Waislamu Mnafeli wapi?

Waislamu Mnafeli wapi?

Mkuu iko hivi Mungu yupo fair Sana

Anatupa nafasi ya Sisi wenyewe kuchagua hatima yetu,Hana upendeleo WA kuteua watu Fulani Tu ndio waje wapate Makao mema

Ndio maana ametufahamisha lipi zuri na lipi Baya,na akatuhimiza kwenda kwenye mazuri na akatutahadharisha na njia mbaya

Then mwisho wa siku ametupa Uhuru WA kuchagua ambao ndio mtihani kwetu,tufaulu au tufeli
Utasema vipi Mungu anatupa nafasi ya kuchagua hatima yetu ikiwa hata kuzaliwa hatuchagui, tunajikuta tu tumezaliwa?
 
Utasema vipi Mungu anatupa nafasi ya kuchagua hatima yetu ikiwa hata kuzaliwa hatuchagui, tunajikuta tu tumezaliwa?
Mkuu hii hoja yako nilishaijibu hapo awali

Lakini ngoja nirudie tena,
Huwezi kuchagua kuzaliwa wakati awali hukuwepo mkuu

Mfano rahisi ni Mimi na wewe sasa hivi tunatembea na mbegu za kizazi chetu katika suruali zetu,je hiki kizazi ambacho hakijatokea au sababu ya kutokea kwake bado haijafanyika Kwa maana bado hatujakutana na mwanamke,je huyu mtoto atachaguaje kuzaliwa wakati bado hajapatikana au hayupo kabisa?
 
Mkuu hii hoja yako nilishaijibu hapo awali

Lakini ngoja nirudie tena,
Huwezi kuchagua kuzaliwa wakati awali hukuwepo mkuu

Mfano rahisi ni Mimi na wewe sasa hivi tunatembea na mbegu za kizazi chetu katika suruali zetu,je hiki kizazi ambacho hakijatokea au sababu ya kutokea kwake bado haijafanyika Kwa maana bado hatujakutana na mwanamke,je huyu mtoto atachaguaje kuzaliwa wakati bado hajapatikana au hayupo kabisa?
Huoni kwamba ukishaanza hoja yako na "huwezi kuchagua kuzaliwa" unakubaliana nami kwamba watu hawapewi uchaguzi wa kuzaliwa au kutozaliwa, na hivyo hoja yote ya kwamba wana uhuru wa kuchagua inatoweka?

Uhuru wa kuchagua kuzaliwa au kutozaliwa ndiyo uhuru mkubwa kabisa katika maisha, sasa utasema vipi tuna uhuru wa kuchagua katika maisha ikiwa hata huko kuzaliwa kwenyewe hatuchagui?

Kwa nini Mungu hakutupa uhuru wa kuchagua kuzaliwa au kutozaliwa, katufanya tujikute tumezaliwa tu?

Unataka kusema Mungu wako muweza yote alishindwa kufanya namna ya kutupa uchaguzi wa kuamua tuzaliwe au tusizaliwe?

Zaidi ya hapo, hata kwenye kuzaliwa hatuna uhuru wa kuchagua tunazaliwa wapi, hatuna uhuru wa kuchagua tunazaliwa na wazazi gani, hatuna uhuru wa kuchagua vinasaba vyetu vikoje, hatuna uhuru wa kuchagua tunazaliwa mwaka gani, siku gani, saa ngapi, na haya ni mambo yanayokuja kuathiri sana maisha yetu, sasa hapo utasemaje tuna uhuru wa kuchagua?
 
Ukishakubali kwamba Mungu hana mwanzo wala mwisho, umeshalibatilisha swali la kuuliza injinia kwa yeyote, kwa sababu ushaonesha kwamba inawezekana kilicho complex kikawepo bila ya injinia wake kuhitajika au kukiumba.

