si kwa sababu siwezi kuona pembetatu ambayo hapohapo ni duara, si kwa sababu siwezi kumuona binti mchanga wa miezi sita leo ambaye ni mama mzazi wa mwanamme mwenye miaka 30 leo, si kwa sababu siwezi kuiona 10 ambayo ni square root ya 2, bali kwa sababu haya mambo yote yana logical inconsistency inayo contradict mantiki muhimu.
Suala la kuona si muhimu katika kuthibitisha uwepo wa kitu.
Kwa sababu.
1. Unaweza kuona kitu ambacho hakipo. Ukiwa barabarani jangwani au sehemu yenye joto, unaweza kuona maji kwa mbali, wakati hakuna maji. Ni mirage tu.
2. Unaweza ukashindwa kuona kitu ambacho kipo. Nimetoa mfano wa electromagnetic waves zilizo tofauti na visible light hapo juu.
3. Unaweza kuona kitu ambacho kipo. Mifano ni mingi hapa.
4. Unaweza kushindwa kuona kitu ambacho hakipo. Mfano pembetatu ambayo hapohapo ni duara katika Euclidean geometry.
Sasa, katika ulimwengu ambao hayo manne yanawezekana, kwa nini kitu kuonekana au kutoonekana kuwe ni muhimu katika uthibitisho kwamba kipo?
Kwa nini tunashindwa kuongelea uwepo au kutokuwepo Mungu katika ngazi ya kidhahania na kimantiki kwa hoja tunduizi, bila kushikilia hoja dhaifu kama ya kitu kuonekana au kutoonekana, ambayo mimi hata sijaitaja?
Katika muktadha gani?Je, unakubali/unaamini dhana ya sayansi isemayo energy can neither be created nor destroyed ?
Huoni kwamba ukishaanza hoja yako na "huwezi kuchagua kuzaliwa" unakubaliana nami kwamba watu hawapewi uchaguzi wa kuzaliwa au kutozaliwa, na hivyo hoja yote ya kwamba wana uhuru wa kuchagua inatoweka?
Uhuru wa kuchagua kuzaliwa au kutozaliwa ndiyo uhuru mkubwa kabisa katika maisha, sasa utasema vipi tuna uhuru wa kuchagua katika maisha ikiwa hata huko kuzaliwa kwenyewe hatuchagui?
Kwa nini Mungu hakutupa uhuru wa kuchagua kuzaliwa au kutozaliwa, katufanya tujikute tumezaliwa tu?
Unataka kusema Mungu wako muweza yote alishindwa kufanya namna ya kutupa uchaguzi wa kuamua tuzaliwe au tusizaliwe?
Zaidi ya hapo, hata kwenye kuzaliwa hatuna uhuru wa kuchagua tunazaliwa wapi, hatuna uhuru wa kuchagua tunazaliwa na wazazi gani, hatuna uhuru wa kuchagua vinasaba vyetu vikoje, hatuna uhuru wa kuchagua tunazaliwa mwaka gani, siku gani, saa ngapi, na haya ni mambo yanayokuja kuathiri sana maisha yetu, sasa hapo utasemaje tuna uhuru wa kuchagua?
Unaelewa kwamba unakubaliana nami kwamba hatupewi uchaguzi wa kuzaliwa au kutozaliwa?Mkuu naona umekaza Sana kwenye hii hoja huenda ndio msumari wako wa mwisho au kete yako ya mwisho katika haya majadiliano.
Kama Mungu angeamua kutupa huo Uhuru unao sema wewe basi WA Kwanza kupewa angekuwa Adamu,maana yeye ndio original yetu na sie wengine ni copy yake Tu,yeye aliumbwa lakini Sisi tumepatikana Kwa kuzaliana.
Je iweje anaezaliwa akawa na uchaguzi wakati ameshatengenezewa formular tayar?
Unaelewa kwamba unakubaliana nami kwamba hatupewi uchaguzi wa kuzaliwa au kutozaliwa?
Hilo unalielewa?
Mungu wako mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ni dikteta?Naweza kusema ndio au hapana kutokana na sababu zifuatazo
Inaweza ikawa ndio endapo tuliomba kupewa Uhuru na hatujapewa,hapo ndio tutasema tulitaka Uhuru hatujapewa
Lakini pili huenda hakukuwa na mantiki yoyote ya kupewa huo uchaguzi
Waislamu mnaamin mko sahii ilo ndo tatizo lenuHuo uongo mkuu
Amini usiamini ni juu yako
Karibu sana
Mkuu hayo yote yanatoka wapiWaislamu mnaamin mko sahii ilo ndo tatizo lenu
Wapi nimekulaumu ebu ntolee kicha chako hapaMkuu hayo yote yanatoka wapi
Mimi na Kiranga katika majadiliano je umeona namlaumu yeye kwa kutomwamini Mungu au yeye Kwa kunilaumu Mimi kuwa muislamu?