Ukikubali Mungu hana mwanzo wala mwisho, halafu ukauliza injinia wa mtu ni nani, umefanya kitu Waingereza wanakiita "You want to eat your cake and still have it". Unataka kuila keki yako uimalize, halafu keki ibakie kuwapo kwenye kisahani chako.

Kwa upande mmoja unakubali kilicho complex si lazima kiwe na muumbaji wala na mwanzo, kwa kusema Mungu hana muumbaji wala mwanzo, halafu kwa upande mwingine unakanusha hilohilo kwa kuhoji mtu kaumbwaje na mwanzo wake ni nini?

This is a contradiction. Chagua upande mmoja. Je, kilicho complex ni lazima kiwe na mwanzo na muumbaji? Au si lazima?

Kama ni lazima kilicho complex kiwe na mwanzo au muumbaji, basi, Mungu hayupo, kwa sababu na yeye atahitaji muumbaji, na akihitaji muumbaji, basi huyo si Mungu.

Kama si lazima kilicho complex kiwe na mwanzo au muumbaji, basi Mungu hahitajiki kama chanzo cha kitu chochote kilicho complex.

Jibu lolote utakalolitoa linatuonesha udhaifu wa hoja ya kuwepo Mungu huyo.

Kwenye swali lako la vitu tusivyoviona lakini vipo, mimi sijawahi kukanusha uwepo wa Mungu kwa sababu haonekani. Nakupa kazi ya kutafuta nilipokanusha uwepo wa Mungu kwa sababu haonekani, hutapata hilo.

Mambo mengi hayaonekani, lakini yapo. Jicho la mtu halioni the electromagnetic spectrum yote, hatuoni heat waves, hatuoni radio waves, hatuoni microwaves, hatuoni ultraviolet waves, tunaona sehemu ndogo tu ya electromagnetic waves, visibke light.

Je, hilo linamaanisha hizo waves zote tusizoziina hazipo? Zipo.

Nimegundua watu wengi wanashindwa kujadiliana kidhahania hapa, kwa sababu hawaelewi hata hoja zangu ni zipi.

Sikatai Mungu yupo kwa sababu haonekani.

Nakataa uwepo wa Mungu muweza yote, mwenye ujuzi wote na upendo wote, kwa sababu uwepo wake ukiulinganisha na uwepo wa dunia hii inayoruhusu mabaya mengi sana kwa vinavyoitwa viumbe wake unatengeneza logical inconsistency, unatengeneza contradiction.

Uwepo wa Mungu huyo ni sawasawa na uwepo wa pembetatu ambayo hapohapo ni duara katika Euclidean geometry. Au uwepo binti mwenye miezi 6 leo, ambaye ni mama mzazi wa mwanamme mwenye miaka 30 leo, au kuambiwa kwamba 10 ni square root ya 2.

Haya mambo yote matatu niliyoyataja hapo juu naweza kuyakanusha na kusema si kweli.

Si kwa sababu siwezi kuona pembetatu ambayo hapohapo ni duara, si kwa sababu siwezi kumuona binti mchanga wa miezi sita leo ambaye ni mama mzazi wa mwanamme mwenye miaka 30 leo, si kwa sababu siwezi kuiona 10 ambayo ni square root ya 2, bali kwa sababu haya mambo yote yana logical inconsistency inayo contradict mantiki muhimu.

Suala la kuona si muhimu katika kuthibitisha uwepo wa kitu.

Kwa sababu.

1. Unaweza kuona kitu ambacho hakipo. Ukiwa barabarani jangwani au sehemu yenye joto, unaweza kuona maji kwa mbali, wakati hakuna maji. Ni mirage tu.

2. Unaweza ukashindwa kuona kitu ambacho kipo. Nimetoa mfano wa electromagnetic waves zilizo tofauti na visible light hapo juu.

3. Unaweza kuona kitu ambacho kipo. Mifano ni mingi hapa.

4. Unaweza kushindwa kuona kitu ambacho hakipo. Mfano pembetatu ambayo hapohapo ni duara katika Euclidean geometry.

Sasa, katika ulimwengu ambao hayo manne yanawezekana, kwa nini kitu kuonekana au kutoonekana kuwe ni muhimu katika uthibitisho kwamba kipo?

Kwa nini tunashindwa kuongelea uwepo au kutokuwepo Mungu katika ngazi ya kidhahania na kimantiki kwa hoja tunduizi, bila kushikilia hoja dhaifu kama ya kitu kuonekana au kutoonekana, ambayo mimi hata sijaitaja?
Je, unakubali/unaamini dhana ya sayansi isemayo energy can neither be created nor destroyed ?
 
Je, unakubali/unaamini dhana ya sayansi isemayo energy can neither be created nor destroyed ?
Katika muktadha gani?

Sayansi hiyo hiyo inasema all energy was created at the Big Bang. Kwa hivyo, kusema kwamba sayansi inasema energy can neither be created nor destroyed bila kuweka muktadha si sawa.
 
Huoni kwamba ukishaanza hoja yako na "huwezi kuchagua kuzaliwa" unakubaliana nami kwamba watu hawapewi uchaguzi wa kuzaliwa au kutozaliwa, na hivyo hoja yote ya kwamba wana uhuru wa kuchagua inatoweka?

Uhuru wa kuchagua kuzaliwa au kutozaliwa ndiyo uhuru mkubwa kabisa katika maisha, sasa utasema vipi tuna uhuru wa kuchagua katika maisha ikiwa hata huko kuzaliwa kwenyewe hatuchagui?

Kwa nini Mungu hakutupa uhuru wa kuchagua kuzaliwa au kutozaliwa, katufanya tujikute tumezaliwa tu?

Unataka kusema Mungu wako muweza yote alishindwa kufanya namna ya kutupa uchaguzi wa kuamua tuzaliwe au tusizaliwe?

Zaidi ya hapo, hata kwenye kuzaliwa hatuna uhuru wa kuchagua tunazaliwa wapi, hatuna uhuru wa kuchagua tunazaliwa na wazazi gani, hatuna uhuru wa kuchagua vinasaba vyetu vikoje, hatuna uhuru wa kuchagua tunazaliwa mwaka gani, siku gani, saa ngapi, na haya ni mambo yanayokuja kuathiri sana maisha yetu, sasa hapo utasemaje tuna uhuru wa kuchagua?

Mkuu naona umekaza Sana kwenye hii hoja huenda ndio msumari wako wa mwisho au kete yako ya mwisho katika haya majadiliano.

Kama Mungu angeamua kutupa huo Uhuru unao sema wewe basi WA Kwanza kupewa angekuwa Adamu,maana yeye ndio original yetu na sie wengine ni copy yake Tu,yeye aliumbwa lakini Sisi tumepatikana Kwa kuzaliana.

Je iweje anaezaliwa akawa na uchaguzi wakati ameshatengenezewa formular tayar?
 
Mkuu naona umekaza Sana kwenye hii hoja huenda ndio msumari wako wa mwisho au kete yako ya mwisho katika haya majadiliano.

Kama Mungu angeamua kutupa huo Uhuru unao sema wewe basi WA Kwanza kupewa angekuwa Adamu,maana yeye ndio original yetu na sie wengine ni copy yake Tu,yeye aliumbwa lakini Sisi tumepatikana Kwa kuzaliana.

Je iweje anaezaliwa akawa na uchaguzi wakati ameshatengenezewa formular tayar?
Unaelewa kwamba unakubaliana nami kwamba hatupewi uchaguzi wa kuzaliwa au kutozaliwa?

Hilo unalielewa?

Tukubaliane hapo kwanza tujue tunapatana sawa mpaka hapo.
 
Unaelewa kwamba unakubaliana nami kwamba hatupewi uchaguzi wa kuzaliwa au kutozaliwa?

Hilo unalielewa?