Usipende kuongea mambo mepesi mepesi Tu mkuu!
Let's say hajatupa Kwa mtazamo wakoMungu wako mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ni dikteta?
Hataki kuwapa watu uhuru wa kuchagua?
Hahaha unaona sasa uvumilivu unakushinda unaanza kuita watu vichaa!Wapi nimekulaumu ebu ntolee kicha chako hapa
Unantuhumu kwa tuhuma za kutunga huo ni ukichaaHahaha unaona sasa uvumilivu unakushinda unaanza kuita watu vichaa!
Asante na uwe na siku njema
Nimekosa Mimi mkuuUnantuhumu kwa tuhuma za kutunga huo ni ukichaa
Siyo kwamba inanifanya niamini kwamba hakuna Mungu.Let's say hajatupa Kwa mtazamo wako
Je hiyo ndo inakufanya uamini kuwa hakuna mungu
Mungu alivyompa Adam uhuru wa kuchagua kati ya mti wa uzima au uzima na ubaya alikua dikteta unajua mambo mengine ni ya ajabu sanaSiyo kwamba inanifanya niamini kwamba hakuna Mungu.
Hilo litaonesha habari nzima ya kwamba Mungu katupa uhuru wa kuchagua ina contradiction. Ni uongo.
Na kama hatuna uhuru wa kuchagua maana yake hizi habari za kwamba Mungu atatuhukumu kwa kuangalia tuliyochagua nayo ni uongo.
Na hapo tutajiuliza, kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote asitupe uhuru wa kuchagua?
Na hapo litatokea swali, huyu Mungu yupo kweli? Au watu wamemtunga tu?
Mbona habari za kuwapo kwake zina contradiction kila sehemu tukizichunguza?
Kuhusu kupewa Uhuru WA kuchagua tumepewa katika mambo mengi Sana,mfano Adam na Hawa waliambiwa wasile mti Fulani WA matunda,lakini wao walichagua Kula na kuyapata waliyoyapataSiyo kwamba inanifanya niamini kwamba hakuna Mungu.
Hilo litaonesha habari nzima ya kwamba Mungu katupa uhuru wa kuchagua ina contradiction. Ni uongo.
Na kama hatuna uhuru wa kuchagua maana yake hizi habari za kwamba Mungu atatuhukumu kwa kuangalia tuliyochagua nayo ni uongo.
Na hapo tutajiuliza, kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote asitupe uhuru wa kuchagua?
Na hapo litatokea swali, huyu Mungu yupo kweli? Au watu wamemtunga tu?
Mbona habari za kuwapo kwake zina contradiction kila sehemu tukizichunguza?
Nakwambia hivi, kama Adam na Hawa hawakuulizwa waumbwe au wasiumbwe, wakajikuta wameumbwa tu, baada ya hapo huwezi kusema wamepeea uhuru.Kuhusu kupewa Uhuru WA kuchagua tumepewa katika mambo mengi Sana,mfano Adam na Hawa waliambiwa wasile mti Fulani WA matunda,lakini wao walichagua Kula na kuyapata waliyoyapata
Iblis aliambiwa amsujudie Adam sijida ya heshima lkn yeye alichagua kukataa kumsujudia
Mungu amesema yeye ni mmoja Tu lakini kuna binadamu wameamua kuchagua miungu Yao mbali mbali,mpaka hapo tunaona binadamu Wana Uhuru WA kuchagua.
Ila linapokuja swala la kuchagua kuzaliwa hapo hatukupewa uchaguzi
Sasa kama kuna baadhi ya mambo tumepewa uchaguzi basi yatosha kusema kuwa Mungu ametupa uchaguzi
Na
Kama tusingepewq kabisa Uhuru WA kuchagua japo Jambo moja Tu,basi hapo ingetosha kusema kuwa hakika Mungu hakutupa uchaguzi kabisa.
Umezungumzia kuwa uwepo wa Mungu kila sehemu Una contradiction,je waeza dhibitisha juu ya Hilo swala?