Naweza kusema ndio au hapana kutokana na sababu zifuatazo

Inaweza ikawa ndio endapo tuliomba kupewa Uhuru na hatujapewa,hapo ndio tutasema tulitaka Uhuru hatujapewa

Lakini pili huenda hakukuwa na mantiki yoyote ya kupewa huo uchaguzi
 
Naweza kusema ndio au hapana kutokana na sababu zifuatazo

Inaweza ikawa ndio endapo tuliomba kupewa Uhuru na hatujapewa,hapo ndio tutasema tulitaka Uhuru hatujapewa

Lakini pili huenda hakukuwa na mantiki yoyote ya kupewa huo uchaguzi
Mungu wako mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ni dikteta?

Hataki kuwapa watu uhuru wa kuchagua?
 
Waislamu mnaamin mko sahii ilo ndo tatizo lenu
Mkuu hayo yote yanatoka wapi

Mimi na Kiranga katika majadiliano je umeona namlaumu yeye kwa kutomwamini Mungu au yeye Kwa kunilaumu Mimi kuwa muislamu?

Usipende kuongea mambo mepesi mepesi Tu mkuu!
 
Mkuu hayo yote yanatoka wapi

Mimi na Kiranga katika majadiliano je umeona namlaumu yeye kwa kutomwamini Mungu au yeye Kwa kunilaumu Mimi kuwa muislamu?

Usipende kuongea mambo mepesi mepesi Tu mkuu!
Wapi nimekulaumu ebu ntolee kicha chako hapa
 
Mungu wako mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ni dikteta?

Hataki kuwapa watu uhuru wa kuchagua?
Let's say hajatupa Kwa mtazamo wako

Je hiyo ndo inakufanya uamini kuwa hakuna mungu
 
Let's say hajatupa Kwa mtazamo wako

Je hiyo ndo inakufanya uamini kuwa hakuna mungu
Siyo kwamba inanifanya niamini kwamba hakuna Mungu.

Hilo litaonesha habari nzima ya kwamba Mungu katupa uhuru wa kuchagua ina contradiction. Ni uongo.

Na kama hatuna uhuru wa kuchagua maana yake hizi habari za kwamba Mungu atatuhukumu kwa kuangalia tuliyochagua nayo ni uongo.

Na hapo tutajiuliza, kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote asitupe uhuru wa kuchagua?

Na hapo litatokea swali, huyu Mungu yupo kweli? Au watu wamemtunga tu?

Mbona habari za kuwapo kwake zina contradiction kila sehemu tukizichunguza?
 
Siyo kwamba inanifanya niamini kwamba hakuna Mungu.

Hilo litaonesha habari nzima ya kwamba Mungu katupa uhuru wa kuchagua ina contradiction. Ni uongo.

Na kama hatuna uhuru wa kuchagua maana yake hizi habari za kwamba Mungu atatuhukumu kwa kuangalia tuliyochagua nayo ni uongo.

Na hapo tutajiuliza, kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote asitupe uhuru wa kuchagua?

Na hapo litatokea swali, huyu Mungu yupo kweli? Au watu wamemtunga tu?

Mbona habari za kuwapo kwake zina contradiction kila sehemu tukizichunguza?
Mungu alivyompa Adam uhuru wa kuchagua kati ya mti wa uzima au uzima na ubaya alikua dikteta unajua mambo mengine ni ya ajabu sana
 
Siyo kwamba inanifanya niamini kwamba hakuna Mungu.

Hilo litaonesha habari nzima ya kwamba Mungu katupa uhuru wa kuchagua ina contradiction. Ni uongo.

Na kama hatuna uhuru wa kuchagua maana yake hizi habari za kwamba Mungu atatuhukumu kwa kuangalia tuliyochagua nayo ni uongo.

Na hapo tutajiuliza, kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote asitupe uhuru wa kuchagua?

Na hapo litatokea swali, huyu Mungu yupo kweli? Au watu wamemtunga tu?

Mbona habari za kuwapo kwake zina contradiction kila sehemu tukizichunguza?
Kuhusu kupewa Uhuru WA kuchagua tumepewa katika mambo mengi Sana,mfano Adam na Hawa waliambiwa wasile mti Fulani WA matunda,lakini wao walichagua Kula na kuyapata waliyoyapata

Iblis aliambiwa amsujudie Adam sijida ya heshima lkn yeye alichagua kukataa kumsujudia

Mungu amesema yeye ni mmoja Tu lakini kuna binadamu wameamua kuchagua miungu Yao mbali mbali,mpaka hapo tunaona binadamu Wana Uhuru WA kuchagua.

Ila linapokuja swala la kuchagua kuzaliwa hapo hatukupewa uchaguzi

Sasa kama kuna baadhi ya mambo tumepewa uchaguzi basi yatosha kusema kuwa Mungu ametupa uchaguzi

Na

Kama tusingepewq kabisa Uhuru WA kuchagua japo Jambo moja Tu,basi hapo ingetosha kusema kuwa hakika Mungu hakutupa uchaguzi kabisa.

Umezungumzia kuwa uwepo wa Mungu kila sehemu Una contradiction,je waeza dhibitisha juu ya Hilo swala?
 
Kuhusu kupewa Uhuru WA kuchagua tumepewa katika mambo mengi Sana,mfano Adam na Hawa waliambiwa wasile mti Fulani WA matunda,lakini wao walichagua Kula na kuyapata waliyoyapata

Iblis aliambiwa amsujudie Adam sijida ya heshima lkn yeye alichagua kukataa kumsujudia

Mungu amesema yeye ni mmoja Tu lakini kuna binadamu wameamua kuchagua miungu Yao mbali mbali,mpaka hapo tunaona binadamu Wana Uhuru WA kuchagua.

Ila linapokuja swala la kuchagua kuzaliwa hapo hatukupewa uchaguzi

Sasa kama kuna baadhi ya mambo tumepewa uchaguzi basi yatosha kusema kuwa Mungu ametupa uchaguzi

Na

Kama tusingepewq kabisa Uhuru WA kuchagua japo Jambo moja Tu,basi hapo ingetosha kusema kuwa hakika Mungu hakutupa uchaguzi kabisa.

Umezungumzia kuwa uwepo wa Mungu kila sehemu Una contradiction,je waeza dhibitisha juu ya Hilo swala?
Nakwambia hivi, kama Adam na Hawa hawakuulizwa waumbwe au wasiumbwe, wakajikuta wameumbwa tu, baada ya hapo huwezi kusema wamepeea uhuru.

Kwa sababu, uhuru wowote watakaopewa umechorewa mistari, wameshazaliwa, hawakuwa na nafasi ya kukataa kuzaliwa.

Ni sawa na kauli ya kumtuhumu mtengeneza magari wa Marekani Ford. Ford aliulizwa kama watu wana uhuru wa kuchagua rangi yoyote wanayoitaka kwenye magari anayotengeneza ya Model T. Ford akasema watu wanaweza kuchagua rangi yoyote, ili mradi rangi wanayochagua iwe nyeusi.

Nikikwambia unaweza kuchagua gari la rangi yoyote, ilimradi hiyo rangi iwe nyeusi, hapo nimekupa uhuru wa kuchagua rangi au nimekuchagulia?

Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote anakuwa contradicted na ulimwengu unaoruhusu mabaya.

Ama ulimwengu unaoruhusu mabaya upo, na Mungu huyo hayupo.

Ama huyo Mungu yupo, na ulimwengu unaoruhusu mabaya haupo.

Viwili hivi haviwezi kuwapo pamoja vyote, that is a logical contradiction.

Tunaona ulimwengu unaoruhusu mabaya upo.

Hivyo, Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.
 
Back
Top Bottom